KKKT labariki unywaji wa Pombe

KKKT labariki unywaji wa Pombe

Walutheri pombe hunyweka kama kawaida hakuna katazo wala fundisho la unywaji pombe.Wasiokunywa pombe ni wapentekoste,akitokea kiongozi wa madhehebu ya kipentekoste anashadidia unywaji pombe jamii ya wakristo wa kipentekoste watashangaa sana juu ya fundisho la kunywa pombe.
pombe imeharishwa na wasiojua maandikiko. pombe haijakatazwa isipokuwa kwa sababu maalumu kutoka kwa Mungu, mf. MMama yake na samson, yohana na makuhani walioteuliwa kwa kazi maalumu. Ukusoma zaburi ya 104:14-15 kuna andiko la kujifunza , Yesu mwenyewe kwenye harusi ya kana , Na akiongea na mafarosayo aliwaambia Yohana alikuja kunywa divai mkamwita pepo ila mimi nimekuwa kunywa na kula mkaniita mlevi.. pana tafsiri flani hapa ambapo mtumishi mwenye biblia atatuambia maana niko kwa Gari naelekea Dareda..
 
Nimesoma comment karibu zote na habari nzima. Naona watu wanatetea interest zao tu na hawagusi swali la Msingi. Swali la msingi si kama Askofu fulani au fulani alisema nini kuhusu suala la Unywaji Pombe. Maaskofu ni wanadamu tu ambao ipo siku watasimama mbele za Mungu Muumba kama mimi na wewe wakijibu mashtaka yao ikiwemo waliwaongoza watu kwenda wapi.

Swali la msingi hapa ni kuwa Je Mungu ameruhusu Kunywa Pombe? Na kama akishuka hapo ulipo utakuwa na ujasiri wa kumsogezea Bingwa moja ili muendelee na maongezi? Hili ndilo swali la msingi ambalo wengi hapa wameliacha.

Na katika swali hili, Askofu sio mwenye mamlaka ya kusema ndio wala hapana. Ni Mungu mwenyewe ndiye pekee ana mamlaka hayo. Neno la Mungu lipo wazi kabisa kuwa hataki watu wake wanywe au kuuza pombe. Ndio maana maandiko mengi tu yanakataza unywaji pombe. Nisiyanukuu kwa sasa nikipata muda nitaweka comment inajitegemea.

Kuwasaidia kupata majibu ya hili kama umekuwa confused, kuna mambo mawili ambayo unapaswa ujue Biblia inasema nini au inasapoti/kukataa:
  1. Je Kuna sehemu yoyote Biblia imeruhusu au kusema kuwa Pombe ni kitu kizuri?
  2. Je kuna sehemu yeyote Biblia imekataza pombe na kusema ni kitu kibaya cha kuepukwa?
Ukipata majibu hapo juu utajua msimamo wa Mungu juu ya pombe. Na huo ndio msimamo sahihi ambao hata mbele ya Mungu siku ya ahadi yako ikifika utakuwa na ujasiri wa kusimama na kujitetea kuwa Ulisema wewe Bwana. Vinginevyo msimamo wa dhehebu au askofu wako hautakusaidia siku hiyo!
 
Pombe sio dhambi ulevi ndio dhambi.hata waislamu walikatazwa kunywa pombe kwa sababu dhamani hizo walidhulumiwa Mali zao kwa kununua pombe.so kutotumia pombe ni katazo la wanadamu na si la Mungu
 
Mkuu ungejua imani yangu ,ungejishangaa kwanini umesema hivyo,miaka kadhaa nikisali ukonga hapo kanisa fulan nilienda kushiriki meza ya bwana,ile kumaliza kupiga ule mnvinyo nilipepesuka na hata nikasahau nilipokuwa nimekaa,mpka baada ya muda ndo nikagundua
Utakuwa ulikuwa una hang over ya jana yake..😀😀😀😀

Ungekunywa supu nzito kabla ya kushiriki meza ya Bwana.
 
Ndugu kumbuka utasimama peki ako mbele ya hukumu na hutamwambi Mungu niliambiwa pombe si dhambi maana wao wanajua zaidi maadii ya Ukristo kuliko sisi kumbuka adam alivojitetea lakini aliadhibiwa so hata hawa viongozi wanaweza kukuangamiza bila kujua kila mtu anapaswa kujua kwa undani anachoamini kwa kusoma neno la Mungu, binafsi maana kila mtu atajibu yake so tujiongeze.Pombe ni dhambi maana ina kilevi na walev wote moton period.

Unajua tofauti kati Kilevi na ulevi au Pombe na ulevi?

Kama hujui. Cheki Wasabato wanavyoangaika kukwepa kilevi. Majani ya chai, soda cocacola nk.

Kama unakunya soda Cocacola, majani ya chai nk vina kilevi hivyo.

Hii itakusaidia kidogo.

Ulevi, ujulikanao pia kama uraibu wa pombe, ni ulemavu tegemevu wa kudhuru. Dalili zake ni unywaji pombe kupindukia bila udhibiti pombe licha ya madhara yake hasi kwa afya ya mnywaji,, mahusiano na hadhi yake machoni pa jamii. Kama matatizo mengine ya kiafya, ulevi ni mojawapo ya magonjwa yanayoweza kutibika.neno " ulevi" limetumika kwa muda mrefu tangu kubuniwa mwaka wa 1849 na Magnus Huss, ila katika nyanja ya utabibu istilahi hii iligeuzwa kuwa "utumiaji pombe vibaya" na " utegemezi pombe" katika miaka ya 1980 DSM III.Aidha mwaka wa 1979 kamati ya wataalamu ya Shirika la Afya Duniani haikupendelea kutumika kwa neno "ulevi" kama istilali ya kiafya, huku ikipendekeza dalili za "utegemezi pombe". Katika karne ya 19 na mapema karne ya 20, utegemezi pombe uliitwa dipsomania kabla ya kubatilishwa kuwa ulevi"

Source: wikipadia.

Bila shaka utakuwa umeelewa.
 
Hasa utapeli na wizi wa sadaka za waumini
hayo ndiyo mahubiri makubwa siku hizi kila kanisa ukienda; mtolee Mungu Zaka na Sadaka, usipotoa una mwibia
unabaki kujiuliza hivi lini Mungu alishawahi kuja na kudai hizo sadaka na zaka?
 
Bado mawili tu watarudi kwenye mstari

1. Heshima na sala kwa mama Bikira Maria

2. Katazo la viongozi wa dini kuwa na familia binafsi tofauti na familia yote ambao ni kanisa
 
Kijana wa mudy umesemaje?
Dini za kuuunga unga ndio zilivyo,jana pombe haramu,leo inafaa,kesho kunywa lakini usinywe sana.
Pombe ina madhara hata kama unatumia kiasi kidogo,kwa afya ya binadamu,ndio maana imeandikwa Pombe ni "hatari kwa afya yako".
Katika uislamu kila kilicho haramu ni kwa waislamu wote,hakuna kutofautiana.
 
Timotheo 5:23 Tokea sasa usinywe maji tuu lakini tumia mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lako......
Hill ni neno la Mungu.
Sasa hizi dhambi za kutungwa na wanadamu msituletee.pombe sio dhambi.ulevi ndio dhambi.kusex sana,kula sana,..ulevi wa kila kitu ndio dhambi.wewe usinywe pombe lakini kumbe unakula sana dhambi yako sawa na mlevi wa pombe.
 
Back
Top Bottom