KKKT labariki unywaji wa Pombe

KKKT labariki unywaji wa Pombe

Chunga hiyo kauli yako....
Maandiko ya biblia yanasema tokeni huko mkatengwe nao.Utukufu wa Mungu hauwezi kuonekana mpaka wamejitenga.Haiwezekani watu wakamuamudu Mungu katika mifumo miwili ya mafundisho yanayopingana.Kumbuka kuwa kuna suala la ubatizo wa maji mengi.
 
Makanisa haya shida tupu... Huku wanaimiza uzinzi watu waoe wanawake wengi, kule bia, hapa ushoga, pale kitimoto na kuitana baba watakatifu. Ukirudi riverside anatwika viroba... Yule wa kufufua nae siasa kibao, katortoise ndo hivyo tena.
Watu na imani zao.
 
nadhani mleta mada kama una shida na malasusa vile na sio unywaji pombe.
mkuu wakati mwingine ni vema kutoka nje ya box na kuwa realistic. Mleta mada hana tatizo na Malasusa, yeye ameleta habari kama ilivyoandikwa na Mwanahalisi, hivyo kama ni shida, gazeti ndio lenye tatizo na Malasusa, ndilo ulilopaswa kulishushia lawama....by the way uongo huondoshwa na ukweli ni vema ukaweka ukweli unaoujua!!
 
Maandiko ya biblia yanasema tokeni huko mkatengwe nao.Utukufu wa Mungu hauwezi kuonekana mpaka wamejitenga.Haiwezekani watu wakamuamudu Mungu katika mifumo miwili ya mafundisho yanayopingana.Kumbuka kuwa kuna suala la ubatizo wa maji mengi.
Wewe ni mbumbumbu...
 
Tutaskia mengi San siku hizi za mwisho
 
Thimotheo 5:23 hai justfy kwamba Divai aliyozungumzia Paul ni hii ya mvinyo.Kumbuka divai ilikuwa inatumika kutibu watu kwa kuwapaka vidonda.ref.Msamaria mwema
Biblia hajaeleza bayana ni divai gani Yesu alitengeneza kwenye harusi ya kana.Labda niulize sigara kwanini inazuiliwa wakati haijaandikwa.Mhimu madhara yake kwa mtu.Galat 5:19 anasema na mambo yanayofanana na hayo.Hivyo walevi msipindishe neno.
 
U
KKKT labariki unywaji wa Pombe

ASKOFU Mkuu wa zamani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, amebariki rasmi unywaji wa pombe katika kanisa hilo kongwe nchini, anaripoti Mwandishi Wetu.

Akizungumza katika mkutano wa 33 wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, wiki iliyopita, huko Seminari ya Kisarawe, mkoani Pwani, Askofu Malasusa amesema, ” katazo la unywaji wa pombe lililetwa na wamisionari, lakini pombe kama pombe haina tatizo.”

Askofu Dk. Malasusa, ndiye askofu mkuu wa kanisa la KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani. Askofu Dk. Malasusa alikuwa akikamilisha majibu yaliyotolewa na Askofu Keshomshahara wa kanisa hilo, Dayosisi ya Bukoba aliyoyatoa kwa swali lilioulizwa na Prof. Mjema wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Katika swali lake, Prof. Mjema alihoji, nafasi ya pombe katika dhana ya Mtume Paulo anapozungumzia kutiwa unajisi kwa vyakula na vinywaji wanavyokunywa wakristo.
Alitaka kupata ufafanuzi wa msiamo wa kanisa juu ya msemo wa “kimuingiacho mtu na kimtokacho mtu.” Awali katika majibu yake, Askofu Keshomshahara amesema, “pombe ni kinywaji tu kama vinywaji na vyakula vingine” na kwamba pombe inapaswa kutumiwa kwa kiasi na kwamba “hata sakramenti takatifu ya Meza ya Bwana inayotumika kanisani mwao ni pombe.”

Baada ya majibu hayo, ndipo Askofu Dk. Malasusa aliposisitiza kuwa makatazo ya pombe kanisani ni “busara ya wamisionari wa kwanza walioleta injili Afrika baada ya kuona Waafrika walikuwa wakilewa bila kiasi na kukosa ustaarabu.”
Aliendelea kusisitiza kuwa “pombe itumike kwa kiasi na hasa kwa wakristo wachanga.”

Majibu hayo ya maaskofu yaliwachanganya wajumbe wengi na kusababisha mijadala baada ya mkutano. Mjumbe mmoja aliyeongea na gazeti hili huku machozi yakimlenga anasema, “nimesikitika sana kuona maaskofu wetu wanalipotosha kanisa. Hivi kweli sakramenti ni pombe?” Dayosisi ya Mashariki na Pwani kupitia katiba yake, inapiga marufuku wazee wa kanisa kutomiliki vitega uchumi vinavyouza pombe.

