KKKT labariki unywaji wa Pombe

KKKT labariki unywaji wa Pombe

Tusome mwanzo 9 kuanzia mstrari wa 20 mpaka ule wa 29 tuone jinsi pombe ilivyomtia aibu Nuhu na baadaye akapata hasira na kumlaani mwanae Hamu.
Kizazi cha huyo hamu kipo mpaka sasa;

20.Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;

21.akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.

22.Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.

23.Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.

24.Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.

25.Akasema,Na alaaniwe Kaanani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.

26.Akasema,Na atukuzwe Bwana,Mungu wa Shemu;Na kaanani awe mtumwa wake.

27.Mungu akamnafisishe Yafethi,Na akae katika hema za Shemu; Na kaanani awe mtumwa wake.

28.Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.

29. Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
INA maana waafrika ndio watoto Wa Hamu wana wa caanan?
 
Tuambie tofauti ya divai iliyo mlewesha Nuhu na ile ya Bwana Yesu aliyo ikuta katika harusi ya kana na ilipo isha akafanya muujiza wa kutengeneza divai iliyo njema. Jiulize zaidi maji na vyombo vilivyo tumika katika huu muujiza uliofanywa na Bwana Yesu hapo harusini kana vilikuwa kwa ajili ya nini? Ndio mjue Neno la Mungu sio lelemama.

Na washawasha!




Tusome mwanzo 9 kuanzia mstrari wa 20 mpaka ule wa 29 tuone jinsi pombe ilivyomtia aibu Nuhu na baadaye akapata hasira na kumlaani mwanae Hamu.
Kizazi cha huyo hamu kipo mpaka sasa;

20.Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;

21.akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.

22.Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.

23.Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.

24.Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.

25.Akasema,Na alaaniwe Kaanani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.

26.Akasema,Na atukuzwe Bwana,Mungu wa Shemu;Na kaanani awe mtumwa wake.

27.Mungu akamnafisishe Yafethi,Na akae katika hema za Shemu; Na kaanani awe mtumwa wake.

28.Na Nuhu akaishi baada ya ile gharika miaka mia tatu na hamsini.

29. Siku zote za Nuhu zilikuwa miaka mia kenda na hamsini, akafa.
 
Nimesoma gazeti la leo, askofu amepinga kubariki wala kuruhusu pombe kwa waumini wake. Tena wameandika dayosisi inajipanga kuwashtaki Mwanahalisis kwa kumchafua. Kama mtakumbuka mwanahalisi wamekuwa wakiandika habari mbaya kila mara kuhusu askofu malasusu. Kuna haja ya kupata ukweli na nia ya hawa mwanahalisi na Malasusa.
 
Looh! Kujipanga tena kushitaki kwenye mahakama hizi za kidunia na sikufanya maombi na kufunga?

Na washawasha!



Nimesoma gazeti la leo, askofu amepinga kubariki wala kuruhusu pombe kwa waumini wake. Tena wameandika dayosisi inajipanga kuwashtaki Mwanahalisis kwa kumchafua. Kama mtakumbuka mwanahalisi wamekuwa wakiandika habari mbaya kila mara kuhusu askofu malasusu. Kuna haja ya kupata ukweli na nia ya hawa mwanahalisi na Malasusa.
 
Wewe Mkristo au Mmussa?

Na washawasha!
Mkuu tunapozungumzia masuala ya dini tunazungumzia tuyemuamini ambae ni Mungu na mungu kuzungumza nae alitumia watu wake Wa kweli na tunaamini maneno yake hayabadiliki hivyo alimpa Mussa na Yesu tunayemuamini ni Maana Wa Mungu alikili maagizo aliyopewa Mussa na Mungu so its unchanged after Jesus waliofuata ni wanafunzi na kuna vigeu geu walioharibu na kupotosha watu haswa Paul.. Please stand with Mussa and Jesus maana Always Master ndio anasikilizwa na si mwanafunzi
 
Naona dhehebu jipya linazaliwa katika zama . zi huku likija na biblia yake yenye vitabu 67.Kitabukitakachoongezwa hakitumimiwi na walutheri . Kitabu hicho nikile Martin Luther alikiondoa kutoka vile wavitumiavyo wakatholical. Nikitabu kinacho ruhusu matumizi ya pombe.
=====
Kuna kitu hakiko sawa KKKT, ingawa mwandishi ana onyesha grudges za hatari dhidi ya Askofu Malasusa.
 
