Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Nakuheshimu sana Mwanakijiji unapokubali makosa kwa lugha za kistaarabu kama hizi. Kwa tulioko hapa nchini dalili za CCM kuanguka baadhi yetu hatuzioni. Ila changamoto kama ile ya mwaka 1995 ipo. Tuidumishe hadi 2015.
 
Hata usipotimia 2010, 2015 utatimia tu kwa sababu kuna limits za uonevu, ubabaishaji! Katika utawala, misingi ya utu inapokiukwa destiny inakuwa ndio mwamuzi. At the end of the day inaamua in favour of the oppressed.
AM WITH YOU MY BROTHER,, kuna muda wa kutosha ndani ya miaka mitano ijayo wa kuitoa CCM katika madaraka ya nchi hii. Ni wazi muda huo utafika ila sio sasa wala mwaka huu. Ikiwa wote tutafikiri na kukubali ukweli kama wewe na mimi!! basi ni kweli kabisa tungewekeza nguvu na muda wetu kuhakikisha tunaenda kupiga kura huku tukihakikisha hatupotezi nguvu zetu un necessarily kama wenzetu wanavyofanya humu.
Kupiga kura mwaka huu kutatupa uwezo wa kutathmini kiwango tulichobakiza kabla ya kuiondoa CCM madarakani ,nguvu iliyobaki ya kuwekeza, strategies na udhaifu( ambao uko wazi), na jinsi ya kumfikia kila mpiga kura na kumuambia ukweli kuhusu ubaya wa CCM.
kinachonipa moyo na kujivunia uchaguzi wa mwaka huu ni jinsi ambavyo vyama vya upinzani(CHADEMA& CUF) wamefanikiwa kufika maeneo mengi ya nchi na kueleweka japo maeneo mengine sio kwa kiasi kikubwa.
Nasikitika kuona wanazi wengi wa CHADEMA ni mambumbumbu kiasi cha kuidharau CUF lakini tathmini toka kwa watu walio katika msafara wa kampeni za LIPUMBA unaonyesha uwezekano mkubwa wa kupata kura nyingi kuliko uchaguzi wa 2005.
Na kuhusu CHADEMA! ni wazi watapata kura nyingi kuliko kipindi chochote hapo kabla.Lakini haina maana kuwa watashinda.
Ni udhaifu wenye kutia aibu kwa mtu mwenye busara zake akiamini kitu kisichowezekana huku akijua kuwa anajidanganya.
Mimi sio miongoni mwa wajidanganyao na hivyo najipanga kwa ajili ya kuing'oa kabisaaa CCM mwaka 2015 bila kuweka mazingira ya kujikatisha tamaa mwaka huu.
GO.. VOTE........ SEE THE RESULT AND GET PREPARED FOR THE TOTAL REPRISAL OF CCM IN 2015
 
Teh teh teh :becky: :smile-big: :becky: :smile-big: :becky: :smile-big: :becky: :smile-big:. Wendawazimu wamepewa keyboard. :becky: :smile-big: :becky: :smile-big: :becky: :smile-big: :becky: :smile-big:.

Tatizo wendawazimu hawajitambui tunawatambua kwa kushindwa kujieleza.
 
Nyange, huyu jamaa Mzee Mwanakijiji, wee acha tuu!, akikusanya makala zake zote na michango yake ya JF na ya kule Mwanakijiji.com, amini usiamini anajaza maktaba ya kijiji. Akizibind atatoa vitabu 100 vyenye nondo za kufa mtu!.
Namfagilia, ana vision. Kuandika issue myaka mitatu iliyo pita leo hii kina sound!
 
Ipo wapi tuisome wengine wakati huo hatukuwa mateja wa JF
 
Ipo wapi tuisome wengine wakati huo hatukuwa mateja wa JF
Subiri wamteja wa JF wakusome halafu watakavyokushukia. mi simo

BTW,
anguko la CCM linatagemea mwamko wa wananchi hasa wale wenye maamuzi na kura zao na sio wale wanaosubiria mabadiliko home.

Mwanakijiji anastahili kudos
 
Anguko la ccm linakaribia lakini sio mwaka huu, naungana na wanaoamini kuwa labda 2015 maana watu wengi wanataka mabadiliko sasa lakini bado kuna vikwazo vingi. Watu wengi hawana imani na usalama wa kura zao baada ya kura i.e hawana imani na mawakala wa upinzani kama hawatanunuliwa na sisiem na pia watu wengi hawajajiandikisha kutokana na ujinga wao na wamekuja kujua umuhimu wa kupiga kura wakiwa wameshachelewa.
 
