Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,379
Nimepata mwaliko wa mtoko weekend hii kutoka kwa kijana aliyekuwa akinitupia nyavu siku nyingi kidogo. Ni takriban miezi nane sasa tangu nitemane na my BF, baada ya kunitenda. Sasa nimeona nitoke na huyu mtupa nyavu ili nijue sera zake kabla sijafanya uamuzi.
Sasa shida ipo kwenye kivazi cha kutokea. Jamani si mnajua tena dada zangu, mtoko wa kwanza unaleta tashwishwi. Hapa nimewaza na kuwazua sijapata jibu. Naombeni msaada wa haraka ili nijue kama itabidi nikimbie Kariakoo fasta fasta maana weekend ndiyo hiyoo inajongea.
Sasa shida ipo kwenye kivazi cha kutokea. Jamani si mnajua tena dada zangu, mtoko wa kwanza unaleta tashwishwi. Hapa nimewaza na kuwazua sijapata jibu. Naombeni msaada wa haraka ili nijue kama itabidi nikimbie Kariakoo fasta fasta maana weekend ndiyo hiyoo inajongea.