Mkuu mimi nakuunga mkono kwamba kuna unafiki,ila unafiki
una viwango na hivyo lawama
tuzipeleke kwa viwango,mpaka sasa huyo ndugu
ni mheshimiwa diwani,na kabla hujawa diwani
kuna mchakato wa jina kupitishwa kwenye
kamati za maadili,je kashfa hizo ulizozitaja
kamati ya maadili ilizijua? na kama ilizijua
ilimpitishaje kuwa mgombea wa udiwani?
Kama haikuzijua mkono uliomfikia sasa hivi
umetokana na chama gani,ambacho wakati huo hakikuwa na dola?
au utawala wa chama gani,ambao kwenye uchaguzi
ulishindwa kuyaibua haya na kumchuja asije akaaibisha chama mbeleni?
Na halafu bila haya wala hofu, wanasema "waliwafahamu miaka kumi. Miaka kumi unafuga waharifu, unawapa uongozi, halafu unajibainisha wewe ni msimamizi wa katiba ya nchi, katiba inayowalinda watanzania!.
Leo unakuja n angonjera za kupambana na uharifu uliouasisi na kuufuga mwenyewe!. Na bahati mbaya agend ahiyo unaidandia kutoka watu wengine kiasi kwamba hata approach yako inathibitisha uwepo wa hila na agenda za kuwainda waharifu wengine.
Hivi ccm watu wakisema ni chama cha majambazi, wanalindana na hata wanapong'ang'ania kuendelea kutawala ni kwa sababu ya kuongopa sherika kwamba wakiachia maovu yao yatakuwa bayana na sherika itawakamata, na kwamba inabidi wakomae tu kwa usalama wa wao, watakuwa wanakosea?
Ccm ndiyo mauti ya Tanzania. Huwezi kuwa na serikali inayofuga waharifu miaka kumi halafu inaanza kubamiza watu innocents kwa maslahi ya kisiasa na visasi vya ki ukoo!.