Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

MKJJ mwana wa mapinduzi ya kifisadi Mungu akubariki sana.

Nimeshangaa sana kukuta huii thread kwani nimeota ndoto ambayo majibu yake ni hii thread, nimeota kuwa Slaa ameshinda uchaguzi wa Rais, yalipotangazwa matokeo nikasikia matarumbeta na kelele nyingi watu wakishangilia kila sehemu, nilifurahi sana, nilipoamka nikamwambia mke wangu akasema ww unasumbuliwa na siasa, lkn, Mungu wa kweli huongea sn na watu juu yayale yajayo kwa njia nyingi lkn sn ndoto imetumika sana.

Naamini ujumbe huu wa mwana wa kijiji mwana wa mkulima, naamini unaukweli kwani umehusiana kwa aslimia 98 na ndoto niliyoiota usiku wa kuamkia leo,neno la Mungu kunasehemu linasema, mmoja atafukuza watu 1000 wawili watafukuza watu 10,000 kwa maombi ya watu wote chochote chaweza tokea, kufumba nakufumbua Slaa awa Rais wa awamu ya tano naamini miaka 5 itakuwa paradiso ndogo kwa wa tz wenye hali duni ila ni jahanamu kwa mafisadi, HAKUNA MAREFU YASIYO NA NCHA.

Makamba atakuwa historia naamini atakuwa informa wa Rais Slaa mara ya kuapiswa kuwa mkuu wa kuongoza watu kwa haki na usawa na hofu ya Mungu itakuwa juu yake.

Ubaarikiwe MKJJ.
 
Maneno yako Mzee Mwanakijiji ni mazito; nimetafuta jina la kukubatiza sijalipata.

Naamini mambo manne ni muhimu ili huu utabiri wako utimie.

Kwanza, watu wapigike sana kimaisha na waweze kuhusisha kikamilifu madhira wanayoyapata na utawala wa CCM. Pili, wananchi walio wengi watakapogundua kuwa CCM ni gari lililokwisha kufa na halikarabatiki hata aje dereva awaye yule, awe Mwinyi, Mkapa, Kikwete, na yeyote yule hii gari haiendi. Tatu, wananchi walio wengi waamini kwamba wana uwezo wa kuitoa CCM madarakani kwa kutumia kura zao. Nne, wananchi wakiangalia pembeni waone chama na viongozi mbadala cha kuwapa hizo kura zao. Yaani, waione gari mpya na dereva aliye mwerevu wa kuiendesha.

Mimi nafikiri wananchi walio wengi tayari wameshapigika sana na maisha na kwamba matumaini waliyopewa na Kikwete yameshayeyuka. Ila sidhani kwamba wananchi walio wengi wameweza kuoanisha sawasawa katika kupigika huko kimaisha na utawala wa CCM. Naamini pia kuwa wananchi walio wengi pia bado wanafikiri kwamba tatizo la CCM ni dereva na sio gari. Yaani, wanafikiri ukibadilisha dereva hamna neno. Hadi pale watakapoelewa kuwa CCM ni gari lililokwisha kufa, halikarabatiki hata aje fundi na dereva wa namna gani hawezi! Naamini kuwa wananchi sasa wanaamini kwamba wanaweza kubadilisha uongozi kwa kura zao. Vinginevyo, upinzani usingepata hao wabunmge wachache waliowapata.

Kuhusu vyama na viongozi mbadala (gari jipya na dereva mwerevu)-Japokuwa mwanga umeanza kupenyeza, nafikiri hapa ndio bado kuna kazi kidogo. Tatizo moja kubwa sana lililopo ni kukosekean kwa umoja wa vyama vya siasa. Watanzania wanapenda sana umoja. Kwa hivyo kwa hili la kuwa kila chama kinajiona bora kuliko chama kingine na kijiendeshea mambo yake chenyewe, ni kikwazo kikubwa kwa vyama vya upinzani kupenyeza katika nyoyo za watanzania. Ndio maana makala yako Mzee Mwanakijiji imenikuna hasa ulipogusia muungano wa vyama vya siasa. Nakwambie siku vyama vya upinzani vikiungana, utakuwa ndio mwanzo wa mwisho wa CCM. Lakini nisisitize hapa kuwa sio muungano, bali muungano miongoni mwa vyama vilivyo makini kwani tunajua kuna vyama vingine ni matawi ya haohao CCM.

