Kuhusu Bajeti Kuu, mmesikia tu deni la Taifa na ufafanuzi wa bajeti ya Tr 56?

Kuhusu Bajeti Kuu, mmesikia tu deni la Taifa na ufafanuzi wa bajeti ya Tr 56?

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,866
Reaction score
4,252
Habari za mchana.
Leo nimepata nafasi ya kusikiliza hotuba ya bajeti toka kwa Waziri. Pamoja na deni la Taifa kuendelea kukua, hii itupe ishara kwamba tunaenda uelekeo usio sahihi. Sijui ni kwa nini wananchi huku chini wanasononeka ila wakubwa huko juu wako kimya.

Kubwa ninalotaka kulisemea hapa ni kule mwanzo wa utangulizi wa bajeti hasa kuhusiana na usalama na amani ya Taifa letu. Waziri kazungumzia kuhusu viashiria vya uvunjifu wa amani na kwamba vita ya kupiganwa sio ya kutangaza bali ni ya kiintelijensia zaidi. Kiukweli hapo wanjua wao zaidi. Anasema tusiruhusu misingi na nguzo za Taifa letu vitikiswe. Kika nani wanatikisa? Kwa nini wanatikisa? Imefikiaje hadi kujua kuna mitikisiko? Ni lazima kuna sababu.
Kwa nini tusingalie sababu kwanza hadi tuje kukimbilia kuonyana na kupeana maneno ya kuogofya? Kama vyombo vyetu havijawahi kushindwa kwenye figisu kadhaa dhidi ya chokochoko za kimataifa na ndani ya nchi, iweje leo wasiojulikana wanaendelea kutojulikana?

Waziri hakupenda kabisa kugusia suala la utekaji na watu waliopotea katika kipindi cha karibuni. Mtizamo wangu hapa ni kwamba, walioko madarakani wanatamani kuendelea kuwepo hapo. Bila kujali ni madhara kiasi gani yanafanyika kwa kudhibiti hali, hawataki kutizama vyanzo vya shida zote. Yaani, watu wanaona mtu kapigwa shoti na umeme umemg'ag'ania.

Yupo mtu kando ya main switch ambapo angeweza kabisa kuzima umeme wote. Shida ni kwamba hataki kugusa swichi ili waendelee kumwona mwathirika katika mwanga na kutafuta mbinu zingine za kumwokoa. Uwepo wa shoti ni faida kwao. Pale ambapo watu wataendelea kunaswa na juhudi za kuwanasua zikifanyika, tena kwa chini ya kiwango, kwao ni faida mara mbili. Kudumisha tatizo na pili ni ushuhuda kwamba wanapambana kuokoa maisha ya wanaonaswa na umeme.

Kwani mtu akinaswa na mkazima umeme wote mnapungukiwa na nini? Kwani mkizuia watu wasipite njia ya huo umeme mnapungukiwa na nini? Kwani mkiondoa umeme kwenye hiyo njia mnapungukiwa na nini? Kwa bahati mbaya ni njia kuu hivyo haina budi watu kuendelea kupita. Mwisho wapitaji wataujua mchezo na watatafuta namna ya kukabiliana na huo umeme
 
Alikuwa waziri wa mambo ya ndani maiti kwenye viroba baharini na mto Ruvu zikipatikana.
Jana hakusemea kama enzi zake kuwa ni za wakumbizi wa Ethiopia na Somalia
 
Habari za mchana.
Leo nimepata nafasi ya kusikiliza hotuba ya bajeti toka kwa Waziri. Pamoja na deni la Taifa kuendelea kukua, hii itupe ishara kwamba tunaenda uelekeo usio sahihi. Sijui ni kwa nini wananchi huku chini wanasononeka ila wakubwa huko juu wako kimya.

Kubwa ninalotaka kulisemea hapa ni kule mwanzo wa utangulizi wa bajeti hasa kuhusiana na usalama na amani ya Taifa letu. Waziri kazungumzia kuhusu viashiria vya uvunjifu wa amani na kwamba vita ya kupiganwa sio ya kutangaza bali ni ya kiintelijensia zaidi. Kiukweli hapo wanjua wao zaidi. Anasema tusiruhusu misingi na nguzo za Taifa letu vitikiswe. Kika nani wanatikisa? Kwa nini wanatikisa? Imefikiaje hadi kujua kuna mitikisiko? Ni lazima kuna sababu.
Kwa nini tusingalie sababu kwanza hadi tuje kukimbilia kuonyana na kupeana maneno ya kuogofya? Kama vyombo vyetu havijawahi kushindwa kwenye figisu kadhaa dhidi ya chokochoko za kimataifa na ndani ya nchi, iweje leo wasiojulikana wanaendelea kutojulikana?

Waziri hakupenda kabisa kugusia suala la utekaji na watu waliopotea katika kipindi cha karibuni. Mtizamo wangu hapa ni kwamba, walioko madarakani wanatamani kuendelea kuwepo hapo. Bila kujali ni madhara kiasi gani yanafanyika kwa kudhibiti hali, hawataki kutizama vyanzo vya shida zote. Yaani, watu wanaona mtu kapigwa shoti na umeme umemg'ag'ania.

Yupo mtu kando ya main switch ambapo angeweza kabisa kuzima umeme wote. Shida ni kwamba hataki kugusa swichi ili waendelee kumwona mwathirika katika mwanga na kutafuta mbinu zingine za kumwokoa. Uwepo wa shoti ni faida kwao. Pale ambapo watu wataendelea kunaswa na juhudi za kuwanasua zikifanyika, tena kwa chini ya kiwango, kwao ni faida mara mbili. Kudumisha tatizo na pili ni ushuhuda kwamba wanapambana kuokoa maisha ya wanaonaswa na umeme.

