mwakweya70
JF-Expert Member
- Feb 13, 2015
- 414
- 106
Nasikia sababu ni majibu mabaya kwa dc wake,ila kwa maneno ya shombo naye yumo kubenea,du awe makini nahisi kama ni asubuhi sana
KawashtAkini waliouza nyumba za serikali na wale wa Escrow.. Hii nchi ni yetu sote. Tunaumia sana mnapojiona Kua nyinyi ndio Watanzania zaidi.kwani hujaona shitaka lake mpaka sasa?
Hii movie imetegenezwa maksudi na Makonda kwa nia ya kuhujumu uchaguzi wa meya wa Kinondoni, Makonda alitengeneza mazingira mabaya jana akijua moja kwa moja kuwa lazima Kubenea atakataa ndipo wakajibizana na yeye kutumia Udikiteta kumkamata Mbunge na polis pasipo kujali nani chanzo cha Tatizo wakaamua kuegemea kwa mkuu wa wilaya kunyanyasa Mbunge, hizi sheria mbovu zinazompa mamlaka mkuu wa wilaya kuweka watu ndani hata kama yeye ndiyo mchokozi lazima zifutwe haraka vinginevyo wakuu wa wilaya wenye Akili za Kazi kwanza fikiri baadae au kazi kwanza tafakari baadae watachomoza kwa kasi na kuendeleza unyanyasaji kwa wananchi.
Niseme tu kuwa sasa nimeanza kumchukia Magufuli.
Kwa hiyo wewe unasupport Kubenea kumtukana Makonda? Kubenea hana adabu na hajaanza leo. Ni swala la muda tu mtawajua vyema. Acha sheria ifuate mkondo wake.
Kila kitu kina mwanzo na mwisho. Kubenea amekuwa akitumia kalamu yake, kama mwandishi, kutukana na kukashfu watu. Kwenye majukwaa ya siasa, amefanya hivyo hivyo. Sasa anasahau kuwa ni mbunge (heshima, busara na hekima hutawala maneno na matendo) na hayuko kwenye ulingo wa siasa tena wala bungeni, kuwa makini na vitendo na maneno yake. Kagusa himaya nyingine mahala pasipo pake, anaisoma namba.
Tusishabikie utovu wa nidhamu.
TAFAKARI CHUKUA HATUA.
So hiyo picha inaashiria tusi gani?hio picha ni ushahidi tosha,huyu mjinga alidhani yuko bungeni nini
Kila kitu kina mwanzo na mwisho. Kubenea amekuwa akitumia kalamu yake, kama mwandishi, kutukana na kukashfu watu. Kwenye majukwaa ya siasa, amefanya hivyo hivyo. Sasa anasahau kuwa ni mbunge (heshima, busara na hekima hutawala maneno na matendo) na hayuko kwenye ulingo wa siasa tena wala bungeni, kuwa makini na vitendo na maneno yake. Kagusa himaya nyingine mahala pasipo pake, anaisoma namba.
Tusishabikie utovu wa nidhamu.
TAFAKARI CHUKUA HATUA.