Mimi ninashawishika sasa kuliko kipindi kingine chochote juu ya nguvu ya ushawishi tulio nayo katika forum hii. Kwa hivyo, nawaombeni ndugu zangu tuanze rasmi kuwapa shinikizo viongozi wa vyama vya siasa wa upinzani waanze mazungumzo ya kuunganisha vyama vyao. Kwa kuanzia ningeomba tuanze na vyama hivi: CHADEMA, CUF, NCCR, TLP na UDP. Ninaamini vyama hivi vikiungana, itakuwa ni nguvu kubwa na itakuwa ndio mwisho wa shutuma za udini na ukabila zinazotusumbua CHADEMA na CUF.

Tunaweza kuanza kwa kuandika barua ambayo wale tunao amini katika muungano tutaisaini. Barua hiyo iwe ni barua rasmi kutoka kwa watanzania wanaoishi nje na iende kwa viongozi wakuu wote wa vyama vya siasa vya upinzani.

Naomba kuwasilisha

Hata mimi naunga mkono asilimia 100 muungano wa hivi vyama vyenye power.. Na hii ndo dua ya CCM always hivi vyama visiungane maana wanajua kuyama kitawafika. Hivi nini kinachowashinda hapa?? Ama ni hao hao mafisadi wanaingiza dudu lao..
 
Mgawanyiko ndani ya CCM uliojitokeza baada ya wanamtandao kufanikiwa kumpitisha Kinara wao JK kuwa mgombea Urais wa CCM na baadaye Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania hapo mwaka 2005, ENDAPO wakimng'ang'ania JK kuendela na U-enyekiti wa CCM baada ya kudhalilishwa na Dr. Slaa kwenye uchaguzi huu na hivyo kupoteza Ikulu na Bunge CCM itamegeka vipande viwili………………..

Ni kawaida ya utamaduni wa demokrasia pale ambapo chama cha kisiasa kinapoteza ridhaa ya wananchi viongozi wake wa juu kujiuzulu kwa sababu ya kimaadili au kuwajibishwa na wanachama kwa kuwa ni mzigo kwa chama.

Haya yote sasa hivi yameanza kujitokeza kwenye fikra za wanachama wa CCM. Lawama anazotupiwa JK na kamati kuu yake ni kuwa wao ni waaumini wa wanamtandao na hivyo kamwe hawataweza kurudisha CCM kuaminika tena machoni mwa watanzania.


Matokeo ya uchaguzi huu yakiwa mabaya kwa CCM, JK na kamati kuu yake itabidi wasalimu amri na kubwaga manyanga kwa sababu watakuwa wamepoteza uhalali wa kuongoza.
 
Nakuheshimu sana Mwanakijiji unapokubali makosa kwa lugha za kistaarabu kama hizi. Kwa tulioko hapa nchini dalili za CCM kuanguka baadhi yetu hatuzioni. Ila changamoto kama ile ya mwaka 1995 ipo. Tuidumishe hadi 2015.

Ndugu zangu saa ya ukombozi ni sasa. Tukisema 2015 watanzania tumeliwa na vuguvugu kama hili litachukua miaka mingine 15 mingine kuja. Nionavyo mimi ccm imeshakuwa ambushed, hapa ndipo pa kushikilia sana, tusiachie wala tusikate tamaa, wakati Mungu aliotupatia kwa ukombozi ni huu, kila dalili zinaonyesha na pia dalili za adui kushidwa ziko wazi. CCM wenyewe wanakimbiana, kampeni zimegeuka za familia, magwiji wa ccm kama akina Malecela wameuchuna, JK anahangaika mwenyewe, huu ndio muda muafaka, watanzania tuungane. Tupige kura, tulinde kura, wakitushinda wakaiba tutapigana hakuna namna ni lazima Tanzania ikombolewe.

Tumechoka kuonewa, tumechoka kunyanyaswa, tumechoka kupuuzwa, unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe na tudhalilishwe, SASA TUNASEMA BASI. WATATOKA KWA SANDUKU LA KURA AMA VINGINEVYO. DAIMA MUNGU YUPO UPANDE WA WANYONGE.
 
