Habari wakuu, misukosuko ya mapenzi iliyonikuta ilinifanya nitende unyama mkubwa sana hapa duniani!
Yule mwanamke naamini hadi anaingia kaburini hata sahau ukatili niliomfanyia, hata awapo na mumewe au na wanawe hii sura lazima itabaki moyoni mwake tuu.
Ni jambo baya zaidi wakuu kwa historia ya nchi. Napata hata shida ya kuliandika hapa maana nahofia serikali isije kunibeba hapa.
Kwa tabia yake ya kujichanga na watu kibao na kujifanya marafiki zake nilipata habari ya uhakika na nilidhibitisha nilichokifanya hiyo siku nilimtafuta yule boya* alienilia tunda langu nikampa kipigo hatari mno japo alifanikiwa kuning'ata ila kipigo nilichompa hadi leo ananiheshimu na hili jambo limenipa heshima mbele ya jamii inayonizunguka.
Huyu mwanamke hakuwa na kwa kukimbilia na hasira ilienda kuishia kwake.
Ni tukio baya sana wakuu hivi nasema bora nisingemfania kwani najutia, nimejiwekea historia mbaya maishani mwang ila kwa kuwa ishatokea nitatafuta jinsi niisahamu hii hali au nimfate nimuombe msamaha tuu yaishe nafsi yangu iwe na amani.