Kumbe mitaani hakuna Biblia Wala Quran halisi!

Kumbe mitaani hakuna Biblia Wala Quran halisi!

Tukianza na historia kabisa tuchukue nakala halisi za historia na nakala za biblia kuanza kukagua mambo, tutagundua hata huyo Yesu hajawai kuwepo maana miaka 2000 iliyopita kama mnavyoaminishana alikuwepo huyo jamaa, hutopata ushahidi wowote wa kihistoria, kijiografia, kifizikia mpaka kibiolojia hakuna huo ushahidi wa uwepo wa yesu wala taifa la israel hapo Middle East zaidi zaidi ilikuwa ardhi ya koloni la wazungu walipoishi waarabu pia na si taifa la israel na wala historia za hao manabii uchwara hazipo.

sasa turudi kwenye mada je hayo maandiko hayajawai kufanyiwa mabadiriko?, kwanini kuna nakala na matoleo mengi?, je maana ktk nakala za zamani una uhakika ndizo hizi hizi unazotumia wewe kanisani?, yaani mzungu mrumi aliyeuchezea ukristo na muanzilishi wa ukristo na kuleta hii migawanyiko utegemee akupe nakala halisi?.

Hivi wafia dini akili huwa mnaweka wapi, soma historia
Acha jazba Nina uwezo wa kuthibitisha Uwepo wa Yesu ,manabii, maandiko ya agano la kale kabla ya Yesu

Wanahistoria wengi ambao hata sio wakristo wamemuandika Yesu ,

Kuna ushahidi wa kisayansi,kimazingira, Kihistoria

Wewe inaonesha Bado una uelewa mdogo sana kwenye swala la historia

Wana historia wasiokuwa Wakristo waliomtaja Yesu kama Josephus, Myahudi wa karne ya kwanza, ambaye aliandika kuhusu Yesu na wafuasi wake, na Tacitus, Myroma, aliyeandika juu ya kifo cha Yesu chini ya Pontio Pilato. Hawa hawakuwa na sababu ya kuunda hadithi za Kikristo, hivyo inaonyesha kwamba Yesu alikuwepo kwa kweli.

Kuhusu mada ya taifa la Israeli, wakati wa Yesu eneo hilo lilikuwa linaitwa Judea na Galilaya, likiendeshwa na Warumi.

Hii inaonyesha kuwa eneo lilikuwepo, watu waliishi na kuna historia ya Wayahudi, ingawa walikosa uhuru wa kisiasa. Kudai hakuna Israeli au historia ya Wayahudi ni kutoelewa muktadha wa wakati huo.

Ni kweli kwamba kuna nakala nyingi na matoleo tofauti, lakini wanasayansi wa maandiko wanachambua tofauti hizi na kuzipima ili kutambua matoleo yaliyo karibu zaidi na maandiko ya awali. Biblia ya sasa inatokana na mfululizo wa manuskripti yenye uthibitisho wa kihistoria, na si kazi ya mtu mmoja wa mzungu kuunda dini. Ukristo ulianza na Yesu na wafuasi wake Wayahudi; baadaye maandiko yakasambazwa na Wazungu, lakini hii haimaanishi walianzisha dini.

Migawanyiko ndani ya Ukristo ni matokeo ya tafsiri tofauti na historia ya maendeleo ya kanisa, si udanganyifu wa mwanadamu mmoja.

FB_IMG_1768310153318.jpg

FB_IMG_1763708567252.jpg
FB_IMG_1769668908589.jpg
 
Huyo Mwanazuoni wako ameupimaje uhalisi wa Biblia?
Jihadhari na kudhani kuwa tunazungumzia yaliyomo ndani ya Biblia. Hapa hoja ni vile vitabu ni nakala ya vitabu halisi ambavyo inawezekana kabisa hatujui hivyo vitabu halisi vipo wapi.
 
Jihadhari na kudhani kuwa tunazungumzia yaliyomo ndani ya Biblia. Hapa hoja ni vile vitabu ni nakala ya vitabu halisi ambavyo inawezekana kabisa hatujui hivyo vitabu halisi vipo wapi.
Haya yote ungemuuliza huyo Mwanazuoni wako. Na kwa sababu unamwamini naamini utayapokea MAJIBU atakayokupa kama yalivyo!. Kwanini ujipe stress wakati Mwanazuoni wako yupo?
 
