Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,898
- 828,498
Kiti kina tafsiri nyingi lakini majumuisho yake ni
Ukuu
Utawala
Enzi
Mamlaka
Uongozi
Niliwahi kuleta simulizi hapa ya "KITI HAPIGWI" Nitaweka link yake kwenye reply
Ndani ya familia kuna kiti cha baba(sijawahi kuona kiti cha mama) pengine chake ni kigoda kwakuwa hata kiimani anatambulika kama msaidizi wa baba
Hata kwenye nyumba zetu za ibada kuna kiti maalum cha mkuu na daima huwa tofauti kabisa na vingine
Mambo ni hayohayo hata kwenye kaliba nyingine za maisha! Kiti cha mgeni rasmi
Kwenye mashindano mbalimbali kiti hutumika kama kiambishi cha yule anayeongoza ama anayeshika namba moja
Kiti kina connection ya moja kwa moja na maisha! Tunavyo viti vya kudumu kwenye maisha yetu ambavyo ni vyetu wenyewe ama kwa kununua kwa pesa zetu au kupewa kama msaada, zawadi, tunu nk.. Hivyo ni vyetu na hubaki kuwa vyetu
Tuna viti vingine vya mpito, vya kukasimiwa, vya muda.. Visivyo vyetu moja kwa moja
Viti kwenye sherehe
Viti kwenye usafiri
Viti kwenye jumuiya
Viti kwenye uongozi nk
Hivi viti ukimaliza jukumu lako unampisha mwingine.. Kama ni kwenye sherehe, ikiisha huondoki na kiti wala hubaki kukikalia.. Watu watakushangaa
Kwenye usafiri ukifika uendapo utashuka na kukiacha kiti mwingine akalie!
Hata kwenye nyumba ya ibada ofisini nk..! Ni nadra sana sana mtumishi anayemaliza muda wake kazini kupewa zawadi ya kiti.. Atapewa vingine vyote lakini sio kiti!
Watu wa pwani wana tamaduni zao tofauti kidogo.. Pamoja na uwepo wa viti.. Mara nyingi ni kiti kimoja cha baba vingine ni vigoda na majamvi! Na kwenye hayo majamvi kuna jamvi maalum la wageni! Jamvi la wageni hilo halitumiki na familia!
Umemaliza safari yako busara ni kukabidhi kiti kwa mwingine anayeendelea na safari.. Huwezi kulazimisha kushuka na kiti kwakuwa si chako mwenyewe ni cha jumuiya!
Ulialikwa kama mgeni rasmi ukaandaliwa kiti kizuri na cha thamani! Umekikalia ukakipenda lakini kamwe huwezi kuondoka nacho! Hata walioalikwa watakushangaa sana!
Niliwahi kuanzisha ugomvi wa wivu chumbani! Nikajifanya bondia ninayeweza kupiga vya kelebu! Kumbe mchumba alikuwa KITI!
Nikaulizwa na sauti ngeni toka kwa mchumba.. Kiti kakukosea nini? Nikawashwa moja takatifu shwaaah! Nikaona maruweruwe!
Sijakaa sawa nikawashwa cha pili huku napewa warningi.. KITI hapigwi, shwaaah! Pa ah! Shwaah! Paah, Paah ..Paah!
Kuna kipigo cha umbwa koko! Na kipigo cha umbwa mwivi! Mimi nilipata vyote!
Using'ang'anie kiti kama sio chako mwenyewe! Wakishindwa kukupokonya..! Watakulazimisha...!
Sikioni kiti..sikioni kigoda! Viko wapi!?
Ukuu
Utawala
Enzi
Mamlaka
Uongozi
Niliwahi kuleta simulizi hapa ya "KITI HAPIGWI" Nitaweka link yake kwenye reply
Ndani ya familia kuna kiti cha baba(sijawahi kuona kiti cha mama) pengine chake ni kigoda kwakuwa hata kiimani anatambulika kama msaidizi wa baba
Hata kwenye nyumba zetu za ibada kuna kiti maalum cha mkuu na daima huwa tofauti kabisa na vingine
Mambo ni hayohayo hata kwenye kaliba nyingine za maisha! Kiti cha mgeni rasmi
Kwenye mashindano mbalimbali kiti hutumika kama kiambishi cha yule anayeongoza ama anayeshika namba moja
Kiti kina connection ya moja kwa moja na maisha! Tunavyo viti vya kudumu kwenye maisha yetu ambavyo ni vyetu wenyewe ama kwa kununua kwa pesa zetu au kupewa kama msaada, zawadi, tunu nk.. Hivyo ni vyetu na hubaki kuwa vyetu
Tuna viti vingine vya mpito, vya kukasimiwa, vya muda.. Visivyo vyetu moja kwa moja
Viti kwenye sherehe
Viti kwenye usafiri
Viti kwenye jumuiya
Viti kwenye uongozi nk
Hivi viti ukimaliza jukumu lako unampisha mwingine.. Kama ni kwenye sherehe, ikiisha huondoki na kiti wala hubaki kukikalia.. Watu watakushangaa
Kwenye usafiri ukifika uendapo utashuka na kukiacha kiti mwingine akalie!
Hata kwenye nyumba ya ibada ofisini nk..! Ni nadra sana sana mtumishi anayemaliza muda wake kazini kupewa zawadi ya kiti.. Atapewa vingine vyote lakini sio kiti!
Watu wa pwani wana tamaduni zao tofauti kidogo.. Pamoja na uwepo wa viti.. Mara nyingi ni kiti kimoja cha baba vingine ni vigoda na majamvi! Na kwenye hayo majamvi kuna jamvi maalum la wageni! Jamvi la wageni hilo halitumiki na familia!
Umemaliza safari yako busara ni kukabidhi kiti kwa mwingine anayeendelea na safari.. Huwezi kulazimisha kushuka na kiti kwakuwa si chako mwenyewe ni cha jumuiya!
Ulialikwa kama mgeni rasmi ukaandaliwa kiti kizuri na cha thamani! Umekikalia ukakipenda lakini kamwe huwezi kuondoka nacho! Hata walioalikwa watakushangaa sana!
Niliwahi kuanzisha ugomvi wa wivu chumbani! Nikajifanya bondia ninayeweza kupiga vya kelebu! Kumbe mchumba alikuwa KITI!
Nikaulizwa na sauti ngeni toka kwa mchumba.. Kiti kakukosea nini? Nikawashwa moja takatifu shwaaah! Nikaona maruweruwe!
Sijakaa sawa nikawashwa cha pili huku napewa warningi.. KITI hapigwi, shwaaah! Pa ah! Shwaah! Paah, Paah ..Paah!
Kuna kipigo cha umbwa koko! Na kipigo cha umbwa mwivi! Mimi nilipata vyote!
Using'ang'anie kiti kama sio chako mwenyewe! Wakishindwa kukupokonya..! Watakulazimisha...!
Sikioni kiti..sikioni kigoda! Viko wapi!?


Si kila utajiri ni lazima uambatane na nguvu za giza la hasha! Lakini kuulinda huo utajiri ama kuuongeza ni lazima kwa asilimia 100 nguvu za giza zihusike! Utajiri moja kwa moja huvutia...