Kubenea apandishwa Mahakamani leo

Kubenea apandishwa Mahakamani leo

salary slip
Niseme tu kuwa sasa nimeanza kumchukia Magufuli.


Chuki zako zinatusaidia nini sie?
 
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea anafikishwa mahakamani Kisutu muda huu.

Huku ni kuiongezea mahakama mrundikano wa kesi zisizo na kichwa wala miguu.

Kwa mtindo huu lazima Makonda ajitafakari mara mbili mbili

=============

UPDATES;

Mbunge wa jimbo Ubungo kupitia Chadema, Saed Kubenea amepandishwa kizimbani kortini Kisutu, jijini Dar es Salaam leo na kusomewa shtaka la kutoa lugha chafu dhidi ya Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.Hata hivyo, Kubenea amekana kufanya kitendo hicho na kesi yake kuahirishwa hadi Desema 29, mwaka huu.

Aachiwa kwa dhamana.

Hii movie imetegenezwa maksudi na Makonda kwa nia ya kuhujumu uchaguzi wa meya wa Kinondoni, Makonda alitengeneza mazingira mabaya jana akijua moja kwa moja kuwa lazima Kubenea atakataa ndipo wakajibizana na yeye kutumia Udikiteta kumkamata Mbunge na polis pasipo kujali nani chanzo cha Tatizo wakaamua kuegemea kwa mkuu wa wilaya kunyanyasa Mbunge, hizi sheria mbovu zinazompa mamlaka mkuu wa wilaya kuweka watu ndani hata kama yeye ndiyo mchokozi lazima zifutwe haraka vinginevyo wakuu wa wilaya wenye Akili za Kazi kwanza fikiri baadae au kazi kwanza tafakari baadae watachomoza kwa kasi na kuendeleza unyanyasaji kwa wananchi.
 
wastage of resources, misallocation of resources! rubbish! what kind of leaders we have? ovyo kabisa!
 
mimi naombeni kujuzwa, kwani mh: Kubenea alitukana kweli? na kama kweli alitukana Sheria inaelekeza vipi?
 
na katika hilo tukio waandishi wa habari si walikowepo na kwann walivunjiwa kamera zao
 
Niseme tu kuwa sasa nimeanza kumchukia Magufuli.

Hakuna muda wa upuuzi puuzi ni muda wa kazi, siasa ya nini wakati umeshinda ubungen suala ni kutumikia wananchi sio kutafuta cheap popularity. Hukuwahi kumpenda Tingatinga hivyo kuanza kumchukia hakuna maana!Hapa Kazi tu
 
It is becoming more obvious day by day kwamba Mradi wa Makonda ulilenga kufanikisha mambo makuu yafuatayo:

1. Kuzima mvuto wa wagombea funali fulani - Urais CCM 2015.
2. Kurudisha imani ya vijana kwa chama cha mapinduzi kupitia ujumbe wake Bunge la Katiba.

Katika haya yote, hakufaulu. Lakini juhudi zake zikapelekea kupewa zawadi ya Ukuu wa Wilaya ya Kinondoni. Inaonekana kwamba uteuzi huo ulilenga kufanikisha jambo lingine - nalo ni kurudisha imani ya Vijana kwa CCM katika jiji la DSM, lakini hasa Kinondoni ambayo ndio wilaya namba moja Tanzania. Lakini tofauti na ilivyotarajiwa, katika mradi huu pia amefeli. Pamoja na jitihada za CCM kugawanya jimbo la ubungo na pia juhudi za Makonda kubuni njia mbalimbali za kushawishi wapiga kura vijana waiunge mkono CCM, Chini ya makonda, CCM imeingia hasara zaidi:

1. Jimbo pekee la CCM Wilaya ya Kinondoni (Jimbo la Kinondoni) limepokonywa na UKAWA chini ya Makonda.
2. CCM imeshindwa kurudisha majimbo iliyopoteza 2010 (Kawe na Ubungo).
3. Mbaya zaidi, hata jimbo jipya lililotengenezwa na CCM (Kibamba), nalo limeenda UKAWA.

Kwa hali hii, Makonda hana tena political legitimacy Kinondoni. Alichobakia nacho ni political authority kupitia. Mamlaka haya haijabadilika tangia ukuloni.

Makonda anatakiwa aelewe kwamba Political Authority pekee yake haiwezi kumsaidia kutatua changamoto husika bila ya kuwa pia na Political Legitimacy.

