Kuidharau Yanga SC ikielekea CAFCC Semi ni Ushamba na Simba SC haijawahi Kucheza Fainali ya CAFCC

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,689
109,104
Kwanza tuelewane chini ya CAF hakuna Shindano la Loosers ( Walioshindwa ) bali Mashindano yote yana Umuhimu na yametenganishwa ili Kukuza zaidi Kiwango cha Soka hasa Kimashindano kwa Bara la Afrika.

Pili kama kuna mwana Simba SC Mwenzangu hapa JamiiForums anabeza Mafanikio haya ya Yanga SC na Jumapili ikifuzu Kihistoria kwa hatua ya Nusu Fainali ya CAFCC hatoishia tu kuwa Mshamba bali atakuwa ni Juha ( Fool ), Mchawi Tukuka na siyo Mwanamichezo.

Tatu na Mwisho Simba SC haijawahi Kucheza Fainali ya CAFCC ila ilicheza Fainali ya Kombe la Washindi Barani Afrika kwa Kucheza na Stella Abidjan ya Ivory Coast.

Tena niwaibieni Siri wana Simba SC Wenzangu hili tusiliendeleze sana kwani hata hilo Kombe lenyewe la Washindi lilikuwa halishirikishi Timu nyingi kama ilivyo sasa katika Kombe la Shirikisho ambalo Yanga SC inashiriki.

Ni Uwendawazimu usio na Mipaka wala Uvumilivu leo hii Kuwabeza Yanga SC wanaoshiriki Michuano yenye Timu nyingi tena wakianzia hatua za Awali ya CAFCC na Kuilinganisha na Michuano ya iliyokuwa Kombe la Washindi ambayo Timu zilikuwa chache na Ushindani wake ukiwa ni Hafifu tofauti na sasa.

Tukubali tu kuwa kwa sasa Watani zetu Yanga SC Gari imewaka Kimataifa na Kitaifa na pia hata Bahati nayo imekaa upande Wao hivyo huu Mjumuiko / Mseto wa haya Mambo yote Mawili yanaifanya Yanga SC izidi Kutakata na Inatakata kweli kweli huku ikituumbua tunayoichukia na kuiombea mabaya Kutwa.

Kama kuna mazuri Kwao tuyaige tu.

Alamsiki nyote.

Mimi ndiyo GENTAMYCINE The King!!!!!
 
Kwanza tuelewane chini ya CAF hakuna Shindano la Loosers ( Walioshindwa ) bali Mashindano yote yana Umuhimu na yametenganishwa ili Kukuza zaidi Kiwango cha Soka hasa Kimashindano kwa Bara la Afrika.

ukia na kuiombea mabaya Kutwa.

Kama kuna mazuri Kwao tuyaige tu.

Alamsiki nyote.

Mimi ndiyo GENTAMYCINE The King!!!!!
Sahihi, pamoja na ubora wa Yanga CAFCC msimu huu imejaa timu ngeni nyingi hivyo timu yenye unafuu ina nafasi kubwa ya kufika mbali.

Ni timu tano tu kati ya 16 zilizoshiriki msimu huu angalau nimewahi kushiriki mara moja au zaidi zingine zote zilikuwa ni debutants tu
 
Kombe la Shirikisho Ndio Hilo lilikuwa linaitwa la Washindi! Ambapo zamani hakukuwa na Makundi. Kwa hiyo kilichobadilika ni Jina na mfumo wa uendeshaji! Kumbuka awali aliyekuwa anashiriki ni Mshindi wa Pili, siku hizi zinashiriki hata Timu za Madara ya chini! Ndio maana Leo Kuna kina Marumo Galaxy ! + Loosers!
 
Kwanza tuelewane chini ya CAF hakuna Shindano la Loosers ( Walioshindwa ) bali Mashindano yote yana Umuhimu na yametenganishwa ili Kukuza zaidi Kiwango cha Soka hasa Kimashindano kwa Bara la Afrika.
Hapa umeongea ukweli kabisa,vivyo hivyo kama kuna mwana yanga mwenzangu ambae hakubali kuwa simba ina hadhi kubwa kwenye soka la afrika kuliko yanga huyo ni zuzu
 
Kombe la Shirikisho Ndio Hilo lilikuwa linaitwa la Washindi! Ambapo zamani hakukuwa na Makundi. Kwa hiyo kilichobadilika ni Jina na mfumo wa uendeshaji! Kumbuka awali aliyekuwa anashiriki ni Mshindi wa Pili, siku hizi zinashiriki hata Timu za Madara ya chini! Ndio maana Leo Kuna kina Marumo Galaxy ! + Loosers!
Unakubali jina limebadilika na mfumo wa uendeshaji alafu unalazimisha kuwa ni lile lile?

