Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuanguka kwa CCM – Unabii Utatimia?

Iko siku ambapo Watanzania wataamka na watakuta kwamba Chama cha Mapinduzi hakishiki tena hatamu za uongozi wa nchi, na badala yake Ikulu na Bunge vimechukuliwa na chama kingine. Siku hiyo ambayo haina jina, itakuwa ni siku ambapo Chama cha Mapinduzi kitaanguka kwa kishindo kikuu na sauti ya kuanguka kwake itasikika kila kona ya Tanzania, na mwangwi wa kuporomoka kwake kurindima katika bara letu la Afrika na mabaki ya mtetemo wa kuvunjikavunjika kwake kusimuliwa kama hadithi za Alfu Leyla wa Uleyla kwa vizazi vijavyo vya Watanzania. Kuanguka kwa Chama cha Mapinduzi kutakuwa ni mwanzo wa msemo, na bila ya shaka kutatungiwa methali.

Siku hiyo ni siku ambayo kina Malecela, Msuya, Kingunge, Kikwete,Lowassa,Makamba,Karume na magwiji wengine wa Chama hicho waombee wasijeiona. Kwani itakuwa ni siku ya huzuni kwa watawala na furaha kwa watawaliwa! Itakuwa ni siku ambapo "nyota ya jaha" itaangazia Taifa letu na nuru ya "jua la haki" itachomoza na miale yake kumulika kila kona ya Taifa letu. Hiyo ni siku ambapo kama mwali atolewaye nje, kila mtu atatamani kuiona isipokuwa wale ambao huyo mwali ni ishara ya wao kukosa mke na wengine kupata!

Bila ya shaka unajiuliza iweje nianze kwa kusema maneno hayo. Nilikuwa natafakari maneno ya Mwalimu aliyoyatoa mwanzoni mwa miaka ya 90 mara baada ya vyama vingi kuruhusiwa tena nchini. Baada ya Mwalimu Nyerere kutoa maneno makali ya "Ikulu inanuka Rushwa" watu wengi walianza kujiuliza mapenzi ya Mwalimu kwa chama alichokiasisi na kama anaweza kujitoa kwenye chama hicho. Alipoulizwa kuhusu kujiondoa CCM, mwalimu alijibu "CCM siyo Mama yangu". Maneno hayo ya Mwalimu yamebakia mawazoni mwangu (na bila shaka ya wengine pia) kama unabii na kama wosia. Hii leo kuna baadhi ya viongozi wa Chama tawala ambao wanasisitiza maneno ya Mwalimu ya "Bila CCM madhubuti Tanzania Itayumba" na kusahau kabisa maneno hayo ya onyo kali kuwa hata kama mtu ana mapenzi kiasi gani na CCM, iko siku anaweza kukiacha na kujitahidi kukivunja! Ni rahisi kukiacha CCM kuliko kumuacha Mama mzazi!

Siku hiyo ambapo Chama hiki maarufu kitakapojikuta kiko katika kambi ya upinzani ndipo viongozi wake na mashabiki wake watakapotambua kuwa "CCM siyo Mama" na Tanzania itaendelea na inaweza kuwepo bila CCM kuwa madarakani! Hiyo siku iso jina, iko, yaja, na yafanya hima kufika! Kwanini basi CCM itakuja kuanguka kwa mshindo mkuu namna hiyo?

Ndugu zangu, punda mnyama wa kazi kuna mahali anafikia kikomo! Na akifikia kikomo, punda hendi hata kwa mijeredi mia. Mtu unaweza kumtwisha punda mizigo, lakini akifikia kikomo chake hata umfanye nini punda hanyanyui mguu. Kuna baadhi ya viongozi ambao wanadhani kuwa Watanzania wataendelea kuinama na kukubali kutwishwa mizigo ya kila namna kana kwamba hawasikii maumivu! Ni hawa viongozi ambao huendelea kutuingiza katika mikataba mibovu, wanaendelea kuvumilia ufujaji wa mali ya umma katika maofisi yao, wanaendelea kupuuzia rushwa hadi imezoeleka na kuonekana kama kawaida. Viongozi hawa wanaimba wimbo na pambio ya uongozi bora wakitumbuiza kwa kasida za maneno ya kizalendo. Mawazoni mwao wanaishi wakifikiri kwamba Watanzania wataendelea kuvumilia. Kama punda iko siku hugoma, iko siku Watanzania nao watasema "Sasa inatosha"!