Tukianza na historia kabisa tuchukue nakala halisi za historia na nakala za biblia kuanza kukagua mambo, tutagundua hata huyo Yesu hajawai kuwepo maana miaka 2000 iliyopita kama mnavyoaminishana alikuwepo huyo jamaa, hutopata ushahidi wowote wa kihistoria, kijiografia, kifizikia mpaka kibiolojia hakuna huo ushahidi wa uwepo wa yesu wala taifa la israel hapo Middle East zaidi zaidi ilikuwa ardhi ya koloni la wazungu walipoishi waarabu pia na si taifa la israel na wala historia za hao manabii uchwara hazipo.
Ukija naomba uanze kwanza kwa kupangua Hawa wanahistoria ambao sio wakristo ni nje kabisa na biblia wanathibitisha uwepo wa Yesu ,na jiografia

Usije na story kama za waislamu,mara hao wanahistoria ni wakristo ,usilete porojo ..


historia ya nje ya Biblia inatupa ushahidi wa kihistoria.

Tacitus, mwandishi wa Kirumi, aliandika karibu mwaka 116 BK kuwa

"Christus, the founder of the name, was executed by Pontius Pilate during the reign of Tiberius."
(Annals 15.44)

Hii inathibitisha kwamba Yesu alikuwapo na aliuawa chini ya utawala wa Kirumi, kama matokeo ya rekodi huru za kihistoria.


Josephus, Myahudi wa karne ya kwanza, katika kitabu chake Antiquities of the Jews (18.63–64), anamtaja Yesu kama mtu aliyeanza mafundisho na kuwa na wafuasi wengi.

Kwa upande wa kijiografia, maeneo kama Judea, Galilaya, Betlehemu na Yerusalemu yalithibitishwa kuwepo kupitia rekodi za Kirumi na ramani za kale. Archaeology imeonyesha miji hii na miundo ya kale

Yerusalemu ya karne ya kwanza (Temple Mount, makaburi ya Wayahudi)
FB_IMG_1767333478259.jpg


Galilaya, milima na mabwawa yaliyoandikwa kama sehemu ya maisha ya Wayahudi na Yesu (Archaeological Encyclopedia of the Holy Land, Levy & Milevski, 2008).
FB_IMG_1766006053855.jpg


Kiakolojia na archaeology pia zinathibitisha uwepo wa Wayahudi na utamaduni wao,shuleni, makaburini, na miundo ya maji (aqueducts), ambazo zinahusiana na maisha ya watu wa wakati huo.
FB_IMG_1768394847761.jpg
Hii inaonyesha kuwa maeneo yaliyotajwa kwenye maandiko yalikuwa halisi, na Wayahudi waliishi pale.

Kwa hivyo, kwa msingi wa wanahistoria wa nje ya Biblia, kijiografia na archaeology,

Yesu aliwahi kuwepo, alifundisha na kuuliwa na utawala wa Kirumi, na maeneo aliyoyatembea yalikuwa halisi.

Hoja kwamba hakuna ushahidi wa kijiografia, kihistoria au kiakolojia ni potofu.

Nimetembea na vyanzo nje ya biblia na vipo vingi tu

Nakusubiri upinge hivo Vyanzo ambayo sio wakristo kabisa
 
Yaan muuza vitumbua anyofoe kurasa za Biblia au Quran na afungie vitumbua wateja wake? Labda kwa wagalatia watasema wanamwachia Yesu atashughulika na muuzaji siku ya mwisho ila wazee wa Kobazi wanafyeka kichwa mchana kweupeee..hawanaga uvumilivu wao kwao Allah anapiganiwa,yaan dini ya Allah inatakiwa ipiganiwe kwa jasho na damu.
😁😁😁😁

Nimecheka kama mazuri ,
 
Haya yote ungemuuliza huyo Mwanazuoni wako. Na kwa sababu unamwamini naamini utayapokea MAJIBU atakayokupa kama yalivyo!. Kwanini ujipe stress wakati Mwanazuoni wako yupo?
Bandiko langu limenyooka halina kipengere na walioliewa kama kina hamis77 na Infropreneur wanalitendea haki.

Hili bandiko halihusu kama yaliyoandikwa ndani ya hivyo vitabu ni sahihi ama si sahihi, bali linahusu maandishi na karatasi zilizohusika kuchapia hivyo vitabu.
 