Hongera sana mwanakijiji, ni kweli hakuna marefu yasiokuwa na ncha:

Hii nchi si mali ya CCM ni mali ya Watanzania, ni urithi wetu tumepewa na Mungu, na ndio maana tumezaliwa ktk ardhi yenye mipaka kamili inayoitwa Tanzania,na ndio maana hatukuzaliwa mahali pengine popote na hakuna aliyeomba kuzaliwa Tanzania, ila ni mpango kamili wa Mungu tuitwe Watanzania na riziki yetu, baraka zetu, amani yetu na uhalali wetu wa kuishi hapa duniani uko katika nchi ya Tanzania. Ndio maana mtanzania hawezi kuishi popote duniani bila ruhusa na kibali maalumu, kwa nini? Sio nchi yako Mtanzania.

Sasa basi kama ulivyosema ni kweli kabisa siku ipo na siku yaja ambapo Tanzania itatoka kwene mikono ya CCM na kurudi kwa Wana na binti waTanzania. Ikiwa ni kweli maisha ya Mtanzania yapo hivi kwa sababu tu ya kitu kinachoitwa CCM, ole kwa watu wa CCM, vizazi vyaweza kupita, miaka ikapita lakini ipo siku Mungu atasema nimesikia kilio cha Watanzania nitashuka kuwatoa katika mikono ya Farao (CCM).

Haijalishi akili na fahamu zetu zinasema bado hatumwoni mtu wa kuindoa Tanzania kwene mikono ya CCM. Kwa sababu siku ya CCM kuondoka ipo, na siku ya Musa kuzaliwa ipo, tena atalelewa kwene nyumba ya CCM ili ajue uvunguni mwake vizuri, hatimae mwaka wa kwanza na mwezi wa kwanza utaanza kwa watanzania. Na maanisha kwamba mtu wa kuitoa CCM madarakani yupo na atakuwa anaifahamu CCM vizuri na wakati ukifika tutabaki tukisema hakika hakuna wa kumzuia bwana kuokoa iwe kwa wengi au wachache.

Nawaombea msonge mbele ninyi nyote wenye uchungu na urithi wa Mtanzania.
 
Kila siku huwa na soma utabiri wako mwanakijiji huwa najiambiwa kuna watu muribalikiwa,na utabiri wako uwe kweli CCm ianguke mweleka chaa ibaki kuwa chama pinzani/
 
Unabii wako Mkjj umetimia. Umenikumbusha sana barua aliyoandika Martin Luther King kwa wafuasi wake, akiwa jela huko Burmingham Alabama.
Aliwatia moyo kuendeleza mapambano na kutabiri mengi ambayo tumeyaona yakitokea nchini Marekani kwenye harakati za civil rights mpaka sasa Obama anashika nchi na haki nyingi kupatiwa weusi. Vivyo vivyo ni sawa na uliyoyasema na kutabiri na sasa tumeanza na bunge, na watanzania wamechoshwa na mizigo kuwekewa kwenye migongo yao kama punda, Inshalah Mungu yuko nasi mapambano bado yananendelea.
 
Na Samson Mwigamba

KWA wasomaji wangu wapenzi, ukweli ni kwamba nipo na sijafyata mkia kama baadhi yenu walivyoanza kufikiria. Niliahidi kupambana mpaka tone langu la mwisho la damu na kwa hiyo ni mazingira ya asili tu ambayo yako nje ya uwezo wangu ndiyo
yanayoweza kunitoa hewani na si vitisho wala ‘kushikishwa' kitu kidogo.

Tangu Januari 11 mwaka huu nilikuwa Zanzibar katika Kisiwa cha Unguja, Mkoa wa Kusini Unguja, Wilaya ya Kati, Jimbo la Uzini. Wao Wazanzibari wanakuita shamba! Nilikwenda kushuhudia kampeni za uchaguzi mdogo wa mwakilishi wa Jimbo hilo kufuatia kifo cha mwakilishi aliyechaguliwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Kwa bahati mbaya sana kule hakuna internet café, hakuna modem ya kampuni yoyote ya simu inayoshika. Ukiandika habari lazima usafiri kwenda mjini ili upate angalau network ya modem uliyonay uweze kutuma. Ukizingatia majukumu mengi niliyokuwanayo nilijikuta mara nyingi nakosa muda wa kuwahi kutuma makala kwa wakati.

