Kuanguka kwa CCM: Kutimilika kwa Unabii...

Hiki kitendo cha mwenyekiti wa ccm rais kikwete kulalamika rushwa ndani ya chaguzi za chama bila yeye kuchukua hatua za muhimu ikiwa ni pamoja kuzifuta chaguzi hizo ni kuzidi kukiingiza kwenye shimo la futi 20 chama hicho..
KWA HILI AMETHIBITISHA KUWA CCM BILA RUSHWA HAIWEZEKANI NA HAWA WANAOPIGA KELELE KINA NAPE HAWANA LOLOTE MAANA VUVUZELA HALIMZUII MCHEZAJI KUCHEZA MPIRA
 
tulishakudharau mwanakijiji, wewe njaa inakusumbua na una double standard

kazi kubwa mwanakijiji amezungumza kutokana na hali halisi anayoiona inaendelea ndani ya ccm. Vile vile hakuna ubaya akazungumzia vyama vingine hali inayojiri huko. La msingi ni yeye kutupa ule ukweli wa mambo na siku ya siku ikitimia mwenye kutaka kuwaongoza watanzania kutoka katika lindi la umaskini atapatikana. Kwa hili sioni double standard unayosema.
 
Ndugu, nina maoni tofauti na kauli ambayo kadiri yangu inaakisi woga usio na msingi wala uthibitisho. Hivi tunapokalia kusema CHADEMA haijajipanga kuchukua uongozi wa nchi tuna maana gani? Je, tunataka tumuone mtu akifanya kazi ya waziri mkuu wakati hajawa bado? Je, lini kikwete, kabla ya kuapisha aliwahi kuonyesha umahiri katika uraisi hata ikawa ndio kigezo cha kumchagua? Na kama ccm inayoongoza sasa ndiyo ilijipanga vizuri kwa kushika dola, kwa hali ilivyo sasa, basi sioni kwanini tuseme chadema haijajipanga. Upo msemo unasema, kanzu haimfanyi mtu kuwa padri au shehe, hawa wanajulikana kanisani au msikitini kwa shughuli zao katika mahali wanapofanyia kazi. Utendaji huu wa akina Mulugo, Pinda, Ngeleja, ndio tuseme ccm ilijipanga jamani? Mimi nadhani katika mabadiliko suala la kuthubutu pia ni la muhimu sana, hatuwezi kusubiri mpaka tuwe na uhakika wa 100% , ambayo haitapatikana, eti ndio tuseme chama kimejipanga. Tuache woga, tuthubutu, kwani hata hiyo chadema ikifanya vibaya, haitakaa hapo milele. Kutafuta evidentia rei kutatugharimu sana na kufanya maisha yetu kuwa magumu zaidi. Twende na hii evidentia credibilitatis, kwasababu nafasi ya kubadili tunayo. Tena basi sasa tunao mchakato wa mabadiliko ya katiba tujilinde kwa kupendekeza kuwa wananchi wapewe fursa ya kuitathmini serikali yao ndani ya kipindi cha utawala wake kwa njia ya kura ya maoni. Hapa atakayeleta gozi gozi anatolewa wakati wowote. Kwa pamoja tutashinda. Naomba kuwakilisha.
 
Sheikh Yahaya mwengine well tukuulize umetumwa ? Kila la kheri we shall see mie sina chama ila nadhani CCM kuanguka ni ngumu sana. Zaidi kwasababu Chadema ni chama hakijajipanga kuchukua nchi hata kidogo. Sana sana kutatokea machafuko tu hasa ya kidini mark my words......

Kwa haya yanayoendelea kutokea...yalipangwa? funguka zaidi mkuu...
 
Makala nzuri MM, ila hujatufafanulia ulitabiri nini 2007, na sasa nini kimetokea/kinatokea.
 
umeshaona hili ni jukwaa la kidding?? just do kidding with your wife and children!!

kwa hiyo hata angesema "Jua Kali" ungesema limuwakie yeye na familia yake.
KUJALIWA UFAHAMU NI THAWABU KUBWA SANA MAISHANI.
 
Ndugu, nina maoni tofauti na kauli ambayo kadiri yangu inaakisi woga usio na msingi wala uthibitisho. Hivi tunapokalia kusema CHADEMA haijajipanga kuchukua uongozi wa nchi tuna maana gani? Je, tunataka tumuone mtu akifanya kazi ya waziri mkuu wakati hajawa bado? Je, lini kikwete, kabla ya kuapisha aliwahi kuonyesha umahiri katika uraisi hata ikawa ndio kigezo cha kumchagua? Na kama ccm inayoongoza sasa ndiyo ilijipanga vizuri kwa kushika dola, kwa hali ilivyo sasa, basi sioni kwanini tuseme chadema haijajipanga. Upo msemo unasema, kanzu haimfanyi mtu kuwa padri au shehe, hawa wanajulikana kanisani au msikitini kwa shughuli zao katika mahali wanapofanyia kazi. Utendaji huu wa akina Mulugo, Pinda, Ngeleja, ndio tuseme ccm ilijipanga jamani? Mimi nadhani katika mabadiliko suala la kuthubutu pia ni la muhimu sana, hatuwezi kusubiri mpaka tuwe na uhakika wa 100% , ambayo haitapatikana, eti ndio tuseme chama kimejipanga. Tuache woga, tuthubutu, kwani hata hiyo chadema ikifanya vibaya, haitakaa hapo milele. Kutafuta evidentia rei kutatugharimu sana na kufanya maisha yetu kuwa magumu zaidi. Twende na hii evidentia credibilitatis, kwasababu nafasi ya kubadili tunayo. Tena basi sasa tunao mchakato wa mabadiliko ya katiba tujilinde kwa kupendekeza kuwa wananchi wapewe fursa ya kuitathmini serikali yao ndani ya kipindi cha utawala wake kwa njia ya kura ya maoni. Hapa atakayeleta gozi gozi anatolewa wakati wowote. Kwa pamoja tutashinda. Naomba kuwakilisha.
Well said mkuu! Umethink logically. Full maevidence. Pokea like yangu.
 
