Kubenea apandishwa Mahakamani leo

Kubenea apandishwa Mahakamani leo

Hii movie imetegenezwa maksudi na Makonda kwa nia ya kuhujumu uchaguzi wa meya wa Kinondoni, Makonda alitengeneza mazingira mabaya jana akijua moja kwa moja kuwa lazima Kubenea atakataa ndipo wakajibizana na yeye kutumia Udikiteta kumkamata Mbunge na polis pasipo kujali nani chanzo cha Tatizo wakaamua kuegemea kwa mkuu wa wilaya kunyanyasa Mbunge, hizi sheria mbovu zinazompa mamlaka mkuu wa wilaya kuweka watu ndani hata kama yeye ndiyo mchokozi lazima zifutwe haraka vinginevyo wakuu wa wilaya wenye Akili za Kazi kwanza fikiri baadae au kazi kwanza tafakari baadae watachomoza kwa kasi na kuendeleza unyanyasaji kwa wananchi.

Alimchokozaje?
 
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea anafikishwa mahakamani Kisutu muda huu.

Huku ni kuiongezea mahakama mrundikano wa kesi zisizo na kichwa wala miguu.

Kwa mtindo huu lazima Makonda ajitafakari mara mbili mbili

=============

UPDATES;

Mbunge wa jimbo Ubungo kupitia Chadema, Saed Kubenea amepandishwa kizimbani kortini Kisutu, jijini Dar es Salaam leo na kusomewa shtaka la kutoa lugha chafu dhidi ya Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.Hata hivyo, Kubenea amekana kufanya kitendo hicho na kesi yake kuahirishwa hadi Desema 29, mwaka huu.

Aachiwa kwa dhamana.
Ndio atambuwe kuwa mbunge hakumaanishi kuwa juu ya sheria
 
Wakati machine za st scan na dawa hakuna hospital in I mnyamwezi makonda anahangaika na kubenea
 
Inasemekana kuwa huyo DC Makonda ameframe charge ya kuwa Kubenea amemtukana kuwa yeye ni mjinga sana!
Duh................. kazi kweli kweli............. kama kila anayeitwa mjinga hapa jijini Dar angefungua mashitaka, basi ingekuwa balaa kubwa.............


Mkapa aliwaita wananchi wapumbavu, mbumbumbu na malofa nani alimfungulia charge . Sembuse huyu kibaka kuelezwa ukweli
 
Inakuwaje yeye hakushtakiwa kwa kumtukana Lowassa na pia kumpiga kibao Warioba?
 
Nadhani Mkuu Wa wilaya tuseme sasa inatosha.Juzi umewaweka ndani watumishi Wa Manispaa Kinondoni Kwa makosa ya kiutendaji ,We we ulimpiga makofi Waziri Mkuu mstaafu Wa nchi hii unadhani watanzania wanafurahi?
 
Makonda ni kibaka mzuri sana kutoka ukoo mkubwa wa vibaka Tz
 
Matumizi mabaya ya fedha, yaani gari la police linatumia mafuta na kupoteza muda wa watu kwenda kusimama mahakamani na labda nje ulinzi mkali kisa mtu katoa maneno mabaya. Maneno mengine wangeitana ofisini kuyamaliza na kujenga umoja katika kutumikia wananchi..Basi
 
Niseme tu kuwa sasa nimeanza kumchukia Magufuli.

Sasa unamchukia kwani ana kontroli roho zao? Subiri na ukimya wake ni anawasoma siku ya kuwabadili su iuwafuta atakuwa ameshajua nini ni nini na iweje na nani yukoje.

Wote tunajua Makamba hakufanya haya mengi hadi Nov 4 alikuwa bizi na wasanii, sherehe, sijui mikutano ya watafuta kazi etcna mengine yasio na ubosi wa kihivi

Sasa sijui ata sliowaahidi kazi aliwapatia ni vituko kwa kweli vya wstskao kujionyesha kisa wasikatwe.
 
Kwa hiyo wewe unasupport Kubenea kumtukana Makonda? Kubenea hana adabu na hajaanza leo. Ni swala la muda tu mtawajua vyema. Acha sheria ifuate mkondo wake.
Unauhakika gani kama Makonda alitukanwa??Kwanini atoe order polisi kunyang'anya kamera za waandishi wa habari??Nani asiyejua Makonda amepata ukuu wa wilaya baada ya kumpiga Mzee Warioba???
 
Magu wala hana tatizo. Tatizo hapa ni kila kiongozi kutaka kuonekana mtendaji, kesho utasikia naye mwenyekiti wa kitongoji kaamurisha flani atiwe ndani, kesho kutwa napo utasikia balozi wa nyumba kumi, yaani bora tu nao waonekane watendaji.

Huku Mbozi kuna mwenyekiti aliruhusu vijana wampige kwa kuhisiwa kuiba simu.Kijana amelazwa.
 
Back
Top Bottom