Kumbe kubandika stika ya BIMA kwenye kioo cha gari ni lazima, hata kama umekata BIMA yako mtandaoni

mkuu maswala ya kisheria na kimfumo yanatakiwa kuandaliwa vyema maana kama unasema wamesema wamesitisha ni vizuri, ila je sheria imefanyiwa marekebisho? je vyombo vingine vya usimamizi wa sheria vimejiandaa kivifaa kwajili ya kuangalia kama mtu anabima ama laaa? yani vyombo vyote lazima vishirikiane na lazima kuwe na mapendekezo ya ubadilishwaji wa sheria. aliyehukumu anauhalali kulingana na sheria alotumia sema inauma maana mtu anabima tayari
Unafahamu kwamba TIRA ipo kisheria? Na maamuzi yake yanatambulika kisheria? , hilo la vifaa vya kuangalia haituhusu wenye magari, ni juu yao
 
mkuu maswala ya kisheria na kimfumo yanatakiwa kuandaliwa vyema maana kama unasema wamesema wamesitisha ni vizuri, ila je sheria imefanyiwa marekebisho? je vyombo vingine vya usimamizi wa sheria vimejiandaa kivifaa kwajili ya kuangalia kama mtu anabima ama laaa? yani vyombo vyote lazima vishirikiane na lazima kuwe na mapendekezo ya ubadilishwaji wa sheria. aliyehukumu anauhalali kulingana na sheria alotumia sema inauma maana mtu anabima tayari
Unaongelea sheria au kanuni
 
sasa ukienda mahakamani mbona unapigwa kirahisii maana sheria inaelekezajeee? ka kunasheria mpya kuhusu namna ya kuweka bima iweke hapa tuone inasemaje?
Mamlaka inayohusika na bima ni TIRA, ipo kisheria, sio kwa tamko; na wametoa tangazo kwa mujibu wa sheria juu ya kutotumia sticker, unataka sheria gani tena?
 
Wana JF

Leo nlisimamishwa na traffic, akakagua kioo na kukuta sina stika ya BIMA, alivyoniuliza nikamwambia BIMA nshakataa mtandaoni, na kwenye system ya TIRA MIMS inaonyesha gari tayari nina BIMA.

Ila kilichonishangaza zaidi ni kuwa huyu jamaa aliniandikia faini, kosa langu ni KUTOKUBANDIKA STIKA YA BIMA kwa kioo cha gari. Kwa kweli hili limenishangza sana kwamba sasa tuna uwezo wa kukata bima kwa simu, na kupata bima yako instantly .! Ila sheria za traffic bado zinatubana kwamba ni lazima ubandike stika ya bima kwenye kioo. !

Sijajua ni nani mwenye jukumu la kubadilisha hii sheria ila ni moja ya sheria ya kijinga sana kuendelea kuwepo, maana kunakua hakuna maana ya vifaa vya traffic kuunganishwa moja kwa moja na mfumo wa TIRA kama bado sheria inataka nibandike stika

Waziri husika tunaomba uliangalie hili.
Hiki kitu hakipo kwa sasa, huyu trafic kakuonea, stika sahizi hazibandikwi kwenye kioo kama zamaini, na hata watoa huduma hawatoi hzo stika
 
wapo kisheria sawa ila hapo ndo tunaita mgongano wa kisheria
Hakuna mgongano, sheria inasema wazi kwamba sheria na kanuni mpya hufunika za zamani, hata kama bado haijafutwa, sheria ipo hivyo na hakuna mgongano hapo; tutajua huko huko mahakamani, huniandikii faini ya kishezi hivyo
 
Wana JF

Leo nlisimamishwa na traffic, akakagua kioo na kukuta sina stika ya BIMA, alivyoniuliza nikamwambia BIMA nshakataa mtandaoni, na kwenye system ya TIRA MIMS inaonyesha gari tayari nina BIMA.

Ila kilichonishangaza zaidi ni kuwa huyu jamaa aliniandikia faini, kosa langu ni KUTOKUBANDIKA STIKA YA BIMA kwa kioo cha gari. Kwa kweli hili limenishangza sana kwamba sasa tuna uwezo wa kukata bima kwa simu, na kupata bima yako instantly .! Ila sheria za traffic bado zinatubana kwamba ni lazima ubandike stika ya bima kwenye kioo. !

Sijajua ni nani mwenye jukumu la kubadilisha hii sheria ila ni moja ya sheria ya kijinga sana kuendelea kuwepo, maana kunakua hakuna maana ya vifaa vya traffic kuunganishwa moja kwa moja na mfumo wa TIRA kama bado sheria inataka nibandike stika

Waziri husika tunaomba uliangalie hili.
Mkuu sheria bado haijabadilishwa nadhani. Tena sheria sio inakutaka ubandike stika tu, inataka ubandike kioo cha mbele upande wa kushoto. Ukubandika pembeni hapo inategemea busara za askari. Ushauri wangu usilipe fine nenda kituoni kaonane na mkuu wa kituo au TIRA. Ukishindwa kufika piga hata simu watakupa maelekezo.
 
Mkuu askari alikagua BIMA kwa machine na kukuta gari kweli ilikua na bima
Tatizo ni kutokuibandika stika kwenye kioo, ni KOSA kisheria na lipo katika moja ya faini za magari kwenye zile machine walizonazo Traffic .!
Ungemuuliza stika ipi sasa?maana huko bima hawatoi hivyo vikaratasi vya kubandika au alitaka ubandike form ya malipo?
 
Mkuu sheria bado haijabadilishwa nadhani. Tena sheria sio inakutaka ubandike stika tu, inataka ubandike kioo cha mbele upande wa kushoto. Ukubandika pembeni hapo inategemea busara za askari. Ushauri wangu usilipe fine nenda kituoni kaonane na mkuu wa kituo au TIRA. Ukishindwa kufika piga hata simu watakupa maelekezo.
fact
 
je kunasheria mpya ya usalama barabarani?
Tofautisha sheria na kanuni zilizopo ndani ya sheria, hiyo kanuni ya sticker katika sheria ya usalama barabarani imeshafunikwa na agizo jipya toka kwa mamlaka ya kisheria inayosimamia hiyo kanuni, kwisha kazi. Mkijisikia kuiondoa ni vizuri zaidi ila ni obsolete kwa sasa, ni kama haipo tu. Na hiyo ndio sheria.
 
Hujui unachokitetea. Sheria ya bima haijabadilika ni lazima gari kukatiwa bima. Kanuni ndo huelekeza kubandika sticker kwenye kioo cha mbele cha gari upande wa kushoto. Waliotengeneza kanuni sio polisi wala bunge, kanuni zilitengenezwa na wasimamizi wa bima ambao kwa sasa ni TIRA na wameshatoa tangazo kuhusu kusitishwa kwa matumizi ya sticker za zamani na kuanza kutumika kwa e sticker kuanzia tarehe 01 april.
 
Hujui unachokitetea. Sheria ya bima haijabadilika ni lazima gari kukatiwa bima. Kanuni ndo huelekeza kubandika sticker kwenye kioo cha mbele cha gari upande wa kushoto. Waliotengeneza kanuni sio polisi wala bunge, kanuni zilitengenezwa na wasimamizi wa bima ambao kwa sasa ni TIRA na wameshatoa tangazo kuhusu kusitishwa kwa matumizi ya sticker za zamani na kuanza kutumika kwa e sticker kuanzia tarehe 01 april.
inawezekana sifahamu ila rejea kusoma sheria ya usalama barabarani
 
Nimesema askari na mtoa mada hawapo updated , sijasema kwamba sheria hiyo haipo. Kuna vitu vinakufa automatically kwa sababu ya technology, ni swala la kutumia tu common sense.

Ni kama vile vocha za kukwangua, haijakatazwa na ipo, lakini kwa wanaojielewa, hakuna sababu ya kununua vocha ilhali kuna uwezekano wa kununua muda wa maongezi na vifurushi kupitia m pesa and the likes

Kada ya Askari kwa wengi ni option ya failures, na ndio sababu tunasumbuana barabarani kwa vitu ambavyo hata havina maana.

Hapo zamani kabla ya mambo ya technology, njia pekee ya kujua uhai wa bima ilikuwa ni kupitia hiyo sticker, na ndio iliwekwa hiyo sheria, siku hizi hata wewe mwenyewe unaweza kulifanya hilo kupitia simu ya mkononi.
Wewe bado hujaelewa, hakuna Sheria inayokufa sababu ya kukua kwa technology
Ukitaka sheria ife basi ni lazima ifutwe, na hiyo Sheria bado ipo haijafutwa.
Umetoa mifano ya vitu ambavyo havihusiani, ungetolea mfano wa Sheria fulani kufa sababu ya technology
 
Back
Top Bottom