Kuchelewa kwa Mishahara ya watumishi wa umma mwezi October 2012

kosa gani ndugu katika sentensi yangu ndugu maana naona unakuja mbogo

Mkuu kimombo chako japo kinaeleweka kuwa ungekuwa wewe ungejiuzulu na kupisha wengine, lkn kina makosa makubwa kiufundi kuanzia tense na viwakilishi.
 
tatizo ni epicor 9? na ni kweli sababu ndio hiyo au posho za watumishi Hazina? emu tulijadili jamani....hii ni aibu sana kwa serikali
 
Hapa nilipo taa ya mafuta kwenye gari inawaka tangu Jana, halafu mfukoni nna Kama 20 ivi. Kichwa kimeshaanza kuuma kwa mbaali, nachek balance kwa nmb mobile mpaka salio limekata, kudadadadeki
 
Mwezi jana tuliambiwa kuwa epicor 9 ndiyo tatizo. Mwezi huu tumesikia eti "payrolls" zimekosewa! Mwezi ujao sijui itakuwa nini tena...!
 
nyie taasisi gani ya serikali ?ambayo hawajatoa mishaara wakati hazina imeshaachia mzigo kwa public servants wote
labda kama wamebadilisha matumizi wakubwa zenu
 
by jingle:kwa kawaida imezoeleka'inapotoka mishahara hususani ya walim huwa inatoka moja kwa moja lakini kwa sasa benk ya NMB wilaya ya bukombe mkoa mpya wa geita imesimamisha zoez hilo baada ya walim walipokwenda kudraw pesa zao,wingine wamepata robo ya mishahara yao wengine hawakupata kabisa.ikoje hiyo?
 
Mbona mishahara (posho) ya interns nayo imechelewa wakati hawamo kwenye payroll. Hapo hazina kuna tatizo ambalo inabidi lifanyiwe kazi.
 
Acheni kulalamika hii ndo hali ya sasa. Kuweni wabunifu wa miradi mingine sio kutegemea mshahara. Kuna siku hamtalipwa mshahara kabisa kwa zaidi ya miezi sita mtakimbilia wapi....?
 
Hapa nilipo taa ya mafuta kwenye gari inawaka tangu Jana, halafu mfukoni nna Kama 20 ivi. Kichwa kimeshaanza kuuma kwa mbaali, nachek balance kwa nmb mobile mpaka salio limekata, kudadadadeki

Zinatosha kununua tiketi ya treni kwa wiki moja.
 
Hivi ni kitu gani kinasababisha mishahara ya watumishi wa umma inachelewa sana siku hizi!
Kwa mafano kuna wizarra hadi leo hazijalipa
 
Hivi ni kitu gani kinasababisha mishahara ya watumishi wa umma inachelewa sana siku hizi!
Kwa mafano kuna wizarra hadi leo hazijalipa

tumezitumia kwenye uchaguzi wa udiwani, tumemuimiza kitilya akusanye kusanye kwa nguvu ili tuwalipe wiki hii, tulianza kulipa za wabunge kwanza jumatatu huku dodoma halafu watumishi wengine mtafuata.tunasingizia mfumo wa EPICAL , pesa ndio hakuna.
 
Sell some weed..........hautangoja mshahara,
kama wao wanavyouza twiga wetu, the diffeence is that weed is medicinal!!
:majani7::majani7::majani7:
 
Hilo lishakuwa janga kubwa. Mimi siku hizi nishaona kawaida sana. Huwa inaenda mpaka tarehe 35 hadi 36
 
Back
Top Bottom