Nawaomba wasomaji mnisamehe sana kwa kutokuwa hewani kwa wiki zote hizo. Nilikuwa na hamu sana ya kushuhudia kampeni na hatimaye uchaguzi huo. Nilikuwa na hamu kutokana na ukweli kwamba CHADEMA, chama kikuu cha upinzani nchini kwetu kwa sasa, kilikuwa kimesimamisha mgombea katika uchaguzi huo. Lakini kilichonipa mcheche wa kutaka kushuhudia kwa macho yangu hiyo kampeni si tu CHADEMA kusimamisha mgombea bali kuna mambo kadhaa.

La kwanza ni kwamba CHADEMA inafahamika kwa sasa na haina ubishi kwamba ndicho chama kikuu cha upinzani nchini.

Pili, inafahamika na haina ubishi kwamba ndicho chama kinachoangaliwa kwa sasa na Watanzania kama chama mbadala ambacho wanaweza kukichagua wakati wowote kuanzia sasa kuwa chama tawala.

Tatu, kumekuwa nminong'ono kwa muda sasa kwamba chama hiki hakikubaliki Tanzania visiwani (Zanzibar), kwa hiyo kimejikita zaidi Bara.

Nne, kwamba kwa sababu hiyo chama kikuu cha upinzani kwa Zanzibar ni CUF ambacho nacho kinadaiwa hakikubaliki Bara, kwa hiyo kimejikita Zanzibar.

Na mwisho, kwamba unaposema Watanzania wanakitazamia CHADEMA kuwa chama mbadala si sahihi bali usahihi ni kuondoa neno
‘Watanzania' kwenye sentensi hiyo badala yake uweke maneno ‘Watanzania Bara' kwa kuwa Wazanzibari wao wanajua CCM na CUF.

Mimi ni mmoja wa watu waliokuwa wakikataa mambo matatu ya mwisho kati ya matano niliyoyataja hapo juu. Sikuamini kwamba kuna mahali katika Tanzania hii (Bara na Visiwani) ambako CHADEMA hakikubaliki. Niliamini kila mahali wamejaa wana CHADEMA hata kama hawana kadi ama hawana mfumo rasmi wa uongozi ulioainishwa kwenye katiba ya chama chao. Lakini wapo Watanzania katika kila eneo la nchi hii, kila taasisi ya nchi hii (hata kwenye majeshi) ambao wanaiunga mkono CHADEMA hadharani ama kwa kificho.

Lakini pia niliamini kwamba ule unabii mkuu uliotolewa kwanza na M.M. Mwanakijiji mwaka 2007 kwamba CCM itaanguka, unatimia tena kwa kasi. Nakumbuka baada ya Mwanakijiji kuandika mwezi wa tano ama wa sita mwanzoni kwamba "kuanguka kwa CCM unabii utatimia" mwezi Julai mwaka huo huo mimi niliandika kwamba "kuanguka kwa CCM unabii utatimia hivi".

Ni katika unabii huo ndipo nilipotabiri kwamba anguko la CCM litatokea mwishoni mwa utawala wa Kikwete. Awamu ya Nne ya utawala wa nchi hii chini ya Kikwete imebakiza miaka zaidi kidogo tu ya mitatu na sasa kila mtu anaona kwamba unabii ule unatimia! Tulipofika Zanzibar katika Jimbo la Uzini wananchi walituambia wanaifahamu CHADEMA japo hawajawahi kuwashuhudia viongozi wake wakuu katika jimbo lao. Lakini walisema wanaifahamu na wanaipenda na kwamba wamekuwa wakifuatilia matendo yake kwenye vyombo vya habari. Walikuwa wanapata shida kutengeneza mkono na kuonyesha vidole viwili lakini walitamani kuonyesha ishara hiyo na mpaka kampeni zinaisha hakuna mwana Uzini asiyejua kuonyesha ishara ya CHADEMA ya vidole viwili na wanajua maana yake kabisa maana walifundishwa.

