Kuhusu uchaguzi nashauri kianzishwe kitengo maalumu ya ushauri nasaha kushauri wanaoshindwa

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Uchaguzi halijawahi kuwa jambo dogo Kwa wanaoshindwa duniani kote ,hata aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump aliwahi kulalamika kuchezewa faulo iliyopelekea kushindwa na Joe Biden Rais wa Sasa wa Taifa Hilo lenye demokrasia kubwa zaidi duniani.

Kutokana na mfano huo wa Trump na Marekani tunapata picha kubwa ya maumivu wanayopitia wanaoshindwa bila kujalisha aina ya kushindwa kwao. Kama Trump analalamika kuchezewa faulo katika Taifa linalofikiriwa kuwa na demokrasia kubwa dunia basi kuanzia Leo tukubaliane tu kushindwa halijawahi kuwa jambo dogo.

Wengine wanashindwa kukabiliana na hali ya kushindwa na kuamua kubeba silaha na kuingia porini, wengine wanapata mshtuko, wengine wanapata msongo mkali wa mawazo na wengine wanafikia hatua ya kujiua , haya yote ni matokeo hasi ya kushindwa.

Kwa kutambua hili ,kulingana na swali langu kwenye heading nililohoji, je uchaguzi uwe wa vipi ili usiwe na malalamiko?

Hili ni swali gumu kidogo maana majibu ya swali hili yatatolewa na walioshindwa na kutokukubali kushindwa na sio walioshindwa na kukubali kushindwa. Aliyeshindwa na kukubali kushindwa wahenga wanamtanbua kama ni mshindani wa kweli, na kwa sifa za watu wa namna hii kwao kushindwa ni changamoto na wana uwezo wa kulibadilisha changamoto hii kuwa fursa na baadaye kuwa washindani Wazuri.

Bahati mbaya watu wa namna hiyo hapo juu hawapo kwenye siasa zetu ila Kuna watu ambao hawakubaliani kushindwa, hawamjui Kuna kushindwa na kushindwa ni tatizo kubwa kwao. Watu hawa ndio msingi wa hoja yangu.

Kama nilivyosema ,matokeo ya kushindwa yanakuja na athari hasi za muda mrefu Kwa baadhi ya watu. Wasiokubali kushindwa wanahitaji ushauri nasaha kuwakinga na athari za kisaikolojia na msongo mkali wa mawazo na mawazo mengi hasi akilini mwao.

Ninashauri Serikali ianzishe kitengo maalumu Cha ushauri nasaha au huduma maalumu ya ushauri nasaha Kwa wote ambao wameathiriwa au wataathiriwa na matokeo ya kushindwa maana wanahitaji ushauri ili wasonge mbele na kuona kushindwa ni changamoto na jambo la kawaida maana katika hali ya kawaida mtu kulalamika miaka mitano naamini jambo hilo ni hatari Kwa afya ya akili.

Ahsante
 
Hakuna Political will Watawala wanataka kupora tu ili wabakie Madarakani.
 
Uchaguzi ili usiwe na malalamiko cha kwanza kusiwe kura bandia zilizo wekwa tiki kwa mgombea wa CCM na kulazimisha ziingizwe ndani ya chumba cha uchaguzi na kuwekwa kwenye sanduku la kura.
 
Ili usiwe na malalamiko wagombea wote washinde kwa kishindo jambo ambalo haliwezekani
 
Uchaguzi halijawahi kuwa jambo dogo Kwa wanaoshindwa duniani kote ,hata aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump aliwahi kulalamika kuchezewa faulo iliyopelekea kushindwa na Joe Biden Rais wa Sasa wa Taifa Hilo lenye demokrasia kubwa zaidi duniani.

Kutokana na mfano huo wa Trump na Marekani tunapata picha kubwa ya maumivu wanayopitia wanaoshindwa bila kujalisha aina ya kushindwa kwao. Kama Trump analalamika kuchezewa faulo katika Taifa linalofikiriwa kuwa na demokrasia kubwa dunia basi kuanzia Leo tukubaliane tu kushindwa halijawahi kuwa jambo dogo.

Wengine wanashindwa kukabiliana na hali ya kushindwa na kuamua kubeba silaha na kuingia porini, wengine wanapata mshtuko, wengine wanapata msongo mkali wa mawazo na wengine wanafikia hatua ya kujiua , haya yote ni matokeo hasi ya kushindwa.

Kwa kutambua hili ,kulingana na swali langu kwenye heading nililohoji, je uchaguzi uwe wa vipi ili usiwe na malalamiko?