Aidha, sherehe zote za kanisa haziruhusiwi kuwa na pombe huku baadhi ya waumini wakipewa adhabu na wachungaji wao kwa kunywa pombe au kufanya biashara ya pombe. Msimamo wa maaskofu hawa wawili unaliweka kanisa Zima la KKKT katika njiapanda ya kulifafanua jambo hili huku waumini wengi wakitishia kuhamia makanisa ya kiroho kukimbia upotoshaji wa wazi wa maakofu wa KKKT. Mkutano huo wa 33 ulijaa vitimbi vingi vinavyoonyesha dayosisi hiyo haiko shwari.

Akiongea kwa uchungu kwenye mkutano huo, Mchungaji wa kanisa hilo usharika wa Kigogo, jijini Dar es Salaam, Richard Ananja alimtaka Askofu Dk. Malasusa kuachia kiti mara moja kwa kuwa amepoteza sifa kwa kashfa za ngono zinazomkabili.

Amesema Dk. Malasusa anakabiliwa na tuhuma nzito za matumizi ya madaraka, uvujaji wa fedha za dayosisi, hujuma kwa Benki ya Maendeleo, kugushi vyeti ya elimu, ukabila, chuki na visasi kwa wachungaji.

Hivyo basi, ili kulinda hadhi na heshima ya kanisa na yeye binafsi, ni vema Askofu Malasusa “akaachia ngazi kwa hiari, badala ya kusuburi kufukuzwa.”
Hoja hiyo ilipozwa na katibu mkuu wa Dayosisi hiyo, Godfrey Nkini aliyedai kuwa kamati ya maadili inashughulikia tuhuma hizo.

Siku moja kabla ya kufungwa kwa mkutano, mchungaji wa kanisa la KKKT, Usharika wa Kibaha, Amani Lyimo katika mahubiri ya ibada ya asubuhi, aliushambulia utendaji wa Askofu Dk. Malasusa kuwa ni wa uonevu, usijali kweli, uliojaa udhalimu, ubabe na matumizi mabaya ya madaraka.
Amesema uongozi wa Dk. Askofu Malasusa unakomoa watu kuliko uongozi wowote uliopita katika dayosisi hiyo.

Kabla ya kufungwa kwa mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati ya maadili wa dayosisi hiyo, Ibrahim Kaduma, alidai kuwa tuhuma juu ya Askofu Dk. Malasusa, si za kweli na zinachochewa na gazeti moja (hakulitaja) lakini akadai ni chuki ya uislamu dhidi ya kanisa.

Maelezo hayo yalipingwa na wachungaji wengi hali inayoonyesha kuwa Askofu Malasusa hayuko vizuri na wachungaji wake. Wachungaji walidai kamati imeleta “majibu mepesi” kwa tuhuma za ngono zinazomkabili Dk. Malasusa na kwamba kinachobakia sasa wao kumwaga hadharani yaliyositiriwa kulilinda kanisa, alisisitiza mmoja wa wachungaji wa kanisa hilo mwenye taaluma ya sheria.

Katika hatua nyingine, ajenda ya marekebisho ya katiba ya dayosisi hiyo, iliburuzwa ili kumwepusha Askofu Malasusa na hoja ya ukomo wa madaraka yake. Siku za karibuni, Askofu Dk. Malasusa amekumbwa na tuhuma mfululizo, zikiwamo matumizi mabaya ya madaraka, ngono na ubaguzi.

Hata hivyo, Dk. Malasusa amekuwa akijibu tuhuma hizo kwa kuwanyooshea kidole waumini wanaotoka mikoa ya Kaskazini kuwa wanamsakama kwa vile katika uchaguzi mkuu uliyopita, limuunga mkono Rais Magufuli na kumsaliti swahiba wake wa miaka mingi, Edward Lowassa.

Chanzo: Mwanahalisionline
Umesikika
 
( مَّثَلُ الْجَنَّةِ الَّتِي وُعِدَ الْمُتَّقُونَ ۖ فِيهَا أَنْهَارٌ مِّن مَّاءٍ غَيْرِ آسِنٍ وَأَنْهَارٌ مِّن لَّبَنٍ لَّمْ يَتَغَيَّرْ طَعْمُهُ وَأَنْهَارٌ مِّنْ خَمْرٍ لَّذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ وَأَنْهَارٌ مِّنْ عَسَلٍ مُّصَفًّى ۖ وَلَهُمْ فِيهَا مِن كُلِّ الثَّمَرَاتِ وَمَغْفِرَةٌ مِّن رَّبِّهِمْ ۖ كَمَنْ هُوَ خَالِدٌ فِي النَّارِ وَسُقُوا مَاءً حَمِيمًا فَقَطَّعَ أَمْعَاءَهُمْ )

محمد (15) Muhammad

Mfano wa Pepo walio ahidiwa wachamngu ina mito ya maji yasiyo vunda, na mito ya maziwa isiyo haribika ladha yake, na mito ya mvinyo yenye ladha kwa wanywao, na mito ya asali iliyo safishwa. Na wao humo watakuwa na kila namna ya matunda, na magh**** kutoka kwa Mola wao Mlezi. Basi hao ni kama watakao dumu Motoni na wakinyweshwa maji yanayo chemka ya kuwakata matumbo yao?