Jimbo la Uzini kule linaitwa Jimbo mama la Chama Cha Mapinduzi (CCM). Mbunge wake (acha mwakilishi) ni Mohammed Seif Khatib (aliyewahi kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na hivi karibuni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano). Ukiingia tu ndani ya jimbo unakutana na bango kubwa lenye picha yake na maandishi yanayosema, ‘Karibu Jimbo la Uzini, Ngome ya CCM.'

Kama mnavyojua siasa za Zanzibar zinatawaliwa na historia. Maeneo yaliyotawaliwa sana na ASP ambayo ilikuja kuungana na TANU na kuleta CCM kote huko ni CCM ndiyo inatawala na hakuna namna ya kuwashawishi kujiunga na CUF.

Kwa upande mwingine maeneo yaliyotawaliwa na Chama cha Hizbu kwa sasa ni CUF ndiyo inatawala huko na hakuna namna ya kuwashawishi kuingia CCM. Katika Jimbo la Uzini nimeelezwa kwamba ndiko Waarabu walikokusanywa na kuuawa wakati wa mapinduzi ya mwaka 1964 yaliyoondoa utawala wa kisultani, Rais wa kwanza wa Zanzibar aliwaahidi wananchi kuwagawia ekari tatu tatu zilizokuwa zinahodhiwa na utawala wa kisultani na alitimiza ahadi hiyo.

Wana Uzini wamefundishwa iwe ni ukweli ama ni propaganda kwamba sera ya CUF ni kuwanyang'anya tena wananchi ardhi hiyo na kuifanya ya serikali. Na wamefundishwa kwamba kama wanataka kuendelea kumiliki ardhi hiyo bila matatizo, waendelee kuichagua CCM. Na mpaka leo wananchi wote tuliofanikiwa kuongea nao wanakiri kwamba ardhi ile hadi leo hawajepewa hatimiliki.

Na kwa hiyo wanapotishwa na watawala kwamba watanyang'anywa wasipoichagua CCM wanatetemeka na kukichagua chama hicho. Kwa sababu ya historia hiyo kila chama kiliingia kwenye kampeni kikiwa na lengo tofauti na imani tofauti. CCM walinuia kuendelea kuonyesha wanavyokubalika na kuonyesha kwamba kwa upande wa Zanzibar wataendelea kuongoza serikali kwa muda mrefu sana na si CHADEMA wala CUF wanaoweza kuwanyima usingizi. CUF waliingia kwa malengo mawili:

Kwanza kuishinda CHADEMA na kufuta machungu ya walivyogaragazwa na CHADEMA kule Igunga, lakini pili walitaka kukishinda CHADEMA kuthibitisha propaganda yao kwamba CHADEMA ni chama cha Bara na Visiwani hakipo. CHADEMA wao waliingia kwa kishindo wakitaka kuchukua jimbo na kuonyesha kwamba ndicho chama mbadala kilicho tayari kuchukua dola na kuiondosha CCM madarakani.

Lakini pia walitaka kufuta propaganda ambazo zimekuwa zikipigwa na CCM kwa kushirikiana na CUF kwamba hiki ni chama cha bara. Katika kufanya hivyo, CHADEMA walitambua kwamba wakienda na historia, hawana chao Zanzibar. Walijua jinsi historia hiyo inavyowadumaza wananchi kuelewa haki zao na kuvifanya vyama vyao kuendelea kuwatumia bila kuzingatia maslahi yao mapana.

Mfano kwa sasa CUF imekubali kuingia kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyoshindwa kazi kuliko hata ile ya Salmin Amour! Kila mzanzibari mwenye uelewa wa mambo tuliyemhoji alithibitisha kwamba heri wakati serikali ni ya CCM na CUF wakiwa wapinzani. Angalau walipiga kelele na kuwatetea. Wanasema tangu Maalim Seif amekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais, hali imekuwa mbaya zaidi na wakiwaambia CUF matatizo yao Maalim Seif anawajibu kwamba yeye na mawaziri wake kutoka CUF hawawezi kuikosoa serikali wakati wamo ndani ya serikali. Lakini ingawa wamo ndani ya serikali hawana sera yoyote ya kwao ya kutekeleza na hatimaye kuleta unafuu wa maisha kama walivyokuwa wakijinadi kabla ya kuingia serikalini. Hii ni kwa sababu sera na ilani ya Uchaguzi inayotekelezwa ni ya CCM. Kwa hiyo wananchi hawaoni haja ya wao CUF kuwamo serikalini.

