The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,535
Jana J'mosi tarehe 21/09/2019 nilikuwa nasafiri na gari yangu binafsi kutoka Shinyanga kwenda Bariadi (Simiyu) kikazi.
Kutoka Shinyanga utapita Maganzo (ulipo mgodi wa almas wa Mwadui) kisha mbele kidogo utakuta kijiji/mji mdogo wa Mwigumbi.
Hapa ni Njiapanda ya Mwanza/Bariadi.
Tuliachana na barabara kuu iendayo Mwanza na kuchepuka kulia kuelekea mashariki kaskazini ndiko iliko Bariadi makao makuu ya mkoa wa Simiyu.
Mpaka hapo Mwigumbi junction ya Mwanza/Bariadi ni umbali wa takribani 40km toka Shinyanga mjini.
Kufika hapo njiani katikati tulipita vizuizi vya polisi vitatu na kote huko kwa kuwa mimi ndiye nilikuwa dereva, sikuwa na tatizo lolote ili mradi unaendesha kwa ku - observe sheria za usalama barabarani unapoendesha gari yako.
Kutoka hapo junction Mwigumbi hadi Bariadi ni takribani 100km na ni takribani 140km ukitoka moja kwa moja Shinyanga - Bariadi.
Lakini kabla ya kufika huko utalazimika kupita mji wa Maswa (wilaya ya mkoa wa Simiyu) ambapo ni umbali wa takribani 55km toka hapo junction ya Mwigumbi.
All the way from Mwigumbi hadi Maswa hatukukutana na kizuizi cha polisi wa usalama barabarani hadi tulipokuwa tunaingia mjini Maswa.
Mwanzoni mwa mji wa Maswa, tulikutana nao hawa jamaa polisi wa usalama barabarani, wakatupiga mkono, tukasimama.
Sikuwahi kuona polisi wa ajabu kama hawa wa Maswa, yaani wanaosimamisha kila gari bila kujali umevunja sheria fulani ya usalama barabarani ama la.
Tulidhani wana ukaguzi maalumu siku hiyo, lakini baada ya uchunguzi wetu wa dakika chache, tuligundua kuwa hakuna kitu kama hicho.
Na kwa namna tulivyowaona kwa uwazi kabisa tuligundua kuwa hawa wana njaa kali na wanatafuta fedha tu hapa iwe jua ama mvua toka kwa madereva na siyo kusaidia madereva na kuchukua hatua kwa very very serious road traffic offences.
I was driving. Jamaa akasogea kwenye gari yetu akaangalia bima, akaona kuwa iko valid.
Akasogea dirishani kwa dereva, akaomba leseni na kadi ya gari, nikampa, ziko very valid.
Hakunirudishia na alibaki navyo kwa dakika kadhaa huku akiwa anaizunguka zunguka gari.
Baadaye akanirudia.Kilichofuata ni, kuniambia naomba nioneshe Fire Extinguisher na triangles.
Bahati nzuri, niko vizuri, ninavyo vyote hivyo nikamwonesha.
Akazunguka kwenye gari, baadae akanirudia tena akaja na hoja ya STIKA YA USALAMA BARABARANI.
Sio kwamba sikuwa nayo, ipo na imebandikwa mbele ya kioo sambamba na stika ya bima lakini ni ya mwaka jana 2018. hiyo ndiyo ikawa ishu na kosa langu.
Nikamwambia angalia hiyo hapo. Akasema nataka ya mwaka huu, 2019.
Nikamwambia mimi niliyonayo ni hiyo na kama mnazo hapo nipeni bandika hapo niwape hiyo 3,000 au 5,000 yenu mtuache sisi tuendelee na safari tunawahi majukumu.
Nilishangaa sana wale askari, kwani walikomaa mpaka balaa na tukajua wazi kuwa hawa watu ni njaa kali sana na wapo hapa kwa misheni ya kutafuta makosa tu hata ambayo hayapo ili mradi wapate fedha au "mpaka ueleweke tu" na uwaachie "hata ya maji tu" kwa lugha yao.
Baada ya kuzozana sana kwa muda kidogo na walipogundua huyu jamaa anaelewa mambo, baadye alikuja nadhani kiongozi wao pale.