Hili ni swali gumu kidogo maana majibu ya swali hili yatatolewa na walioshindwa na kutokukubali kushindwa na sio walioshindwa na kukubali kushindwa. Aliyeshindwa na kukubali kushindwa wahenga wanamtanbua kama ni mshindani wa kweli, na kwa sifa za watu wa namna hii kwao kushindwa ni changamoto na wana uwezo wa kulibadilisha changamoto hii kuwa fursa na baadaye kuwa washindani Wazuri.

Bahati mbaya watu wa namna hiyo hapo juu hawapo kwenye siasa zetu ila Kuna watu ambao hawakubaliani kushindwa, hawamjui Kuna kushindwa na kushindwa ni tatizo kubwa kwao. Watu hawa ndio msingi wa hoja yangu.

Kama nilivyosema ,matokeo ya kushindwa yanakuja na athari hasi za muda mrefu Kwa baadhi ya watu. Wasiokubali kushindwa wanahitaji ushauri nasaha kuwakinga na athari za kisaikolojia na msongo mkali wa mawazo na mawazo mengi hasi akilini mwao.

Ninashauri Serikali ianzishe kitengo maalumu Cha ushauri nasaha au huduma maalumu ya ushauri nasaha Kwa wote ambao wameathiriwa au wataathiriwa na matokeo ya kushindwa maana wanahitaji ushauri ili wasonge mbele na kuona kushindwa ni changamoto na jambo la kawaida maana katika hali ya kawaida mtu kulalamika miaka mitano naamini jambo hilo ni hatari Kwa afya ya akili.

Ahsante
Kwanza nakubaliana na ww ukishindwa ni jambo linalouma sana, na hii sio kwenye siasa tu bali ni kwenye Kila jambo, kuanzia mapenzi, michezo, biashahara nk. Na hali hii imepelekea malalamiko ya Kila aina.

Nitatoa mfano mdogo wa kwenye mchezo wa soka. Huko duniani wenzetu wenye akili na kupenda haki kutendeka na mshindi apatikane kwa uhalali, baada ya kuwa na malalamiko ya muda mrefu wakaamua kuwepo na technology ya VAR. Technology hii haijamaliza malalamiko kwa 100%, lakini imefanya matokeo kuwa na uhalali mkubwa kuliko kabla ya mfumo huo kuanza kutumika.

Tuje hapa kwetu hasa kwenye upande wa siasa. Wote tunajua kwa sasa kuwa ccm inakaa madarakani kwa njia zisizo halali na za halali kwa sehemu ndogo sana, na sababu hasa ni mfumo mzima wa uchaguzi na katiba yetu. Cha ajabu inatakiwa uwepo mfumo wa tume huru Ili mshindi halali apatikane, ila wanaofaidika na mfumo ulio na matatizo hawataki ipatikane VAR Ili mshindi halali apatikane! Wanashurutisha mfumo uwe huo huo, ambao mshindi anaweza kutangazwa nje ya kura halali. Vitimbwi vya wazi kabisa hufanyika kwenye chaguzi zetu, kichekesho unakuja na kebehi ya kitengo Cha kukubali kushindwa! Kinachotakiwa kwanza ni kuwa na tume huru ya uchaguzi (VAR) kisha hicho kitengo chako Cha ushauri nasaha kianze kazi, maana wateja wengi watakuwa ni Hawa wanaotangazwa washindi Sasa kwa mizengwe. Kinyume na hapo tutaendelea kuona chaguzi zilizopuuzwa na wananchi wenye uelewa.
 
Kura zote zihesabiwe kituoni na kila wakala aone na watu wote wabakie kituoni hadi hatma ya mwisho waone
Utashangaa Hawa wanaosema wanashinda kwa kishindo Sasa hawatataka iwe hivyo!
 
Mimi ninadhani kwa sasa wapinzani waandaliwe kisaikolojia kukubaliana kuwa Mama Samia atashinda kwa kishindo mwaka 2025. Pia Sugu kule Mbeya aandaliwe sana kisaikolojia endapo Spika kijana Tulia Ackson atapata nafasi ya kugombea tena kupitia CCM.
 
Ushawahi kujiuliza kwanini hilary clinton alimshinda Trump kwa kula lakin hakuwa rais wa marekani! Je ushawahi kusikia kuhusu invisible government ya marekani!

Unachopaswa kujua nikuwa demokrasia inaushetani mkubwa ndani yake, pia duniani hakuna chaguzi za haki.

Mtu anapokwenda kupiga kura akae akijiua kuwa sytem ishaamua nani awe mshindi katika uchaguzi huo na ndie atakayekua kiongozi.
 
Back
Top Bottom