Yesu hakukuta biblia popote, tengua kauli
Yesu kazikuta biblia agano la kale , Septuaginta imeandikwa karibu miaka 250BC kule Alexandria

Muwe mnasoma historia vijana ,sasa hivi Dunia ni Kijiji

Yesu kanukuu maandiko mengi kwenye agano la kale

Ukitaka ushahidi nakupa

Cha kwanza kafatilie kwanza BIBLIA ya kiyahudi SEPTUAGINTA LXX ambayo ipo had Leo imeandikwa lini ,Tena ipo kwa Kigiriki kile cha koine ,

Hapo sijakugusia DEAD SEA scrolls ambazo zenyewe ni za mapema zaidi

NIPO NASOMA KOZI YA BIBLE & ARCHEOLOGY sijaimaliza ,kwahiyo hapa ni uwanja wa nyumbani

FB_IMG_1767071833781.jpg
 
Biblia wahuni waliichakachua kitambo sana
biblia og ipo ithiopia

Anyway ile kubwa uki roll inatoa misokoto 4 mpaka 5
Ile ndogo 2
Nimebaki na kava tu
Thank yu!
 
sasa turudi kwenye mada je hayo maandiko hayajawai kufanyiwa mabadiriko?, kwanini kuna nakala na matoleo mengi?, je maana ktk nakala za zamani una uhakika ndizo hizi hizi unazotumia wewe kanisani?, yaani mzungu mrumi aliyeuchezea ukristo na muanzilishi wa ukristo na kuleta hii migawanyiko utegemee akupe nakala halisi?.

Hivi wafia dini akili huwa mnaweka wapi, soma historia
Nataka hii mada ya nakala halisia uje na data na ushahidi mwingi

Hizi propaganda za kuwa sijui warumi ,sijui nani kabadili biblia inakubidi uwe na ushahidi wakutosha

Biblia kama Septuaginta ambayo ni agano la kale ipo kabla hata ya Yesu ,ipo kabla hata ya Roman empire

Kabla ya Roma ya kidini ,

Hata Dead sea scrolls zimeandikwa mapema sana kama ilivyodhaniwa awali ,miaka 300 kabla ya Yesu ,

Unapokuja na hoja ya waroma sijui vatican wamebadili uwe na data zilizoshiba

Biblia ndio kitabu pekee duniani chenye Manuscript nyingi kuliko chochote kile unachokijua

Manabii walikuwa wakiandika ,wanasambaza miji yote wapate nakala

Ndio maana kila Sinagogi lilikuwa na nakala

New testament tu ambalo ni agano jipya nakala zake zipo kabla ya hao waroma wakidini

FB_IMG_1767027166494.jpg


Biblia imekuwa na nakala nyingi na matoleo tofauti, hasa kabla ya uchapaji wa kisasa. Hii ni kutokana na namna maandiko yalivyoandikwa kwa mikono, nakala zilizosambazwa kwa watu mbalimbali, na tafsiri kidogo za lugha (Kiebrania, Kikiebrania cha Kale, Kigiriki cha Kiyunani, Kilatini, nk).

Lakini wanasayansi wa maandiko (textual critics) wamefanya uchambuzi mkubwa wa manuskripti, wakiunganisha nakala zote zilizopatikana, na kuunda matoleo yaliyo karibu zaidi na maandiko ya awali.

Mfano mzuri ni Codex Sinaiticus (karibu 330–360 BK) na Codex Vaticanus (karibu 325–350 BK), ambazo ni baadhi ya manuskripti za Biblia ya Kigiriki cha Awali.

Uchambuzi wa tofauti ndogo za maneno unaonyesha kuwa mabadiliko haya hayabadili maana kuu ya maandiko, ukitaka hata mifano nitakupa .

Wanasayansi wana uhakika mkubwa kwamba matoleo tunayoyatumia sasa ni karibu sana na maandiko ya awali.,kwa asilimia 99.99%

FB_IMG_1767073359176.jpg
 
Biblia na quaran halisi vinalindwa pale kwenye maktaba Yao vatcan!

Hawawezi kuacha ukweli ukawa wazi coz ukweli huo ndio unatumika na elites kutawala wanadamu Kwa njia za kiuchumi,kisiasa,kijamii na hatari zaidi no kifikra !!