Pombe sio dhambi ulevi ndio dhambi.hata waislamu walikatazwa kunywa pombe kwa sababu dhamani hizo walidhulumiwa Mali zao kwa kununua pombe.so kutotumia pombe ni katazo la wanadamu na si la Mungu
hv unajua kuwa ikiisha itwa pombe tayari inakuwa ni kilevi, hata kama ukinywa usilewe lkn tayar umekwisha tumia kileo yan kunywa tu tayar umeshalewa maana ili iitwe pombe lazima iwekewe kilev hata kama ni 0.001% tayari hiyo ni pombe maana ina kilev hata kama ni kidogo namna gani na ukiionja automatically umetumia kilev.
 
KKKT labariki unywaji wa Pombe

ASKOFU Mkuu wa zamani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, amebariki rasmi unywaji wa pombe katika kanisa hilo kongwe nchini, anaripoti Mwandishi Wetu.

Akizungumza katika mkutano wa 33 wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, wiki iliyopita, huko Seminari ya Kisarawe, mkoani Pwani, Askofu Malasusa amesema, ” katazo la unywaji wa pombe lililetwa na wamisionari, lakini pombe kama pombe haina tatizo.”

Askofu Dk. Malasusa, ndiye askofu mkuu wa kanisa la KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani. Askofu Dk. Malasusa alikuwa akikamilisha majibu yaliyotolewa na Askofu Keshomshahara wa kanisa hilo, Dayosisi ya Bukoba aliyoyatoa kwa swali lilioulizwa na Prof. Mjema wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Katika swali lake, Prof. Mjema alihoji, nafasi ya pombe katika dhana ya Mtume Paulo anapozungumzia kutiwa unajisi kwa vyakula na vinywaji wanavyokunywa wakristo.
Alitaka kupata ufafanuzi wa msiamo wa kanisa juu ya msemo wa “kimuingiacho mtu na kimtokacho mtu.” Awali katika majibu yake, Askofu Keshomshahara amesema, “pombe ni kinywaji tu kama vinywaji na vyakula vingine” na kwamba pombe inapaswa kutumiwa kwa kiasi na kwamba “hata sakramenti takatifu ya Meza ya Bwana inayotumika kanisani mwao ni pombe.”

Baada ya majibu hayo, ndipo Askofu Dk. Malasusa aliposisitiza kuwa makatazo ya pombe kanisani ni “busara ya wamisionari wa kwanza walioleta injili Afrika baada ya kuona Waafrika walikuwa wakilewa bila kiasi na kukosa ustaarabu.”
Aliendelea kusisitiza kuwa “pombe itumike kwa kiasi na hasa kwa wakristo wachanga.”

Majibu hayo ya maaskofu yaliwachanganya wajumbe wengi na kusababisha mijadala baada ya mkutano. Mjumbe mmoja aliyeongea na gazeti hili huku machozi yakimlenga anasema, “nimesikitika sana kuona maaskofu wetu wanalipotosha kanisa. Hivi kweli sakramenti ni pombe?” Dayosisi ya Mashariki na Pwani kupitia katiba yake, inapiga marufuku wazee wa kanisa kutomiliki vitega uchumi vinavyouza pombe.

Aidha, sherehe zote za kanisa haziruhusiwi kuwa na pombe huku baadhi ya waumini wakipewa adhabu na wachungaji wao kwa kunywa pombe au kufanya biashara ya pombe. Msimamo wa maaskofu hawa wawili unaliweka kanisa Zima la KKKT katika njiapanda ya kulifafanua jambo hili huku waumini wengi wakitishia kuhamia makanisa ya kiroho kukimbia upotoshaji wa wazi wa maakofu wa KKKT. Mkutano huo wa 33 ulijaa vitimbi vingi vinavyoonyesha dayosisi hiyo haiko shwari.

Akiongea kwa uchungu kwenye mkutano huo, Mchungaji wa kanisa hilo usharika wa Kigogo, jijini Dar es Salaam, Richard Ananja alimtaka Askofu Dk. Malasusa kuachia kiti mara moja kwa kuwa amepoteza sifa kwa kashfa za ngono zinazomkabili.

Amesema Dk. Malasusa anakabiliwa na tuhuma nzito za matumizi ya madaraka, uvujaji wa fedha za dayosisi, hujuma kwa Benki ya Maendeleo, kugushi vyeti ya elimu, ukabila, chuki na visasi kwa wachungaji.

