Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,947
- 95,237
Miradi mingi itabakia kwenye maandishi tu na itasahaulika kabisa.Ukweli mwingine ambao mpaka sasa hausemwi.
Makosa yaliyofanyika awamu ya tano yataitesa hii nchi kwa miaka miiingi sana, na huu ukweli ni ngumu kuonekana au kusemwa kwa sababu ya unafiki wetu na staili ya uongozi wa propaganda awamu iliyopita..
Madeni yaliyoachwa, big projects zilizoachwa kila mahala huku nchi ikitegemea funds za kuunga unga kuendesha miradi, diplomasia mbovu kuanzia ya uchumi, siasa na jamii ni misalaba itakayomtesa sana mama... Propaganda na brainwashing iliyofanyika kwa watu kama special project ni changamoto nyingine kwenye utawala wa mama maana akili zilijaa propaganda kuliko uhalisia wa mambo..