KKKT labariki unywaji wa Pombe

KKKT labariki unywaji wa Pombe

bado kukubali ushoga taratibu tunaelekea huko

Acha hizi akili za rejareja, kuna mcha Mungu asiyejua kuhusu sodoma na gomora, Labda shetani na mawakala wake maana kwao sodoma na gomora ni sifa na utukufu.

Na washawasha!
 
Sasa unashangaa pombe wakati wanafungisha ndoa za mashoga?

Wewe ungejua Bwana Yesu alivyo tutahadharisha kuhusu mambo yatakavyo kuwa kuelekea siku hizi za mwisho wa dunia hii wala usinge andika hiki ulicho kiandika. Sitaki kuamini eti mtu wa aina yako haelewi kwamba shetani anatenda kazi hata ndani ya kanisa.

Na washawasha!
 
Acha hizi akili za rejareja, kuna mcha Mungu asiyejua kuhusu sodoma na gomora, Labda shetani na mawakala wake maana kwao sodoma na gomora ni sifa na utukufu.

Na washawasha!
hata pombe pia ni wakala wa shetani
 
hata pombe pia ni wakala wa shetani

Sio kila pombe ni wakala wa shetani, Bwana Yesu alituamrisha katika chakula cha Bwana kanisani, tufanye hivyo kwa ajili ya kumbukumbu ya mwili na damu yake iliyo mwagika msalabani kwa ajili ya msamaha wa dhambi kwa aliye muamini na kutubu dhambi zake.

Ndio maana nimeuliza hapa divai ni nini? Je Biblia haija taja neno divai? Wote kimya hamna aliye jibu, imepotezewa.

Na Askofu alikuwa sawa aliposema pombe imezuiliwa na wamissionari, kwani kuna amri ya Bwana Yesu aliyowapa wanafunzi wake ya kufunga na kufungulia kitu hapa duniani na kikapata kibali mbinguni. Divai/Pombe inayonywewa kanisani kama sehemu ya chakula cha Bwana kamwe sio na wala haitakaa iwe dhambi.

Divai imetajwa kwenye Biblia hata wakati wa last supper ya Bwana Yesu ambapo ndipo aliitoa hii amri ya kumkumbuka kwa kupitia mkate na divai , sasa kwa nini Mkristo aone aibu/haya kusema kuhusu huu ukweli?

Na washawasha!
 
Sawa ni zipi amri za Yesu? Maana tunajua Bwana Yesu alisema hakuja kuitangua taurati bali kuitimiliza. Kwa nini unamtuhumu Mtume Paulo? Hebu tupe sababu za msingi za kufanya hivyo.

Na washawasha!
Yesu hakuleta Sheria zaidi ni ufafanuzi baada ya watu walikuwa wamekwama fafanuzi na utambuzi... But Sheria za Mungu zinaremain intact.. Paul we have seen na maandiko yake mengi yapo opposite na Maandiko ya Mussa na kuchange Watu from Dini ya uyahudi na kuleta Ukatoliki dini ya wataliano ikachanganywa na Baadhi ya mambo ya kiyahudi ili ionekane dini ya wakati Wa kisasa wenye kukubalisha mambo aliyokataza Mungu ambayo ni magumu kuyashika au kuyafuata ikawa dini ya starehe ila watu wanatakiwa kuelewa Kishika dini na starehe haviendani
 
Labda ni anzie hapa, mimi nime zungumzia kuhusu amri. Wewe umesema sheria. Kuna tofauti kati ya sheria na amri?

Na washawasha!


Yesu hakuleta Sheria zaidi ni ufafanuzi baada ya watu walikuwa wamekwama fafanuzi na utambuzi... But Sheria za Mungu zinaremain intact.. Paul we have seen na maandiko yake mengi yapo opposite na Maandiko ya Mussa na kuchange Watu from Dini ya uyahudi na kuleta Ukatoliki dini ya wataliano ikachanganywa na Baadhi ya mambo ya kiyahudi ili ionekane dini ya wakati Wa kisasa wenye kukubalisha mambo aliyokataza Mungu ambayo ni magumu kuyashika au kuyafuata ikawa dini ya starehe ila watu wanatakiwa kuelewa Kishika dini na starehe haviendani
 
Yesu hakuleta Sheria zaidi ni ufafanuzi baada ya watu walikuwa wamekwama fafanuzi na utambuzi... But Sheria za Mungu zinaremain intact.. Paul we have seen na maandiko yake mengi yapo opposite na Maandiko ya Mussa na kuchange Watu from Dini ya uyahudi na kuleta Ukatoliki dini ya wataliano ikachanganywa na Baadhi ya mambo ya kiyahudi ili ionekane dini ya wakati Wa kisasa wenye kukubalisha mambo aliyokataza Mungu ambayo ni magumu kuyashika au kuyafuata ikawa dini ya starehe ila watu wanatakiwa kuelewa Kishika dini na starehe haviendani
Dah, kazi ipo, kaka unahitaji msaada mkubwa wa kuonyeshwa njia, regeza kongwa ili upate Elimu sahihi ya uhusiano wa Musa, Manabii na Yesu
 
