Kulikoni Diaspora Ya "Wachache" Marekani

Jabali

New Member
Sep 23, 2008
2
1
Kwa wadau wanaoishi Marekani..haswa wa Houston. Kuna tetesi kwamba Dr Tenende wa Houston na wenzake wachache wako mbioni kuandaa mkutano wa diaspora ya watanzania wanaoishi marekani. Cha kushangaza ni kwamba waandaaji hawajafanya jitihada zozote za kuwashirikisha watanzania wengine katika maandalizi ya huu mkutano. Mkutano huu unaandaliwa kinyemela.

Kwa watu wenye data za maandalizi ya huu mkutano, naomba majibu ya maswali yafuayo.

1. Mikutano kama hii huwa na lengo la kuwanufaisha watanzania wote. Kama nia ni hiyo kwa nini watanzania wengine hawajataarifiwa kupitia mitandao ya jumuiya za watanzania katika miji mbalimbali?

2. Balozi Sefue mwaka jana alikuja kwenye mkutano wa diaspora uliofanyika Houston. Baada ya mkutano wa diaspora Sefue alikutana na watanzania wengine. Akaulizwa kwanini mkutano wa diaspora 2008 ulihusisha watu wachache. Alijibu kwamba huo ulikua mkutano wa kwanza na kwamba mikutano ya mbele itahusisha wengi. Sasa tupo 2009 na mkutano huu pia unafanywa kinyemela. Kwanini? Mh. Sefue, tunaomba jibu.

3. Mkutano wa 2009 utafanyika lini?

4. Kwanini waandaaji wanakua "hand picked"? Inasemekana waandaaji wote ni marafiki.

5. Je mafanikio ya diaspora ya UK ni nini. Au tunapoteza muda tu?
 
Kwa wadau wanaoishi Marekani..haswa wa Houston. Kuna tetesi kwamba Dr Tenende wa Houston na wenzake wachache wako mbioni kuandaa mkutano wa diaspora ya watanzania wanaoishi marekani. Cha kushangaza ni kwamba waandaaji hawajafanya jitihada zozote za kuwashirikisha watanzania wengine katika maandalizi ya huu mkutano. Mkutano huu unaandaliwa kinyemela.

Kwa watu wenye data za maandalizi ya huu mkutano, naomba majibu ya maswali yafuayo.

1. Mikutano kama hii huwa na lengo la kuwanufaisha watanzania wote. Kama nia ni hiyo kwa nini watanzania wengine hawajataarifiwa kupitia mitandao ya jumuiya za watanzania katika miji mbalimbali?

2. Balozi Sefue mwaka jana alikuja kwenye mkutano wa diaspora uliofanyika Houston. Baada ya mkutano wa diaspora Sefue alikutana na watanzania wengine. Akaulizwa kwanini mkutano wa diaspora 2008 ulihusisha watu wachache. Alijibu kwamba huo ulikua mkutano wa kwanza na kwamba mikutano ya mbele itahusisha wengi. Sasa tupo 2009 na mkutano huu pia unafanywa kinyemela. Kwanini? Mh. Sefue, tunaomba jibu.

3. Mkutano wa 2009 utafanyika lini?

4. Kwanini waandaaji wanakua "hand picked"? Inasemekana waandaaji wote ni marafiki.

5. Je mafanikio ya diaspora ya UK ni nini. Au tunapoteza muda tu?

Wakati unaandaa mkutano inabidi uchague watu serious. Unaowaona longo longo unawaacha waendelee na longo longo zao.

Nawapongeza Tenende na wenzake kwa kuthubutu kufanya kitu kama hicho. Hata mbuyu ulianza kama mchicha.
 
Mapinduzi,

1. Huu si mwanzo, hii ngoma ipo mwaka wa pili. Post yako inaashiria wengine woote ambao wapo kizani sio serious.
 
Kama unaona unafaa kuwa mmoja wao, kwa nini usiombe mualiko?

Tabia kama hizi zako pengine zinawapelekea kina Tenende ukafanya mambo haya na baadhi ya watu. Hamridhiki mnaishia majungu na kulalama. Ukialikwa utasema wanajingonga kwako, usipoalikwa utasema umebaguliwa na kwamba Tenende anafanya kazi na anaowajua. Ndio acha afanye na anaowajua pengine ndio utajifunza nini maana na umuhimu wa networking.
 
Je ni lini itafanyika "diaspora" ya watanzania walioko Vijijini (kirua vunjo, isimani, ifunda etc??
 
Naomba niulize je hiki ni kile kikundi cha wale 'wabarikiwa' wachache wanaosemekana kuwa na mshiko wa nguvu pale Huston? Kama ndio basi tusiwahukumu haraka haraka bila kujua kulikoni, wako wanasema kuwa hawa mabwana walijitenga kutokana na wengine kutokuwa serious, lakini pia wako wanaosema kuwa hawa watu wanataka kufanya mambo ya uhakika hivyo wakaamua kuachana na walalahoi.
 
Je ni lini itafanyika "diaspora" ya watanzania walioko Vijijini (kirua vunjo, isimani, ifunda etc??