Hivyo basi, ili kulinda hadhi na heshima ya kanisa na yeye binafsi, ni vema Askofu Malasusa “akaachia ngazi kwa hiari, badala ya kusuburi kufukuzwa.”
Hoja hiyo ilipozwa na katibu mkuu wa Dayosisi hiyo, Godfrey Nkini aliyedai kuwa kamati ya maadili inashughulikia tuhuma hizo.

Siku moja kabla ya kufungwa kwa mkutano, mchungaji wa kanisa la KKKT, Usharika wa Kibaha, Amani Lyimo katika mahubiri ya ibada ya asubuhi, aliushambulia utendaji wa Askofu Dk. Malasusa kuwa ni wa uonevu, usijali kweli, uliojaa udhalimu, ubabe na matumizi mabaya ya madaraka.
Amesema uongozi wa Dk. Askofu Malasusa unakomoa watu kuliko uongozi wowote uliopita katika dayosisi hiyo.

Kabla ya kufungwa kwa mkutano huo, Mwenyekiti wa kamati ya maadili wa dayosisi hiyo, Ibrahim Kaduma, alidai kuwa tuhuma juu ya Askofu Dk. Malasusa, si za kweli na zinachochewa na gazeti moja (hakulitaja) lakini akadai ni chuki ya uislamu dhidi ya kanisa.

Maelezo hayo yalipingwa na wachungaji wengi hali inayoonyesha kuwa Askofu Malasusa hayuko vizuri na wachungaji wake. Wachungaji walidai kamati imeleta “majibu mepesi” kwa tuhuma za ngono zinazomkabili Dk. Malasusa na kwamba kinachobakia sasa wao kumwaga hadharani yaliyositiriwa kulilinda kanisa, alisisitiza mmoja wa wachungaji wa kanisa hilo mwenye taaluma ya sheria.

Katika hatua nyingine, ajenda ya marekebisho ya katiba ya dayosisi hiyo, iliburuzwa ili kumwepusha Askofu Malasusa na hoja ya ukomo wa madaraka yake. Siku za karibuni, Askofu Dk. Malasusa amekumbwa na tuhuma mfululizo, zikiwamo matumizi mabaya ya madaraka, ngono na ubaguzi.

Hata hivyo, Dk. Malasusa amekuwa akijibu tuhuma hizo kwa kuwanyooshea kidole waumini wanaotoka mikoa ya Kaskazini kuwa wanamsakama kwa vile katika uchaguzi mkuu uliyopita, limuunga mkono Rais Magufuli na kumsaliti swahiba wake wa miaka mingi, Edward Lowassa.

Chanzo: Mwanahalisionline
Kunywa pombe siyo zambi,zambi ni pale unaposhindwa kuimudu pombe hiyo we mnywaji.
 
Sasa unashangaa pombe wakati wanafungisha ndoa za mashoga?
 
kitafute mkuu ikiwezekana na mstari.
halafu sijakupata unaposema bibilia ya wakatoliki kwani wakatoliki wanabibilia tofauti na madhehebu mengine?
Kitabu cha biblia cha wakatoliki kina vitabu Saba zaidi tofauti na biblia ya waprotestanti.

Mojawapo ni hicho kitabu cha Sila.
 
Si vizuri MTU Kuleta hoja isiyo na mashiko na kuleta mambo bila uthibitisho .Mleta ma da angetaja aina ya pombe anayotumia na najina ya wanawake na wao kuthibitisha Kwa mahojiano kituo cha redio.Huyu bwana ananjaa ! Sina uhakika ni ya nini?
 
Sawa ni zipi amri za Yesu? Maana tunajua Bwana Yesu alisema hakuja kuitangua taurati bali kuitimiliza. Kwa nini unamtuhumu Mtume Paulo? Hebu tupe sababu za msingi za kufanya hivyo.

Na washawasha!

Mkuu tunapozungumzia masuala ya dini tunazungumzia tuyemuamini ambae ni Mungu na mungu kuzungumza nae alitumia watu wake Wa kweli na tunaamini maneno yake hayabadiliki hivyo alimpa Mussa na Yesu tunayemuamini ni Maana Wa Mungu alikili maagizo aliyopewa Mussa na Mungu so its unchanged after Jesus waliofuata ni wanafunzi na kuna vigeu geu walioharibu na kupotosha watu haswa Paul.. Please stand with Mussa and Jesus maana Always Master ndio anasikilizwa na si mwanafunzi
 
Back
Top Bottom