Lakini kibaya zaidi ni kwamba Maalim Seif hivi sasa na yeye anapigiwa ving'ora kusafisha barabara anapopita. Kumwambia ajiuzulu na kujiondoa kwenye serikali ya umoja wa kitaifa kwa kuwa imeshindwa kutekeleza sera murua za chama chake zinazoweza kumtoa mwananchi wa kawaida kwenye lindi la umaskini, ni jambo lisiloweza kueleweka kwa Maalim Seif. Ndipo hapo wananchi wanapohitaji chama kingine cha kuwasemea dhidi ya CCM na mshirika wake CUF.

Wanapoangalia kwenye vyama vilivyopo wanaiona CHADEMA. Kwa hiyo CHADEMA Zanzibar hawana kazi kujieleza mpaka wakubalike. Wana agenda tatu tu ambazo wamezisisitiza sana kwenye uchaguzi mdogo wa Uzini.

Moja ni kwamba Malengo ya Mapinduzi yametelekezwa. Wanawakumbusha Wazanzibari malengo yaliyowafanya wampindue Sultani na kuonyesha jinsi Rais wa Kwanza wa Visiwa hivyo alivyojitahidi kuyatekeleza katika miaka michache ya utawala wake. Mpaka leo ardhi kwa wananchi wa kawaida waliopewa bure na serikali baada ya mapinduzi ni jambo la kumbukumbu kubwa.

Majengo marefu na ya kawaida waliyojengewa wananchi wa Zanzibar ni kumbukumbu tosha ya utawala wa Karume wa Kwanza wa kutekeleza malengo ya Mapinduzi. Katika Tanzania hii ni Zanzibar pekee ambako mwananchi wa kawaida kabisa maskini anaishi aidha bure kwenye nyumba ya serikali ama kwa kulipia kodi kidogo sana. Ulizia nyumba za National Housing za Tanzania Bara uambiwe habari yake! Karume wa kwanza alijenga hospitali na vituo vya afya, alijenga barabara na skuli kila mahali, aliimarisha ulinzi na usalama wa nchi, na kadhalika. Lakini waliofuatia wamesahau maslahi ya umma na kuangalia ya kwao.

Nenda katazame majengo ya maghorofa na ya kawaida yaliyojengwa na Karume wa kwanza yalivyochakaa. Hayafanyiwi hata ukarabati tu achilia mbali kuendeleza kuyajenga pale mzee alipoishia maana alikuwahajamaliza. Ni juzi juzi tu Karume mdogo amejitahidi angalau kuongezea pale alipoishia baba yake.

Nimezungukia vituo vya afya na skuli za maeneo mengi ya Zanzibar si Uzini peke yake, hali inatisha! Zimechakaa si mchezo.

Utawala bora umetoweka, rushwa inatawala kila mahali kuanzia polisi mpaka mahakamani. Ugonjwa wa usalama wa taifa, polisi na tume ya uchaguzi kujigeuza na kuwavyombo vya CCM badala ya vyombo vya serikali hakika nasema bila kumng'unya maneno kwamba afadhali hata Bara kuliko kule Visiwani.

Kweli panahitajika third alternative pale! Agenda ya pili ya CHADEMA ni ile niliyokwisha ielezea vizuri, ndoa kati ya CCM na CUF.

Wameitumia vizuri na wameeleweka sana. Agenda ya mwisho ni kubadili siasa za Zanzibar kutoka siasa za historia kuwa siasa za hoja kama ilivyo kwa Bara. Hii ndiyo agenda ngumu kuliko zote na mafanikio ya chama chochote kingine nje ya CCM na CUF kule Zanzibar maana yake agenda hii imeanza kufanya kazi. Wamejitahidi kuwashawishi Wazanzibari sasa kuangalia mbele badala ya nyuma.