Siku moja ambayo ipo, Watanzania watajiuliza iweje viongozi wetu wanunue rada Bilioni 40 wakati hospitali yetu ya kijiji yenye kugharibu shilingi milioni moja haina hata bomba la maji! Hiyo siku Watanzania watajiuliza iweje ili kupata elimu nzuri ni lazima wapeleke watoto wao kwenye shule binafsi wakati shule za serikali zilizokuwa zikisifika huko nyuma zikibakia historia? Hawa wana na mabinti wa Tanzania wataamka siku moja na kusema "Imetosha".

Chama cha Mapinduzi kitaunguka pia kwa sababu hatimaye Watanzania wataelewa ya kwamba kuendelea kukaa kwa chama hicho madarakani ni kujitakia kutokuendelea na kurudi nyuma kwa maisha yao. Wataelewa kuwa CCM haina lengo hata chembe la kutimiza na zaidi ya kutimiza ahadi zake ambazo imekuwa ikizitoa tangu uhuru. Itadhihirika kuwa CCM iko madarakani ili kuendelea kujikita katika kutawala huku wakifanya mambo machache ya manufaa kwa wananchi huku viongozi wao na watu wachache waliobarikiwa na chama hicho wakiishi katika paradiso ya Bongo.

CCM itaunguka kwa sababu hata kipofu akigonga ukuta anauzunguka! Kutokuona siyo kikwazo cha kujua kukwama. Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikifanya mambo kana kwamba Watanzania wote ni vipofu na viziwi. Miaka nenda rudi tumewapa imani kuwa labda watabadilika. Wanavutia kwa maneno matamu na nyimbo za shangwe, wanafurahisha kwa rangi nzuri za mavazi yao, na mvuto wa kupepea kwa vibendera vyao vya kijani! Lakini wamekuwa kama makaburi yaliyopakwa chokaa, lakini ndani yake ni mifupa mitupu! Siku hiyo watanzania watakuwa kama kipofu aliyeona mwezi. Watagundua kuwa CCM siyo jua bali ni mwezi mchanga na mwanga ambao watu wamekuwa wakiusifia si mwangaza wa jua, bali mmuliko wa mbalamwezi. Watagundua kuwa wanachotaka kimulike maisha yao na kuanzia maisha ya watoto wao ni chama na viongozi wenye nuru ya jua, ambao mwangaza wao hautegemei kuakisiwa na kitu kingine bali unatoka ndani yao wenyewe! Wataamua kuachana na Chama ambacho miaka nenda rudi kimekuwa kikijificha kati yao mwangaza wa jua na hivyo kuwapa kivuli cha "kupatwa jua". Watu wamekuwa wakiogopa kuwa huo mwezi ukiondoka kati yao na jua, dunia itafikia mwisho! Kumbe zote hizo ni porojo. Mwezi huzija jua, lakini hatimaye hupisha!

Chama hicho kitaanguka si kwa sababu hakina watu wenye sura nzuri, na watanashati kwani wamejaa tele, siyo kwa sababu hakina watu waliosoma na kubobea katika nyanja mbalimbali kwani wapo bwelele, bali kwa sababu wale waliodhaminiwa uongozi katika chama hicho na kwa kupitia chama hicho nchi yetu, ni viongozi wasio na maoni, waliolala hadharani, wenye kutetea maslahi ya matumbo yao na ya wanawe, wakihangaika kutwa kucha kufikiri ni jinsi gani watamegeana fedha za walipa kodi. Kwa kutumia vipaji vyao na elimu yao baadhi ya viongozi wa vyama hivyo wamebuni miradi hewa ya kugereshea umma huku fedha nyingi za miradi hiyo zikiishia vibindoni mwao. Watanzania hatimaye watatambua kuwa wakati wa kuangalia onesho la mazingaombwe umepita, na watataka kitu halisi! CCM haiwezi kubadilika, imelewa ugimbi wa madaraka na kuvimbiwa na mlo wa uchu! Ndiyo! Watanzania watagundua ya kuwa kuwa na CCM au kutokuwa nayo yote ni sawa! Hawana cha kupoteza tena. Kama miaka yote hiyo CCM imeshindwa kuboresha elimu yetu, sekta ya afya na maji, matatizo ya nishati n.k itakuwaje waweze kufanya hivyo miaka arobaini ijayo wakati kizazi kinachoingia madarakani sasa ni cha wana na wajukuu wa viongozi wa chama hicho!? Watanzania watasema "CCM Asante, lakini Kwaheri"!