Cha kufurahisha ni kwamba hicho kidogo ambacho wamekiachia Mungu mkuu mwenye nguvu amekitumia dhidi yao na kupata challenge ya kutosha Kwa hao elites!!

"Majeshi ya ottoman yalipoipiga vatican na kuingia ,yalishangaa kuziona kopi za quran humo!

Moja kati ya sentence yenye kuogofya na kushangaza Kwa wanahistoria na wafia dini!!
 
Biblia wahuni waliichakachua kitambo sana
biblia og ipo ithiopia

Anyway ile kubwa uki roll inatoa misokoto 4 mpaka 5
Ile ndogo 2
Nimeka na kava tu
Thank yu!
Acha propaganda Mzee ,ilichakachuliwa lini na wapi ?

NIshawaambieni Dunia ni Kijiji ukitaka kusema biblia imechakachuliwa upo tayari ufanyiwe cross examination?

Hiyo biblia ya Ethiopia ipo Hadi Leo na Kuna Uzi niilezea humu,na wala Haina umri mkubwa ,ni biblia yenye MICHORO
FB_IMG_1770627214870.jpg


𝗚𝗔𝗥𝗜𝗠𝗔 𝗚𝗢𝗦𝗣𝗘𝗟𝗦 NI 𝗕𝗜𝗕𝗟𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗔𝗟𝗘 𝗬𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗠𝗜𝗖𝗛𝗢𝗥𝗢,

Ndani ya Abba Garima Monastery, kaskazini mwa Ethiopia, zinahifadhiwa Garima Gospels maandiko yanayotambulika kama Biblia ya Kikristo ya michoro ya kale zaidi duniani.
Ziliandikwa kati ya karne ya nne hadi ya saba baada ya Kristo, SASA karne ya 4-7 si juzi hapa Muhamad yupo

Zimeandikwa kwa lugha ya Ge’ez, lugha ya kale ya Ethiopia

Zinajumuisha Injili nne Mathayo, Marko, Luka na Yohana

Zina michoro hai ya matukio ya Biblia na sura za watu wa Maandiko

Hizi si hadithi, bali ni maandiko halisi yanayothibitisha uwepo wa Injili Ethiopia mapema sana katika historia ya Ukristo.

𝗧𝗢𝗙𝗔𝗨𝗧𝗜 𝗠𝗨𝗛𝗜𝗠𝗨: 𝗚𝗔𝗥𝗜𝗠𝗔 𝗚𝗢𝗦𝗣𝗘𝗟𝗦, 𝗗𝗘𝗔𝗗 𝗦𝗘𝗔 𝗦𝗖𝗥𝗢𝗟𝗟𝗦 𝗡𝗔 𝗦𝗘𝗣𝗧𝗨𝗔𝗚𝗜𝗡𝗧𝗔
Ni muhimu kutofautisha maandiko haya ili kuepuka kuchanganya historia.

Dead Sea Scrolls
• iliandikwa kati ya karne ya tatu kabla ya Kristo hadi karne ya kwanza baada ya Kristo
• Ni maandiko ya Kiyahudi (Agano la Kale)
• Hayana Injili wala habari za Yesu

Septuaginta
• Tafsiri ya Agano la Kale kutoka Kiebrania kwenda Kigiriki
• Iliandikwa takribani karne ya tatu kabla ya Kristo
• Ilitumika sana na mitume, lakini si Injili

Garima Gospels
• Ni Injili za Kikristo
• Ziliandikwa baada ya Kristo
• Ni Biblia ya michoro, si magombo ya jangwani
• Zinathibitisha kuenea kwa Injili barani Afrika mapema sana

Hivyo, Garima Gospels si mbadala wa Dead Sea Scrolls wala Septuaginta, bali ni ushahidi wa hatua inayofuata: Injili ikifika mataifa.

𝗝𝗘, 𝗚𝗔𝗥𝗜𝗠𝗔 𝗚𝗢𝗦𝗣𝗘𝗟𝗦 𝗭𝗜𝗡𝗔𝗙𝗔𝗡𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔 𝗕𝗜𝗕𝗟𝗜𝗔 𝗡𝗬𝗜𝗡𝗚𝗜𝗡𝗘?

