Kufunga Mwaka 2021: Jamii Forums na kusanyiko la watoto takribani 600 wa dini mbalimbali

Maxence Melo

JF Founder
Feb 10, 2006
4,230
13,415
Katika kufunga Mwaka 2021, Jamii Forums mnamo Desemba 30 ilidhamini kusanyiko la watoto takribani 600 wa dini mbalimbali waliokutana Magomeni jijini Dar na kula, kunywa na kucheza pamoja kwa furaha kuuaga mwaka 2021.

Kusanyiko hili liliwezekana kwa kubuniwa na kuratibiwa na Padre Christian Caristus Likoko Nyumayo ambapo watoto bila kujali tofauti zao za kiimani waliburudika pamoja.

Ilikuwa siku ya furaha kwangu na wenzangu kuweza kuwa na watoto hawa kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 10 jioni.

Nilipata muda wa kuongea na Padre, Masheikh na Wachungaji walioshiriki katika kusanyiko hili. Tulikuwa familia moja, Taifa moja na ndugu kupitia watoto hawa.

Mwaka 2022 tunatarajia kuwa na watoto zaidi ya 1,500 kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar.. Tuunge mkono ukiweza!

Naambatanisha baadhi ya picha:

E2C44D1A-9D0B-45ED-A13B-C1832E818ADF.jpeg
F318EB39-BF9A-42D6-9645-497510803742.jpeg
C1331599-CF6A-41B4-BA86-A8033A218568.jpeg
FA818E92-DC14-4315-8F2B-38BE5EB05A68.jpeg
7E4A7E30-368B-4CBC-9432-C484D3BBABDB.jpeg
7495AB84-6C9D-4327-BC14-8D047E456C5D.jpeg
E710A554-AB58-478C-AFEB-5D9651F42464.jpeg
B0C3C2FA-67A0-4D1F-8E05-184D06BD1E59.jpeg
35FFB2B5-B24E-4880-8432-06D9BFE6448C.jpeg
 
Hili ni wazo zuri mara kumi ya wazo la kukutanisha members,mijitu mizima huishia kutamaniana tu,na kuombana namba za simu ,ukidhani kuna mpango mzuri

Kumbe anania ya kufanya mwenzie mpango wa kando.

Irudiwee hyo ...mwishon mwa mwaka.
 
I believe the children are our future

Teach them well and let them lead the way

Show them all the beauty they possess inside

Give them a sense of pride to make it easier

Let the children's laughter remind us how we used to be.

W. Houston

Safi Sana Melo
 
Katika kufunga Mwaka 2021, Jamii Forums mnamo Desemba 30 ilidhamini kusanyiko la watoto takribani 600 wa dini mbalimbali waliokutana Magomeni jijini Dar na kula, kunywa na kucheza pamoja kwa furaha kuuaga mwaka 2021.

Kusanyiko hili liliwezekana kwa kubuniwa na kuratibiwa na Padre Christian Caristus Likoko Nyumayo ambapo watoto bila kujali tofauti zao za kiimani waliburudika pamoja.

Ilikuwa siku ya furaha kwangu na wenzangu kuweza kuwa na watoto hawa kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 10 jioni.

Nilipata muda wa kuongea na Padre, Masheikh na Wachungaji walioshiriki katika kusanyiko hili. Tulikuwa familia moja, Taifa moja na ndugu kupitia watoto hawa.

Mwaka 2022 tunatarajia kuwa na watoto zaidi ya 1,500 kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar.. Tuunge mkono ukiweza!

Naambatanisha baadhi ya picha:

View attachment 2064566View attachment 2064567View attachment 2064568View attachment 2064569View attachment 2064570View attachment 2064571View attachment 2064572View attachment 2064573View attachment 2064574
Hongera kiongozi.
 
Namkumbuka vizuri sana
Hivi kwa mtazamo wako tu unaona wapo sawa yule na huyu wa sasa?

mijadala yake ya hitajio la katiba mpya kipindi kile na ukosoaji wake kipindi kile kuhusu CCM na serikali yake,alafu baada ya teuzi kawa sio yuleeeee,,,wa kipindi kileeeeeee!

Achana na teuzi kasomi utaisha.
 
Back
Top Bottom