Watakishukuru chama hicho kwa kutujengea misingi ya udugu, umoja na mshikamano. Watakishukuru chama hicho kwa kutulindia utaifa wetu na kuhakikisha kuwa tunabakia kuwa huru kisiasa. Watakishukuru Chama hicho kwa kutujengea utambulisho wetu wa "watanzania" na kutufutia hisia ya ukabila na udini. Ndiyo, watakishukuru chama hicho kwa yale machache mazuri ambayo kimefanya kwa muda mrefu, barabara chache za lami, shule, mahospitali, n.k Ndiyo, Watanzania watasema "asante"!!

Lakini wana hao na mabinti hao wa Kitanzania pia watasema "Kwaheri"! Watakiambia chama hicho kwaheri kwa kushindwa kujenga misingi mizuri ya utawala wa kidemokrasia! Watakiaga chama hicho kwa mamia baada ya kugundua kuwa hakina lengo la dhati la kuwashughulikia wala rushwa wakubwa na viongozi wabadhirifu! Watakiaga chama hicho baada ya kuona kuwa Mikakati yake mingi yenye majina ya ajabu ni sehemu ya mazingaombwe hayo! Wataangalia maisha ya viongozi hao na watoto wao na kuona kuwa wenzao wananeemeka wakati wao wanaganga njaa! Ndiyo! Watakiaga chama hicho kwa sababu, hatimaye watagundua ya kuwa njia pekee ya kukifundisha somo la utawala ni kuwaweka nje ya madaraka na kuwanyima nafasi nyingine ya kura na kula! Ndiyo, CCM itaanguka! Watatambua ya kuwa CCM ni chama cha kisiasa na siyo mama yao mzazi! Watakiaga na kushukuru kwa onesho lao la mazingaombwe, lakini wakati umefika wa kuingia kazini!

Ni matumaini yangu kuwa maandamano ya wapinzani yanayofanyika jijini Dar hayatakuwa ni ishara tu ya kuchukizwa na matendo ya serikali ya CCM na ufisadi uliokithiri. Ni matumaini yangu kuwa viongozi wa vyama vya upinzani watadhamiria kushirikiana siyo katika kupiga kelele kwa kutumia vipaza sauti hapo Jangwani bali ushirikiano wa kweli utakaofanya waziunganishe nguvu zao na kuunda chama kipya cha siasa chenye itikadi inayoakisi matamanio na matarajio ya Watanzania wengi, na chenye viongozi ambao kwao utumishi wa Taifa lao ndio kitu kinachowasukuma!