Yaliyopita ni historia ambayo haina msaada mkubwa kwetu zaidi ya kuwa kumbukumbu tu ya tulikotoka na wakati mwingine kujifunza tu kutokana na uzoefu tuliopitia. Lakini muhimu zaidi ni kule tuendako! Na hili ndilo kubwa ninalowaasa wazanzibari kulitia maanani. Waamue nani wa kuwaongoza kwa kuzingatia mustakabali wa maisha yao na ya vizazi vyao na si historia. Kwenye uchaguzi wa Uzini propaganda zimepigwa sana dhidi ya CHADEMA, tena kikichangiwa na CCM na CUF kwa pamoja wakishirikiana kuwadanganya Wazanzibari kwamba chama hicho ni cha Bara tu na kwamba hakiwapendi Wazanzibari na kwamba ni cha kanisa. CHADEMA wamejibu hoja zote na wananchi wamekipatia chama chao nafasi ya pili mbele ya CUF. Kwa wenye macho hawaambiwi tazama bali wanaanza kuuona mwisho wa CCM madarakani kwa macho yao wenyewe.

Ukweli kwamba CCM imeshinda kwa kishindo si hoja kwa sasa kwa kuwa inanihitaji makala nzima kuainisha ushindi wa CCM umepatikanaje kule Zanzibar. Kwamba CCM waendelee kulala usingizi huku wakizipiga na kujaribu kuzifungia kalamu zinazojaribu kuwaamsha usingizini kama hii ya Mwigamba, na kwamba waje kugutuka wakiwa tayari ni chama cha upinzani, ndilo ombi la dhati la mwandishi wa makala hii! Mungu ibariki


Chanzo: Tanzania Daima
 
Kwa anayesoma alama za nyakati anajua ni nini kitatokea tuendako.
 
Asante sana Mwanakijiji kwa forecast. nikitazama ulivyoiona hii mwana 2007 na ilivyo wazi sana sasa, nakukubali mkuu kuwa uliona mbali, japo kwa any simple great thinking, ni wazi sana kuona mwisho wa CCM. actually kwa sasa CCM is dead. Taifa tukae tayari kuishi nje ya utawala wa CCM kwani ni wazi CCM hii haiwezi tena kutawala Tz hii kwa njia halali asilani. hata njia zisizo halali tayari mianya inazibwa na sasa ni kutarajia tu mwisho wake.

Kilicho wazi ni kuwa, utakuwa mwanzo mzuri sana kwa Tz. Hofu ya kuingia chama kingine madarakani utafikia mwisho. WaTz watakuwa huru kukiweka chama chochote madarakani na kuamua kukitoa kama hakitimizi matakwa ya wapiga kura. Hii kwa Tz ni kama kuzaliwa kwa mara ya pili, baada ya kuzaliwa kupitia uhuru. kwa kuwa na uwezo wa kuweka na kuwatoa watawala madarakani kutaanzisha enzi mpya kwa nchi ambako mtawala anawajibika kwa mtawaliwa, na wote wanawajibika kwa nchi. Bila shaka hii ndiyo Tz tunayoitaka kuwaachia wanetu kwa faida yao wenyewe. Mungu endelea kuibariki Tz na uwe nasi kuiondoa CCM madarakani na kuanzisha enzi mpya ya uongozi wa Tz yetu!
 
Nimekaa nikajifikira sana hii Serikali yetu na Miongo yake 4 inaelekea wapi!???
Tangu tupate Uhuru mwaka 1961 nchi yetu imetawaliwa na marais 4 hadi sasa kila kukicha nafikiria bora ya jana.

Awamu ya kwanza: Mwl. J K Nyerere(RIP) alipigania haki na kufanikisha kuwaondoa wakoloni weupe (wazungu) katika nchi yetu tukawa Jamuhuri. ( tukapewa uhuru) Tuliweza kujitawala, alipinga vitendo vya rushwa, nakumbuka enzi zile za fagio la chuma lilikuwa halichagui linapita popote bila woga.