Shida Sana
 
Kwanza tuelewane chini ya CAF hakuna Shindano la Loosers ( Walioshindwa ) bali Mashindano yote yana Umuhimu na yametenganishwa ili Kukuza zaidi Kiwango cha Soka hasa Kimashindano kwa Bara la Afrika.
Hujawahi, nasema hujawahi tena, yaani hujawahi kuniangusha. Hizi timu 2 zimekosa kabisa Wasemaji zaidi ya kubaki na Wachambaji. Ahmed anaamini kuibeza Yanga ndo kick, Alli anaamini kuibeza Simba kunampandisha. Hawa ndo catalyst ya ujinga wa mashabiki Kwa Sasa. Alianza Manara akaungwa Sana mkono na warugaruga, lakini Aina Ile ya Usemaji haipo timu zinazojitambua. Ile ni hamasa ya kishamba siyo Usemaji.
 
Uko sahihi. The king
Afu Nina kero moja mkuu Gentamycine. Kwanini hawa mods huwa wanakupiga ban. Infact wanatukosea maana mods wanachangia kwa asilimia nyingi baadhi ya members wenye manufaa humu kulikimbia jukwaa for good.

Au yawezekana jf imeajiri mods ambao ni wana usalama wa serikali wanaofanya intentional sabotage?
With this trend of banning members jf is likely not to be the same in 10 yrs to come and all content moderators will be jobless. Probably maxence melo and the co- founder will realize this when it is too late.

Jf ilikuwa jf haswaa sio huu upuuzi wa sasa.
 
Uko sahihi. The king
Afu Nina kero moja mkuu Gentamycine. Kwanini hawa mods huwa wanakupiga ban. Infact wanatukosea maana mods wanachangia kwa asilimia nyingi baadhi ya members wenye manufaa humu kulikimbia jukwaa for good.

Au yawezekana jf imeajiri mods ambao ni wana usalama wa serikali wanaofanya intentional sabotage?
With this trend of banning members jf is likely not to be the same in 10 yrs to come and all content moderators will be jobless. Probably maxence melo and the co- founder will realize this when it is too late.

Jf ilikuwa jf haswaa sio huu upuuzi wa sasa.
Thanks for your concern Chief ila naomba nisiseme lolote bali Nimtagi Mwenyewe JamiiForums Founder Maxence Melo na baadhi ya Moderators YinYang, Paw, Active, Cookie, Moderator na JamiiForums wanaweza wakakupa Jibu sahihi au kukupa Ufafanuzi zaidi juu ya Kero yako.

Happy Union Day Mkuu.
 
Kombe la Shirikisho Ndio Hilo lilikuwa linaitwa la Washindi! Ambapo zamani hakukuwa na Makundi. Kwa hiyo kilichobadilika ni Jina na mfumo wa uendeshaji! Kumbuka awali aliyekuwa anashiriki ni Mshindi wa Pili, siku hizi zinashiriki hata Timu za Madara ya chini! Ndio maana Leo Kuna kina Marumo Galaxy ! + Loosers!
Usishau hata club bingwa zamani walikuwa hawachukui mshindi wa pili katika ligi bali ni bingwa tu wa ligi kwenye nchi husika.
 
Kombe la Shirikisho Ndio Hilo lilikuwa linaitwa la Washindi! Ambapo zamani hakukuwa na Makundi. Kwa hiyo kilichobadilika ni Jina na mfumo wa uendeshaji! Kumbuka awali aliyekuwa anashiriki ni Mshindi wa Pili, siku hizi zinashiriki hata Timu za Madara ya chini! Ndio maana Leo Kuna kina Marumo Galaxy ! + Loosers!
Kijana wa rage
 
Back
Top Bottom