Anguko la ccm linakaribia lakini sio mwaka huu, naungana na wanaoamini kuwa labda 2015 maana watu wengi wanataka mabadiliko sasa lakini bado kuna vikwazo vingi. Watu wengi hawana imani na usalama wa kura zao baada ya kura i.e hawana imani na mawakala wa upinzani kama hawatanunuliwa na sisiem na pia watu wengi hawajajiandikisha kutokana na ujinga wao na wamekuja kujua umuhimu wa kupiga kura wakiwa wameshachelewa.
Katavi, amini usiamini, kwa wale ninao wafahamu, huwa nachomekea msg ya mwaka huu msitunyime kura, tuchague ili tutoe elimu na afya bure kwa kodi zetu. Naungwa mkono kinoma, its a good sign for success.
 
Anguko la ccm linakaribia lakini sio mwaka huu, naungana na wanaoamini kuwa labda 2015 maana watu wengi wanataka mabadiliko sasa lakini bado kuna vikwazo vingi. Watu wengi hawana imani na usalama wa kura zao baada ya kura i.e hawana imani na mawakala wa upinzani kama hawatanunuliwa na sisiem na pia watu wengi hawajajiandikisha kutokana na ujinga wao na wamekuja kujua umuhimu wa kupiga kura wakiwa wameshachelewa.

Anguko la CCm ni lazima liwe sasa, masuala yakusema watu ni waoga kwa hiki na kile haileti maana ,kawni tunauhakika gani hiyo 2015 uoga utakuwa umekwisha au tunauhakika gani kile kinachowafanya waogope sasa hakitakuwepo tena? na ngoja niseme tu kama kweli waTz ni waoga kiasi hicho basi tusitegemee badiliko lolote daima maana imesemwa "Cowards never begin/try"
 
Hata usipotimia 2010, 2015 utatimia tu kwa sababu kuna limits za uonevu, ubabaishaji! Katika utawala, misingi ya utu inapokiukwa destiny inakuwa ndio mwamuzi. At the end of the day inaamua in favour of the oppressed.

Hapana mkuu ni lazima iwe 2010, watanzania tukipoteza fursa hii hatipati mpaka baada ya muda mrefu. Waswahili wanasema "mchuzi wa punda uunywe ungali wa moto, ukipoa haunyweki"
 
Niliwahi kupata article iliyo andikwa na mwanakijiji ikitabili kuanguka kwa ccm, yapata miaka mitatatu iliyo pita. Niliipata kwenye forum hii nikai-print. Katika kupekua nondo zangu, nimeiona na kuisoma kama vile aliandika jana!

Big up mwanakijiji, unaona mbali. Naandika hapa kuomba Mods wairudishe isomwe upya, inatisha, imetoa sura na mwelekeo mpya wa nchi tunayoitegemea baada ya 31/10/2010.

CCM haizewezi kuanguka labda baada ya miaka 30 toka sasa, lakini kama mfumo wa sasa utaendelea ambapo viongozi wote muhimu organisations kama tume ya uchaguzi, msajili wa vyama, igp n.k haya hiyo miaka 30 sahau kabisa. Wacha tutawale maana watanzania wanatawalika. Au kuna mtu anategemea malaika watashuka toka mbinguni kuja kuongoza vyama
 
Kuna watu wametamani kuisoma hii tena.. embu nijinukuu kidogo...

Lakini wana hao na mabinti hao wa Kitanzania pia watasema "Kwaheri"! Watakiambia chama hicho kwaheri kwa kushindwa kujenga misingi mizuri ya utawala wa kidemokrasia! Watakiaga chama hicho kwa mamia baada ya kugundua kuwa hakina lengo la dhati la kuwashughulikia wala rushwa wakubwa na viongozi wabadhirifu! Watakiaga chama hicho baada ya kuona kuwa Mikakati yake mingi yenye majina ya ajabu ni sehemu ya mazingaombwe hayo! Wataangalia maisha ya viongozi hao na watoto wao na kuona kuwa wenzao wananeemeka wakati wao wanaganga njaa! Ndiyo! Watakiaga chama hicho kwa sababu, hatimaye watagundua ya kuwa njia pekee ya kukifundisha somo la utawala ni kuwaweka nje ya madaraka na kuwanyima nafasi nyingine ya kura na kula! Ndiyo, CCM itaanguka! Watatambua ya kuwa CCM ni chama cha kisiasa na siyo mama yao mzazi! Watakiaga na kushukuru kwa onesho lao la mazingaombwe, lakini wakati umefika wa kuingia kazini!
 
