KKKT labariki unywaji wa Pombe

KKKT labariki unywaji wa Pombe

Mkuu ungejua imani yangu ,ungejishangaa kwanini umesema hivyo,miaka kadhaa nikisali ukonga hapo kanisa fulan nilienda kushiriki meza ya bwana,ile kumaliza kupiga ule mnvinyo nilipepesuka na hata nikasahau nilipokuwa nimekaa,mpka baada ya muda ndo nikagundua
labda ulizidisha kiwango ila kwa vijikombe vidogo vile ambavyo hata watoto wanatumia then wewe ukalewa na kupepesuka kabisa...Inashangaza.
 
Hivi ungepewa habari hiyo, halafu ukaambiwa andika kichwa cha habari baada ya kusoma kweli ungesema KKKT yabariki unywaji wa pombe?

Una tatizo la ziada ndugu
 
Hata shetani lazima amshangae huyo askofu. Hivi hata kwa kuangalia madhara ya pombe kijamii tu haitoshi mtu kuelewa kuwa pombe ni kitu haramu ambacho Mungu mtakatifu anayejali ustawi wa viumbe wake ansingewez kuruhusu pombe kuwa sehemu ya mpango wa chakula au kinywaji kwa viumbe wake. Hii haihitaji kuwa mtaalamu wa Biblia kulielewa bali common sense. Wanaounga mkono unywaji wa pombe ni mateka wa Shetani ambao wamepotoshwa na mafundisho potofu ya kanisa Katoliki na mabinti zake yanayohalalisha pombe kwa kutafsiri Biblia kulingana na tamaa zao.
Leta uthibitisho wa biblia na si maneno yako tu.
 
Hata shetani lazima amshangae huyo askofu. Hivi hata kwa kuangalia madhara ya pombe kijamii tu haitoshi mtu kuelewa kuwa pombe ni kitu haramu ambacho Mungu mtakatifu anayejali ustawi wa viumbe wake ansingewez kuruhusu pombe kuwa sehemu ya mpango wa chakula au kinywaji kwa viumbe wake. Hii haihitaji kuwa mtaalamu wa Biblia kulielewa bali common sense. Wanaounga mkono unywaji wa pombe ni mateka wa Shetani ambao wamepotoshwa na mafundisho potofu ya kanisa Katoliki na mabinti zake yanayohalalisha pombe kwa kutafsiri Biblia kulingana na tamaa zao.
Madhara ya sumu ya panya kwa jamii unayajua?
 
Hata shetani lazima amshangae huyo askofu. Hivi hata kwa kuangalia madhara ya pombe kijamii tu haitoshi mtu kuelewa kuwa pombe ni kitu haramu ambacho Mungu mtakatifu anayejali ustawi wa viumbe wake ansingewez kuruhusu pombe kuwa sehemu ya mpango wa chakula au kinywaji kwa viumbe wake. Hii haihitaji kuwa mtaalamu wa Biblia kulielewa bali common sense. Wanaounga mkono unywaji wa pombe ni mateka wa Shetani ambao wamepotoshwa na mafundisho potofu ya kanisa Katoliki na mabinti zake yanayohalalisha pombe kwa kutafsiri Biblia kulingana na tamaa zao.
kwani shetani uliwahi kumwona, yuko sahihi naunga mkono hoja
 
Hata shetani lazima amshangae huyo askofu. Hivi hata kwa kuangalia madhara ya pombe kijamii tu haitoshi mtu kuelewa kuwa pombe ni kitu haramu ambacho Mungu mtakatifu anayejali ustawi wa viumbe wake ansingewez kuruhusu pombe kuwa sehemu ya mpango wa chakula au kinywaji kwa viumbe wake. Hii haihitaji kuwa mtaalamu wa Biblia kulielewa bali common sense. Wanaounga mkono unywaji wa pombe ni mateka wa Shetani ambao wamepotoshwa na mafundisho potofu ya kanisa Katoliki na mabinti zake yanayohalalisha pombe kwa kutafsiri Biblia kulingana na tamaa zao.
Unazungumzia madhara ya pombe au madhara ya Ulevi?
 
Juzi nilialikwa kwenye. Misa moja huko shinyanga,ilikuwa ikifanyikia nyumbani kwa mtu! Basi baada ya Misa ukawadia wasaa wa misosi na vinywaji,baada ya mlo vijana wakaanza kusambaza vinywaji mchanganyiko,pale mbele kwenye meza kuu alikuwepo padri,zikapelekwa kreti mbili za bia,padri akafunuliwa chupa ya Safari lager! Akaipiga paaaaap!! Ikabaki nusu! Akairudia tena paaap!! Ikawa empty!! Jamaa aliyeandaa Misa hiyo akanniita nikajumuike nao hapo mbele nikamwambia tu asante mkuu!!japo nnnnilikuwa natamani ila nisingekuwa comfortable kuchapa kinywaji na mtumishi wa Mungu.
Wewe ndio mnafiki wa kutupwa....Inaonesha wewe ni mnywaji wa pombe ila mbele ya watu hujifanya hunywi ila mafichoni unakunywa vizuri tuu...

