Huyu bwana anajisahau anafikiri yeye anaweza kuwaburuza hao wanyakyusa wa Kyela kama anavyotaka yeye; asisahau kuwa kuwa kabla yake kulikuwepo wakina Kasyupa ambao sasa wamechuja na yeye anaweza kuchuja vile vile na Kyela ikapata mbunge mwingine!!
JK alikuwepo mwenyewe Kyela na muda wote kushangiliwa. Iweje sasa eti wananchi wamechukia yeye kupigiwa kampeni?
Msaidieni mbunge wenu na wilaya yenu kusonga mbele na sio porojo kila siku. JK atashinda kwa kura nyingi Kyela.
JK atashinda kwa kura nyingi Kyela.
JK alikuwepo mwenyewe Kyela na muda wote kushangiliwa. Iweje sasa eti wananchi wamechukia yeye kupigiwa kampeni?
Msaidieni mbunge wenu na wilaya yenu kusonga mbele na sio porojo kila siku. JK atashinda kwa kura nyingi Kyela.
Mwakyembe anatetea kiti cha ubunge kwa tiketi ya CCM hivyo kumsifia bosi wake sio tatizo.Tanzania tunachagua wabunge kupitia vyama vya siasa sio mgombea binafsi,sasa mlitaka afanye je amsifu Dr Slaa?
Mwakyembe anatetea kiti cha ubunge kwa tiketi ya CCM hivyo kumsifia bosi wake sio tatizo.Tanzania tunachagua wabunge kupitia vyama vya siasa sio mgombea binafsi,sasa mlitaka afanye je amsifu Dr Slaa?
.Hotuba ya Dr, mwakyembe leo iliambatana na mbwembwe, matusi na dharau za kila aina, Lakini matusi yalizidi pale alipotaka wananchi wamchague kikwete na wananchi kupinga wazi wazi. Alianza kumpigia debe Kikwete kwa kuwaeleza watu kuwa kikwete anampango wa muda mrefu wa kuleta maendeleo kyela, wananchi walipinga wazi wazi na akawaambia kuwa yeye alidhani anaongea na watu wenye akili, hakutegemea watu kupiga kelele za kupinga. Akuishia hapo akasema kama kuna mwanaume apite mbele ya mkutano na kisha wampigie simu Dr Slaa kwa pamoja halafu waone simu ya nani nitapokelewa. Hivyo yeye anamfahamu Dr Slaa na kusema hawezi kuwa na maendeleo kwa Kyela. Dr mwakyembe leo haliishiwa hoja kabisa.
Mkutano wake ulianza vizuri kwa kuleta stori za kupitisha jina lake ndani ya chama, na alimaliza huku akiacha watu wamechukia na wengine kuondoka pale alipomtetea kikwete na kutaka watu wamchague; upinzani alioupata ni somo kwake kuwa huyu mtu abebeki. Watu wamemshauri ni bora ajipie kampeni yeye na mengine amwachie Kikwete mwenyewe.
hapana kule ni kata ya kanga wilaya ya chunyaHivi jamani huko Kyela sio kule JK alikopondwa mawe miaka kadhaa iliyopita?
Siasa za MBEYA naona hazitabiliki, mie nathani wanasiasa waangalie lugha wanazotumia............
.Hizo ni siasa za Mbeya na kwa kadiri kampeni zinavyoendelea ndivyo ambavyo mambo yanazidi kuwa complicated. Kuna vitu ambavyo Mwakyembe anatakiwa kuvi-avoid katika kampeni zake kwa kuwa zinaweza kumgharimu sana asipokuwa makini.
Kwanza, mama wa mipasho alipoenda Kyela hakupata mapokezi mazuri na aliondoka bila mafanikio kwa kuwa siasa za makundi bado zinaendelea hata baada ya kura za maoni.
Pili, JK alipoenda Kyela, ni Dr. Mwakyembe aliyewaomba wananchi na hasa wazee wasimwangushe na hivyo wajitokeze kwa wingi kwenye mikutano ya kampeni zake and it was successful [haya yako documented hapa JF].
Tatu, kuna makosa ambayo wameyafanya ya kumpa uchifu JK pale uwanja wa Sokoine. Nadhani hilo halikuwagusa watu wa Kyela maana mambo ya Mbeya mjini hayawahusu. Tatizo ni huu uchifu wa juzi ambao alisimikwa Riz1. Kwa kiasi kikubwa, hata kama ni ceremonial bado kwa mtu anayeamini mila zake na conservative kama ndugu zangu wanyaki wa Kyela, hilo haliwezi kupita kimya kimya.
As if hayo yote hayatoshi, ugomvi wa Mwakyembe vs Mwakipesile bado uko pale pale, haujaisha. Wote ambao wako pro-Mwakyembe wanataka Mwakipesile aondoke asiwe RC wa Mby, apelekwe mikoa mingine. The only person ambaye anaweza kumtoa ni JK. Ilishaandikwa kwenye magazeti kwamba wakulu hao wawili [Mwakyembe na Mwakipesile] walishashitakiana huko juu kwamba RC anahujumu maendeleo ya wilaya ya Kyela kwa sababu ya chuki za kushindwa kura za maoni.