Ndiyo.
• Vitabu ni vile vile: Injili nne
• Ujumbe ni ule ule: Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu
• Hakuna Injili mpya, wala mafundisho mapya
Tofauti iko katika:
👉 lugha
👉 mtindo
wa sanaa
👉 utamaduni wa kuhifadhi maandiko
Lakini imani ni ile ile ya mitume.


SASA NILETEE TOFAUTI YA BIBLIA YA ETHIOPIA NA HII UNAYOSEMA IMECHAKACHULIWA


NATAKA MJADALA WA KIELIMU KUHUSU NAKALA ZA BIBLIA NA QURAN ,SIO POROJO AU STORY ZA VIJIWENI ZA KUSIKIA
 
😁😁😁😁

Nimecheka kama mazuri ,
Usicheke mkuu😁😁😁😁.Kobazi hawana masihara linapofika swala la kuchezea kitabu chao mnyazi kisicho na shaka ndani yake. Allah alishaahidi kukilinda kisichezewe wala kuzihakiwa na binadamu sasa jichanganye uone. Yapo matukio watu walifyekwa shingo kwa kwa jambia walipojaribu kuikojolea au kuichoma moto Quran ya mnyazi.
 
Usahihi ni nini?

Nimekwambia mimi siamini. Sina imani ya aina yoyote ile.

Siamini kwenye kuamini.

Sihitaji kuamini, nahitaji kujua kwa uhakika, ushahidi na uthibitisho.
Kwa muktdha huo wewe sio binadamu wa kawaida kitu ambacho umeshindwa kuniconvice, binadamu Mimi na wewe hatuna tofauti Kama Mimi naamini it means na wewe unahizo feeling because your human lakin si lazima ziwe directly Kwenye the samething na ninachoamini.
That's why huamini Kwenye kuamini..

Lakini unahitaji kujua Kwa ushahidi na uthibitsho which means hivyo vitu vikipatikana na kuthibitika utavunja kanuni Yako ya kuamini kwasababu utakua umejua.

Mimi nimewahi kuota ndoto niko ikulu ya marekani naongea na Trump na tunaelewana kabisa na nikaja nikakupa muonekano wa ikulu ya marekani exactly Kama ilivyo lakini Kama wewe uliwahi kufika utakubali kwakua umewahi kufika marekani ikulu lakini Mimi nikikwambia sijawahi ata kukanyaga marekani huwezi kunielewa. Kwahio lazima uelewe Kuna level ya Elimu ambayo huna ambayo inayokufanya kuwa katka situation uliyonayo, hivyo wew kupinga Kwako ni kwasababu ya levo ya Elimu ulonayo kuhusu maarifa ya uungu.

Zamani nilipokua mdogo tulikua na tabia ya kuchezea zile cassette zenye uzi mweusi, na kipindi hicho tulikua tunabishana kuhusu watu wanaoimba music wako ndani ya zile nyuzi imagine! Ni kwasabu level yetu ya uelewa katka Hilo eneo ulikua mdogo hivyo wewe unakataa uchawi ni Elimu ambayo huna tu, lakini ikienda ujerumani Kuna chuo kikuu, naskia na Nairobi kimefunguliwa ukienda pale chuoni unaweza rudi namtazamo tofauti kabisa
 
hamis77 hii hoja kuwa Biblia na Quran halisi zimefungiwa huko Vaticani Ina ukweli kiasi gani?

Qurani ilifikajefikaje Vatican?
Ni story za VIJIWENI tu kama hiyo hapo juu ya kuwa biblia halisi ipo Ethiopia 😂

Hizi story miaka ya nyuma watu wamelishwa sana uongo ,

Kwa sasa Dunia imeendelea sana kiteknolojia

Quran imeundwa hapo Al Azhar University 1924, mchakato wake unajulikana kabisa

Nakala za Quran zilizopo ni za karne ya 8 Hadi 9, zipo Birmingham na sanaa , na ni vipande ambayo vinatofautiana na hii Quran ya Leo

Nakala za Quran ya mwisho alikuwa nayo Uthman ,cha ajabu alichoma moto zote ,aliyobaki nayo haijawahi kupatikana

FB_IMG_1769530386976.jpg


Story ya ipo Vatican na imefichwa ni propaganda tu

Vatican Library ina mamia ya manuskripti za Biblia, maandiko ya kale ya Kilatini, Kigiriki, na Kiarabu, lakini Qurani yenyewe haikuwa sehemu ya hifadhi rasmi ya Vatican .

