Kumtetea Dumbya ni kazi wazee

Kumtetea Dumbya ni kazi wazee

Rico redi

Senior Member
Joined
Jul 15, 2023
Posts
167
Reaction score
354
Toka amekuja tuliamini ni international striker ambaye atatoa quality ambayo huwezi kuipata Kwa local players matokeo yake imekua ni tofauti

Kapewa muda,katiwa moyo na mashabiki alipelekewa mpaka kuku + mabango ya kwamba tuko pamoja lakini wapi goli ambalo katengenezewa leo kakosa ambalo morice kamalizia limefanya niishiwe nguvu

Nashindwa kuelewa kocha naona kitu gani ambacho si hatukioni mgunda kapewa dk chache angalia effect yake goli mbili za mwisho zimeanzia kwake ni upuuzi kuendelea kumpa nafasi mtu ambaye anahitaji muda huku ukiacha mtu ambaye yupo tayari na anaweza kukupa matokeo

Kocha anatakiwa ajifunze kutoa nafasi Kwa wachezaji wakiprove wapewe namba mfano kelvin nashon,mgunda etc sio unang'ang'ania mtu mmoja
 
Toka amekuja tuliamini ni international striker ambaye atatoa quality ambayo huwezi kuipata Kwa local players matokeo yake imekua ni tofauti

Kapewa muda,katiwa moyo na mashabiki alipelekewa mpaka kuku + mabango ya kwamba tuko pamoja lakini wapi goli ambalo katengenezewa leo kakosa ambalo morice kamalizia limefanya niishiwe nguvu

Nashindwa kuelewa kocha naona kitu gani ambacho si hatukioni mgunda kapewa dk chache angalia effect yake goli mbili za mwisho zimeanzia kwake ni upuuzi kuendelea kumpa nafasi mtu ambaye anahitaji muda huku ukiacha mtu ambaye yupo tayari na anaweza kukupa matokeo

Kocha anatakiwa ajifunze kutoa nafasi Kwa wachezaji wakiprove wapewe namba mfano kelvin nashon,mgunda etc sio unang'ang'ania mtu mmoja
Ulikuwa unaiangalia Simba au Doumbia?
 
Ndugu zangu yule Doumbia ni Osimhen mtupu! Mpeni muda mtakuja kuyafaidi matunda yake.
 
Toka amekuja tuliamini ni international striker ambaye atatoa quality ambayo huwezi kuipata Kwa local players matokeo yake imekua ni tofauti

Kapewa muda,katiwa moyo na mashabiki alipelekewa mpaka kuku + mabango ya kwamba tuko pamoja lakini wapi goli ambalo katengenezewa leo kakosa ambalo morice kamalizia limefanya niishiwe nguvu

Nashindwa kuelewa kocha naona kitu gani ambacho si hatukioni mgunda kapewa dk chache angalia effect yake goli mbili za mwisho zimeanzia kwake ni upuuzi kuendelea kumpa nafasi mtu ambaye anahitaji muda huku ukiacha mtu ambaye yupo tayari na anaweza kukupa matokeo

Kocha anatakiwa ajifunze kutoa nafasi Kwa wachezaji wakiprove wapewe namba mfano kelvin nashon,mgunda etc sio unang'ang'ania mtu mmoja
Kikubwa tuneshinda ushindi mnono sana
 
Doumbya hana tatizo lolote. Wenye matatizo ni benchi la ufundi la Simba. Nadhani benchi la ufundi lote la Simba haliko timamu. Haiwezekani timu kubwa kama Simba ije kukuza kipaji ambacho hakipo kabisa tena cha mchezaji wa kimataifa. Doumbya mpaka sasa amecheza mechi 10+ za mashindano na za kirafiki lakini hakuna kitu cha maana anachokifanya uwanjani zaidi ya:
1. Kuzuia pasi zisifike kwa wachezaji wenzake
2. Kuzuia mipira inayoingia kwenye goli la timu pinzani.
2. Kuanguka anguka uwanjani.
3. Kucheza off position. Badala abaki juu apress mabeki wa timu pinzani yeye anarudi katikati ya uwanja na kuwaacha mabeki wa timu pinzani wafanye buid up wasogee mpaka mstari wa katikati. Sijui akikaa pale benchi huwa haangali anachokifanya Mpanzu. Kila mechi anayoingia huyu mwamba anafanya Simba ianze kuelemewa kwa sababu hatimizi wajibu wake uwanjani anaacha viungo na mabeki wa Simba wafanye kazi ya ziada kuzuia.
4. Kushangilia magoli waliyofunga wenzake.

