Elections 2010 Kumkapenia Kikwete kwamgarimu Mwakyembe

Mtumishi wa Mungu,

Naona LIGI ya siasa za Kyela inarudi tena, japo naona inarudi kwa watu kutumia user name/ID mpya. Sina muda na ligi hiyo.

Naomba uelewe wazi kwamba sina interest yoyote na Mwakyembe au mwana CCM yeyote anayejiita mpiganaji, na ndio maana kwenye post yangu ya awali niliwaita hao wapiganaji kwamba ni wanafiki, including Mwakyembe.

Hizo habari za kuzomea hazitokani na Mwakyembe kushindwa ku-deliver, maana kama angekuwa alishindwa ku-deliver, basi hata kwenye kura za maoni asingepata ushindi wa tsunami alioupata. Kura za huruma haziwezi kuwa zaidi ya 80%. Pia kama alishindwa ku-deliver, basi wapinzani wake kwenye kura za maoni wangetumia huo mwanya kummaliza na hivyo kuondoa dhana ya hujuma. Ajabu ni kwamba sikuona mahali wapinzani wakisema kwamba Mwakyembe ameshindwa kuwaunganisha wananchi wa Kyela na kuwapelekea maendeleo. Tuliishia kulishwa kasa na Afande Samwel ambaye alipotea mara baada kura za maoni. Sasa sijui karudi tena?

Mwisho, naomba usije ukaanza kuleta habari kama za Afande Samwel ambaye alikuwa anataka watu waamini habari zake tu na zile ambazo zilizoandikwa na magazeti yote alikuwa akisema haziko sahihi. Haiwezekani magazeti yote yakaandika habari ambazo si za kweli. Ukiona hivyo basi lazima kuna kasoro. Nimehitimisha mjadala na hutaniona nikijibu tena mabandiko yako.
Keil
I enjoyed your news analysis!!
 
Mtumishi wa Mungu,

Naona LIGI ya siasa za Kyela inarudi tena, japo naona inarudi kwa watu kutumia user name/ID mpya. Sina muda na ligi hiyo.

Naomba uelewe wazi kwamba sina interest yoyote na Mwakyembe au mwana CCM yeyote anayejiita mpiganaji, na ndio maana kwenye post yangu ya awali niliwaita hao wapiganaji kwamba ni wanafiki, including Mwakyembe.

Hizo habari za kuzomea hazitokani na Mwakyembe kushindwa ku-deliver, maana kama angekuwa alishindwa ku-deliver, basi hata kwenye kura za maoni asingepata ushindi wa tsunami alioupata. Kura za huruma haziwezi kuwa zaidi ya 80%. Pia kama alishindwa ku-deliver, basi wapinzani wake kwenye kura za maoni wangetumia huo mwanya kummaliza na hivyo kuondoa dhana ya hujuma. Ajabu ni kwamba sikuona mahali wapinzani wakisema kwamba Mwakyembe ameshindwa kuwaunganisha wananchi wa Kyela na kuwapelekea maendeleo. Tuliishia kulishwa kasa na Afande Samwel ambaye alipotea mara baada kura za maoni. Sasa sijui karudi tena?

Mwisho, naomba usije ukaanza kuleta habari kama za Afande Samwel ambaye alikuwa anataka watu waamini habari zake tu na zile ambazo zilizoandikwa na magazeti yote alikuwa akisema haziko sahihi. Haiwezekani magazeti yote yakaandika habari ambazo si za kweli. Ukiona hivyo basi lazima kuna kasoro. Nimehitimisha mjadala na hutaniona nikijibu tena mabandiko yako.
.

Upuuzi mtupu.
Unapochemka kubali na sio visingizo wa kubadili ID.
Kwann nibadili ID?.Ninakuogopa wewe?.


Binafsi sina muda wa kufanya Ligi na wewe.,mtu ambaye hakuna unalolijua kuhusu unachoaandika zaidi ya ngojera za magazeti kama ulivyosema mwenyewe.

Ilikuwa kila siasa za kyela zikiongelewa,basi swali enginneer kapotelea wapi.Sasa ni kila siasa za kyela afande samweli kapotelea wapi.Ndiyo ukasuku wenyewe huo ndugu yangu Keil.Ulikoelekeza ndiko hukohuko.Acha ukasuku.
 
Jamani nani kwa nini wanyakyusa mmempa uchifu riziwani?, dharau hiiiiii
 
Mtumishi wa God na Keil,

Mbona mnabishana na wakati huohuo mnaongea jambo lilelile?