Pombe haijawai kukatazwa sehemu yoyote kwenye maandiko Matakatifu
 
KKKT labariki unywaji wa Pombe

ASKOFU Mkuu wa zamani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, amebariki rasmi unywaji wa pombe katika kanisa hilo kongwe nchini, anaripoti Mwandishi Wetu.

Akizungumza katika mkutano wa 33 wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, wiki iliyopita, huko Seminari ya Kisarawe, mkoani Pwani, Askofu Malasusa amesema, ” katazo la unywaji wa pombe lililetwa na wamisionari, lakini pombe kama pombe haina tatizo.”

Askofu Dk. Malasusa, ndiye askofu mkuu wa kanisa la KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani. Askofu Dk. Malasusa alikuwa akikamilisha majibu yaliyotolewa na Askofu Keshomshahara wa kanisa hilo, Dayosisi ya Bukoba aliyoyatoa kwa swali lilioulizwa na Prof. Mjema wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Katika swali lake, Prof. Mjema alihoji, nafasi ya pombe katika dhana ya Mtume Paulo anapozungumzia kutiwa unajisi kwa vyakula na vinywaji wanavyokunywa wakristo.
Alitaka kupata ufafanuzi wa msiamo wa kanisa juu ya msemo wa “kimuingiacho mtu na kimtokacho mtu.” Awali katika majibu yake, Askofu Keshomshahara amesema, “pombe ni kinywaji tu kama vinywaji na vyakula vingine” na kwamba pombe inapaswa kutumiwa kwa kiasi na kwamba “hata sakramenti takatifu ya Meza ya Bwana inayotumika kanisani mwao ni pombe.”

Baada ya majibu hayo, ndipo Askofu Dk. Malasusa aliposisitiza kuwa makatazo ya pombe kanisani ni “busara ya wamisionari wa kwanza walioleta injili Afrika baada ya kuona Waafrika walikuwa wakilewa bila kiasi na kukosa ustaarabu.”
Aliendelea kusisitiza kuwa “pombe itumike kwa kiasi na hasa kwa wakristo wachanga.”

Majibu hayo ya maaskofu yaliwachanganya wajumbe wengi na kusababisha mijadala baada ya mkutano. Mjumbe mmoja aliyeongea na gazeti hili huku machozi yakimlenga anasema, “nimesikitika sana kuona maaskofu wetu wanalipotosha kanisa. Hivi kweli sakramenti ni pombe?” Dayosisi ya Mashariki na Pwani kupitia katiba yake, inapiga marufuku wazee wa kanisa kutomiliki vitega uchumi vinavyouza pombe.

Aidha, sherehe zote za kanisa haziruhusiwi kuwa na pombe huku baadhi ya waumini wakipewa adhabu na wachungaji wao kwa kunywa pombe au kufanya biashara ya pombe. Msimamo wa maaskofu hawa wawili unaliweka kanisa Zima la KKKT katika njiapanda ya kulifafanua jambo hili huku waumini wengi wakitishia kuhamia makanisa ya kiroho kukimbia upotoshaji wa wazi wa maakofu wa KKKT. Mkutano huo wa 33 ulijaa vitimbi vingi vinavyoonyesha dayosisi hiyo haiko shwari.

Akiongea kwa uchungu kwenye mkutano huo, Mchungaji wa kanisa hilo usharika wa Kigogo, jijini Dar es Salaam, Richard Ananja alimtaka Askofu Dk. Malasusa kuachia kiti mara moja kwa kuwa amepoteza sifa kwa kashfa za ngono zinazomkabili.

Amesema Dk. Malasusa anakabiliwa na tuhuma nzito za matumizi ya madaraka, uvujaji wa fedha za dayosisi, hujuma kwa Benki ya Maendeleo, kugushi vyeti ya elimu, ukabila, chuki na visasi kwa wachungaji.

Hivyo basi, ili kulinda hadhi na heshima ya kanisa na yeye binafsi, ni vema Askofu Malasusa “akaachia ngazi kwa hiari, badala ya kusuburi kufukuzwa.”
Hoja hiyo ilipozwa na katibu mkuu wa Dayosisi hiyo, Godfrey Nkini aliyedai kuwa kamati ya maadili inashughulikia tuhuma hizo.

Siku moja kabla ya kufungwa kwa mkutano, mchungaji wa kanisa la KKKT, Usharika wa Kibaha, Amani Lyimo katika mahubiri ya ibada ya asubuhi, aliushambulia utendaji wa Askofu Dk. Malasusa kuwa ni wa uonevu, usijali kweli, uliojaa udhalimu, ubabe na matumizi mabaya ya madaraka.
Amesema uongozi wa Dk. Askofu Malasusa unakomoa watu kuliko uongozi wowote uliopita katika dayosisi hiyo.

