KKKT labariki unywaji wa Pombe

KKKT labariki unywaji wa Pombe

Kasomeni maoni ya Mungu kuhusu Askofu na shemasi wanapaswa kuwa watu wa namna gani. Hasa pale anapogusia unywaji wa kileo. 1Timotheo 3:1-8.
 
2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;

1 Timotheo 3 :2

3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

1 Timotheo 3 :3

8 Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.

1 Timotheo 3 :8
 
Ulevi ni mbaya ...kama unajua kunywa kwako Pombe kunakupelekea kwenye dhambi acha kabisa au kunywa kiasi ambacho utamudu kudhibiti matendo yako. Hatuwezi kupiga marufuku bodaboda kwavile zinaua sana kwa sababu ya uzembe wa madereva....hapo tatizo bodaboda au dereva? Hapo uweke sheria kudhibiti bodaboda au madereva wazembe?
 
duh,hahaaaaa aya wenye din yenu polen sana ila tafuten ukwel juu ya din zenu nadhan mtaupata tu ukwel,..prof, mjema nadhan ashaanza kujua na kubain ukwel ndo mana akauliza juu la swali kubwa na zito juu ya vinywaji,na vyakula ktk din zenu...prof mjema tafuta ukwel mung atakuongoa zaid
 
KKT walishamaliza uhasama na RC kwa kukubali kuwa mafundisho ya Luther yalikuwa na makosa na tofauti ya uelewa juu ya injili! Hivyo mwaka 2017 KKT, RC na Makanisa washirika wataanzimisha jublei ya 50yrs tangu kushuka malikia wa patmo( for RC), 500yrs tangu martin Luther kujitenga na RC, jublei tangu KKT na RC kumaliza uhasama ( hii ni ya ajabu kwani jublei hii ni ya chini ya 25yrs) n.k Kwa kifupi wataanzimisha jublei kama 8! Na jarida lishatolewa kwa ajili ya Mafundisho! Kwahiyo si ajabu kuona KKT wakianza kufundisha mafundisho yenye misingi ya RC na kuacha yale ya Luther!
Ni KKKT(Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania) sio KKT
 
Bora waruhusu hadharani sio yale mambo wanakuwa na sherehe mngungaji au mwinjilisti akiwepo kileo kinafichwa kwanza hadi aondoke ndio wanatoa kwa wageni unafiki mtupu unakuwa unamficha nani sasa Mungu au hao watumishi?
 
Full mchanganyiko..na ukweli utaeleweka....mm binafsi...pombe ni kama kinywaji tu...sema ukinywa ukazidiwa, akili zikaruka ukaanza kukwaza watu na Mungu wapo hapo ndo tatizo lilipo...mtu anaekunywa pombe akalewa ni sawasawa na mtu aliekula chakula na kuvimbiwa.....POMBE si dhambi lkn ni mzizi wa dhambi..inaweza kusababisha ukatenda dhambi..kwa maoni yangu mtu akinywa pombe akalewa chakali..then akaingia kwake akalala mpaka asubuhi bila kufanya chochote..hana dhambi....Lkn akinywa akaanza tukana watu, ugomvi, uzinzi n.k hapo ndo dhambi...Hivyo bac kila mtu ajipimie..ukionwa ukipuga glass moja...inakua shida achana na pombe..but kama ukinywa na aman inakuwepo..hamna shida
 
Walutheri pombe hunyweka kama kawaida hakuna katazo wala fundisho la unywaji pombe.Wasiokunywa pombe ni wapentekoste,akitokea kiongozi wa madhehebu ya kipentekoste anashadidia unywaji pombe jamii ya wakristo wa kipentekoste watashangaa sana juu ya fundisho la kunywa pombe.
Ongezea kabisa Na hii......Na wale wanao amini ya kwamba Yesu Kristo ni bwana na Mwokozi wa maisha yetu.....hao pia watashangaa
 
Mtu yeyote anywaye pombe kajivua Ukristo ....kimsingi katika Ile vita kuu ya Rohoni huyu ni mpagani tu...someni wagalatia 5:13-26...Na muwe na sikukuu iliyo njema..ya ujio wa Mwokozi Yesu..mamlaka tuliyoporwa Eden kwa jina lake tunayo sasa.....Amina
 
so tatizo ni pombe au malasusa?...
Inapotokea kiongozi anashadidia pombe ni tatizo.Hakupaswa kuzungumzia habari ya pombe.Hii ikiachwa ipite tu ataibuka kiongozi mwingine na kusema kuoa wanawake wengi haina shida na maandiko yapo kutetea hoja yake.Viongozi wa namna hii huleta utata mkubwa sana kwa jamii wanazoziongoza
 
Unaonekana kuwa na uelewa mdogo au bifu kwa Askofu Dr. Malasusa

Kilichokataliwa katika Biblia Takatifu ni "ULEVI"

ULEVI hata wa Chakula kingi ni dhambi kabisa kama ilivyo Uzinzi, Wizi n.k

Unaweza kunionesha mstari wowote katika biblia unaokataza POMBE?
Watu wengi hawaelewi maandiko matakatifu. Wanakariri tu ili mradi nao waonekane wamo. Unyenyekevu ni asset kubwa sana ambayo wengi tunaikosa kwenye dunia ya leo
 
Back
Top Bottom