Manuskripti chache za Qurani za kale zimetumika kwa tafsiri au ulinganisho wa kidiplomasia na Wazungu, lakini si kwamba Qurani zimefichwa Vatican.

Kihistoria karne za 17–19, baadhi ya Qurani za zilipelekwa Vatican kwa ajili ya tafiti za lugha na tafsiri, sio kufungiwa ,hii ni sawa na sasa Waislamu wanauana ,wasema ni MOSAD NA USA .,

Hii ilifanyika kupitia mawasiliano ya kidiplomasia na baadhi ya wanasayansi wa Kiislamu waliokuwa wanashirikiana na Wazungu.

Ndio maana hata Nakala ya Quran iliyopo ipo Birmingham UINGEREZA.


Anayesema Nakala za biblia zimefichwa Vatican itabidi atueleze mbona Septuaginta LXX biblia ya kiyahudi ya karne ya 3 kabla ya Yesu inafanana kwa 99.99% na hii tuliyo nayo Leo na ndio biblia mitume walikuwa wanazitumia

Na Roma ya kdini imekuja karne ya 3 baada ya Yesu ,

Itabidi atueleze inakuwaje hapo .,sio porojo za nilisikia sheikh Fulani akisema
 
UGUNDUZI MWINGINE WA NYARAKA AMBAO NI ZAIDI YA DEAD SEA SCROLLS

Magombo ya Fedha ya Ketef Hinnom

Maandishi ya Kale Zaidi ya Biblia Kuwahi Kugunduliwa
Mwaka 1979, ugunduzi wa kipekee wa akiolojia uliofanyika karibu na Yerusalemu ulitoa uthibitisho muhimu sana wa kihistoria kuhusu ukale na uaminifu wa Biblia.


Wakati wa uchimbaji wa eneo la mazishi huko Ketef Hinnom, kusini-magharibi mwa Mji wa Kale wa Yerusalemu, wanaakiolojia waligundua magombo mawili madogo ya fedha yaliyokunjwa, yaliyokuwa yamewekwa ndani ya kaburi la kipindi cha Hekalu la Kwanza.

Vitu hivi vya kale, vinavyojulikana kama Magombo ya Fedha ya Ketef Hinnom, vina maandishi ya kibiblia yaliyo ya kale zaidi kuwahi kupatikana hadi sasa.


Uchambuzi wa kitaalamu wa mwandiko wa kale (paleografia) ulionyesha kuwa magombo hayo yaliandikwa kati ya mwishoni mwa karne ya 7 na mwanzoni mwa karne ya 6 kabla ya Kristo.

Hivyo, yaliandikwa kabla ya kuharibiwa kwa Yerusalemu na Wababeli mwaka 586 KK.

Ugunduzi huu unatangulia Magombo ya Bahari ya Chumvi kwa zaidi ya karne nne, na kwa kiasi kikubwa unapingana na madai ya baadhi ya wakosoaji waliodai kuwa maandiko ya Biblia yaliandikwa katika nyakati za baadaye.

Kwa sababu ya udhaifu mkubwa wa magombo hayo, wataalamu walihitaji karibu miaka mitatu ya kazi ya makini sana ili kuyaondoa na kuyafungua bila kuyaharibu.
FB_IMG_1770634591416.jpg



Baada ya maandishi hayo kufanikiwa kusomeka, umuhimu wake ulionekana mara moja. Ndani yake kunapatikana toleo la Baraka ya Kikuhani kutoka kitabu cha

Hesabu 6:24–26, inayosema

BWANA akubariki na kukulinda…”

jambo linalothibitisha kuwa kifungu hiki kilikuwa tayari kinajulikana na kutumiwa karne nyingi kabla ya uhamisho wa Babeli.


Jambo la kuvutia zaidi ni kwamba neno la kwanza linalotambulika wazi katika magombo hayo ni YHWH, jina takatifu la agano la Mungu.

Ugunduzi huu ulikuwa wa kipekee sana kwa sababu, wakati huo, hakukuwa na maandishi mengine yaliyogunduliwa ndani ya Yerusalemu yenye jina la Mungu kutoka kipindi hicho cha mapema.

