Kama nilivyosema unahitaji ELIMU tena kubwa tu:
1. Hakuna kundi la kijajusi la kijajusi lenye jina LTK, hili ni neno la kisheria linalotumika kumpa mtu au maofisa wa ngazi fulani kinga wanapotekeleza operation/mission ya kinchi iwe ndani au nje ya nchi. Na kwa nchi yetu kinga hii hutolewa na Rais pekee. Sasa ni kuongopeana mtu akisema mkuu wa LTK akatoa oda ya kumuua mtu bahati mbaya mwandishi hakuonyesha kama huyo mkuu alimaanisha Rais. Hivyo nimepingana nae kwa hoja hii.
2. Mwakyembe anaweza kuwa na maadui lakini si kwa nchi yetu, definition yako ya hatari kwa mafisadi ingefaa kama ripoti ingeweka wazi kuwa waliotumika hapo ni kikundi cha kimafia na hawana affiliation na serikali....again ningehoji mafia na ujanja wao wote kamwe hawana uhusiano na Usalama wa taifa katika nchi yoyote je hawa waliowaleta KGB mafia gani? Labda hujui ngoja nikwambie hakuna ndege inaweza kuingia nchini bila jeshi kujua. Sasa kama hawa walikuja na kutua private haiingii akilini kwa kweli.
3. Hao uliowataja hawana ulinzi zaidi ya madereva wao, kama watu hao wamediriki kuwawekea sumu kwa kuwafuata maeneo husika walishindwa nini kuwa tumia majambazi au hata njia zingine kuliko hizo zilizotajwa? Wamekunywa sumu kibao bado wanadunda jamani hata sumu ya panya lazima itakufikisha hospitali vipi wenzetu wadunde tu kwa misumu ya kutisha? So fiction kwa kweli
4. Suala la Rais kuwatumia majasusi kumfanyia mtu mwingine ni la kudhania sana, upo huo uwezekano lakini si kwa hili, kwanza nahisi unahitaji elimu ya mfumo wa usalama wa taifa ila nitasamehe mi sio mahiri eneo hilo. Kifupi Rais sio mtu mmoja ni taasisi hakuna anachokifanya bila watu wengine ndani ya taasisi yake kufahamu. Na pia akiamua fulani afe wala hana haja ya kuitikisha kikao Movenpick au kuagiza sumu urusi na Bulgaria. Walipona makomandoo waliotaka kupindua nchi ndo wawe hawa.
Sitakulazimisha ufuate maoni yangu maana wapo watu wataikubali ripoti hii kwa utashi wao wa kisiasa na wengine kama sie tutaikaa kwa weledi wetu maana ripoti za aina hii ni rahisi kuona mapungufu ukiwa NEUTRAL kuliko ukilalia upande wa kushoto. kwahiyo naelewa kuwa mjadala huu unategemea sana na unaelemea upande gani, kama ule wa vidole viwili utajulikana, kama wa Nyundo na Jembe pia utajuliakana na bahati mbaya wengine tusio na upande tutawekwa huu wa Nyundo.....sitajali ila kikubwa nina asilimia MIA MOJA kuwa THIS IS NOT EVEN CLOSE TO THE TRUTH.
fiksiman unapojibu mtu soma vizuri na kuelewa halafu tumia akili.
1. Sijasema LTK ni kundi la kijasusi, Kwa mjibu wako "hili ni neno la kisheria linalotumika kumpa mtu au maofisa wa ngazi fulani kinga wanapotekeleza operation/mission ya kinchi iwe ndani au nje ya nchi", LTK ni kifupi "acronym" ya "License To Kill", kwa mujibu wa mwandishi ametumia neno LTK kama kundi lilopewa ruhusu ya kuua, na mahali pengine ametumia hilo neno akimaanisha mtu aliyepewa ruhusa ya kuua alipoandika kwa mfano LTK/DBK (huu ni mfano tu). Na mwandishi ameandika vizuri na yuko sahihi na anaeleweka licha ya maana yako ya kukariri. Nikisema unajuaje kama LTK haijapewa go-ahead na rais? Naweza kumaanisha unajuaje kama rais hajatoa ruhusu/idhini ya kuua? kwa mjibu wa maana yako ya LTK, au unajuaje kama rais hajaliruhusu hilo kundi kuua? Kwa mjibu wa mwandishi. Hata mwandishi katika maelezo yake mengine amemaanisha "license". Na narudia tena katika maelezo yako mengi umeonesha kwamba rais wako hawezi kufanya mambo fulani, sio hapa Tz labda kama unamaanisha rais wa nchi nyingine! Nina uhakika hapa Tz kwa jinsi siasa zilivyo rais anaweza kufanya jambo lolote hata kama linamshangaza mtoto wa chekechea!
2. "Mwakyembe anaweza kuwa na maadui lakini si kwa nchi yetu",
Hii kauli yako umetumia nini kuiandika? Yaani Mwakyembe hawezi kuwa na maadui Tz? Au unamaanisha nchi gani? Na wale mafisadi wa Richmond aliowaumbua sio maadui zake kweli? Yaani kama mtu wa kawaida tu ambaye sio mwanasiasa anaweza kuwa na maadui, unadai kwa Mwakyembe haiwezekani?
Unaniuliza " je hawa waliowaleta KGB mafia gani?" Katika maelezo yangu sijaongelea KGB.
3. Unawapangia wauaji njia gani watumie kuua watu! Wao ndio wanaojua ipi inafaa na kwa nini? Ni sawa na mtu ameuawa kwa kupigwa risasi halafu wewe unadai kwa nini wasingemuua kwa kumpiga rungu?
4. "Suala la Rais kuwatumia majasusi kumfanyia mtu mwingine ni la kudhania sana, upo huo uwezekano lakini si kwa hili, kwanza nahisi unahitaji elimu ya mfumo wa usalama wa taifa ila nitasamehe mi sio mahiri eneo hilo...."
Kwa nini unakuwa hauko makini kihivyo? Angalia juu kabisa kwenye habari yangu, msitari wa kwanza, nimeandika hivi "Sisemi kama ripoti ni sahihi au sio sahihi, isipokuwa:" Sikusema kama ripoti ni sahihi au sio sahihi, ila nimeonesha mambo ambayo kwa nchi yetu yanawezekana yenye uhusiano wa karibu na hii ripoti.
5. Wewe umeonesha kuwa ripoti sio sahihi, pinga basi kwa "logic", toa "concrete reasons", onyesha ushahidi inapowezekana ili kuwashawishi watu unachokiamini, kama mimi nilivyoandika kwamba ndani ya Tz kuna mambo mengi maovu yanawezekana, kwa kuwataja wahusika na baadhi ya matukio yaliyowakumba au waliyoyasababisha. Sio unaandika oh sidhani, haiwezekani, kwa nini wasingefanya hivi, najua n.k?
6. "Kama nilivyosema unahitaji ELIMU tena kubwa tu".
Elimu gani unataka kunipa? Unadhani kati ya mimi na wewe yupi anahitaji elimu?