Kumradhi wakuu!

Maxence Melo

JF Founder
Feb 10, 2006
4,230
13,415
Wakuu, kilichotakiwa kufanyika kilifanyika kwa ufanisi (kuimarisha usalama wa data) lakini tulichokumbana nacho njiani kimepelekea maumivu makubwa!

Database yetu ni kubwa kuliko tulivyotarajia, - 30GB hivyo kufanya backup ikabakia salama ilikuwa ni bahati nasibu. Baada ya kufanya marekebisho muhimu na kutaka kuirejesha JF hewani mnamo saa 9 za usiku (kwa muda wa Tanzania) database ilionekana iko corrupted, tulijaribu kila namna tuwezayo kuirejesha sawa lakini ilikuwa ngumu SANA kufanyika vile.

Tumeshirikiana na wataalam wengine toka Marekani kwa malipo makubwa tu, lakini nao wakakiri kushindwa!

Tunasikitika kuwa tumepoteza hoja zote kuanzia saa 7 kamili usiku wa kuamkia tarehe 13 mpaka saa 4 kamili usiku wa tarehe 13 (takribani masaa 21) kwani tulilazimika kurejesha database ambayo ilikuwepo ikiwa safi na mijadala ya mpaka saa 7 kamili usiku wa kuamkia tarehe 13. Muda wote ninaotaja ni kwa nyakati za Tanzania.

Aidha, wote waliojisajili katika kipindi hicho TUMEWAPOTEZA na tunawaomba sana samahani kwani pamoja na jitihada zetu za kuhakikisha hakipotei kitu mambo yameenda tofauti kabisa na matarajio yetu.

Kwa niaba ya wenzangu, tunapenda kuomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa kupoteza data hizo na tunafanya jitihada kuona kama kuna ambacho kinaweza kufanikisha kurejesha data hizo ili tuziongeze kwenye database yetu.

Topic ninazoweza kukumbuka kuwa zilikuwa zimeanzishwa na zilikuwa na wasomaji wakubwa ni: Hii ndiyo Richmond ya Kikwete (aloianzisha Mwanakijiji) na ya Water Front Project iliyoanzishwa na Invisible.

Kuna nyingine zaidi lakini siwezi kukumbuka kila kitu. Naomba muda kidogo nilale (walau saa 1) nikirejea nitajibu maswali tutayoulizwa (kama yatakuwepo).

Ahsanteni,

Maxence
 
Aha poleni sana ndio majukumu hayo
Asante Shy,

Japo tumefanikiwa kufanya maintenance muhimu lakini data hizo tuna wataalam wamesema watajitahidi walau za 12hrs zipatikane, zikipatikana tutaziunganisha haraka iwezekanavyo. Wale walioanzisha mijadala flani na wanaona haipo nawaomba waianzishe tena, mods watarekebisha endapo kutakuwa na kujirudia kwa namna yoyote iwayo.

Ahsante
 
hivi nikuulize lakini si zinaweza kupatikana kwa feeds ambazo zimetumwa kwa muda huo zilipopotea ?
 
Ok Mkuu poleni kwa kazi ngumu. Naona na thread yangu ya "the dark side of the Mwalimu Nyerere" imekatikia huko huko... siioni tena.
 
hivi nikuulize lakini si zinaweza kupatikana kwa feeds ambazo zimetumwa kwa muda huo zilipopotea ?
Shy,

Uko sahihi, ukweli nimechoka kwa sasa maana sijalala takribani masaa 27 hivi, wengi mmepata feeds hizo, kama kuna wanaoweza kuzileta mtakuwa mmefanya jambo la busara sana.

Ok Mkuu poleni kwa kazi ngumu. Naona na thread yangu ya "the dark side of the Mwalimu Nyerere" imekatikia huko huko... siioni tena.
Mkuu Shapu, imeenda na maji, very sorry mkuu.
 
Asante Shy,

Japo tumefanikiwa kufanya maintenance muhimu lakini data hizo tuna wataalam wamesema watajitahidi walau za 12hrs zipatikane, zikipatikana tutaziunganisha haraka iwezekanavyo. Wale walioanzisha mijadala flani na wanaona haipo nawaomba waianzishe tena, mods watarekebisha endapo kutakuwa na kujirudia kwa namna yoyote iwayo.

