Kujenga umoja wa kitaifa kunatugharimu kupoteza lugha zetu za makabila yetu. Nini kifanyike?

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,224
22,304
Ninawasalimu kwa jina la chama pendwa CCM.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza ni kwamba hili jambo limenitafakarisha sana. Tukumbuke mara baada ya uhuru waasisi wa taifa walipambana sana kujenga umoja wa kitaifa kwa mbinu nyingi na juhudi kubwa.

Kiswahili kilitumika na kinaendelea kutumika taifa zima la Tanzania. Ni nadra sana kukuta nchi ya kiafrika inaongea lugha moja. Tanzania tumeweza. Kutoka Mutukula hadi Mbamba Bay lugha ni moja KISWAHILI.

Waasisi hawakuishia kwenye lugha tu. Hata kwenye elimu na ajira walimtoa wa kaskazini nakumpeleka kusini na wa mashariki kwenda magharibi ili watu wachanganyike na kuzidi kuangamiza ukabila. Hili pia limefanikiwa sana.

Nyakati za uchaguzi hapa nchini huwa watu wanapigania vyama na ni ngumu kukuta mambo ya ukabila yanazungumzwa. Ni bahati mbaya kwenye utawala uliopita ndo kidogo karibia utuletee mambo ya ukabila Mungu akaepusha.

Lakini kwa bahati mbaya zoezi la watu wa makabila tofauti kuoana limeleta changamoto ya watu wengi kutojua lugha za makabila yao. Mojawapo ya mambo muhimu kwenye kulinda utamaduni wetu ni kuwarithisha vizazi lugha zetu za asili.

Vijana wengi kwa sasa hawajui tena lugha za makabila yao. Mtu ni mchaga lakini hawezi kuongea kichaga. Au Msukuma lakini hajui Kisukuma.

Binafsi napongeza waasisi kwa huu umoja wetu ila kama taifa tufikirie namna gani tunaweza linda lugha zetu zisipotee kabisa. Kwenye kizazi cha miaka ya 2000 wapo watu wachache wanaoweza zungumza lugha za makabila yao. Nadhani sisi wa 80's ndo angalau wengi tunajua lugha za asili zetu. JE, NINI KIFANYIKE?
 
Siku za nyuma, nilitoa wazo hili hapa chini. Bahati mbaya watu wengi walitafsiri kama ni kujenga au kuleta ukabila!

 
Siku za nyuma, nilitoa wazo hili hapa chini. Bahati mbaya watu wengi walitafsiri kama ni kujenga au kuleta ukabila!
Taifa lisilokuwa na utamaduni wake sio taifa. Tukiendelea hivi tutapoteza ludha zote 120.
 
Taifa lisilokuwa na utamaduni wake sio taifa. Tukiendelea hivi tutapoteza ludha zote 120.
Kuna ukweli halafu kuna uongo katika wazo lako.Hivi,kwa mfano,Wamarekani wana makabila?Zaidi ya wale Wahindi wekundu,wengine wote lugha kuu ni kiingereza.Mbona taifa halijafa.Nakuchokoza.
 
Kuna ukweli halafu kuna uongo katika wazo lako.Hivi,kwa mfano,Wamarekani wana makabila?Zaidi ya wale Wahindi wekundu,wengine wote lugha kuu ni kiingereza.Mbona taifa halijafa.Nakuchokoza.
Wewe huna tofauti na wale wanaosema Kiswahili kitumike kufundishia hadi Chuo Kikuu huku watoto wao wakisoma International School kuanzia sekondari hadi chuo kikuu..
 
Wamarekani watabaki kuwa wamarekani. Sisi tujadili yanayotuhusu. Kumbuka wamarekani hadi kufikia walipofikia kuna njia zao walizopitia. Je tuko tayari kupita njia zao?
Tukiwa na hiyari tutakuwa tayari.Lugha zako za asili/lugha mama/lugha za kienyeji siyo kigezo cha maendeleo.Sanasana zitufundishe uchawi tulogane.Maana hatuwezi kulogana kwa manuizo ya kiingereza.
 
.

Binafsi napongeza waasisi kwa huu umoja wetu ila kama taifa tufikirie namna gani tunaweza linda lugha zetu zisipotee kabisa. Kwenye kizazi cha miaka ya 2000 wapo watu wachache wanaoweza zungumza lugha za makabila yao. Nadhani sisi wa 80's ndo angalau wengi tunajua lugha za asili zetu. JE, NINI KIFANYIKE?
Mkuu hivi kwanini tuzilinde zisipotee?

Maana kama haja ni mawasiliano tayari lugha adhimu ya kiswahili inafanya kazi hiyo.

Kuzilinda hizi lugha ndio mwanzo wa kuurudisha ukabila. Kwa sasa tunawaza kuwa wanaAfrika Mashariki tunao zungumza kiswahili na kiingereza kidogo.
 
Ninawasalimu kwa jina la chama pendwa CCM.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza ni kwamba hili jambo limenitafakarisha sana. Tukumbuke mara baada ya uhuru waasisi wa taifa walipambana sana kujenga umoja wa kitaifa kwa mbinu nyingi na juhudi kubwa.

Kiswahili kilitumika na kinaendelea kutumika taifa zima la Tanzania. Ni nadra sana kukuta nchi ya kiafrika inaongea lugha moja. Tanzania tumeweza. Kutoka Mutukula hadi Mbamba Bay lugha ni moja KISWAHILI.

Waasisi hawakuishia kwenye lugha tu. Hata kwenye elimu na ajira walimtoa wa kaskazini nakumpeleka kusini na wa mashariki kwenda magharibi ili watu wachanganyike na kuzidi kuangamiza ukabila. Hili pia limefanikiwa sana.

Nyakati za uchaguzi hapa nchini huwa watu wanapigania vyama na ni ngumu kukuta mambo ya ukabila yanazungumzwa. Ni bahati mbaya kwenye utawala uliopita ndo kidogo karibia utuletee mambo ya ukabila Mungu akaepusha.

Lakini kwa bahati mbaya zoezi la watu wa makabila tofauti kuoana limeleta changamoto ya watu wengi kutojua lugha za makabila yao. Mojawapo ya mambo muhimu kwenye kulinda utamaduni wetu ni kuwarithisha vizazi lugha zetu za asili.

Vijana wengi kwa sasa hawajui tena lugha za makabila yao. Mtu ni mchaga lakini hawezi kuongea kichaga. Au Msukuma lakini hajui Kisukuma.

Binafsi napongeza waasisi kwa huu umoja wetu ila kama taifa tufikirie namna gani tunaweza linda lugha zetu zisipotee kabisa. Kwenye kizazi cha miaka ya 2000 wapo watu wachache wanaoweza zungumza lugha za makabila yao. Nadhani sisi wa 80's ndo angalau wengi tunajua lugha za asili zetu. JE, NINI KIFANYIKE?
Utawala wa machifu urudishwe. Machifu wawe na tawala zao za ndani na serikali iwape ruzuku za kujiendesha kama ilivyo Uganda au South Africa
 
Back
Top Bottom