Kuhujumiwa kwa Mwakyembe kulikuwepo ila si kwa kiasi kikubwa sana kama ambavyo nina imani Mwandosya alihujumiwa.

Mwakyembe kutumia hiyo kama SABABU pia kulikuwepo sana tu. Nina imani hata kama ni mie ningeligombea, bado angesema nimetumwa na Mwakipesile au Mafisadi.
Ila wanasema njia ya Muongo ni fupi. Kama akiingia Dr. Slaa, basi lazima ujuwe madhambi ya Mwakyembe yote yataenda nje maana atakuwa hana tena sababu ya kusema anahujumiwa. Na kwa sababu Slaa mwenyewe atasimamia ufisadi, huyu Mwakyembe atabaki Mweupe kama ganda la muwa ambalo hata Sisimizi analikimbia.
.
Sikonge,
Inawezekana Mwakyembe alikuwa anahujumiwa pengine katika chaguzi na sio kuhusu suala la maendeleo wilayani kyela kama kasuku Keil anvyotaka tumwamini.
 
JK alikuwepo mwenyewe Kyela na muda wote kushangiliwa. Iweje sasa eti wananchi wamechukia yeye kupigiwa kampeni?

Msaidieni mbunge wenu na wilaya yenu kusonga mbele na sio porojo kila siku. JK atashinda kwa kura nyingi Kyela.

Walikuwa wanafuatilia mgao wao wa T-shirt na mshiko wa book mbilimbili!!!! Hujui kuwa mambo sasa ni kula CCM kura CHADEMA!!!!
 
Wakati wa siasa za unafiki na za kichama umepita, wagombea Ubunge wenye nia ya kutumikia wananchi wanatakiwa kusoma alama za nyakati ili wasije wakapoteza hiyo nafasi. So, Mwakyembe anaweza kuwa na mtihani, maana wapiga kura wake wanamuona yeye ni SAFI, lakini JK si safi na kitendo cha JK kuendelea kumweka Mwakipesile kuwa RC Mby kinazidi kuharibu hali ya hewa ya Kyela.
kEIL

Ni kweli kabisa, wakati wa siasa za unafiki umekwisha... lakini je, wanasiasa wanaelewa hayo?? maana si chadema, kafu wala ccm, mambo ya unafiki yako palepale

Nimeshindwa kuelewa mtu na usomi wote anasimama, tena kwa mbwembwe na kuanza kuponda wenzake na kusifia wale waliompa wakati mgumu kwa miaka yote mitano... HYPOCRISY NI BALAAH

we have a long way to go
 
JK alikuwepo mwenyewe Kyela na muda wote kushangiliwa. Iweje sasa eti wananchi wamechukia yeye kupigiwa kampeni?

Msaidieni mbunge wenu na wilaya yenu kusonga mbele na sio porojo kila siku. JK atashinda kwa kura nyingi Kyela.

Kweli mkuu, ndugu zangu hawa wanashindwa kuwa strategic katika maendeleo yao kiwilaya.
Mbunge wanaye ,na kwa sasa yuko sambamba na JK. Traditionally Kyela si jimbo la vyama vingine zaidi ya CCM lakini haya majikanganyiko yanayotokea watu wanajikita zaidi katika mabishano na kupigana vijembe vya hapa na pale.
Muda huu wangeutumia kupanga mikakati ya kuomba serikalini vitega uchumi na huduma kwa wananchi wangekuwa wametumia muda huu vizuri sana.Ni vyema wana Kyela wakajifunza mbinu za kuvutia maendeleo kutoka sehemu nyingine nchini,leo hii barabara ya lami inajengwa kule Hai baada ya wananchi kuchachamaa nakuidai serikali.
Tujifunze
 
JK hakubaliki Kyela, alipokwenda kyela alikwenda na watu wake na magari, hii ndio hasara yake
 
Propaganda, to be effective, must be believed. To be believed, it must be credible. To be credible, it must be true -
 
Hotuba ya Dr, mwakyembe leo iliambatana na mbwembwe, matusi na dharau za kila aina, Lakini matusi yalizidi pale alipotaka wananchi wamchague kikwete na wananchi kupinga wazi wazi.

Alianza kumpigia debe Kikwete kwa kuwaeleza watu kuwa Kikwete anampango wa muda mrefu wa kuleta maendeleo Kyela, wananchi walipinga wazi wazi na akawaambia kuwa yeye alidhani anaongea na watu wenye akili, hakutegemea watu kupiga kelele za kupinga.

