Mkuu
Fundi Mchundo , with due respect, hili sio suala la imani, kama imani za dini watu kuaminishwa Mungu yuke kule juu mbinguni, peponi ni mawinguni, na kuna motoni, hivyo watu wakisali wanapiga magoti kumuomba Mungu aliye juu, wakati ukweli, ni Mungu wa kweli yuko ndani yako!, mbinguni, peponi, motoni, jehanum, ni hapa hapa duniani.
Kwenye hii issue, this is something real, sio mambo ya imani!, barua ya ukweli, bonafide genuine, imeandikwa kweli na Chadema, kwenye letter head bonafide genuine ya Chadema, na kusainiwa na Chadema officer bearer, (mimi najua ni saini ya nani) ikapelekwa NEC kwa despatch ya Chadema, the despatch book Chadema wanayo, kiserikali, barua zote za serikali, zinapelekwa two copies, zikiisha pokelewa, ile copy inagongwa muhuri wa received, na wao kupewa copy yao!, aliyepeleke barua ya Chadema yupo, na copy alipewa, sasa kama ofisi haina kumbukumbu, hayo sasa ni mambo yao ya ndani, waulizane tuu vizuri wenyewe kwa wenyewe ndani kwa ndani, lakini amini nakuambia hao wabunge hawakujiteua, waliteuliwa
Je, wabunge 19 wa CHADEMA walijiteua? Je, CC ya CHADEMA ni Kangaroo Court? Je, Baraza Kuu litabariki ukangaroo ule?
What for, NEC na Bunge hitaji lao ni wabunge, wamewapata!, they have no bussiness with Chadema!. Kama kulikuwa na fojari yoyote, it was upon Chadema sio kulalamika bali kuripoti kunakohusika.
Hapo Mkuu Fundi, liondoe Bunge, has no bussiness kwenye issue ya uteuzi, Spika kapelekewa wabunge na Tume through proper channels. Mapendekezo ya majina ya vitu maalum yanafanywa na vyama na kupeleka Tume, ambayo ndio inawapa barua za uteuzi. na kuripoti Bungeni. Bunge has no business with uteuzi wa vyama, ndio maana kuna wakati waliteua watoto wao, dada zao, vidumu vyao, wapenzi wao hadi vimada wao, michakato ya ndani ya vyao ni kwa vyama vyenyewe, Tume ikipokea majina inawateua na kumpa Spika!
Hakuna barua yoyote ya Chadema bungeni, kule ni barua za uteuzi za Tume!, hakuna barua yoyote iliyofichwa na Bunge, barua ya Chadema ni kwa Tume!
Tume ifanye yote haya for what?!.
Utaratibu wa kijinai uko wazi very clear, mimi na wewe ni majirani, ikatokea wewe umenunua Range Sport ya gold!,
View attachment 3574838
Siku moja umeamka asubuhi, gari huioni!, imeibiwa!. Kwa vile gari hii ilitengenezwa moja tuu custom made kwa ajili yako, unaamua usiripoti polisi kuibiwa kwasababu ikiendeshwa popote, utaiona!.
Ukiwa juu ghorofani kwako, ukaona Range ya gold kama yako imepaki kwangu, je utakuja kuniomba nikuonyeshe kadi yangu, au utaripoti kwanza polisi kuwa umeibiwa gari, kisha utatoa ripoti kuwa umeiona gari kama hiyo nyumbani kwangu, polisi watakuja na search warrant, ndio mamlaka pekee ya uchunguzi wa kijinai ndani ya JMT.
Baada ya Chadema kuona wabunge wameapishwa na KM wa Chadema, JJ Mnyika kuthibitisha kuwa yeye ndie the only signatory wa barua za chama na hajaandika barua yoyote wala kusaini barua yoyote ya uteuzi wa wabunge hao, hivyo barua iliyowasilishwa Tume, ni barua ya kughushi, wameiba bonafide headed paper ya Chadema, wameiba the official seal ya Chadema ambayo inakaa ofisini kwa KM, wakaandika barua fake ya uteuzi, mtu akaisaini kwa kujifanya ni KM, na kuiwasilisha Tume.
Kitu cha kwanza Chadema kufanya, ni kutangaza hawajaandika barua, kitu cha pili ni kuripoti polisi kuwa kumefanyika jinai ya kughushi, hivyo polisi kama mamlaka ya uchunguzi, ndio wenye mamlaka ya kuomba barua ya uteuzi inayodaiwa ni ya Chadema na kuifanyia a forensic investigations, wakikuta ni fojari, polisi ndio wanaiarifu Tume, hiyo barua ni fojari, Tume inatengua uteuzi wao, ndipo kisha waitane na kutimuana!.
Mchakato wa ndani ni issues za vyama zenyewe, Tume kazi yake ni kupokea tuu barua za majina na kufanya uteuzi.
Huku kutakuwa ni kuingilia mambo ya ndani ya vyama yasiyomhusu!.
Tunarudi kule kule, wewe unaedai hujaandika barua, ndio mwenye jukumu la kuripoti hiyo fojari, na ni mamlaka ya uchunguzi ndio yenye uwezo wa kufanya uchunguzi wa kijinai wa fojari !.
Ni kweli, hili hufanyika, kama Chadema wangetanguliza kuomba copy kabla ya kutuhumu, wangepewa, lakini ukiisha tuhumu, then this is a police case, you must prove!.
Spika has nothing to do with this!
Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi
Najua kuna wengi humu wana mapenzi sana na Chadema na wana mahaba sana na Chadema, lakini hawaisadii kwa kuiambia ukweli, huku akina sisi tunao ikosoa Chadema ndio tunaisaidia
Niliwahi kuandika humu
Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?
Hata ile 2015, ilikuwa Watanzania tuwape nchi Chadema, sisi wazalendo, tukawafungua macho wananchi
GE2015 - CHADEMA ikipewa Nchi, Oktoba 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!
Niliwahi kuuliza
Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?
Chadema, bado sana!.
P