Kuwepo kwa jina YHWH katika maandishi ya matumizi binafsi ya kidini kunathibitisha si tu ukale wa ibada ya Waisraeli, bali pia nafasi ya msingi ya Mungu wa Biblia katika maisha ya kila siku ya waumini wa wakati huo, muda mrefu kabla ya mapokeo ya baadaye ya uhariri wa maandiko.


Kwa ujumla, Magombo ya Fedha ya Ketef Hinnom yanapinga kwa nguvu madai kwamba sehemu muhimu za Agano la Kale ziliandikwa au kurekebishwa kwa kiasi kikubwa wakati wa au baada ya uhamisho wa Babeli.

Badala yake, yanaonyesha wazi kwamba maandiko ya msingi ya Biblia ikiwemo lugha inayotambulika kutoka Hesabu 6 yalikuwa tayari yameandikwa, yakisambazwa, na kuheshimiwa karne nyingi kabla.

Magombo haya yanasimama kama ushahidi mzito wa akiolojia unaothibitisha kuwa Maandiko hayakuwa uvumbuzi wa kidini wa baadaye, bali yalikuwa kiini cha imani iliyohifadhiwa kwa uangalifu katika Israeli ya kale.
FB_IMG_1770634514352.jpg
FB_IMG_1770634512296.jpg
 
Ni kweli kuna ukakasi. Kuna vitabu vinaitwa "apocrypha" havipo kwenye bibilia tunazotumia, viliondolewa na kanisa katoliki.
Hivi kwanini mtu kama kitu huna elimu nacho unakitolea maelezo Tena zama hizi za uwazi, zama teknolojia

Vitabu vya apokrifa waprotestant ndio walivikataa na sababu ziliwekwa

Wakatoliki ndio wenye navyo kwenye biblia zao

Na Kuna vitabu vingi tu vya apokrifa wakatoliki hawajavijumuisha

Vitabu vya apokrifa vimeandikwa vipindi ambavyo Mungu hakutuma manabii ,mfano kutoka kitabu cha Malaki Hadi kitabu cha Mathayo Kuna gepu la miaka 500 Hadi 600

Kipindi hicho ndio vimeandikwa sana vitabu vya makabayo, bin sira ,na vingi tu vile ambavyo vinaruhusu Hadi unywaji wa pombe

Halafu Kuna vitabu vingine vya apokrifa vimeandikwa sana kwenye miaka 250AD had 500AD hivi hata wakatoliki walivikataa ,na asilimia kubwa ndio vimeunda sana Quran hii unayoiona ,

Hata ile injili ya Barnaba imeandikwa baada ya muhamad,ila kuna apokrifa za mwaka 250AD Hadi 500AD ,zimekopiwa sana na Quran na Hadith za kiislamu.

Mfano kitabu cha Henoko ni apokrifa kinabaki kama kitabu cha historia tu, au kitabu cha makabayo kina historia ya hapo kuishia nabii Malaki Hadi Mathayo hilo gepu la miaka 500 Hadi Yesu anakuja kulikuwa na upagani mwingi, historia za Antioko Epifan , utakuzikuta humo

Waprotestant hawakuviingiza kwenye canonization ya biblia kwasababu

Havikuwa kwenye Biblia ya Kiebrania (Agano la Kale la Wayahudi) kama Septuaginta hata dead sea scrolls wamekuta kitabu kimoja tu ambacho hakipo kwa biblia ya Leo, kitabu cha BOOK OF GIANTS

Wayahudi walitambua vitabu 39 tu; Apokrifa havikuwemo.
Yesu na mitume hawakuvinukuu kama Maandiko

Hakuna sehemu Yesu au mitume wakivitaja wazi kuwa ni Neno la Mungu.

Viliandikwa baada ya kipindi cha manabii

Vingi viliandikwa kati ya 400 KK – 100 BK, kipindi kilichoonekana hakikuwa na ufunuo wa kinabii.

Mafundisho yake yanakinzana na Biblia nyingine
Mfano maombi kwa wafu, wokovu kwa matendo, n.k.


Kanisa la awali halikuvikubaliana kwa kauli moja

Mababa wengi wa kanisa walivitazama kama vitabu vya kusomwa tu, si Maandiko.


Reformation ilisisitiza “Scripture alone (Sola Scriptura)”

Waprotestant walikubali vitabu vilivyokuwa na uthibitisho mpana wa kihistoria na kitume.
 
Back
Top Bottom