Awamu ya Pili: Mzee Mwinyi aliuwa Azimio la Arusha, alituwezesha kufunguka macho akatuwezeza kuweza hata kununua magari yetu binafsi nk. Kifupi alikuwa ni Mzee wa kuruhusu kila kitu hakuwa na hiyana hadi akapewa jina la Mzee Ruksa. Mianya nimgi ya rushwa ilianzia hapa na kuonekana, hela nje nje, kipindi hii cha mwinyi ndipo watu wengi waliweza kutengeza hela madawa ya kulevya (unga) yaliuzwa kwa wingi na kuingiza pia kwa wingi, hiki ndio kile kipindi cha Mzee wa kiraracha (Mrema) alipokamata shehena ya unga airport na kupoteza ajira yake ya Unaibu waziri mkuu kisa aliingia ambako hakuingili na mengineo mengi.

Awamu ya Tatu: Mzee Mkapa wa zama za ukweli na uhakia aliuwa viwanda na mashirika yote ya uma kwa zana ya ubinafisishaji. hapo ndipo tupokiona chamoto, ajira nyingi zilipotea uozo mwingi ulionekana kubebana kukaanza mikataba mibovu ya madini, tanesco, dawasco (city water) na mengineo

Awamu ya Nne: Hii ndio janga la kitaifa yaani kila kukicha vioja kuanzia bungeni hadi uraiyani. kifupi awamu hii ndio maziko ya ccm yaliko fikia tukimaliza awamu hii ya nne salama kila mmoja wetu atowe sadaka iwe msikitini ana makanisani, urafiki na uswaiba umeifikisha nchi yetu pabaya, kiongozi wa nchi hana maamuzi nchi yetu inapelekwa bora liende tu yaani alimradi kila kukicha bora ya jana. Nashindwa kuelewa kigugumizi kwa rais wetu kinatoka wapi kama ni gari ndio linaingia shimoni na sio mtaroni. Ni shimo kubwa ambalo hatujui ndani yake kuna nini. Viongozi hawana uchungu na nchi yao, hawana uchungu na wananchi walio wachagua wanajali maslai yao binafsi na familia zao, soko huria limechukua hadi familia zetu tumeuzwa hadi ndani ya familia bila kujitambua. Kila siku maisha yanazidi kuwa magumu, elimu ni shida, matibabu ndio usiseme, hakuna maji, umeme yaani kila kitu ni shagala bagala, asilimia kubwa chakula ni mlo mmoja miundo mbinu haifai ni mibovu miaka ya 50 ya uhuru wa mkoloni mweupe ni sawa na hakuna tunajivunia nini tangu mwaka 1961 hadi 2012.

Watanzania wenzangu tunafanya nini hadi sasa kwani tusiamke mapema kuliokoa gari letu kabla gari halijazama shimoni kwani ndani ya shimo kuna giza nene na zito hatujuia kuna wadudu wa aina gani wakutudhuru, tuchukue tahadhari mapema chombo kimekwenda mrama kabla hakijazama.

Naomba kuwasilisha.
Bontwon!
 
WanaJF kuna yaliyosemwa na hasa Historia juu ya dola kubwa ya Rumi ukuwaji na kutoweka kwa dola hii kubwa katika uso wa dunia. Dola ya Rumi ilisambaratika kwa baadhi ya falme na tawala ndogo ndogo kujiondoa katika falme Kuu. Leo hii tunaona Chama kikuu Tanzania kilichojipachika jina "tutawala daima na milele" kuondokewa na wanachama na baadhi ya viongozi wake. Je, itaendelea kusimama au ndo kama dola ya Rumi? Tudadavue wanaJF.
 
WanaJF kuna yaliyosemwa na hasa Historia juu ya dola kubwa ya Rumi ukuwaji na kutoweka kwa dola hii kubwa katika uso wa dunia. Dola ya Rumi ilisambaratika kwa baadhi ya falme na tawala ndogo ndogo kujiondoa katika falme Kuu. Leo hii tunaona Chama kikuu Tanzania kilichojipachika jina "tutawala daima na milele" kuondokewa na wanachama na baadhi ya viongozi wake. Je, itaendelea kusimama au ndo kama dola ya Rumi? Tudadavue wanaJF.
Mimi nafikiri ni upepo tu utapita.
 
Back
Top Bottom