Kumekuwa na wimbi la wauza maziwa mitaani na barabarani, Je maziwa hayo ni salama?

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Oct 28, 2012
18,653
20,988
Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kuuza maziwa fresh na mtindi mitaani, Je maziwa hayo huwa ni salama kwa afya za watumiaji?

Niliwahi fanya tafiti kidogo kwa kumuuliza kijana mmoja muuzaji wa maziwa haya, aliniambia wanayanunua ubungo na hivyo wao huyauza tena mitaani kwa faida kidogo.

Je, ni maziwa ya ngombe?


IMG_20240314_143626_197.jpg
 
Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kuuza maziwa fresh na mtindi mitaani, Je maziwa hayo huwa ni salama kwa afya za watumiaji?, Niliwahi fanya tafiti kidogo kwa kumuuliza kijana mmoja muuzaji wa maziwa haya, aliniambia wanayanunua ubungo na hivyo wao huyauza tena mitaani kwa faida kidogo, Je ni maziwa ya ngombe? View attachment 2934332
Kama Morogoro Msamvu waliweza kula mishikaki ya Iringa bila kujua tena kwa muda mrefu basi siyo ajabu watu wakanywa maziwa ya kitoweo hichohicho
 
Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kuuza maziwa fresh na mtindi mitaani, Je maziwa hayo huwa ni salama kwa afya za watumiaji?, Niliwahi fanya tafiti kidogo kwa kumuuliza kijana mmoja muuzaji wa maziwa haya, aliniambia wanayanunua ubungo na hivyo wao huyauza tena mitaani kwa faida kidogo, Je ni maziwa ya ngombe? View attachment 2934332
mbona ni sawa na maji ya kunywa na mishkaki ya town 🐒

ni kwa Neema na Baraka za Mungu inaliwa, na mtu anatembea mbele bila mbambamba yoyote tumboni 🐒
 
Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kuuza maziwa fresh na mtindi mitaani, Je maziwa hayo huwa ni salama kwa afya za watumiaji?, Niliwahi fanya tafiti kidogo kwa kumuuliza kijana mmoja muuzaji wa maziwa haya, aliniambia wanayanunua ubungo na hivyo wao huyauza tena mitaani kwa faida kidogo, Je ni maziwa ya ngombe? View attachment 2934332
Mkuu maziwa ya Punda tena?

Kuna Kijiji nilienda kufanya kazi miaka fulani

Imefika muda wa Lunch nikaenda kula mamantilie na wenyeji maana kule Kijijini hakukuwa na migahawa ya kueleweka zaidi ya Mamantilie

Nikaagiza wali nyama, mboga za majani na Pepsi baridi

Mwenyeji wangu akaniambia unakulaga nyama ya Punda? Mbona umeagiza wali nyama?

Kumbe wenyeji pale wanakula nyama ya Punda kuliko Ng'ombe/Mbuzi

Kutokea hapo nikawa nakula Samaki hadi namaliza ule mradi wa watu na kuondoka.

Tuweni waangalifu🙌
 
Hayo ni maziwa halali ya ng'ombe pamoja na mtindi.
Hao wachuuzi wanajumua kutoka viwanda vya maziwa CHAWAKIMU na Kingine TREASURE vilichopo Kiluvya madukani vinachoendeshwa na wafugaji wa Kisarawe, Kibaha, Dar es salaam na Baadhi ya Bagamoyo.
Kama kuna uchakachuaji basi waamue kuongeza maji kidogo ili kupata faida zaidi ila hiyo kwa watu wenye tamaa.

Na mteja kama amewahi kuonja maziwa hayo yakiwa hayajachakachuliwa akionja yenye uchakacjuaji atajua tu na wateja atawapoteza.
 
Hayo ni maziwa halali ya ng'ombe pamoja na mtindi.
Hao wachuuzi wanajumua kutoka viwanda vya maziwa CHAWAKIMU na Kingine TREASURE vilichopo Kiluvya madukani vinachoendeshwa na wafugaji wa Kisarawe, Kibaha,Dar es salaam na Baadhi ya Bagamoyo.
Kama kuna uchakachuaji basi waamue kuongeza maji kidogo ili kupata faida zaidi ila hiyo kwa watu wenye tamaa. Na mteja kama amewahi kuonja maziwa hayo yakiwa hayajachakachuliwa akionja yenye uchakacjuaji atajua tu na wateja atawapoteza.
NAKAZIA HAPA.
Nafanya hii shughuli, kuongeza maji ni utaahira sababu utapoteza wateja.
Shda ni hawa matajiri wanadoubt kila kitu cha mtaani.

Juz juz bhana nkanunua mchele kwenye duka kubwa wao wanajiita WAKALA WA MCHELE aisee mpaka hapa najuta ni takataka tena kwa bei ya juu..

mwisho.. JUST B'CAUSE IT IS SOLD AT A HUGE/FAMOUS STORE/SUPERMARKET DOESN'T MEAN IT IS OF THE BEST QUALITY.
 
Kumekuwa na wimbi kubwa la vijana kuuza maziwa fresh na mtindi mitaani, Je maziwa hayo huwa ni salama kwa afya za watumiaji?

Niliwahi fanya tafiti kidogo kwa kumuuliza kijana mmoja muuzaji wa maziwa haya, aliniambia wanayanunua ubungo na hivyo wao huyauza tena mitaani kwa faida kidogo.

Je, ni maziwa ya ngombe?

daah ila watani zangu wa singida hii sio poa
 
Back
Top Bottom