Hakuishia hapo akasema kama kuna mwanaume apite mbele ya mkutano na kisha wampigie simu Dr Slaa kwa pamoja halafu waone simu ya nani nitapokelewa. Hivyo yeye anamfahamu Dr Slaa na kusema hawezi kuwa na maendeleo kwa Kyela. Dr. Mwakyembe leo haliishiwa hoja kabisa.

Mkutano wake ulianza vizuri kwa kuleta stori za kupitisha jina lake ndani ya chama, na alimaliza huku akiacha watu wamechukia na wengine kuondoka pale alipomtetea kikwete na kutaka watu wamchague; upinzani alioupata ni somo kwake kuwa huyu mtu abebeki.

Watu wamemshauri ni bora ajipie kampeni yeye na mengine amwachie Kikwete mwenyewe.


Propaganda, to be effective, must be believed. To be believed, it must be credible. To be credible, it must be true
 
Huleee happy at last,Mbeya ina wapiganaji wengi,hawaogopi mageuzi.Sipati picha siku Slaa akiibuka huko.Nadhani atachafua hali ya hewa.
 
JK alikuwepo mwenyewe Kyela na muda wote kushangiliwa. Iweje sasa eti wananchi wamechukia yeye kupigiwa kampeni?

Msaidieni mbunge wenu na wilaya yenu kusonga mbele na sio porojo kila siku. JK atashinda kwa kura nyingi Kyela.
siku ya kikwete watu walisombwa na malori na kulipwa....akishaondoka watu hawapigi kelele bure bana.......hata hao wanalipwa wapige mayowe hawatapigia kura CHICHIEMU mwaka huu......
 
.
Sikonge,
Inawezekana Mwakyembe alikuwa anahujumiwa pengine katika chaguzi na sio kuhusu suala la maendeleo wilayani kyela kama kasuku Keil anvyotaka tumwamini.

HAKIKA WEWE NI AFANDE SAMWEL!
By the way, kuna watu wamenipigia simu kwamba wanampigia mgombea wa CHADEMA ubunge ili kumkomoa
Mwakyembe, japo hawaijui CHADEMA! Na hao ndiyo type hii ya akina Afande Samwel aka Mtumishi wa God......
 
JK alikuwepo mwenyewe Kyela na muda wote kushangiliwa. Iweje sasa eti wananchi wamechukia yeye kupigiwa kampeni?

Msaidieni mbunge wenu na wilaya yenu kusonga mbele na sio porojo kila siku. JK atashinda kwa kura nyingi Kyela.

JK hapendwi Kyela kwa sababu ya kwalazimisha kutawaliwa na Mwakipesile ambaye alishindwa kura za maoni na Mwakyembe 2005. Mwaka 2005 JK alipata kura nyingi sana za wanaKyela. Hata mwakyembe anajua kuwa JK hapendwi tena. Kumkampenia ilikuwa kutimiza formality tu. Mara baada ya kutangazwa matokeo ya kura za maoni 2010 ambapo mwakyembe alishinda kwa kishindo, wanaKyela waliandamana wakiimba: "Mbunge wetu, Dr Mwakyembe! Rais wetu, Dr Slaa!!"
 
Hivi jamani huko Kyela sio kule JK alikopondwa mawe miaka kadhaa iliyopita?

TIME WILL TELL. IN FACT IT IS UNCOVERING THE PAST ALREADY! Keepit up... for everything is due to be upside down soon! Mungu Baba usikae mbali,filimbi sasa hivi inapulizwa!
 
jk alikuwepo mwenyewe kyela na muda wote kushangiliwa. Iweje sasa eti wananchi wamechukia yeye kupigiwa kampeni?

Msaidieni mbunge wenu na wilaya yenu kusonga mbele na sio porojo kila siku. Jk atashinda kwa kura nyingi kyela.

waliokuwa wakimshangilia jk huko kyela na kwingineko husombwa na malori na mbasi usiku kucha, juzi juzi jeshi mojawapo limeandikisha vijana zaidi ya 10000 kwa ajili ya kazi maalum za kumshangilia kikwete. Kuzomewa kwa mbunge kama huyo baada ya kikwete kuondoka ni uthbitisho kuwa watu wamemchoka na amuchuja.

you can cheat sometimes and not always!!!!!!!
 
Back
Top Bottom