Endapo wapinzani wataishia kuwa waandamanaji, na wapiga kelele lakini wakishindwa kuungana na kutuonesha kuwa wako makini na mafanikio ya nchi yetu, basi CCM itaendelea kupeta kila kukija uchaguzi! Wapinzani wasililie huruma ya CCM ili wabadilishe Katiba au kuwajengea mazingira mazuri ya kushindana nao! Wapinzani wachukua hatima yao mikononi mwao wao wenyewe! Wawaambie Watanzania kuwa lengo lao mwaka 2010 ni kulichukua Bunge la Tanzania kwani limeendelea kuwa kicheko na dhihaka katika utawala wetu wa Demokrasia! Bunge lenye kutoa azimio la kulaani filamu ya mapanki kabla hawajaiona, na likakaa kimya kwenye mikataba ya madini na nishati bila kutoa azimio la kulaani mikataba hiyo, wabunge wa bunge hilo waondolewe kwa kura! Bunge ambalo linatumia siku 60 kuzungumzia maneno ya watu wawili na kushindwa kutumia siku moja kuzungumzia suala la rada, Richmond, IPTL, ATC n.k hilo ni bunge uchwara!! Bunge lenye spika anayeangalia matumizi ya maneno "kukaza" na "kutia" badala ya kuangalia matumizi ya shilingi Bilioni 80 ya vitu tusivyovihitaji Bunge hilo ni karibu ya Bunge la serikali ya nchi ya Wagagagigikoko! Kama kweli wanataka kuwapa Watanzania matumaini viongozi wote wa upinzani ifikapo 2010 wagombee Ubunge wakiwa wamuengana na kuhamasisha Watanzania wawachague wanachama wao! Kama Watanzania watataka Kikwete apewe nafasi nyingine hilo lao, lakini Bunge lisiende CCM!

Wapinzani wakiweza kunyakuwa wingi katika Bunge la Muungano, basi mwanzo wa CCM kuporomoka utakuwa umefika! Wakiweza kuwashawishi Watanzania baada ya wao kuungana kuwa wanamaanisha wanachosema basi CCM itaanza kutikisika! Watakapochaguliwa Wabunge na wakaanza kusimamia na kupitisha sheria ambazo zina manufaa kwa wananchi watamlazimisha Rais azikubali au atumie uwezo wake wa turufu. Na akifanya hivyo kwenye miswada fulani mara kadhaa avunje Bunge na uchaguzi mpya utafanyika! Huo utakuwa ni mwisho wa Kikwete, huo utakuwa ni mwisho wa CCM!

Je wapinzani wako tayari kusimama na kuchukua nafasi yao ambayo historia imewatengenezea? Je wako tayari kuitwa majina na kujipanga mstari kuongoza Taifa letu? Je, ndani ya vyama hivyo wapo kweli viongozi ambao Tanzania inaweza kuwaangalia na kuwategemea kuwavusha kutoka katika jangwa la utawala wa CCM.

Kuna maneno ya Maandiko Matakatifu yanayosema "Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha, geukeni upande wa kaskazini." (Kumb. 2:3). Ndugu zangu Watanzania, tulivyouzunguka mlima wa CCM sasa imetosha! Tulivyouimbia kwa kuuzoea na kuusifia utawala mbovu wa chama hicho sasa inatosha! Tulivyozoea mazingaombwe na mikataba iliyodumaza uchumi wetu sasa inatosha! Ndiyo CCM inaweza kuwa na watu wachache waadilifu, wamwogopao Mungu, na waipendao nchi yao! Ndiyo inawezekana kuna wale wanaojaribu kuibadilisha toka ndani ili ikidhi mahitaji ya Taifa letu, hata hivyo kuombea watu hawa wapo, inatosha! CCM imefanya mambo mengi mazuri kwa Taifa lakini yakipimwa na yale mabaya kwenye mizani ya Mama Haki, mambo mabaya yanazidi kwa uzito na wingi wake yale mazuri! Kuombea kuwa miaka mitano ijayo mambo yatabadilika inatosha! Tugeuke upande tofauti! Labda tutafika iliko NCHI YA AHADI!

Kwani kuanguka kwa chama hicho kupo, kunakuja, na kunafanya hima kutufikia. CCM siyo mama yetu! Unabii huo utatimia!!!

( nitasahihisha kesho)
😂😂😂😂
 
Angalia ZWAZWA lingine hili! Hivi ni nani aliyesema hadharani CCM kuna mafisi? Nini aliyesema hadharani ccm kuna makizi makubwa lakini nazuiwa kuyataja hadharani na viongozi wa juu? Ni nani aliyesema ccm kuna majizi makubwa nikiyataja hadharani mtashangaa? Acha kuonyesha UJUHA wako hadharani.

Ametambua kuwa alikuwa anapoteza muda wake na walaghai wanaojiita wapinzani...
 