Nakiri kabisa kuwa mimi ni mmoja wa watu wanaoamini kuwa Paul Peter ni bora kuliko Mgunda. Lakini alichokifanya Mgunda leo ni bora mara mia kuliko madudu anayofanya Doumbya kila siku. Huwa najiuliza benchi la ufundi linataka kuona nini kipya kwa Doumbya ambacho hawajakiona kiasi kila mechi lazima acheze? Je ni mkataba wake ndio unasema lazima Doumbya apangwe kama ilivyokuwa kwenye mkataba wa Saidoo Ntizabazonkiza? Hivi mbona Loemba hapangwi kila mechi ili kufufua kipaji chake ambapo bora yeye tumeshakiona japo mwenyewe kuna mahali kazembea.

Uwezo tu wa Bashir Kibaila yule dogo wa Simba "B" Doumbya haiingi hata chembe lakini utakuta mshahara wa Doumbya ni zaidi hata ya mara ishirini ya mshahara wa Bashir. Na sio huyo tu uwezo wa Chasambi ni mkubwa kuliko Doumbya lakini yeye Chasambi hajavumiliwa kaachwa. Vipi huyo Doumbya aliyemleta ni nani pale Simba ambaye anahakikisha sio tu kwamba Doumbya aendelee kuwepo pale Simba bali kila mechi lazima acheze.

Kwa alichokifanya Mgunda leo benchi la ufundi la ufundi la Simba likimpa jezi Doumbya mechi ijayo basi litakuwa ni sehemu ya wanoikujumu Simba na utakuwa ni upuuzi wa hali ya juu na itakuwa kumkosea heshima Mgunda. Na hiyo itakuwa pia ni sawa na kuwakosea heshima wachezaji wazawa. Kwa mtizamo wangu mimi naona Doumbya hastahili tena kukaaa hata kwenye benchi la Simba. Kuanzia sasa inatakiwa Mgunda na yeye apewe mechi 10+ mfululizo tuone ana nini na sio kulazimisha Doumbya acheze tu wakati ni garasa linaonekana wazi. Mbaya zaidi hata pasi aliyopewa yeye leo ili aguse tu mpira uingie golini umempita tobo ukamkuta Abraham Morice ndio akamalizia.

Ni mtizamo tu.
 
Doumbia kasajiliwa na Mo ni lazima acheze, shida sio bench la ufundi bali maagizo ya Tajiri. Mhindi wetu hataki aonekane amesajili ghalasa la mpira.
 
Doumbia kasajiliwa na Mo ni lazima acheze, shida sio bench la ufundi bali maagizo ya Tajiri. Mhindi wetu hataki aonekane amesajili ghalasa la mpira.
Hii naweza kuamini maana sio kwa kulazimisha kule acheze kila mechi ili kiwango kipande. Na Mungu si Juma Nature huyo Doumbya mechi 10+ jamaa bado kituko. Mwenzanke Mgunda assist moja na pre assist 1 kwenye mechi moja . Kwa mtindo huu hata ile ya Loemba kuwa kaletwa na Jayrutty kwa hiyo asicheze ni kama kuna kaukweli fulani hivi. Maana kwanza wamefrustrate Loemba naye kaingia kwenye mfumo maana sasa hivi kama kachanganyikiwa fulani hivi halafu wanamuweka benchi anaoza taratibu ili ikifika dirisha dogo wakimtema kusiwe na kelele.
 
Doumbia kasajiliwa na Mo ni lazima acheze, shida sio bench la ufundi bali maagizo ya Tajiri. Mhindi wetu hataki aonekane amesajili ghalasa la mpira.
Hii naweza kuamini maana sio kwa kulazimisha kule acheze kila mechi ili kiwango kipande. Na Mungu si Juma Nature huyo Doumbya mechi 10+ jamaa bado kituko. Mwenzanke Mgunda assist moja na pre assist 1 kwenye mechi moja . Kwa mtindo huu hata ile ya Loemba kuwa kaletwa na Jayrutty kwa hiyo asicheze ni kama kuna kaukweli fulani hivi. Maana kwanza wamefrustrate Loemba naye kaingia kwenye mfumo maana sasa hivi kama kachanganyikiwa fulani hivi halafu wanamuweka benchi anaoza taratibu ili ikifika dirisha dogo wakimtema kusiwe na kelele.
Ni kweli, pale Simba mchezaji asipoletwa na pesa ya Mo, huyo mchezaji hana nafasi kwenye kikosi.
Ile timu kiuongozi haina umoja ni makundi kama ilivyo kwa vyama vya siasa. Viongozi wote pale ni wapiga debe kwa wachezaji wanaoletwa na upande wa wadhamini.
Fuatilia tu utagundua namna Mo alivyo na mhimili uliojichimbia chini
 
Back
Top Bottom