Mwakyembe ana haki ya kumpigia debe JK, lakini mazingira hayaruhusu. Bado tunarudi kule kule kwamba ukishakuwa ndani ya CCM lazima uwe mnafiki. Mfano, wale waliokuwa wanajiita makamanda wa ufisadi, siku zote walikuwa wanamuweka JK nje ya kundi la mafisadi, na kumsifia kwamba JK ana nia ya kupiga vita ufisadi, lakini ukweli ni kwamba JK mwenyewe ni fisadi na ndio mlinzi mkuu wa mafisadi wenzake. Hapo ndio akina Lowassa, RA, Chenge na wengineo walikuwa wanawashangaa hao wanaojiita makamanda kwa kumuona JK ni safi na ilihali dili zao zote za kifisadi wamepiga na JK na mgawo anashika kama kawa.
Wakati wa siasa za unafiki na za kichama umepita, wagombea Ubunge wenye nia ya kutumikia wananchi wanatakiwa kusoma alama za nyakati ili wasije wakapoteza hiyo nafasi. So, Mwakyembe anaweza kuwa na mtihani, maana wapiga kura wake wanamuona yeye ni SAFI, lakini JK si safi na kitendo cha JK kuendelea kumweka Mwakipesile kuwa RC Mby kinazidi kuharibu hali ya hewa ya Kyela.
.
Mkuu.
Mbona unakuwa kama kasuku?
Upuuzi wa kusema Mkuu wa mkoa anahujumu maendeleo ya wilaya ni ujinga. Mbona Slaa kule mbulu alizungukwa kila upande, lakini alifanikiwa kwa kuwashawishi wafadhili wa ndani na nje ya nchi kusaidia? Mbona kyela kuna watu wengi binafsi wanajitolea kutafuta wafadhili na kusaidia kwa manufaa ya wananchi wa kyela na Mbunge yeye ni kilio cha kusema anahujumiwa.
Mpesya (mbeya mjini), amezungukwa na wana mtandao, lakini hatujawahi kusikia anahujumiwa?
.Mtumishi wa Mungu,
Sijawa Kasuku, nilichoandika ni kile ambacho kimeandikwa kwenye magazeti, sijaweka neno langu hata moja kwenye hilo sakata. Naomba nikuulize, je, Mwakyembe hajawahi kulalama kwamba anahujumiwa? Je, hakukuwa na juhudi za wazee wa Mby kutaka kuwasuluhisha Mwakyembe na Mwakipesile? Kama majibu yake ni NDIYO, then mimi sio kasuku. Nenda kam-face Mwakyembe umwambie aache kulialia au kupiga kelele kwamba anahujumiwa.
By the way, kwanini JK hataki kumhamisha Mwakipesile kwenye huo mkoa? Maana siyo Mwakyembe pekee aliyepiga kelele, bali pia Prof. Mwandosya alilalamika wakati wa uchaguzi wa CCM mwaka 2007 kwamba Mwang'onda alikuwa anabebwa na RC. Bado kwenye mchakato wa kuelekea kwenye kura za maoni, Mwandosya alilalama kwamba anahujumiwa na huyo huyo RC kwa kufanya mikutano na watu kutoka jimbo la Rungwe Mashariki [hapa anaongelewa Stephen Mwakajumilo pamoja na yule mwalimu aliyekwenda kutubu kanisani kwamba ameshiriki dhambi ya majungu ya kuandaa mikakati ya ushindi wa kura za maoni] pamoja na vile vikao haramu vya kuanzisha SACCOs. Yote hayo yako kwenye kwenye magazeti, sijaongeza maneno yangu.
Ushauri wangu ni huu: Hili sakata la Mwakyembe na Mwakipesile, linampa Mwakyembe ujiko na umaarufu jimboni mwake. Kwa hiyo atakuwa analitumia kama mtaji kila uchaguzi ukifika, maana tayari ana excuse ya kuhujumiwa na Mkuu wa Mkoa. Mimi ningekuwa ni Mwakipesile, ningeomba uhamisho ili kuepuka hiyo conflict of interest. Ni sakata hilo hilo lilimpa Mwakyembe ushindi wa Tsunami kwenye kura za maoni. Maana ukishasakiziwa kwamba una-support ya Mwakipesile basi watu wote wanakuona wewe umeletwa/pandikizi au unashirikiana na RC kuzorotesha maendeleo ya wilaya, of which, claims hizo zinaweza kuwa si za kweli bali zinatumika kisiasa tu.
.
Ukasuku ni hali ya kufuatilia kilekile kilichoandikwa na kusema vilevile.
Mwakyembe,amelia miaka mitano kuwa anahujumiwa jimboni kwake,lakini ukweli ni kwamba hakuna anayemhujumu.Ameshindwa kushirikiana na wananchi wa kyela katika kuleta maendeleo kwa kisingizio cha kuhujumiwa.Na kweli amefanikiwa kupata kura za huruma.Dr Slaa amehujumiwa miaka zaidi ya kumi jimboni mwake,lakini tumeona jinsi alivyokuwa akiangaika kuwataufuta wafadhili na kuunganisha nguvu ya wanananchi pamoja.
Sasa ukisema magazeti yaliandika,magazeti yaliandika nk.ndiyo ukasuku wenyewe.
Ushauri wangu ni kwamba, umefikia wakati watu kama wewe Kail, kuacha kufuata hayo magazeti yako na kusema ukweli kuwa hakuna anayemhujumu huyu bwana.pengine ndiyo maana watu sasa wameanza ata kumuzomea.
Unaporudia yaleyale ya magazeti,ambayo yamekuwa yakiandika uongo kwa muda wa miaka mitano ndiyo, ukasuku wenyewe.
Magazeti yenyewe yaligawaganyika;kulikuwa na 1.Magazeti ccm wapiganaji na
2.Magazeti ccm mafisadi.
Sasa wewe unakuwa kasuku wa magazeti ya upande mmoja tu?