so far? Soo goood!!!!!
Wait to here more!
This will never happen coz the prez has immunity so far.Baada ya kusema hivyo je mahakama inaweza ikamwamuru huyu mzee Mkapa kuja kutoa ushahidi? au naye ataunganishwa katika hili sakata...hatuwezi tegemea kitu kama hiki kitokee kwa serikali yetu hii sijui...
This will never happend coz the prez has immunity so far.
Ndo hapo mi napo choka lakini alisamehe kwa lengo la kusaidia taifa?
Vp tumpeleke kwenye mahakama za kimataifa nini kama si tunaogopa kumshitaki.
Kitendo cha Mramba kusema ni maekezo toka juu, anamaanisha ni Cabinet na ndio rais na serikali nzima. Maamuzi yoyote ya cabinet yanabeba sura ya collective resiponsibilities, hata kama ni Mramba aliyapigia debe kwenye Cabinet, yakishapita na kutoka, siyo ya Mramba tena, ni ya Rais na serikali yote, huwezi kumsulubu Mramba kwa uamuzi wa Cabinet. Nasisitiza hii kesi hamna kitu..je, Mramba ana uwezo wa kuithibitishia mahakama kwamba Raisi Mkapa ndiye aliyemtuma kufanya madudu aliyoyafanya?
Pasco,
..utaratibu ni kwamba client humlipa contractor baada ya project consultant kukagua na kuhakiki kazi iliyofanyika.
..hata mimi naona ni vigumu kuwatia Liyumba na Kweka hatiani unless walikiuka maelekezo ya project consultant.
Huo Ubavu tunao?
Sasa mbona umesema kwenye kichwa cha thread kwamba kamtaja Mkapa?
Hivi mbona Watanzania tumezoea kuongopeana?
Kwani nilisema hakueleweka? Nimesema aliongopa, sio hakueleweka. Alieleweka akisema Mkapa hakutajwa, lakini alidanganya kwenye kichwa cha thread akisema Mkapa katajwa. Ukimuelewa muongo alificha nini haina maana hakuongopa, eti kwa vile ni rahisi kung'amua ukweli.
Unasema watu hawakuona tatizo, lakini hiyo ni kwa sababu wewe uko out of touch, una anasa ya kusoma habari mtandaoni. Kuna watu ambao wakiona vichwa vya habari hawana anasa ya kujaribisha kwa lengesha-na-bonyeza kuona kilichomo ndani. Inabidi wanunue gazeti kung'amua huo uongo.
Huo ndio ubaya wa uongo kama wa Halisi. Na ubaya wa watu out of touch kama wewe. Hajui au huna uchungu, huna sensitivity na hali halisi ya Mtanzania. Mfano mwingine, wasomaji jana wameibiwa hela yao na gazeti la THE CITIZEN ambalo liliandika kichwa habari "DECI Yaamrishwa Kurudisha Hela" kumbe ndani ya habari ni mapendezo ya wananchi tu, si amri ya serikali. Wamenunua gazeti kwa kulaghaiwa. JF tunakataa tabia za waandishi kama hao. Halisi aliyejijengea uaminifu na kujulikana kwa umakini, leo anaanza kupotosha habari?
Hongera: Naona umeingia JF kwa kasi mpya. Ni vizuri ukatusaidia kutuelimisha tusio na elimu kama yako. Ni vizuri pia ukatusaidia kutupasha habari za uhakika ulizo nazo kama zile za kutueleza ni nani aliyekuwa Rais wakati Mramba akiwa Waziri wa Fedha na mtu akisema hakumtaja jina lakini sote tunajua kwamba ni nani alikua Rais, Ni MKAPA. Kama uko Tanzania soma magazeti ya Mtanzania na Tanzania Daima pamoja na The Citizen utaona
TheCitizen Newspaper
Mtanzania limeandika, "Mramba amtwisha msalaba Rais Mkapa"
Tanzania Daima, "Mramba 'amlipua' Mkapa"
bahati mbaya Mtanzania na Tanzania Daima hayapo mtandaoni
Kwani nilisema hakueleweka? Nimesema aliongopa, sio hakueleweka. Alieleweka akisema Mkapa hakutajwa, lakini alidanganya kwenye kichwa cha thread akisema Mkapa katajwa. Ukimuelewa muongo alificha nini haina maana hakuongopa, eti kwa vile ni rahisi kung'amua ukweli.
Unasema watu hawakuona tatizo, lakini hiyo ni kwa sababu wewe uko out of touch, una anasa ya kusoma habari mtandaoni. Kuna watu ambao wakiona vichwa vya habari hawana anasa ya kujaribisha kwa lengesha-na-bonyeza kuona kilichomo ndani. Inabidi wanunue gazeti kung'amua huo uongo.
Huo ndio ubaya wa uongo kama wa Halisi. Na ubaya wa watu out of touch kama wewe. Hajui au huna uchungu, huna sensitivity na hali halisi ya Mtanzania. Mfano mwingine, wasomaji jana wameibiwa hela yao na gazeti la THE CITIZEN ambalo liliandika kichwa habari "DECI Yaamrishwa Kurudisha Hela" kumbe ndani ya habari ni mapendezo ya wananchi tu, si amri ya serikali. Wamenunua gazeti kwa kulaghaiwa. JF tunakataa tabia za waandishi kama hao. Halisi aliyejijengea uaminifu na kujulikana kwa umakini, leo anaanza kupotosha habari?