Huu uzi nimeusoma Tz Daima, Shukrani mkuu MM kwa kazi yako. Kwa sasa kila mtanzania anajua kuwa CCM ipo ICU inapumulia Machine

kwataarifa tu ni kwamba kwa nje ccm inaoneka kama iko icu lakini mipango ya ndani ya ccm daima haiwezi kujulikana nilichokishuhudia jana huko Arusha kwenye kambi ya CHADEMA ni kigumu sana kuhadithia asikuambie mtu sisiemu wanajipanga chini kwa chini na wakiibuka utashangaa tutabaki tanalalamika tu kwamba wameeiba kura pesa iliyomwaga Arusha mungu ndiye anayejua na kampeni sasahivi inafanywa nyumba kwa nyumba tena usiku na baadhi ya vijana wameanza kurudi sisiemu kwa siri kubwa ukisikia majungu yanaoyopikwa kwa Godbless Lema ndio utajua kuwa ccm wamejipanga vilivyo.
inaoneka kama hukumu yake inaweza kutupiliwa mbali na ukaitishwa uchagu na ccm wakalitwaa jimbo hata kwa ushindi wa kura Moja.

msifikiri wakati Chadema wakipambana na M4C ccm wamelala ni kama kwenye mchezo wa mpira usifikiri wakati wa mchezo unapofunga mwezako ni kwamba mwezako hachezi

nakuambia ccm wanacheza kuliko unavyofikiri na tusipokuwa makini 2015 ni ccm tena na hatutakuwa na jinsi ya kufanya ila ndio utakuwamwisho wa chame maana watu wengi watakufa moyo

sisiemu wanajipa kwa mengi ikiwemo nguvu ya jeshi na fedha kama uliona juzi jeshi liliiingia mitaani basi ujue hiyo ni sample ya 2015 baada ya uchaguzi nakuambia hawatakubali kutema tonge lililoko mdomo kiurahisi kama tunavyofkiri na haswa ikizingatiwa kuwa huu ni utamaduni wa Afrika na mfano mzuri ni Kenya.
wanajua mwisho wa siku ni kuunda kwa serekali ya umoja wa kitafa kuliko kuachia madaraka, na bado hawajawa tayari ni kwamba tu watatumia kila njia kuhakukisha wanrudi madarakani wanajua kitakachofwata ni baadhi ya wananchi kuingia mitaani na wamekwishakujipanga kwa hilo jinsi ya kuadhibiti ndio maana watu wataongea sana sana na wao hawajali kitu.


Tuache siasa za kwenye net na twende mitaani kuangalia hali halisi sio kwamba sisiemu watashinda bali watangangania madara na kosa la kwanza lilikwisha fanyika kwenye uchaguzi uliopita na wanamejifunza sio kwamba walishinda bali waleweza kuendelea kuongoza na watafanya hivyo hivyo ndio maana wanajitahidi kuoyesha nguvu waliyonayo kuwatisha wananchi ili wengi wetu tusisubutu kuingia mitaa baada ya uchaguzi wa 2015.

unajua ccm wanawapima wananchi kwa mambo mengi kuanzia tunavyo chukulia baadhi ya mabo yanvyotokea sasa hivi kwa mfano ulipotokea mgomo wa madaktari pale ndipo nguvu ya umma ilitakiwa iweze kuact kwa namna ambayo serekali ilngeweza kulishughulikia
hilo swala na kuhakikisha kuwa limekwisha lakini kama kila kitu kimewekwa kiporo na raia tumekaa kimya inamaa hata wakichakachua matokeo kwa mara nyingine watatuzima tu.

UKWELI NI KUWA CCM WANAPAMBANA KUIZIMA CHADEMA NA UPINZANI NA KWA HAPO KWA KIASI FULANI WANAFANIKIWA HAPA ARUSHA WAMEWADHIBITI HAWANA MAALI PA KUFANYIA MKUTANO NA SASA WANAJARIBU KUINGIA KWA VIJANA KUPITIA MLANGO WA HALI YA KIUCHUMI NA KUWAWESHA NA HAPO NDIPO MAALI WATAKAPOFANIIWA, KAMA HAMJUI WANACHOKIFANYA TOKENI NJE MKAANGALIE
 
kwasababu zamani watu walikuwa wanaogopa kutangaza sela za vyama vingine ata kuvaa sale za vyama vyaupinzani lakini sasahivi mambo yamebadilika tunaona makada na wanachama wa ccm wanaanza kuogopa kupita mijini wakiwa wamevaa sale za chama chao ...
 
kwasababu zamani watu walikuwa wanaogopa kutangaza sela za vyama vingine ata kuvaa sale za vyama vyaupinzani lakini sasahivi mambo yamebadilika tunaona makada na wanachama wa ccm wanaanza kuogopa kupita mijini wakiwa wamevaa sale za chama chao ...

Nahitaji viatu. Wapi kuna sale leo?
 
Huu uwezo wa kusema lazima umeutoa wapi kwani kura mnapiga wewe na familia yako kuichukia ccm sawa na kuwachukia wazazi wako.
 
kwasababu zamani watu walikuwa wanaogopa kutangaza sela za vyama vingine ata kuvaa sale za vyama vyaupinzani lakini sasahivi mambo yamebadilika tunaona makada na wanachama wa ccm wanaanza kuogopa kupita mijini wakiwa wamevaa sale za chama chao ...

huo ni ukweli tena ukweli mtupu
 
RAZIMA poti

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom