Kuhusu Rais kutumia lugha ya Kiingereza

Kuhusu Rais kutumia lugha ya Kiingereza

Mbona Rais wa Vietnam hatumii English?? Why Magufuli then???

By the way watanzania takribani asilimia 90 hawajui lugha ya Queen. Hivyo kuongea lugha hiyo ni kutokuwatendea haki kwa kuwanyima habari.

Queen Esther

Mtatafuta kila kigezo kuhalalisha ungumbaru wetu wa kiingereza, lakini suala la kujifunza kiingereza fasaha halina mjadala. Na hasa kwa rais wetu.
 
Hilo swali ulipaswa ujiulize wewe pia kwa maana unajibu vipi kitu kisichokuhusu? Nimemjibu mwingine wewe unamjibia wapi na wapi?
nimekuuliza kwani kwa komenti yako,mjadala mzima unataka kumiss its intended aim!mkuu,ulicho komenti kinasaidia nini mjadala huu mzuri?
 
Siku kadhaa kulikuwepo na ubishani mkali sana humu 'ukumbini' kuhusu ufaha wa lugha ya kiingereza kwa Mheshimiwa Rais.Mimi nawamegea hii niliyokutana nayo leo LIVE kwenye mkutano wa wawekezaji wa VIETNAM na Tanzania (Business Forum) kwenye Ukumbe wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (nilihudhuria!).Ujumbe wa Vietnam uliongozwa na Rais wao Trương Tấn Sang.Kwa upande wa TZ kiongozi mkuu alikuwa ni PM na waziri wa viwanda Mhe.Mwijage.Shughuli za ufunguzi zikaanza kwa Kimombo,Mhe.Waziri wa viwanda=Kimombo,PM= Kimombo,MC=kimombo,Dr.wa IPP Ltd= Kimonbo.Sasa ikafika zamu ya H.E Rais wa Vietnam!Akaanza kuhutubia kwa Ki-Vietnam,wasaidizi wake nao lugha yao,wauliza maswali nao kivietnam isipokuwa MD wa Halotel Tz ambaye alisoma hotuba yake kwa kiingereza na haikueleweka vizuri kwa sababu hajakulia kwenye kizungu.HADITHI HII INATUFUNDISHA NINI?
inatufundisha kuwa ung'eng'e kwenye zao hauna issue Kwa viongozi
 
Sasa kama hujui lugha vizuri ya nini kuitumia?Bora kuongea lugha unayoimudu kiufasaha kuliko kujifanya mjuaji wa lugha nyingine usiyoijua.Hili ndo swala la msingi.Ogopa mtu asiejua lakini anajifanya anajua.
 
RAIS WA VIETNAM ANATUMIA LUGHA YAO NA SIO ENGLISH!!! SASA KWANINI NA SISI TUSIJIVUNIE LUGHA YETU???

Queen Esther
Sisi Tanzania bado kuna malimbukeni mengi majinga yanadhani kuongea Kingereza ni Akili hawajui kuwa kule London kuna wazungu wazaliwa wa pale hawakwenda shule lakini wanaongea hiyo lugha , huu Ulimbukeni sijui utakwisha lini!?
 
Yaani natamani tuanze humu JF mabandiko yote yawe ya lugha ya Malkia tuone Kama hawajahama jukwaa. WANAFIKI wakubwa.

Queen Esther

Sisi Tanzania bado kuna malimbukeni mengi majinga yanadhani kuongea Kingereza ni Akili hawajui kuwa kule London kuna wazungu wazaliwa wa pale hawakwenda shule lakini wanaongea hiyo lugha , huu Ulimbukeni sijui utakwisha lini!?
 
Kiukweli nampongeza Rais wetu kwa kuonyesha uzalendo wa kutumia lugha yetu ya taifa, sio kwamba hajui English, mbali na iyo kiwango chake cha elimu kinathibitisha, PhD ya Magu sio ya kupewa ni ya kusomea, so naona Yuko sawa kutumia lugha ya Kiswahili
 
Kiukweli nampongeza Rais wetu kwa kuonyesha uzalendo wa kutumia lugha yetu ya taifa, sio kwamba hajui English, mbali na iyo kiwango chake cha elimu kinathibitisha, PhD ya Magu sio ya kupewa ni ya kusomea, so naona Yuko sawa kutumia lugha ya Kiswahili
hajui kiiengereza,ndio maana ili kuficha aibu zenu,mpo umu kuimba mapambio kwa magufuli kuongea kiswahili
 
Hili suala la lugha yetu na lugha yao halina nafasi sana kwa wakati tulionao.
mwishowe tutasema dini zao na dini zetu. Afrika tulishapoteza utambulisho wetu zamani tu kupitia imani.
Je, kwa kukataa Kiingereza au kifaransa na kadhalika tunaweza pia kuyakataa majina kama John, Mathew, Ahmad ? Tulikuwa na majina yetu kama Siri, Majuto, Juakali n.k.
 