Alichokifanya kwa Mbunge wa Ubungo (Chadema) ni matumizi mabaya ya madaraka. Ni kitendo cha aibu na ni liability kisiasa kwa CCM.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kama ambavyo imeripotiwa kwenye vyombo vya habari na njia zingine za upashanaji habari tangu jana kuwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA, Ndugu Saed Kubenea aliwekwa chini ya ulinzi na kuamriwa kwenda kituo cha polisi kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye inadaiwa hakutaka mbunge huyo azungumze na wananchi ambao ni Wafanyakazi wa Kiwanda cha Tanzania Took Garment, waliokuwa wamemuita mbunge huyo kwa ajili ya kumweleza matatizo wanayokumbana nayo kazini hapo, ikiwa ni pamoja na ujira kidogo na mazingira magumu ya kazi.

Aidha akitambua kuwa alichofanya matumizi mabaya ya dhamana ya uongozi, hivyo akakusudia kuficha umma usijue uovu huo, katika tukio hilo Makonda aliwaagiza polisi wakamate kamera za waandishi wa habari waliokuwa katika eneo hilo wakitimiza wajibu wao wa kikazi na kitaaluma kwa jamii.

Katika hatua ya sasa, tunaomba kusema ifuatavyo;

1. Tukitambua kuwa mamlaka ya DC kuamuru watu kukamatwa yamefafanuliwa kisheria na kuwekewa mipaka yake ambayo Makonda amedhihirisha kuivuka katika nyakati tofauti sasa, Mkuu huyo wa wilaya hana mamlaka ya kisheria wala ya kisiasa kuhalalisha amri aliyoitoa ya kumkamata mbunge, tena aliyekuwa anatekeleza wajibu wake, tunamtaka DC Makonda amwachie Ndugu Kubenea mara moja huku tukitoa wito kwa mamlaka zilizomteua kumwangalia kwa makini kama bado anazo sifa za kuwa kiongozi wa ngazi hiyo.

2. Kwa kuwa amri hiyo si halali kwa sababu haina msingi wowote wa kisheria, tunatoa wito kwa Jeshi la Polisi kumuachia Ndugu Kubenea ili aendelee na uhuru wake huku akitekeleza wajibu wake wa kuwawakilisha wananchi wa Ubungo badala ya kumsumbua kwa mambo yasiyokuwa ya msingi.

3. Halikadhalika, Jeshi hilo liwarudishie waandishi wa habari vifaa vyao vya kazi vikiwa katika hali salama na bila athari yoyote ama ya vifaa vyenyewe au materials yaliyoko ndani yake.

4. Tunalitaka Jeshi la Polisi kutoa kauli ya kuwahakikishia usalama waandishi wa habari na vifaa vyao kila wanapotimiza wajibu wao kwenye matukio yanayomhusisha Makonda kwa sababu tayari ushahidi unaonesha anaweza kuwa tishio kwao binafsi na vitendea kazi vyao hususan pia wanapokuwepo polisi.

5. Kwa kitendo cha DC Makonda kuamuru kiongozi wa wananchi akamatwe bila kuwepo kosa lolote la kisheria, CHADEMA tutachukua hatua za kisheria dhidi ya DC huyo ili liwe fundisho kwake mwenyewe, wakuu wa wilaya wengine na utawala mzima wa Serikali ya CCM chini ya Rais John Magufuli, ili watambue kuwa suala la kuongoza nchi kwa kuzingatia Haki, Katiba, Sheria na taratibu si suala la kupenda bali ni lazima kuzingatiwa kwa ajili ya amani na utulivu wa kweli.

Tutachukua hatua hizo huku tayari kukiwa na kumbukumbu za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBU) ambayo hivi karibuni ilimuonya DC Makonda na wakuu wa wilaya wengine na wakuu wa mikoa ambao wameanza tabia ya kuendesha nchi kwa amri ambazo hazina uhalali wowote zikiwa nje ya mamlaka yao ya kisheria kufanya hivyo.

Tuliamini angalizo hilo la THUB ambacho ni chombo huru cha serikali, lingeweza kuwa mwongozo sahihi kwa viongozi wa serikali na kwamba kosa la awali la Makonda kuwaweka mahabusu watumishi wa Wilaya ya Kinondoni walioko chini yake lingechukuliwa kama fundisho kwake, lakini bahati mbaya watawala wanaweka nta masikioni linapofika suala la haki za binadamu na uongozi bora.

Imetolewa leo Jumanne, Nov. 15, 2015 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
 
Back
Top Bottom