Miaka karibu 4 baadaye utabiri wako unaelekea kutimia sasa..kama muujiza vile. MMJ ulipata maono nini?
 
Kweli mkuu nimekukubali, unatisha kwa makala halisi
 
Mi nalia vyombo vya dola tu. CCM si lolote si chochote bila nguvu ya vyombo hivi na hasa wateule wa Rais kwenye vyombo hivi.
 
Endapo wapinzani wataishia kuwa waandamanaji, na wapiga kelele lakini wakishindwa kuungana na kutuonesha kuwa wako makini na mafanikio ya nchi yetu, basi CCM itaendelea kupeta kila kukija uchaguzi! Wapinzani wasililie huruma ya CCM ili wabadilishe Katiba au kuwajengea mazingira mazuri ya kushindana nao! Wapinzani wachukua hatima yao mikononi mwao wao wenyewe! Wawaambie Watanzania kuwa lengo lao mwaka 2010 ni kulichukua Bunge la Tanzania kwani limeendelea kuwa kicheko na dhihaka katika utawala wetu wa Demokrasia! Bunge lenye kutoa azimio la kulaani filamu ya mapanki kabla hawajaiona, na likakaa kimya kwenye mikataba ya madini na nishati bila kutoa azimio la kulaani mikataba hiyo, wabunge wa bunge hilo waondolewe kwa kura! Bunge ambalo linatumia siku 60 kuzungumzia maneno ya watu wawili na kushindwa kutumia siku moja kuzungumzia suala la rada, Richmond, IPTL, ATC n.k hilo ni bunge uchwara!! Bunge lenye spika anayeangalia matumizi ya maneno "kukaza" na "kutia" badala ya kuangalia matumizi ya shilingi Bilioni 80 ya vitu tusivyovihitaji Bunge hilo ni karibu ya Bunge la serikali ya nchi ya Wagagagigikoko! Kama kweli wanataka kuwapa Watanzania matumaini viongozi wote wa upinzani ifikapo 2010 wagombee Ubunge wakiwa wamuengana na kuhamasisha Watanzania wawachague wanachama wao! Kama Watanzania watataka Kikwete apewe nafasi nyingine hilo lao, lakini Bunge lisiende CCM!

Wapinzani wakiweza kunyakuwa wingi katika Bunge la Muungano, basi mwanzo wa CCM kuporomoka utakuwa umefika! Wakiweza kuwashawishi Watanzania baada ya wao kuungana kuwa wanamaanisha wanachosema basi CCM itaanza kutikisika! Watakapochaguliwa Wabunge na wakaanza kusimamia na kupitisha sheria ambazo zina manufaa kwa wananchi watamlazimisha Rais azikubali au atumie uwezo wake wa turufu. Na akifanya hivyo kwenye miswada fulani mara kadhaa avunje Bunge na uchaguzi mpya utafanyika! Huo utakuwa ni mwisho wa Kikwete, huo utakuwa ni mwisho wa CCM!

Mkuu MKJ,
Niliisoma hii habari siku nying kule kijijini kwako, lakini leo naiona ikiwa kama vile inazidi kunikosha! I am not emotional, but today I have droped some tears.........
May God Bless us all to bring up change that we desparately need

Mungu ibariki Tanzania. Wape ujasiri NEC wa kutopendelea chama tawala. Mpe ujasiri Davis Mwamunyange aache uswahiba na JK, bali awe tayari kuzuia ghasia ambazo CCM imejiandaa kufanya ili kuchakachua matokeo. Mpe maono Said mwema kwamba nchi hii ni ya wote, asithubutu kutumia jeshi lake kutishia watu ili kushinikiza matokeo. CCM imeangunka kabla ya Oct 31. JK anajua hili. ila hatakubali, na hapo ndipo penye shida......
 
Back
Top Bottom