Kosa lilikuwa la nani hapa?

Kosa lilikuwa la nani hapa?

Ila kuna wanawake viazi kwa kweli?? Wewe unajua hata mzunguko wako kweli Mbona unaonekana mjinga sana🚮
 
Siku moja baada ya kutoka kibaruani, kuna mtu aliniita Bar ya hapo jirani na ofisini kwetu nikaenda hapo tukawa tumekaa nikaagiza chakula nikawa nakula, kuna ndugu yangu akaniambia anakuja kwahiyo nikamwambia apitie hapo kama vipi tuondoke wote, sasa mimi nikawa napiga stori na huyo mbaba.

Nikamaliza kula akaniambia niagize kinywaji nikamwambia sijisikii kunywa pombe kwani huwa zinanisumbua naamka kichwa kizito akaniagizia sijui ni Whisky ile inaitwa Black and White sasa mambo hayo mimi sijazoea nilichanganya na soda nikashindwa kuinywa naiona kali ikabidi niagize tu juisi ya matunda.

Sasa yule ndugu yangu akaja ni wakike so tukawa tupo watatu hapo kwenye meza yetu mimi yule mbaba na huyo ndugu yangu, sasa kuna mbaba mwingine alikuwa yupo kwenye process za kunitongoza nilishamwambiaga huyu ndugu yangu alikuwa anamjua, sasa ndugu yangu alivyofika pale akawa ameniambia mbona fulani nimemuona hapo nyuma yetu na yupo na mdada eeeh! Nikashtuka ikabidi nigeuke kuangalia kweli.

Amekaa na msichana mrembo mweupe, nikatoka nikaenda chooni yule mbaba aliyekuwa amekaa na msichana hapo nyuma akanifata eti umekuja kufanyaje mbona hujaniambia kama unakuja na yule umekaa nae nani, heeeh yaani yeye kajisahau kama yupo na mwanamke mwingine pale, nikamwambia meseji zangu huwa hujibu ndiyo maana sijakwambia na yule ni rafiki yetu tunafahamiana naye. Nikamuuliza na yeye yule aliye naye pale ni nani akajifanya hamjui yupo mwenyewe ila wanaume 😁😁🙌

Mimi nikarudi zangu kukaa nilipokaa mwanzo, huyu mbaba akaja pale akajifanya anasalimia akawa kaingiwa na wasiwasi hadi unamuona kabisa akarudi kwenye meza yake akawa hamsogelei kabisa yule msichana sasa sijui alienda wapi huyo msichana akawa anaongea na wahudumu hadi wanacheka wanagonga na mikono mara akarudi akamuitia usafiri yule mdada akaondoka na yeye akaenda nje kuongea na simu, na mimi na ndugu yangu tukaondoka.

Nilichoshukuru Mungu ni kwamba nimemjua mapema kabla sijampa kwahiyo hakuambulia kitu kabisa.

Ikumbukwe yule mbaba ambaye nilikaa nae mwanzo hakuwa mtu wangu alikuwa ananiitaga tu akiwa anataka kampani na unaweza kukaa nae hata akitokea mtu akaja hapo hawezi kujua kama mpo pamoja nilipata taarifa zake baadae kuwa ni mtu wa mademu sana ndiyo maana anafanya hivyo.
Nitakupata tu
 
Siku moja baada ya kutoka kibaruani, kuna mtu aliniita Bar ya hapo jirani na ofisini kwetu nikaenda hapo tukawa tumekaa nikaagiza chakula nikawa nakula, kuna ndugu yangu akaniambia anakuja kwahiyo nikamwambia apitie hapo kama vipi tuondoke wote, sasa mimi nikawa napiga stori na huyo mbaba.

Nikamaliza kula akaniambia niagize kinywaji nikamwambia sijisikii kunywa pombe kwani huwa zinanisumbua naamka kichwa kizito akaniagizia sijui ni Whisky ile inaitwa Black and White sasa mambo hayo mimi sijazoea nilichanganya na soda nikashindwa kuinywa naiona kali ikabidi niagize tu juisi ya matunda.

Sasa yule ndugu yangu akaja ni wakike so tukawa tupo watatu hapo kwenye meza yetu mimi yule mbaba na huyo ndugu yangu, sasa kuna mbaba mwingine alikuwa yupo kwenye process za kunitongoza nilishamwambiaga huyu ndugu yangu alikuwa anamjua, sasa ndugu yangu alivyofika pale akawa ameniambia mbona fulani nimemuona hapo nyuma yetu na yupo na mdada eeeh! Nikashtuka ikabidi nigeuke kuangalia kweli.

Amekaa na msichana mrembo mweupe, nikatoka nikaenda chooni yule mbaba aliyekuwa amekaa na msichana hapo nyuma akanifata eti umekuja kufanyaje mbona hujaniambia kama unakuja na yule umekaa nae nani, heeeh yaani yeye kajisahau kama yupo na mwanamke mwingine pale, nikamwambia meseji zangu huwa hujibu ndiyo maana sijakwambia na yule ni rafiki yetu tunafahamiana naye. Nikamuuliza na yeye yule aliye naye pale ni nani akajifanya hamjui yupo mwenyewe ila wanaume 😁😁🙌

Mimi nikarudi zangu kukaa nilipokaa mwanzo, huyu mbaba akaja pale akajifanya anasalimia akawa kaingiwa na wasiwasi hadi unamuona kabisa akarudi kwenye meza yake akawa hamsogelei kabisa yule msichana sasa sijui alienda wapi huyo msichana akawa anaongea na wahudumu hadi wanacheka wanagonga na mikono mara akarudi akamuitia usafiri yule mdada akaondoka na yeye akaenda nje kuongea na simu, na mimi na ndugu yangu tukaondoka.

Nilichoshukuru Mungu ni kwamba nimemjua mapema kabla sijampa kwahiyo hakuambulia kitu kabisa.

Ikumbukwe yule mbaba ambaye nilikaa nae mwanzo hakuwa mtu wangu alikuwa ananiitaga tu akiwa anataka kampani na unaweza kukaa nae hata akitokea mtu akaja hapo hawezi kujua kama mpo pamoja nilipata taarifa zake baadae kuwa ni mtu wa mademu sana ndiyo maana anafanya hivyo.
Kuna rafiki yangu alinisimulia hivi.

Alikutana na mchepuko wake Lodge. Kila mchepuko akiwa anatoka kuchepuka. Mchepuko wa kiume (rafiki yangu) anatoka ndani na mwanamke, na mchepuko wa kike unatoka ndani na mwanaume. Hapo wote wamemaliza kutumika.

Mchepuko mwanaume akausalimia mchepuko wake, Mambo vipi? Mchepuko wa kike haukuitikia badala yake ulimzushia varangati mchepuko wa kiume inakuwaje anatoka na mwanamke mwimgine ilihali yeye yupo. Kuona hivyo yule mwanaume na mwanamke michepuko ya michepuko wakala kona. Mchepuko wa kike alimshushia maneno mbofumbofu huyo rafiki yangu, yeye kwa hekima akaamua kukaa kimya ila kuanzia siku hiyo alimwacha hata hajamtafuta wala kupokea simu zake sembuse sms kujibu. Ukawa mwisho.

Wanawake sometimes wanazijua wao akili zao.

Sasa wewe Binti sayuni03 unaona kabisa jamaa ana demu na wewe ulishamkataa halafu unamuuliza huyo nani? Shida ni nini? Nini kilikuwa kinakukereketa
 
Back
Top Bottom