Huyu kidogo alikuwa na busara fulani. Akatoa maelezo kuwa, Stika ya usalama barabarani inatolewa na Regional Traffic Motor Vehicle (RTO) baada ya kuwa ameikagua gari yako na kujiridhisha kuwa iko OK na ina sifa ya kuwa barabarani.
Akaendelea kuelimisha kuwa, ukifika Bariadi fika polisi, onana naye ukaguliwe na upate Stika mpya ya 2019.
Baada ya dakika kama 30 kuwepo pale, walituruhusu tukaendelea na safari, hatukulipa chochote wala kutuandikia faini nadhani ni baada ya kuzozana nao kwa hoja sana pale.
Sasa maswali yangu tunapojadili hoja hii ni haya yafuatayo na wenye ujuzi wa mambo haya mtusaidie kwa lengo la kuelimishana tu;
1. Hivi gari yako kutokuwa na Stika ya polisi ni miongoni mwa Road Traffic related offences?
2. Je, ni sahihi kweli stika hizi ziwe zinatolewa siku ya nenda kwa usalama barabarani tu ama kila dereva kwenda kumtafuta RTO eti ili akague gari yako na kukupa Stika hiyo?
3. Je, siyo vyema kuwa hawa polisi wanaosimama barabarani siku zote wakapewa mamlaka ya kugaua kila gari ambayo inakuwa haina Stika na wakajiridhisha kuwa iko OK wanatoa Stika hiyo hapohapo na mtu kulipia pesa yao badala ya jukumu hilo kuwa chini ya mtu mmoja tu aitwaye RTO?
Tulifanya shughuli yetu jana na kulala hukohuko Bariadi. Sikuwa na muda wa kwenda kuonana na RTO Bariadi eti ili anipe hiyo Stika. Nimefika nyumbani Shinyanga takribani masaa mawili yaliyopita na nilipita Maswa na safari hii hawakutusimamisha kabisa.
Kiukweli sikuupenda usumbufu huo na tulicheleweshwa kwa zaidi ya dakika 30 for no reason at all kwa sababu gari yangu iko very ok mechanically.
Naomba kuwasilisha na karibuni kwa mjadala.
Kutoka Shinyanga utapita Maganzo (ulipo mgodi wa almas wa Mwadui) kisha mbele kidogo utakuta kijiji/mji mdogo wa Mwigumbi.
Hapa ni Njiapanda ya Mwanza/Bariadi.
Tuliachana na barabara kuu iendayo Mwanza na kuchepuka kulia kuelekea mashariki kaskazini ndiko iliko Bariadi makao makuu ya mkoa wa Simiyu.
Mpaka hapo Mwigumbi junction ya Mwanza/Bariadi ni umbali wa takribani 40km toka Shinyanga mjini.
Kufika hapo njiani katikati tulipita vizuizi vya polisi vitatu na kote huko kwa kuwa mimi ndiye nilikuwa dereva, sikuwa na tatizo lolote ili mradi unaendesha kwa ku - observe sheria za usalama barabarani unapoendesha gari yako.
Kutoka hapo junction Mwigumbi hadi Bariadi ni takribani 100km na ni takribani 140km ukitoka moja kwa moja Shinyanga - Bariadi.
Lakini kabla ya kufika huko utalazimika kupita mji wa Maswa (wilaya ya mkoa wa Simiyu) ambapo ni umbali wa takribani 55km toka hapo junction ya Mwigumbi.
All the way from Mwigumbi hadi Maswa hatukukutana na kizuizi cha polisi wa usalama barabarani hadi tulipokuwa tunaingia mjini Maswa.
Mwanzoni mwa mji wa Maswa, tulikutana nao hawa jamaa polisi wa usalama barabarani, wakatupiga mkono, tukasimama.
Sikuwahi kuona polisi wa ajabu kama hawa wa Maswa, yaani wanaosimamisha kila gari bila kujali umevunja sheria fulani ya usalama barabarani ama la.
Tulidhani wana ukaguzi maalumu siku hiyo, lakini baada ya uchunguzi wetu wa dakika chache, tuligundua kuwa hakuna kitu kama hicho.
Na kwa namna tulivyowaona kwa uwazi kabisa tuligundua kuwa hawa wana njaa kali na wanatafuta fedha tu hapa iwe jua ama mvua toka kwa madereva na siyo kusaidia madereva na kuchukua hatua kwa very very serious road traffic offences.
I was driving. Jamaa akasogea kwenye gari yetu akaangalia bima, akaona kuwa iko valid.
Akasogea dirishani kwa dereva, akaomba leseni na kadi ya gari, nikampa, ziko very valid.
Hakunirudishia na alibaki navyo kwa dakika kadhaa huku akiwa anaizunguka zunguka gari.
Baadaye akanirudia.Kilichofuata ni, kuniambia naomba nioneshe Fire Extinguisher na triangles.
Bahati nzuri, niko vizuri, ninavyo vyote hivyo nikamwonesha.
Akazunguka kwenye gari, baadae akanirudia tena akaja na hoja ya STIKA YA USALAMA BARABARANI.
Sio kwamba sikuwa nayo, ipo na imebandikwa mbele ya kioo sambamba na stika ya bima lakini ni ya mwaka jana 2018. hiyo ndiyo ikawa ishu na kosa langu.
Nikamwambia angalia hiyo hapo. Akasema nataka ya mwaka huu, 2019.
Nikamwambia mimi niliyonayo ni hiyo na kama mnazo hapo nipeni bandika hapo niwape hiyo 3,000 au 5,000 yenu mtuache sisi tuendelee na safari tunawahi majukumu.
Nilishangaa sana wale askari, kwani walikomaa mpaka balaa na tukajua wazi kuwa hawa watu ni njaa kali sana na wapo hapa kwa misheni ya kutafuta makosa tu hata ambayo hayapo ili mradi wapate fedha au "mpaka ueleweke tu" na uwaachie "hata ya maji tu" kwa lugha yao.
Baada ya kuzozana sana kwa muda kidogo na walipogundua huyu jamaa anaelewa mambo, baadye alikuja nadhani kiongozi wao pale.
Huyu kidogo alikuwa na busara fulani. Akatoa maelezo kuwa, Stika ya usalama barabarani inatolewa na Regional Traffic Motor Vehicle (RTO) baada ya kuwa ameikagua gari yako na kujiridhisha kuwa iko OK na ina sifa ya kuwa barabarani.
Akaendelea kuelimisha kuwa, ukifika Bariadi fika polisi, onana naye ukaguliwe na upate Stika mpya ya 2019.
Baada ya dakika kama 30 kuwepo pale, walituruhusu tukaendelea na safari, hatukulipa chochote wala kutuandikia faini nadhani ni baada ya kuzozana nao kwa hoja sana pale.
Sasa maswali yangu tunapojadili hoja hii ni haya yafuatayo na wenye ujuzi wa mambo haya mtusaidie kwa lengo la kuelimishana tu;
1. Hivi gari yako kutokuwa na Stika ya polisi ni miongoni mwa Road Traffic related offences?
2. Je, ni sahihi kweli stika hizi ziwe zinatolewa siku ya nenda kwa usalama barabarani tu ama kila dereva kwenda kumtafuta RTO eti ili akague gari yako na kukupa Stika hiyo?
3. Je, siyo vyema kuwa hawa polisi wanaosimama barabarani siku zote wakapewa mamlaka ya kugaua kila gari ambayo inakuwa haina Stika na wakajiridhisha kuwa iko OK wanatoa Stika hiyo hapohapo na mtu kulipia pesa yao badala ya jukumu hilo kuwa chini ya mtu mmoja tu aitwaye RTO?
Tulifanya shughuli yetu jana na kulala hukohuko Bariadi. Sikuwa na muda wa kwenda kuonana na RTO Bariadi eti ili anipe hiyo Stika. Nimefika nyumbani Shinyanga takribani masaa mawili yaliyopita na nilipita Maswa na safari hii hawakutusimamisha kabisa.
Kiukweli sikuupenda usumbufu huo na tulicheleweshwa kwa zaidi ya dakika 30 for no reason at all kwa sababu gari yangu iko very ok mechanically.
Naomba kuwasilisha na karibuni kwa mjadala.