Ahsante

Nimekuelewa Mkuu. Poleni sana kwa kazi kubwa.
Bora hata zile thread za MWIBA za jana za mambo ya usalama zilizokuwa zinataka kutuchafulia anga zetu nazo zimekumbwa na hii kitu. Tafadhali msizirudishe tena hapa.
 
Tuko pamoja mkuu,

pole sana, punzika usije anguka kwa uchovu ukiamaka utakuwa na akili mpya.
 
Dah Poleni sana na kazi dada Farida najua upo busy sana.
Watu wakiambiwa Mods hawalali usiku kucha ili kuliweka libeneke sawa wana bisha siku moja jaribu kuzima JF masaa 8 tu uone watu watakavyo anza kulalamika.
 
Pole sana wakulu! Vipi mlivamiwa tena?
Si kasema ni mentenensi lakini madude yamegomea njiani? Mimi huwa ninazinyonya zote kwenye disk ngumu yangu hivyo naanza kuwamegea kila kitu kama mlivyobandikiwa jana.
 
lim (x³-7x²) = ∞;612075 said:
Si kasema ni mentenensi lakini madude yamegomea njiani? Mimi huwa ninazinyonya zote kwenye disk ngumu yangu hivyo naanza kuwamegea kila kitu kama mlivyobandikiwa jana.

Na jana ulizinyonya?
 
Ndio maana nilikuwa nashangaa ni nini kimeingia hapa ndani afadhali umesema mwenyewe

Je mmejiandaaje ili next time tatizo kama hili lisitokeee?
 
Shy,

Uko sahihi, ukweli nimechoka kwa sasa maana sijalala takribani masaa 27 hivi, wengi mmepata feeds hizo, kama kuna wanaoweza kuzileta mtakuwa mmefanya jambo la busara sana.Mkuu Shapu, imeenda na maji, very sorry mkuu.

Thanks mkuu!

Kuwa makini na hii JF unahatarisha ndoa yako!
 
Dah Poleni sana na kazi dada Farida najua upo busy sana. Watu wakiambiwa Mods hawalali usiku kucha ili kuliweka libeneke sawa wana bisha siku moja jaribu kuzima JF masaa 8 tu uone watu watakavyo anza kulalamika.

Ningejua Farida yuko tight kihivyo walau ningekuwa naPM kimtindo!
 
Mkuu Max nenda kampunzike nilitaka kupita ofc pale japo nikupe Gahawa utoe uchovu. Pole mpwa pumnzika kaka
 
lim (x³-7x²) = ∞;612075 said:
Si kasema ni mentenensi lakini madude yamegomea njiani? Mimi huwa ninazinyonya zote kwenye disk ngumu yangu hivyo naanza kuwamegea kila kitu kama mlivyobandikiwa jana.

Mkuu Do the necessary! Kuna thread yangu bwana ya the dark side of mwalimu...ilikuwa inaenda vizuri ingawa upinzani ulikuwa mkubwa naomba ui-movezishe hapa tena. pse do it kama uliifyonza kwenye disk ngumu yako.
 
Na jana ulizinyonya?
Si umeona nimezishusha kwa uchache. Nilizipata kwenye feeds za JF, muda mwingi nipo site mkuu. Wahandisi kuwa online ni nadra kamanda wangu.

Ndio maana nilikuwa nashangaa ni nini kimeingia hapa ndani afadhali umesema mwenyewe

Je mmejiandaaje ili next time tatizo kama hili lisitokeee?
Mambo ya teknolojia ni ∞ maana anytime anything can happen na unaweza kukosa hata kujinasua. Waulize Demonoid.com website kubwa kabisa, wao walipoteza database ya kila kitu hata majina ya waliojisajili na pwd zao. Kurudisha hata hivi jamaa nimewakubali ni wakali.

Karibu katika ulimwengu wa Maths :)
 
Back
Top Bottom