NAOMBA NIANDIKE TU KWA KIREFU KWA FAIDA YA WENGINE!! Narudia tena kusema ni wivu tu watu wa dar wanaona kwa vile Arusha hatuteseki kama wao 😀
Kwanza Arusha kuna Ardhi kubwa open spaces ni nyingi, hakuna joto, kuna population optimal Arusha hata ukiingia kwenye mall au coffee shops kuna ustaarabu unakutana na watu wa mataifa kibao kuna mataasisi makubwa ya kimataifa kwenye eneo dogo tu kama EAC, Mahakama ya Afrika, PAPU n.k lakin pia ni mji mdogo ambao vitu vingi hutumii muda mrefu au gharama kubwa kuvipata au kuvifikia kuna hakuna misongamano kwenye huduma za kijamii kama hyo dar yenu
NB: Hakuna mgeni yoyote atakayetoka nje atachagua dar over Arusha
Arusha ni Jiji la kitalii kwa nlichokiona hapa wengi waliofika Arusha wanacomment kwa morombo, ngarenaro na ungalimited hata nairobi ndo mji wenye slums kubwa afrika za kibera na mathare lakin huwez fananisha na hio dar yenu yani wanapick zile sehemu za uswazi kuonesha kipato Chao kilivo hovyo yani unaenda Arusha unafikia mromboo mwingine kaandika picnic sjui shivas yan mtu wa Arusha ukimwambia ulfkia huko hzo sehemu ni ile mitaa kama ya kimboka kwa malaya waliochoka wa buku 3
* Mwingine kaandika kwanza Arusha hamna foleni kama Dar yeye anaona foleni ndo maandeleo eti hawa watu wakapimwe Akili
MWISHO; Arusha kama majiji yote ya utalii duniani inahitaji uwe na kipato cha uhakika ndo maana watu wa mikoa mingine lazma wacomment chuki dhidi ya Arusha ili wajfariji mioyo yao 😀 kwasababu Arusha huwezi kuishi kwa uwinga au kuuza mitumba alafu utegemee utaweza kuspend Arusha.
Wanaovimba Arusha ni matajiri walioko kwenye Madini au Utalii na ndio maana Arusha ni ya pili kwa makusanyo mengi ya TRA ilhali sio moja ya mikoa yenye watu wengi sasa ukigawanya hapo utaelewa Arusha ni mji wa namna gani kama ingewekewa miundombinu ya kutosha Arusha ndio ungekua mji pekee wa kuiwakilisha nchi kama kigali au Pretoria kwa mandhari yake sio huo utopolo wenu Dar au jangwa lenu la dodoma😀
*Na ndio maana kwa makasiriko mtoa mada ambae ameenda Arusha na kuishia kwa mromboo anabaki anasonya tu ni sawa na uende dar ufikie vingunguti unatuonyesha tu ulikua na kipato gan😀
Kwa ambacho hamjui watu wa dar, Arusha ilikuaga na gated community ya kwanza kabla ya dar na hata sasa hivi zipo nyingi tu kuna mitaa ili uingie ni lazima uwe na kibali huko huingii tu hovyohovyo ndo maana inabidi mtu akuonyeshe mitaa, Arusha ndo nyumbani kwa mabwanyenye haswa wanje na wazawa kama kina mawalla kuna estates zina airport ndani hukohuko, kuna ma settler kibao walikuwepo Arusha kabla ya uhuru na wazawa pia wakawa na utajiri mkubwa kutokana na kufanya biashara na massetler na ndio maana nyerere alianzisha azimio la Arusha kulipa jina Arusha manake pale Arusha ndo kwenye kitovu chenyewe cha matajiri mpaka leo Arusha kuna mashamba makubwa yanamilikiwa na massetler ya kahawa na maua ukiwa njian kutoka Arusha kwa pande zote unayaona na unapoongelea leisure facilities Arusha ndo by far inaongoza hapa nchini hapo tunaongelea bata la hela ndefu tatizo vitu vya matajiri havitangazwagi fesibuku😀
Tafta hela ukaenjoy Arusha au Google places to visit in Arusha sikunyingine usituletee hizi mada za kitoto hujiulizi kwanini mikutano yote mikubwa ikiletwa tz inafanyikia Arusha na Arusha sio mji mkuu??? Ni ili kufuta aibu mjionyeshe tz na nyie mnamji wenye hali hewa nzuri na mandhar ya kijani Dar mliletewa mkutano mmoja tu na barabara zikafungwa hamna kwenda hata shule na kazin😀 imagine mnavoishi hovyo hadi inabidi wageni wafichwe kero mnazokutana nazo manake nchi itadhalilika sasa
Lakini tusiwalaum hawa watu maisha ya dar yanawapeleka race sana hamna kutulia ni purukushan kila mahali Mental Health is real in Dar imagine unatoka kazini unatumia masaa 3 kufka nyumban huyo mtu unadhan atakua normal kweli? Hapo bado umepigwa na jua bila sunscreen hutoboi😃 So naelewa kwakwel mnayoyapitia wakaz wa dar mmevurugwa haswa ila ndo hivo sasa lazma mbanane huko ili mkono uende kinywan lakin maisha ya Dar ni mateso matupu ndio hvo tu mnajifariji lakin deepdown mnajua 😀 Nmeattach hapo sasa muone hadi google inavowakataa