Kwani mtu akinaswa na mkazima umeme wote mnapungukiwa na nini? Kwani mkizuia watu wasipite njia ya huo umeme mnapungukiwa na nini? Kwani mkiondoa umeme kwenye hiyo njia mnapungukiwa na nini? Kwa bahati mbaya ni njia kuu hivyo haina budi watu kuendelea kupita. Mwisho wapitaji wataujua mchezo na watatafuta namna ya kukabiliana na huo umeme

Mwigulu aliwahi kusema kuwa kwa mtazamo wake watu tunaosema wametekwa na kupotezwa huenda wamesafiri kwenda nchi za mbali na huenda watarudi baadaye.

Huu ulikuwa mkakati wa kuzima hoja kwa kupindua meza kihuni wakati anaujua ukweli wote. Alionyesha ujasiri wa kujitoa ufahamu.

Tangu siku hiyo nilipunguza kasi ya kusikiliza hotuba zake.

Mwigulu ni msema chochote, vyovyote, na kwa yeyote. Haonekani kufahamu social epistemology ya Kitanzania.

Na ni power monger asiyechoka. Sasa hotuba ya bajeti na mipasho ya kisiasa iliyojaa kwenye 50% ya kurasa za hotuba ya bajeti wapi na wapi?

The budget speech was unfocused, verbose and epistemologically wanting...
 
Mwigulu aliwahi kusema kuwa kwa mtazamo wake watu tunaosema wametekwa na kupotezwa huenda wamesafiri kwenda nchi za mbali na huenda watarudi baadaye.

Huu ulikuwa mkakati wa kuzima hoja kwa kupindua meza kihuni wakati anaujua ukweli wote. Alionyesha ujasiri wa kujitoa ufahamu.

Tangu siku hiyo niliacha kusikiliza hotuba zake.

Mwigulu ni msema chochote, vyovyote, na kwa yeyote. Haonekani kufahamu social anthropology ya Kitanzania.

Na ni power monger asiyechoka. Sasa hotuba ya bajeti na mipasho ya kisiasa iliyojaa kwenye 50% ya kurasa za hotuba wapi na wapi?
Alivuka mipaka ya hotuba yake. Aliuvaa urais, uwaziri wa mambo ya ndani, u IGP, usalama, n.k. Hapakuwa na haja ya yeye kuzungumzia yote hayo. Alipaswa kutueleza ni vipi tunadili na deni.la taifa, na mambo kama hayo
 
Alikuwa waziri wa mambo ya ndani maiti kwenye viroba baharini na mto Ruvu zikipatikana.
Jana hakusemea kama enzi zake kuwa ni za wakumbizi wa Ethiopia na Somalia
Inahitaji ujasiri wa hali ya juu kusimama pale na kupindisha hoja za kiusalama kama alivyofanya
 
Habari za mchana.
Leo nimepata nafasi ya kusikiliza hotuba ya bajeti toka kwa Waziri. Pamoja na deni la Taifa kuendelea kukua, hii itupe ishara kwamba tunaenda uelekeo usio sahihi. Sijui ni kwa nini wananchi huku chini wanasononeka ila wakubwa huko juu wako kimya.

Kubwa ninalotaka kulisemea hapa ni kule mwanzo wa utangulizi wa bajeti hasa kuhusiana na usalama na amani ya Taifa letu. Waziri kazungumzia kuhusu viashiria vya uvunjifu wa amani na kwamba vita ya kupiganwa sio ya kutangaza bali ni ya kiintelijensia zaidi. Kiukweli hapo wanjua wao zaidi. Anasema tusiruhusu misingi na nguzo za Taifa letu vitikiswe. Kika nani wanatikisa? Kwa nini wanatikisa? Imefikiaje hadi kujua kuna mitikisiko? Ni lazima kuna sababu.
Kwa nini tusingalie sababu kwanza hadi tuje kukimbilia kuonyana na kupeana maneno ya kuogofya? Kama vyombo vyetu havijawahi kushindwa kwenye figisu kadhaa dhidi ya chokochoko za kimataifa na ndani ya nchi, iweje leo wasiojulikana wanaendelea kutojulikana?

Waziri hakupenda kabisa kugusia suala la utekaji na watu waliopotea katika kipindi cha karibuni. Mtizamo wangu hapa ni kwamba, walioko madarakani wanatamani kuendelea kuwepo hapo. Bila kujali ni madhara kiasi gani yanafanyika kwa kudhibiti hali, hawataki kutizama vyanzo vya shida zote. Yaani, watu wanaona mtu kapigwa shoti na umeme umemg'ag'ania.

Yupo mtu kando ya main switch ambapo angeweza kabisa kuzima umeme wote. Shida ni kwamba hataki kugusa swichi ili waendelee kumwona mwathirika katika mwanga na kutafuta mbinu zingine za kumwokoa. Uwepo wa shoti ni faida kwao. Pale ambapo watu wataendelea kunaswa na juhudi za kuwanasua zikifanyika, tena kwa chini ya kiwango, kwao ni faida mara mbili. Kudumisha tatizo na pili ni ushuhuda kwamba wanapambana kuokoa maisha ya wanaonaswa na umeme.

Kwani mtu akinaswa na mkazima umeme wote mnapungukiwa na nini? Kwani mkizuia watu wasipite njia ya huo umeme mnapungukiwa na nini? Kwani mkiondoa umeme kwenye hiyo njia mnapungukiwa na nini? Kwa bahati mbaya ni njia kuu hivyo haina budi watu kuendelea kupita. Mwisho wapitaji wataujua mchezo na watatafuta namna ya kukabiliana na huo umeme
Pesa wakikopa wanaita pesa za watanzania wakianza kuzitumbua unasikia pesa za mama.
 
Back
Top Bottom