Kituko Makongo Juu, waweka msiba kumbe hajafariki

Kituko Makongo Juu, waweka msiba kumbe hajafariki

Hili jambo limewahi kumtokea classmate wetu wote tulijua alishaga fariki
 
Huyo Jamaa akijua waliweka matanga atamind sanaaaa
 
Hao waliorudi wanalia na kusambaza uongo huo mawazo yao yalikuwa kwenye kugawana mali za marehemu.
 
du poleni sana mkuu bila shaka waliotoa taarifa ni wanawake maana akili za wanawake wanazijua wao tu.
Mcpende kuwarushia tuhuma wanawake kwa kila jambo linaloonekana lina negative impact kwa jamii. Nao ni binadam na wanahisia na mapungufu yao. Mbona mama yako hakukuminya ww hadi umefikia hapo ulipo? So dada zako, mwanao wa kike ukija kupata, shangazi zako na huyo unayemshughulikia taahira asiye na akili nao n hvyohvyo!!!!

Polen mtoa habari hutokea hayo.
 
Kwa hio hizo pesa za rambirambi kapewa huyo mgonjwa au
 
Duuh tuweni makini, naikumbuka ile issue ya kubeba jeneza bila maiti watu wakaenda kuzika baadaye wanarudi nyumbani wakakuta mwili wa marehemu kitandani. ...watu wacha watoke mbio na imani tofauti kumbe mwili ndio haukuwekwa ndani ya jeneza
 
Wewe acha kuleta habari za KIJINGA wewe....
Soma post namba 35.
Ss mbona sikuelewi naona acha ujinga....kwani hiyo post uliyonidirect na hicho nilichoandika kina tofauti gani??? Mm nilikuwa namuelekeza huyo aliyewasema wanawake na kumwambia si kila chenye negative impact kwenye jamii kinafanywa na wanawake tu na km n hivyo bac anamaanisha wanawake wote hawana akili akiwemo mzazi wake aliyemlea hadi leo, mwanae wa kike, dada zake hata mkewe.

Haya huo ujinga wangu na hicho ilichooandika ww tofauti yake nn. Kumbe nawe hukupendezwa na alichosema kwa ku generalise
 
Jambo la ajabu limetendeka Makongo juu, mgonjwa kapelekwa hospitali Mwananyamala juzi akalazwa. Walioenda kumjulia hali jana asubuhi wakarudi wanalia kwamba mtu wetu kafariki. Taarifa zikasambaa ukawekwa msiba, maturubai, watu kibao tumelala msibani. Rambirambi zimechangwa.

Ajabu asubuhi hii aliyeenda hospitali kukamilisha taratibu za huko kaleta taarifa kuwa mgonjwa alikuwa hajafa, ila alihamishwa kitanda! Hivi ndo kila mtu kabaki mdomo wazi. Ndo tunaondoa maturubai na kurudisha makochi ndani.

My take: Tuwe makini, kabla ya kusambaza taarifa mtu kafa, tucomfirm kabisa na daktari na ikibidi ushuhudie mwili kabisa. Usumbufu mkubwa watu wamepata na itaathiri sana maisha katika familia ya mgonjwa.

Mungu aendelee kumponya. Amen.


Ana mali za kuweza watu kurithi?
 
Rambi rambi iliisha fika ngapi labda itasaidia matibabu
Usikute hapo huyo alowekewa msiba hata dawa hana watu wanadai hali ngumu lakini kwenye msiba wamemchangia huyo Marehemu
 
Ukiuguza ndugu wa karibu hospital unachanganyikiwa..Piga picha asubuhi unaingia pale Muhimbili unapita Mwaisela unakuta vilio vimetamalaki...unachsnjs zako mbuga sewahaji unakuta mgonjwa hayupo kitandani!!!

Acheni tu..Mungu awape moyo wote wanaouguza..Pole kwa hyo familia.
 
Ukiuguza ndugu wa karibu hospital unachanganyikiwa..Piga picha asubuhi unaingia pale Muhimbili unapita Mwaisela unakuta vilio vimetamalaki...unachsnjs zako mbuga sewahaji unakuta mgonjwa hayupo kitandani!!!

Acheni tu..Mungu awape moyo wote wanaouguza..Pole kwa hyo familia.
Kabisa mkuu..
 
Poleni sana wana familia, ndugu, jamaa, marafiki na majirani kwa usumbufu huo mlioupata.
Mtoa taarifa inaonekana alikupuka bila kumuuliza daktari au nesi sehemu alipo mgonjwa. Hii ni hatari sana tena sana.
 
Jambo la ajabu limetendeka Makongo juu, mgonjwa kapelekwa hospitali Mwananyamala juzi akalazwa. Walioenda kumjulia hali jana asubuhi wakarudi wanalia kwamba mtu wetu kafariki. Taarifa zikasambaa ukawekwa msiba, maturubai, watu kibao tumelala msibani. Rambirambi zimechangwa.

Ajabu asubuhi hii aliyeenda hospitali kukamilisha taratibu za huko kaleta taarifa kuwa mgonjwa alikuwa hajafa, ila alihamishwa kitanda! Hivi ndo kila mtu kabaki mdomo wazi. Ndo tunaondoa maturubai na kurudisha makochi ndani.

My take: Tuwe makini, kabla ya kusambaza taarifa mtu kafa, tucomfirm kabisa na daktari na ikibidi ushuhudie mwili kabisa. Usumbufu mkubwa watu wamepata na itaathiri sana maisha katika familia ya mgonjwa.

Mungu aendelee kumponya. Amen.
Hivi taratibu mtu anapofariki hospitalini, anayetoa taarifa za mgonjwa kufariki si daktari jamani! Jitu from no where unapokuta mgonjwa kabadilishiwa wadi, kwako tayari kafa!
Lakini mara nyingi niliishaona, mtu akizushiwa kifo, huwa ni dalili mbaya.
Tumuombee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom