Freed Freed
JF-Expert Member
- Jun 27, 2017
- 6,232
- 6,479
Nafuatlia Mahafali ya kumi na moja ya Chuo Cha Cha ulinzi wa Taifa-NDC kupitia TBC. Mimi nimekuwa nikivutiwa na mambo ya Jeshi mfano gwaride na tifaki mbalimbali za Kijeshi.
Sasa leo nachukua Rimoti nashusha kila channel nakuta mambo niyapendayo. Nakuta Mahafali ya Chuo chetu Cha ulinzi wa Taifa-NDC.
Mimi siku zote nilijua hiki ni chuo cha kijeshi tu. Nimeona watu mbalimbali kutoka JWTZ, Tanzania Police, Uhamiaji, Magreza, Zima Moto, Majeshi ya nchi jirani na mbali kutoka China, India, Thailand, Egypt nk wakitunukiwa uhitimu chuoni hapo.
Sasa kilichonishangaza ni kuwaona raia kutoka Wizara zetu mbalimbali Kama kilimo, Ujenzi, mifugo, uvuvi nk nao wakitunukiwa uhitimu chuoni hapo. Je imekaaje hili?
National Defence College maana yake ni Chuo Cha ulinzi wa Taifa-NDC. Mgeni Rasmi ni Makamu wa Rais.
Nisaidieni ni kwanini hao watumishi au raia wa kawaida wanaofanya kazi wizarani, inakuwaje wamesoma na kuhitimu pamoja na maafisa wa Kijeshi?
Sasa leo nachukua Rimoti nashusha kila channel nakuta mambo niyapendayo. Nakuta Mahafali ya Chuo chetu Cha ulinzi wa Taifa-NDC.
Mimi siku zote nilijua hiki ni chuo cha kijeshi tu. Nimeona watu mbalimbali kutoka JWTZ, Tanzania Police, Uhamiaji, Magreza, Zima Moto, Majeshi ya nchi jirani na mbali kutoka China, India, Thailand, Egypt nk wakitunukiwa uhitimu chuoni hapo.
Sasa kilichonishangaza ni kuwaona raia kutoka Wizara zetu mbalimbali Kama kilimo, Ujenzi, mifugo, uvuvi nk nao wakitunukiwa uhitimu chuoni hapo. Je imekaaje hili?
National Defence College maana yake ni Chuo Cha ulinzi wa Taifa-NDC. Mgeni Rasmi ni Makamu wa Rais.
Nisaidieni ni kwanini hao watumishi au raia wa kawaida wanaofanya kazi wizarani, inakuwaje wamesoma na kuhitimu pamoja na maafisa wa Kijeshi?