Naamini wale waliokuja kuleta neno ndio walikuwa wanaweka kanuni zao kulingana na eneo. Huku walijua kabisa ulabu ndio chanzo kikuu cha matendo maovu wakaona watafute njia ya kupunguza kwa kuutamka kabisa kuwa ni dhambi kwetu waafrika.
Nasikia hata wahubiri walipoenda kwa Waeskimo Kule kwenye baridi Kali ikaonekana ukiwaambia kuwa dhambi itakupeleka kwenye moto wa milele kwao ni kama unawaambia humo kuna maisha mema kwani wamechoka na baridi hivyo wakaambiwa unatupwa kwenye shimo la barafu na hadi Leo wanaiogopa dhambi kwa sababu za shimo la barafu
 
Nasoma thread huku nakunywa mvinyo taratiib
Naam, kama unaunywa taratibu huku moyoni ukimsifu Mungu kwa kukuwezesha kufika mwaka mpya kwa nini usibarikiwe?
Sio mtu anasema hanywi pombe ni dhambi lakini moyoni kajaa kiburi, masengenyo na chuki, hakika huo ni ubatili mtupu. Ngoja nami nishushie kidogo kamvinyo nipate kuburudisha mwili. Karibu
 
Acheni kumlisha tafsiri yenu ;
Hakuna mahali Askofu ameruhusu pombe kwa Mkristo MTU aliyeokoka

😛ombe bila sheria ya Bwana haina tatizo
 
KKKT labariki unywaji wa Pombe

ASKOFU Mkuu wa zamani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, amebariki rasmi unywaji wa pombe katika kanisa hilo kongwe nchini, anaripoti Mwandishi Wetu.

Akizungumza katika mkutano wa 33 wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, wiki iliyopita, huko Seminari ya Kisarawe, mkoani Pwani, Askofu Malasusa amesema, ” katazo la unywaji wa pombe lililetwa na wamisionari, lakini pombe kama pombe haina tatizo.”

Askofu Dk. Malasusa, ndiye askofu mkuu wa kanisa la KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani. Askofu Dk. Malasusa alikuwa akikamilisha majibu yaliyotolewa na Askofu Keshomshahara wa kanisa hilo, Dayosisi ya Bukoba aliyoyatoa kwa swali lilioulizwa na Prof. Mjema wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Katika swali lake, Prof. Mjema alihoji, nafasi ya pombe katika dhana ya Mtume Paulo anapozungumzia kutiwa unajisi kwa vyakula na vinywaji wanavyokunywa wakristo.
Alitaka kupata ufafanuzi wa msiamo wa kanisa juu ya msemo wa “kimuingiacho mtu na kimtokacho mtu.” Awali katika majibu yake, Askofu Keshomshahara amesema, “pombe ni kinywaji tu kama vinywaji na vyakula vingine” na kwamba pombe inapaswa kutumiwa kwa kiasi na kwamba “hata sakramenti takatifu ya Meza ya Bwana inayotumika kanisani mwao ni pombe.”

Baada ya majibu hayo, ndipo Askofu Dk. Malasusa aliposisitiza kuwa makatazo ya pombe kanisani ni “busara ya wamisionari wa kwanza walioleta injili Afrika baada ya kuona Waafrika walikuwa wakilewa bila kiasi na kukosa ustaarabu.”
Aliendelea kusisitiza kuwa “pombe itumike kwa kiasi na hasa kwa wakristo wachanga.”

Majibu hayo ya maaskofu yaliwachanganya wajumbe wengi na kusababisha mijadala baada ya mkutano. Mjumbe mmoja aliyeongea na gazeti hili huku machozi yakimlenga anasema, “nimesikitika sana kuona maaskofu wetu wanalipotosha kanisa. Hivi kweli sakramenti ni pombe?” Dayosisi ya Mashariki na Pwani kupitia katiba yake, inapiga marufuku wazee wa kanisa kutomiliki vitega uchumi vinavyouza pombe.

Aidha, sherehe zote za kanisa haziruhusiwi kuwa na pombe huku baadhi ya waumini wakipewa adhabu na wachungaji wao kwa kunywa pombe au kufanya biashara ya pombe. Msimamo wa maaskofu hawa wawili unaliweka kanisa Zima la KKKT katika njiapanda ya kulifafanua jambo hili huku waumini wengi wakitishia kuhamia makanisa ya kiroho kukimbia upotoshaji wa wazi wa maakofu wa KKKT. Mkutano huo wa 33 ulijaa vitimbi vingi vinavyoonyesha dayosisi hiyo haiko shwari.