Mkuu angalia tarehe ya huu uzi. Ni wa miaka ya nyuma ambayo wakati huo jamaa alikuwa hawivi chungu kimoja na wahuni wa maccm.
Sijawahi kusoma maneno mazito ya toka kwa mwanakijiji kama haya.Hakika umechoka na kukinai ufisadi wa CCM.
 
Angalia ZWAZWA lingine hili! Hivi ni nani aliyesema hadharani CCM kuna mafisi? Nini aliyesema hadharani ccm kuna makizi makubwa lakini nazuiwa kuyataja hadharani na viongozi wa juu? Ni nani aliyesema ccm kuna majizi makubwa nikiyataja hadharani mtashangaa? Acha kuonyesha UJUHA wako hadharani.
Si kama mlivyomsema Lowassa halafu mkaenda kumpigia kampeni.
Relax. Na wewe siku yako ikifika utaamka toka usingizini.
 
Kura za maoni CCM imeteua watoa rushwa
Mwenyekiti kawasamehe akina Lugola wakati alisema wameiingiza nchi hasara
Anafanya manunuzi ya midege bila ridhaa ya bunge, halafu mwanakijiji anafagilia serikali hii dhalimu, ongo sana
 
Mimi na fisadi lowassa wapi na wapi! Sikumkubali akiwa na wahuni wa maccm skumkubali ndani ya Chadema. Mimi si bendera FUATA UPEPO!
1603908893244.png


Si kama mlivyomsema Lowassa halafu mkaenda kumpigia kampeni.
Relax. Na wewe siku yako ikifika utaamka toka usingizini.
 

Attachments

  • EQjS1XeX0AAwrhE.jpg
    EQjS1XeX0AAwrhE.jpg
    41.1 KB · Views: 8
  • images.jpg
    images.jpg
    9.4 KB · Views: 6
  • EcVI5W7WkAAlIpO.jpg
    EcVI5W7WkAAlIpO.jpg
    50.6 KB · Views: 7
  • thumbnail_1560181784337.jpg
    thumbnail_1560181784337.jpg
    19 KB · Views: 8
kama mlivyomsema Lowassa halafu mkaenda kumpigia kampeni.
Relax. Na wewe siku yako ikifika utaamka toka usingizini.
 
Si kama mlivyomsema Lowassa halafu mkaenda kumpigia kampeni.
Relax. Na wewe siku yako ikifika utaamka toka usingizini.
 
Ametambua kuwa alikuwa anapoteza muda wake na walaghai wanaojiita wapinzani...
Si kama mlivyomsema Lowassa halafu mkaenda kumpigia kampeni.
Relax. Na wewe siku yako ikifika utaamka toka usingizini.
Seriously unaamini hivi sasa Mwanakijiji anasukumwa na mahaba yake kwa CCM?!

Yaani hadi leo hufahamu kwamba Mwanakijiji ni kivuli cha Dr. Slaa?!

Hadi leo hujui kwamba Mwanakijiji bado ana kinyongo cha Dr. Slaa "kukatwa" na CHADEMA ile 2015?!

Mengine yanayochochea mwelekeo wa kisiasa wa Mwanakijiji ni aibu hata kuyasema!!
 
Mkuu mambo mengine yanashangaza sana. Eti Mzee Mwanakijiji huyu ambaye aliipinga sana ccm kwa kila hali leo hii anasukumwa na mahaba tele kuipigia chapuo na kudai hajui kura fake zinapigwaje hahahahahaha. UNAFIKI nao ni kipaji Mkuu. Thanks God I am extra careful dealing with people on this forum ila huyu jamaa nilimuamini sana hadi kuwa karibu kumpa particulars zangu but my sixth sense warned me.

Seriously unaamini hivi sasa Mwanakijiji anasukumwa na mahaba yake kwa CCM?!

Yaani hadi leo hufahamu kwamba Mwanakijiji ni kivuli cha Dr. Slaa?!

Hadi leo hujui kwamba Mwanakijiji bado ana kinyongo cha Dr. Slaa "kukatwa" na CHADEMA ile 2015?!

