Kuhusu Manji: Shikamoo Tanzania

Kuhusu Manji: Shikamoo Tanzania

Hata kama mtu alituhumia na alitajwa kwa tuhuma basi sio tiketi ya kumtuhumu kwa uongo lazima watu wapige kelele.

Hii inaonyesha kuwa wapinzani hawana chuki binafsi walimpinga alipokosea wanamtetea anapoonewa.
Kabisa mkuu,sisi ni watetezi wa haki.
 
Sinauhakikakamamunguanafurahiauwepowetuwatanzaniaduniani.
 
Hatutetei majambazi wanao hujumu uchumi tunatetea ukiukwaji sheria manji kama kakutwa na makosa kwa mujibu wa sheria sweka selo naye si Mtz ama!
 
Mimi naungana kabisa na juhudi za serikali zinazotamkika kama kulikomboa taifa. Tunachopinga ni taratibu mbaya na kuwalinda waharifu wengine kwa kisingizio cha kutokufukua makaburi.

Tatizo ccm hawataki kukubali kwamba wanadandia agenda zisizokuwa zao, na hata naman ya kuzitekeleza hawajui ndipo wanaopoishia kuharibu kabisa kabisa. Hakuna mtu anayepngana na agenda. Tatizo ni approach mbovu ambayo inatoa mwanya wa kupenyezwa kwa hila, maudhui ya kulipa visasi, kukomoa watu makusudi, double standards na kuwaokoa waharifu wengine kwa makusudi.

Ninaimani umenielewa.
Hivi samski tulio kamata waliishia wapi vilee?
 
Ukiona hivyo ujue kwenye ukweli watanzania wanasema ukweli kwenye kuonea mtu na dhuluma pia watanzania wanapinga huwezi sema tulitaka alale mahabusu yaan dhamira ya kwanza alale mahabusu kisha tumpeleke mahakamani watu wameshaona mahabusu ni sehemu sahihi ya watu kulala bogus kabisa
 
Tumeonesha unafki wa kiwango cha lami... Mungu hatatusamehe hasa kizazi cha kuanzia miaka ya 70 mpaka leo.
Kuanzia Mafisadi Papa yupo..(wote tulipaza sauti)
Kagoda (yupo wote tulipaza sauti)
PSPF & NSSF (yupo wote tulipaza sauti)
TANESCO (yupo wote tulipaza sauti)
COCO BEACH (Yupo na wote tulipaza sauti).

Watafuna nchi kumi (yupo wote tulipaza sauti)
Leo mungu kasikia dua zenu, mumebadilika completely kila mtu kaonewa mara chuki.

Tuacheni unafki Mungu anatuona mjue?....
NB: I have enough resources to respond to whoever comes with logical questions.
Usisahau kuuza NYUMBANI za Serikali....
Unafki mkuu hakuna kingine...
 
Meli ya kwenda bagamoyo ile mbovu na sasa wamepewa wajeda aliruhusu nani inunuliwe, je nyumba za serikali vipi?
 
Taratibu zifuatwe hakuna atakaye lalamika! Jinsi hali ilivyo nahisi wanataka kumsafisha kiana, Kama vile Idd Azan alivyochomoa vile!
 
Tumeonesha unafki wa kiwango cha lami... Mungu hatatusamehe hasa kizazi cha kuanzia miaka ya 70 mpaka leo.
Kuanzia Mafisadi Papa yupo..(wote tulipaza sauti)
Kagoda (yupo wote tulipaza sauti)
PSPF & NSSF (yupo wote tulipaza sauti)
TANESCO (yupo wote tulipaza sauti)
COCO BEACH (Yupo na wote tulipaza sauti).

Watafuna nchi kumi (yupo wote tulipaza sauti)
Leo mungu kasikia dua zenu, mumebadilika completely kila mtu kaonewa mara chuki.

Tuacheni unafki Mungu anatuona mjue?....
NB: I have enough resources to respond to whoever comes with logical questions.
Kwa nini hakukamatwa kwa hayo yaliyo wazi, aje kukamatwa kwa haya ya kuhisiwa?
 
Kuanzia Mafisadi Papa yupo..(wote tulipaza sauti)
Kagoda (yupo wote tulipaza sauti)
PSPF & NSSF (yupo wote tulipaza sauti)
TANESCO (yupo wote tulipaza sauti)
COCO BEACH (Yupo na wote tulipaza sauti).
Mkuu mimi nakuunga mkono kwamba kuna unafiki,ila unafiki
una viwango na hivyo lawama
tuzipeleke kwa viwango,mpaka sasa huyo ndugu
ni mheshimiwa diwani,na kabla hujawa diwani
kuna mchakato wa jina kupitishwa kwenye
kamati za maadili,je kashfa hizo ulizozitaja
kamati ya maadili ilizijua? na kama ilizijua
ilimpitishaje kuwa mgombea wa udiwani?

Kama haikuzijua mkono uliomfikia sasa hivi
umetokana na chama gani,ambacho wakati huo hakikuwa na dola?
au utawala wa chama gani,ambao kwenye uchaguzi
ulishindwa kuyaibua haya na kumchuja asije akaaibisha chama mbeleni?
 
Kaka tatizo si Chama wala siasa kwenye uzi huu, suala ni tuhuma dhidi ya Manji, walienda wawili tuu mkafunga barabara central, je wangeitwa watafuna nchi kumi siku moja si Dar nzima ingesimama? Tuwe na subira jamani.

Aliyeleta uzi, alisema "Wapinzani", naomba usiwe mwepesi kusahau na mgumu kuelewa.

Hao waliofungiwa barabara na wananchi, walifungiwa kwa sababu ni waharifu ila tu hatutaki washughulikiwe?

Sifunze kuelewa mada. Tatizo ni kukiukwa kwa taratibu. Mchakato mzima alivyoupeleka huyu jamaa, sasa umewafanya waharifu wengi kuharibu ushahidi. Siyo kila kitu ni kusema "Ndiyooooo" au Hapanaaaa. Yapo masuala ya kitaalamu, yanahitaji taaluma. Lakini pia taaluma ina maadili yake makubwa ambayo ni kweli na haki. Kwa kufanyika vibaya kwa kazi hapatakuwa na matokeo ambayo yangepatikana kama zoezi lingefanywa kitaalam na kwa nia njema.

Hivi wewe unamtaja Mbowe kwa sababu za kisiasa, Gwajima kwa chuki za kitemi, wakati huo huo unawakwepesha makusudi watu wanaofahamika kimataifa, halafu unalazimisha tupige makofi tukisema "kazi ni njema"?

BTW, Watu waliandamana polisi ajili ya Gwajima. Gwajima aliyetajwa unayemsema ni adui, je ni kweli sasa ni shabaha sahihi? Kazi zingine hazihitaji ushabiki na wala hazina kura. Ni suala la kweli, na haki kwa mujibu wa sheria. Makonda ana mamlaka gani ya kuwaita watu kwenda kituo cha polisi?

Jifunze kuchambua, kutofautisha na kuwaelewa watu kile wanachokisema. Epuka sana kubeba mambo mzobemzobe kwa bei ya jumla kwa sababu unanunua mauti ililyopambwa kwa marham!.
 
kweli kaonewa, kwani uongo.....?

kaishavuna mali za watanzania sa hivi analia kivulini ndio namuonea wivu....

kwanini msimkamate kipindi kile anapanda na kuvuna mali za wananchi wakati serikali ni ile ile ya ccm....?

Basi mmemkamata, mbona anapewa tuhuma ambazo hazina mahusiano yoyte..
 
Wahindi waoga sana wa Dola, hivyo ndivyo walivyo wafanyabiashara wazuri wote. Kwahiyo Manji kupiga dili za Kagoda, Tanesco, Escrow, NSSF, Coco na kwingineko ni sawa na Kobe kupanda juu ya mti, ambapo unajua kabisa kapandishwa. Ufisadi wa nchi hii hauwezi kuutenganisha na chama tawala, hivyo kumhukumu Manji sasa kwa 'kumtafutia' kesi ni kumuonea. Kama kweli tunataka haki, tuanze na Chenge na wenzake.
 
Tumeonesha unafki wa kiwango cha lami... Mungu hatatusamehe hasa kizazi cha kuanzia miaka ya 70 mpaka leo.
Kuanzia Mafisadi Papa yupo..(wote tulipaza sauti)
Kagoda (yupo wote tulipaza sauti)
PSPF & NSSF (yupo wote tulipaza sauti)
TANESCO (yupo wote tulipaza sauti)
COCO BEACH (Yupo na wote tulipaza sauti).

Watafuna nchi kumi (yupo wote tulipaza sauti)
Leo mungu kasikia dua zenu, mumebadilika completely kila mtu kaonewa mara chuki.

Tuacheni unafki Mungu anatuona mjue?....
NB: I have enough resources to respond to whoever comes with logical questions.

Uliyoyasema hapo juu yote yaweza kuwa sawa kabisa kabisa ila sasa hisia za uonevu zinakuja pale mamlaka husika zinaposhindwa kumfikisha mahakamani ndani ya masaa 48 kama sharia inavyotaka na kubakia kumuhangaisha ndiyo maana sura ya uonevu inaibuka machoni pa wananchi na si vinginevyo.
 
Back
Top Bottom