Akiongea kwa uchungu kwenye mkutano huo, Mchungaji wa kanisa hilo usharika wa Kigogo, jijini Dar es Salaam, Richard Ananja alimtaka Askofu Dk. Malasusa kuachia kiti mara moja kwa kuwa amepoteza sifa kwa kashfa za ngono zinazomkabili.

Amesema Dk. Malasusa anakabiliwa na tuhuma nzito za matumizi ya madaraka, uvujaji wa fedha za dayosisi, hujuma kwa Benki ya Maendeleo, kugushi vyeti ya elimu, ukabila, chuki na visasi kwa wachungaji.

Hivyo basi, ili kulinda hadhi na heshima ya kanisa na yeye binafsi, ni vema Askofu Malasusa “akaachia ngazi kwa hiari, badala ya kusuburi kufukuzwa.”
Hoja hiyo ilipozwa na katibu mkuu wa Dayosisi hiyo, Godfrey Nkini aliyedai kuwa kamati ya maadili inashughulikia tuhuma hizo.

Siku moja kabla ya kufungwa kwa mkutano, mchungaji wa kanisa la KKKT, Usharika wa Kibaha, Amani Lyimo katika mahubiri ya ibada ya asubuhi, aliushambulia utendaji wa Askofu Dk. Malasusa kuwa ni wa uonevu, usijali kweli, uliojaa udhalimu, ubabe na matumizi mabaya ya madaraka.
Amesema uongozi wa Dk. Askofu Malasusa unakomoa watu kuliko uongozi wowote uliopita katika dayosisi hiyo.

Kabla ya kufungwa kwa mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati ya maadili wa dayosisi hiyo, Ibrahim Kaduma, alidai kuwa tuhuma juu ya Askofu Dk. Malasusa, si za kweli na zinachochewa na gazeti moja (hakulitaja) lakini akadai ni chuki ya uislamu dhidi ya kanisa.

Maelezo hayo yalipingwa na wachungaji wengi hali inayoonyesha kuwa Askofu Malasusa hayuko vizuri na wachungaji wake. Wachungaji walidai kamati imeleta “majibu mepesi” kwa tuhuma za ngono zinazomkabili Dk. Malasusa na kwamba kinachobakia sasa wao kumwaga hadharani yaliyositiriwa kulilinda kanisa, alisisitiza mmoja wa wachungaji wa kanisa hilo mwenye taaluma ya sheria.

Katika hatua nyingine, ajenda ya marekebisho ya katiba ya dayosisi hiyo, iliburuzwa ili kumwepusha Askofu Malasusa na hoja ya ukomo wa madaraka yake. Siku za karibuni, Askofu Dk. Malasusa amekumbwa na tuhuma mfululizo, zikiwamo matumizi mabaya ya madaraka, ngono na ubaguzi.

Hata hivyo, Dk. Malasusa amekuwa akijibu tuhuma hizo kwa kuwanyooshea kidole waumini wanaotoka mikoa ya Kaskazini kuwa wanamsakama kwa vile katika uchaguzi mkuu uliyopita, limuunga mkono Rais Magufuli na kumsaliti swahiba wake wa miaka mingi, Edward Lowassa.

Chanzo: Mwanahalisionline
Aagh! Huyu muandika mada amelewa. Shit!
 
naona wakubwa wanatumia mitandao na magazeti kumalizana mada imeanza vizuri kuhnusu pombe ghafla zikaanza tuhuma nzito za mtu mmoja je mtoa mada unataka kutuaminisha kuwa mabaya hayo uliyoyasema juu ya askofu yamesababishwa na kunywa kumya pombe kupita kiasi au maana sielewi tuhuma za ngono na matumizi mabaya ya madaraka zimeingiaje hapa?
Je siyo kwamba mdoa mada upo kazini yaani kuna upande umekulipa ili kushambulia upande mwingine na katika mashambulizi yako kwa askofu malasusa hujaonesha hata mazuri yake Je kwa miaka yote hiyo kafanya mabaya tu? hebu tuwekee na mazuri yake kisha tuyapime .
maana hii mitandao kuna mtu mmoja alikuwa anaitwa Dr. Ramadhani dau alishambuliwa sana humu kwenye mitandao na tukaamini ni mtu mbaya na mchafu kabisa asiyefaa kwa jamii leo ni balozi na hakuna kesi yoyote iliyofunguliwa zidi yake na kama angekuwa na ubaya huyu mzee wa kukurupuka asingemvumilia , hivyo hivyo kwa lowasa tangu miaka hiyo tunaambiwa ni fisadi lakini hakuna hata siku kapelekwa mahakamani.
tusikubali kutumika kushambulia wengine hata kama umeahidiwa dongo nzuri ....... tunza utu wako.
 
Back
Top Bottom