Interested Observer
JF-Expert Member
- Mar 27, 2006
- 2,657
- 3,035
KeilMtumishi wa Mungu,
Naona LIGI ya siasa za Kyela inarudi tena, japo naona inarudi kwa watu kutumia user name/ID mpya. Sina muda na ligi hiyo.
Naomba uelewe wazi kwamba sina interest yoyote na Mwakyembe au mwana CCM yeyote anayejiita mpiganaji, na ndio maana kwenye post yangu ya awali niliwaita hao wapiganaji kwamba ni wanafiki, including Mwakyembe.
Hizo habari za kuzomea hazitokani na Mwakyembe kushindwa ku-deliver, maana kama angekuwa alishindwa ku-deliver, basi hata kwenye kura za maoni asingepata ushindi wa tsunami alioupata. Kura za huruma haziwezi kuwa zaidi ya 80%. Pia kama alishindwa ku-deliver, basi wapinzani wake kwenye kura za maoni wangetumia huo mwanya kummaliza na hivyo kuondoa dhana ya hujuma. Ajabu ni kwamba sikuona mahali wapinzani wakisema kwamba Mwakyembe ameshindwa kuwaunganisha wananchi wa Kyela na kuwapelekea maendeleo. Tuliishia kulishwa kasa na Afande Samwel ambaye alipotea mara baada kura za maoni. Sasa sijui karudi tena?
Mwisho, naomba usije ukaanza kuleta habari kama za Afande Samwel ambaye alikuwa anataka watu waamini habari zake tu na zile ambazo zilizoandikwa na magazeti yote alikuwa akisema haziko sahihi. Haiwezekani magazeti yote yakaandika habari ambazo si za kweli. Ukiona hivyo basi lazima kuna kasoro. Nimehitimisha mjadala na hutaniona nikijibu tena mabandiko yako.
I enjoyed your news analysis!!