Kabla ya kufungwa kwa mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati ya maadili wa dayosisi hiyo, Ibrahim Kaduma, alidai kuwa tuhuma juu ya Askofu Dk. Malasusa, si za kweli na zinachochewa na gazeti moja (hakulitaja) lakini akadai ni chuki ya uislamu dhidi ya kanisa.

Maelezo hayo yalipingwa na wachungaji wengi hali inayoonyesha kuwa Askofu Malasusa hayuko vizuri na wachungaji wake. Wachungaji walidai kamati imeleta “majibu mepesi” kwa tuhuma za ngono zinazomkabili Dk. Malasusa na kwamba kinachobakia sasa wao kumwaga hadharani yaliyositiriwa kulilinda kanisa, alisisitiza mmoja wa wachungaji wa kanisa hilo mwenye taaluma ya sheria.

Katika hatua nyingine, ajenda ya marekebisho ya katiba ya dayosisi hiyo, iliburuzwa ili kumwepusha Askofu Malasusa na hoja ya ukomo wa madaraka yake. Siku za karibuni, Askofu Dk. Malasusa amekumbwa na tuhuma mfululizo, zikiwamo matumizi mabaya ya madaraka, ngono na ubaguzi.

Hata hivyo, Dk. Malasusa amekuwa akijibu tuhuma hizo kwa kuwanyooshea kidole waumini wanaotoka mikoa ya Kaskazini kuwa wanamsakama kwa vile katika uchaguzi mkuu uliyopita, limuunga mkono Rais Magufuli na kumsaliti swahiba wake wa miaka mingi, Edward Lowassa.

Chanzo: Mwanahalisionline
Sema una visa na Malasusa..kichwa cha habari na maelezo ya tuhuma wapi na wapi..nilitegemea ueleze alivyotetea uhalali wa pombe..umeishia kuzungumzia tuhuma..Mungu anakuona...
 
Wrong, askofu Malasusa ana hofu ya Mungu hii sio kauli yake
 
Kwenye Dini ya Kikristo hasa kwa viongozi wakuu kama maaskofu. Matamko yao yana leta adhali sana katika ustawi au kutokustawi kwa kanisa.

Watu hawajui Theolojia ya dini ya kikristo(Elimu) ni kitu kizuri sana lakini pia ni kibaya sana.

wachungaji wanaoenda nje kusomea elimu ya dini (theolojia) ukiwauliza watakwamba kwamba wanapata wakati mgumu sana kuhusu baadhi ya mafundisho katika Biblia.

Kunywa Pombe sio dhambi ila ni maadili ya kanisa waliyojiwekea. Yesu alipo tengeneza Divai SIO juice Bali Ilikuwa POMBE. WENGI wachungaji wanahangaika bure na hili kwa kukwepesha kwepesha ilikuwa ni pombe.

Kunywa Pombe kwa waamini sio dhambi na bado huyu mtu atakwenda mbinguni. shida ni kwamba pale mtu anapoitumikia pombe inapochukua nafasi ya Mungu.(kwa kutokufanya mapenzi ya Mungu kwa sababu ya Pombe).

Katika Biblia hauna sehemu palipokatazwa kunywa pombe isipokuwa kuna maangalizo tu kwa watu maalum kama viongozi wa kanisa wasitumie pombe kwa maana hawatakuwa sahihi katika kutoa maamuzi (Si unakumbuka Mzee wa Upako angekuwa mtu mwingine ambaye hana cheo au si kiongozi wa dini lilikuwa ni jambo dogo sana).

Hata hivyo waamini ndiyo wanaharibu kanisa. Siku moja Askofu mmoja aliwahi kusema ushoga ni dhambi lakini si tofauti na dhambi zingine kama uongo, ugomvi,uuaji nk, kwa hiyo waacheni mashoga wawe makanisani watabadirika kama waongo na wafiraji na waasherati na wazinzi wanavyobadilika wakiwa makanisani" Huyo askofu alisuswa mpaka alipofariki wakimshutumu ni mwenye dhambi kwa kutamka hivyo.
u
Nilitaka kusema tangu. Tuwasililize viongozi wetu wa dini, kwa maana wao wanajua zaidi maadii ya Ukristo kuliko sisi.

NB: Sishangai kabisa nikiona kanisa la KKKT likikatika vipande vipandi kwa sababu viongozi wao wote wanapelekwa kusoma elimu ya Dini Ujerumani ambapo hao ualimu wao hawamwamini Mungu, inaamini ushoga na haki za binadamu.
Ndugu kumbuka utasimama peki ako mbele ya hukumu na hutamwambi Mungu niliambiwa pombe si dhambi maana wao wanajua zaidi maadii ya Ukristo kuliko sisi kumbuka adam alivojitetea lakini aliadhibiwa so hata hawa viongozi wanaweza kukuangamiza bila kujua kila mtu anapaswa kujua kwa undani anachoamini kwa kusoma neno la Mungu, binafsi maana kila mtu atajibu yake so tujiongeze.Pombe ni dhambi maana ina kilevi na walev wote moton period.
 
Back
Top Bottom