Mengine yanayochochea mwelekeo wa kisiasa wa Mwanakijiji ni aibu hata kuyasema!!
 
Mkuu mambo mengine yanashangaza sana. Eti Mzee Mwanakijiji huyu ambaye aliipinga sana ccm kwa kila hali leo hii anasukumwa na mahaba tele kuipigia chapuo na kudai hajui kura fake zinapigwaje hahahahahaha. UNAFIKI nao ni kipaji Mkuu. Thanks God I am extra careful dealing with people on this forum ila huyu jamaa nilimuamini sana hadi kuwa karibu kumpa particulars zangu but my sixth sense warned me.
Mzungu anasema follow your instincts
Upinzani wa kweli ni wachache sana
Lissu ni mpinzani wa kweli huwa nashindwa kumtafakari huyu Mzee
ccm ya Mkapa ndio ile ile ya Kikwete Magufuli sasa kipi ambacho kimebadilika hapa?
Ukiangalia kwa undani sana sana sana ni maslahi binafsi
Slaa aliikosoa sana ccm leo yupo kuiunga mkono ( utekaji na makubwa ya hayo kupotezana etc)
Naona ni vita yao na Mbowe wala sio Chama

*** Sheria inasemaje kuzuia matokeo tuhesabu upya au uchaguzi ufutwe kabisa
Welcome Belarus action
 
Shukrani sana kusema kweli sijui what’s next maccm hayana aibu wala woga yanatawala kwa kujificha nyuma ya vyombo vya dola ambavyo ndivyo vinavyoiweka madarakani.

Matokeo ya urais pamoja na ushahidi tele wa mawakala wa Chadema kutokuwepo kwa kupigwa, kuondolewa vituoni kwa nguvu, kutoapishwa, kutopewa nakala za matokeo na kura fake Chadema haiwezi kuyapinga kokote sheria inakataza 😢😢 eti sheria inazuia haki!!!

Matokeo ya Wabunge yanaweza kupingwa mahakamani lakini tunajua bwana yule alivyoziweka mahakama mfukoni kwake.
 
Mkuu mambo mengine yanashangaza sana. Eti Mzee Mwanakijiji huyu ambaye aliipinga sana ccm kwa kila hali leo hii anasukumwa na mahaba tele kuipigia chapuo na kudai hajui kura fake zinapigwaje hahahahahaha. UNAFIKI nao ni kipaji Mkuu. Thanks God I am extra careful dealing with people on this forum ila huyu jamaa nilimuamini sana hadi kuwa karibu kumpa particulars zangu but my sixth sense warned me.
Man,

Machale yalikucheza sana manake mtu wa aina hii haaminiki hawezi kuaminika hata kidogo!! Ni bora kumwamini mtu anayejitambulisha with their true colors kuliko watu aina ya mwanakijiji!!! Ni bora uwaamini watu kama akina Bia Yetu au Magonjwa Mtambuka kuliko kuwaamini watu aina ya MKJJ!

Mwanzoni kabisa nilidhani tatizo la Mzee Mwanakijiji lilikuwa Lowassa kukaribishwa CHADEMA kwa miguu miwili, jambo ambalo wengi tulipinga lakini baadae nikagundua a core issue sio Lowassa bali Dr. Slaa kutopewa nafasi ya kugombea urais, na matokeo yake, ghafla tu CCM na Magufuli wake ndio taasisi bora kabisa inayostahili kuongoza nchi!!
 
Njaa kitu kibaya sana Mkuu. Mtu angeniambia huyu angekuwa MNAFIKI kiasi hiki na kuwa bega kwa bega na wahuni wa maccm ningemkatalia kata kata. Leo huyo kaibuka kujikomba kwa kutetea uchaguzi FAKE ili kusaka TEUZI ndani ya Serikali hii haramu.
Tuseme ukweli mwaka 2015 upinzani uliounda UKAWA na hasa kinara CHADEMA ulikosea kumfanya Lowassa mgombea wao na kuwatendea uhuni wapambanaji walioufikisha upinzani juu kama Dr. Slaa.

Haya yanayotokea 2020 ni zao la makosa hayo. CHADEMA na wenzie wanalipa GHARAMA za kusaliti watu wao waliosimamia itikadi yenye maono.
 
....lakini huyo aliyedhulumu Wakulima wa korosho, wafanyakazi, wafanyabiashara kudharau katiba, kudharau Bunge, kudharau mahakama, kuteka, kutesa na kuua kupitia wasiojulikana, kutumia 2 trillions kununua ndege ambazo zinaingiza hasara ya mabilioni, kuwadhulumu wahanga wa tetemeko bilioni zao kupora 2.7 trillions hazina kama ripoti za CAGs zilivyosema hii GHARAMA kubwa huyo anayejiita jiwe hakustahili kuilipa!!!

Pamoja na kudai kafanya mengi kuliko marais wote waliomtangulia na rais wa wanyonge lakini HAKUTHUBUTU kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki kwa kusimamiwa na tume huru.

JIONGEZE! Acha KUKURUPUKA kuandika PUMBA!
Tuseme ukweli mwaka 2015 upinzani uliounda UKAWA na hasa kinara CHADEMA ulikosea kumfanya Lowassa mgombea wao na kuwatendea uhuni wapambanaji walioufikisha upinzani juu kama Dr. Slaa.

Haya yanayotokea 2020 ni zao la makosa hayo. CHADEMA na wenzie wanalipa GHARAMA za kusaliti watu wao waliosimamia itikadi yenye maono.
 
....lakini huyo aliyedhulumu Wakulima wa korosho, wafanyakazi, wafanyabiashara kudharau katiba, kudharau Bunge, kudharau mahakama, kuteka, kutesa na kuua kupitia wasiojulikana, kutumia 2 trillions kununua ndege ambazo zinaingiza hasara ya mabilioni, kuwadhulumu wahanga wa tetemeko bilioni zao kupora 2.7 trillions hazina kama ripoti za CAGs zilivyosema hii GHARAMA kubwa huyo anayejiita jiwe hakustahili kuilipa!!!

Pamoja na kudai kafanya mengi kuliko marais wote waliomtangulia na rais wa wanyonge lakini HAKUTHUBUTU kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki kwa kusimamiwa na tume huru.

JIONGEZE! Acha KUKURUPUKA kuandika PUMBA!
Ungesoma na kutafakari kwa umakini, ukajitahidi kuondoa chuki au mahaba ungejua KAMA kosa la 2015 lisingefanywa basi huenda huyo usiyempenda hasingemshinda mgombea wa UKAWA ambae ni tofauti na Lowassa.

Tulichofanya tuliomchagua Magufuli 2015 na 2020 (Kama atashinda) ni kumchagua wa afadhali kwa maslahi ya taifa letu kati ya wagombea wenzie wengi waliokosa sifa kwa asilimia nyingi.
 
....lakini huyo aliyedhulumu Wakulima wa korosho, wafanyakazi, wafanyabiashara kudharau katiba, kudharau Bunge, kudharau mahakama, kuteka, kutesa na kuua kupitia wasiojulikana, kutumia 2 trillions kununua ndege ambazo zinaingiza hasara ya mabilioni, kuwadhulumu wahanga wa tetemeko bilioni zao kupora 2.7 trillions hazina kama ripoti za CAGs zilivyosema hii GHARAMA kubwa huyo anayejiita jiwe hakustahili kuilipa!!!

Pamoja na kudai kafanya mengi kuliko marais wote waliomtangulia na rais wa wanyonge lakini HAKUTHUBUTU kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki kwa kusimamiwa na tume huru.

JIONGEZE! Acha KUKURUPUKA kuandika PUMBA!
Mkuu BAK, utabiri wenu vipi! Sasa mmebaki kuomba dua ovu lakini mtarejea kushukuru uamuzi wa WaTz kukipa CCM nafasi nyingine ya kutawala.

Iwapo ilani ya CCM, 2020 ikitekelezwa vizuri, ifikapo 2025 Tanzania itakuwa nchi ya dunia mpya. Nakuwekra uisome kwa umakiniView attachment ILANI YA CCM 2020.pdf
 
Back
Top Bottom