Quran inasema kuna mito ya chang'aa huko peponi na inafaa kunywewa na nani?.
Huko full mipombe.
Bibles inasemaje??

Habakuki 2 : 15 - Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili kuutazama uchi wao!
Biblia inakataa pombe kabisa rafiki
Shekh kwako wewe kinacholevya ni pombe tu??
 
Hii mada ni sensitive sana! Sitaki kwenda deep sana! Nafuatilia mjadala kwa ukaribu!
 
Hata shetani lazima amshangae huyo askofu. Hivi hata kwa kuangalia madhara ya pombe kijamii tu haitoshi mtu kuelewa kuwa pombe ni kitu haramu ambacho Mungu mtakatifu anayejali ustawi wa viumbe wake ansingewez kuruhusu pombe kuwa sehemu ya mpango wa chakula au kinywaji kwa viumbe wake. Hii haihitaji kuwa mtaalamu wa Biblia kulielewa bali common sense. Wanaounga mkono unywaji wa pombe ni mateka wa Shetani ambao wamepotoshwa na mafundisho potofu ya kanisa Katoliki na mabinti zake yanayohalalisha pombe kwa kutafsiri Biblia kulingana na tamaa zao.
Ubarikiwe sana mwana wa Mungu aliyehai
 
Moja ya baraka za kibiblia ni mtu kubarikiwa kwa kuwa na mashamba ya mizabibu inayozaa. Kazi za zabibu ni nini?

Lakini Yesu alitoa mfano wa kuwa yeye ni mzabibu na Baba yake ni mkulima na tawi lisilo zaa atalikata. Zabibu ni zao lililokuwa la thamani kubwa enzi hizo na ndio maana tuna ona Bwana Yesu kujitolea mfano kwa kitu cha thamani ili waliokuwa wakisikiliza mahubiri yake wamuelewe kwa urahisi.

Na uliza tena kazi ya zabibu enzi hizo na sasa ni nini? Je divai ni nini?

Kumbuka kuwa kitu kingine cha thamani na muhimu enzi hizo ni chumvi, na Bwana Yesu alitoa pia mfano wa kuhusu chumvi.

Tusianze kuukimbia ukweli sijui Pentekosti, Wasabato, Jehova Mashahidi nk. Je Biblia haija taja neno divai, divai ni nini? na je inatokana na nini?


Na washawasha!
 
Wee weeww mapyaYaja;please changia madaa TUACHE SISI NA KANISA LETU AU UMETMWA,???SISI NDIYO WAFIA DINI YETU,KATOLIKI,KAMA NZURI KAMA BAYA NI YETU, BASIII UMENIUZI KWELI STP WA HED,
 
Hata methylated spirit inayotumika katika vidonda leo hii ina some alcohol percentage, sijui unatuambia nini kuhusu hili? Na mfano wa msamaria mwema ulikuwa wa kufikirika hakuwa kitu halisi kilichotokea.

Na washawasha!

Thimotheo 5:23 hai justfy kwamba Divai aliyozungumzia Paul ni hii ya mvinyo.Kumbuka divai ilikuwa inatumika kutibu watu kwa kuwapaka vidonda.ref.Msamaria mwema
Biblia hajaeleza bayana ni divai gani Yesu alitengeneza kwenye harusi ya kana.Labda niulize sigara kwanini inazuiliwa wakati haijaandikwa.Mhimu madhara yake kwa mtu.Galat 5:19 anasema na mambo yanayofanana na hayo.Hivyo walevi msipindishe neno.
 
Tusipende kujustify unywaji pombe kwa reasoning nyepesi hivyo........

Pombe ni haramu na hakuna lugha yoyote utakayoitumia kuihalalisha kuwa ni halali....

Ni vyema Maaskofu hao 2 wakaamua kwa hiyari yao wenyewe kulihama kanisa la KKKT na kuhamia kanisa la mzee wa upako, ili waweze kumjoin huyo Askofu mwenzao katika kupata ile kitu inaitwa bapa.........
ASANTE SANA
 
Watu wanasahau kwamba hata kuzidisha pilau ni dhambi. Pombe kiasi kama kinywaji au chochote si dhambi!
Hao walutheri was Ujerumani wanakunywa pombe. Ndiyo waliotuletea dini yenyewe.

Pombe inawaumiza kichwa
 
Back
Top Bottom