Inashangaza sana kuona Tanzania ambayo ndio chimbuko la Kiswahili na zaidi sana kuwa lugha ya saba ulimwenguni,Lugha ya pili Afrika kuzungumzwa baada ya kiarabu bado tunajadili lugha ambayo wanapaswa kutumia viongozi wetu.Ingependeza sana kama katika awamu hii ya tano ya JPM kitumike kiswahili bila kuhangaika na kiingereza kwenye hafla kama mtoa mada alivyojaribu kutuonyesha.Hii ni fursa kwa waliobobea kwenye kiswahili ili waanze ukalimani katika mikutano na hafla kama hizo.Hizi kasumba za kulazimisha kiingereza kutumika eti kwa kuwa kiingereza ndio lugha ya ulimwengu imepitwa na wakati.
Rais wa Cuba , America kusini yote , Korea zote, China, Mongolia , Italy , GERMAN , Spain , ureno , Nchi za shengeni zote , ufaransa , Pakistan , Uarabuni nk , viongozi wao popote wawapo Duniani hawazungumzi English hutumia Lugha zao ikibidi mkalimani hutafasiri kila kitu . Huu Ulimbukeni upo Tanzania tu , Nchi zingine hawana malimbukeni Kama Tanzania .
 
Tanzania lugha zote mbili kiingereza na kiswahili zinatumika kufundishia. wanafunzi upimwa pia na kupewa alama za ushindi au kushindwa.....hatutegemei ktk mazingira hayo mtu awe na PhD asiongee na kufanya mawasilisho yake ktk lugha fasaha za kiingereza na kisw.

hata ivyo nikubaliane na wengi kuwa lugha yetu ni kiswa....tuipende na tuitumie....

Rais ana nafasi ya kuboresha kiingereza chake...Kabila amefanya hivyo ktk lugha ya kifaransa....kujifunza hakuna mwisho....
 
Sio lazima kwani Rais hata Kama hajui Kingereza Nchi itaenda vizuri tu , acha Ulimbukeni angalia Mataifa yaliyoendelea Dunia marais wa huko hawajui Kingereza kabsa.
 
Siku kadhaa kulikuwepo na ubishani mkali sana humu 'ukumbini' kuhusu ufaha wa lugha ya kiingereza kwa Mheshimiwa Rais.

Mimi nawamegea hii niliyokutana nayo leo LIVE kwenye mkutano wa wawekezaji wa VIETNAM na Tanzania (Business Forum) kwenye Ukumbe wa mikutano wa Mwalimu Nyerere (nilihudhuria!).

Ujumbe wa Vietnam uliongozwa na Rais wao Trương Tấn Sang.Kwa upande wa TZ kiongozi mkuu alikuwa ni PM na waziri wa viwanda Mhe.Mwijage.Shughuli za ufunguzi zikaanza kwa Kimombo,Mhe.Waziri wa viwanda=Kimombo,PM= Kimombo,MC=kimombo,Dr.wa IPP Ltd= Kimonbo.

Sasa ikafika zamu ya H.E Rais wa Vietnam!Akaanza kuhutubia kwa Ki-Vietnam,wasaidizi wake nao lugha yao,wauliza maswali nao kivietnam isipokuwa MD wa Halotel Tz ambaye alisoma hotuba yake kwa kiingereza na haikueleweka vizuri kwa sababu hajakulia kwenye kizungu.

HADITHI HII INATUFUNDISHA NINI?
Mtanzania sijui utamweleweshaje mpaka akubali kuwa kujua kiingereza sio kuonyesha mtu ni bora na ana akili. Sijui ni madhara ya kutawaliwa au nini lakini mimi nafikiri ni kwa sababu ya elimu duni tuliyoipata kwenye shule zetu hivyo inatufanya tusijiamini. Magufuli kiingereza chake ni kizuri na kinaeleweka. Kuna marais na viongozi wa nchi nyimgine ukisikia kiingereza chao ni majanga lakini huwezi kukuta wananchi wao wanapoteza muda kuwajadili kama sisi.
 
Rais wa Cuba , America kusini yote , Korea zote, China, Mongolia , Italy , GERMAN , Spain , ureno , Nchi za shengeni zote , ufaransa , Pakistan , Uarabuni nk , viongozi wao popote wawapo Duniani hawazungumzi English hutumia Lugha zao ikibidi mkalimani hutafasiri kila kitu . Huu Ulimbukeni upo Tanzania tu , Nchi zingine hawana malimbukeni Kama Tanzania .
ndio,wanaongea aidha kifaransa,kiitaliano,kiarabu,kijerumani,kihispania au kireno!nchi nyingi ulizozitaja hapo juu hasa za Latina America zinaongea aidha kihispania,au kireno lugha za wakoloni walio watawala!mnapiga kelele humu kwa kuwa magufuli kiingereza hajui,angekuwa anajua povu lote hili lisinge watoka
 
Back
Top Bottom