Nijuavyo mimi, Diaspora ni massive movement of people often associated with forced migration due to among other reasons war, slavery, to leave the motherland and live in foreignland. Sasa hii itakuwa diaspora ya watu waishio vijijini itakuwa ya kivipi maana wako makwao walikozaliwa na kukulia... kwao kabisa kwa stahili yao bila kulazimishwa na mtu au kitu!
Kwa sasa niko kijijini kwangu ..hebu unishawishi ili nione mantiki ya kikao hiki endapo kingefanyika.
 
Nijuavyo mimi, Diaspora ni massive movement of people often associated with forced migration due to among other reasons war, slavery, to leave the motherland and live in foreignland.

WoS;
Asante kwa kunijuza manake sisi huku kijijini hatutumii hili neno. Kumbe halituhusu.

Swali: Sasa hao watanzania huko uk na us wamekuwa forced na nini kukimbia nchi yao?? Kwa kuwa definition yako inasema "forced migration"! Huku tanzania kuna vita? utumwa? or what? Naomba unijuze pia!
 
'Diaspora' tunalitumia jina tuu labda atoke mdau mwangalifu atuelezee ni nini hasa na ina tofauti gani na 'meeting''gathering' 'summit' may be ndo mkanganyiko unatokea hapo
 
WoS;
Asante kwa kunijuza manake sisi huku kijijini hatutumii hili neno. Kumbe halituhusu.

Swali: Sasa hao watanzania huko uk na us wamekuwa forced na nini kukimbia nchi yao?? Kwa kuwa definition yako inasema "forced migration"! Huku tanzania kuna vita? utumwa? or what? Naomba unijuze pia!

Tz kuna UFISADI unaopelekea kufanya maisha yawe magumu kwani fursa za uchumi - ajira, biashara etc zimebanwa sana.Ugumu wa maisha unalazimisha baadhi ya wenzetu kutafuta maisha au mbadala kwinginewe! So there is forced migration bcoz of that.
 
View attachment 566354


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum, akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya kongamano la nne la kitaifa la Watanzania wanaoishi nje litakalofanyika tarehe 23 na 24 Agosti hapa Zanzibar. Hafla hiyo imefanyika Ikulu mjini Zanzibar.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum, akitoa taarifa kwa waandishi wa habari juu ya kongamano la nne la kitaifa la Watanzania wanaoishi nje litakalofanyika tarehe 23 na 24 Agosti hapa Zanzibar. Hafla hiyo imefanyika Ikulu mjini Zanzibar.

Mkurugenzi wa PPR Pascal Mayalla akiuliza suali katika mkutano na waandishi wa habari uliozungumzia Kongamano la kitaifa la Watanzania wanaoishi nje uliofanyika Ikulu mjini Zanzibar.

Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Uratibu wa Wazanzibari wanaoishi nje ya nchi Bi. Adila Hilali Vuai akijibu masuali yaliyoulizwa na wandishi wa habari kuhusu maandalizi ya kongamano la kitafa litalofanyika tarehe 23 na 24 Agosti hapa Zanzibar. (kushoto) Muandishi wa habari Rahma Suleiman wa Chuchu Fm Redio.
Picha na Makame Mshenga.
Wanabodi.

Declaration of interest. Japo mimi Paskali Mayalla sio mwana Diaspora, bali nimewahi kuishi nje kwa muda mfupi mfupi katika nchi mbalimbali, na nimewahi kufanya kazi tena sio kubeba box, bali kubeba zege ndani ya jiji la London, hivyo nina mwanga kidogo kuhusu diaspora, ila kwenye hili
Kongamano la Nne la Diaspora, litakalo fanyika Zanzibar, tarehe 23 na 24 Agosti, I have a role to play.

Hivyo hili ni bandiko la kuomba ushirikiano wenu, kwa ushiriki wako kwenye kongamano hili, physically or by proxy, ili kutoa mawazo yako Tanzania ikusaidiaje ili kukuwezesha wewe kuisaidia nchi yako.

Tanzania itajengwa na Watanzania wote wakiwemo wana diaspora. Kitu cha kwanza ni kuomba ushiriki wako physically kwa wale wenye nafasi to make it home, wajisajili kupitia
DIASPORA: Home Page
or
4TH Tanzania Diaspora Conference 2017 - Diaspora and SMEs ...

Kwa wale ambao hawatapata nafasi ya kuwepo physically, wanaweza kushiriki by proxy, kwa vile dunia sasa ni kijiji kimoja, wanaweza kushiriki by proxy.

Kwanza The Official Opening ya Kongamano lenyewe litatangazwa live za TV za Tanzania. Pili tutatangaza live kupitia video streaming kwenye youtube hivyo wana diaspora wote wenye nafasi wanaweza kufuatilia kupitia youtube, facebook, tweeter na mitandao ya kijamii.

Hapa naomba ushirikiano wako tujadiliane how to reach you out ili tupate maoni na mawazo yako, Tanzania ikusaidiaje wewe mwana Diaspora ili uweze kuisaidia nchi yako?.

Uzalendo sio kujiuliza "Tanzania Ikusaidie nini, bali ni wewe kujiuliza jee nimeisaidia nini nchi yangu Tanzania?". Kwa vile wana diaspora wengi wako nchi za nje na wamepata bahati ya kupata exposure kubwa, tunaomba mawazo yenu, Tanzania iwasaidieje ili muweze kuisaidia nchi yako Tanzania.

Natanguliza Shukrani.

Pascal Mayalla
+255 784 270403
pascomayalla@gmail.com
 
Back
Top Bottom