Kitendo cha kutaka kuhamisha familia 400 zinazozunguka eneo la kimondo cha Ndolezi Mbozi bila fidia ni cha kishenzi

Nakumbuka nilivokua chuo tulienda kwenye iko kimondo.

Kipo overrated sana.
 
Nakumbuka nilivokua chuo tulienda kwenye iko kimondo.

Kipo overrated sana.
Kiko overrated kivipi? Kwamba siyo kimondo?

Kimondo ni jiwe lililodondoka kutoka angani hivyo ni kivutio hasa kwa wanasayansi kukifanyia uchunguzi na utafiti ili kuifahamu vizuri anga!
 
Chanzo Cha Matatizo(CCM) kipo kazini. Walianza na Ngorongoro tukachukulia poa. Sasa wamehamia Mbeya, wachaga mkae mkao wa kuondoka kandokando ya mlima Kilimanjaro maana huyu CEO wa kampuni hatanii. Atatania na kurembua kwenye kuwachukulia hatua wapigaji wa fedha za umma lakini sio kuhamisha watu ili kuwapa eneo waarabu
 
Na nchi ilivyo na machawa wengi sasa!
huku kulikuwa na MTU 100 tu ilikomboa hekta 1700 ni kijiji wakaja mpaka jwt jamaa wakasema mtuue hapahapa ila eneo hatutoi na hatuhami serikar ikabidi itii amri
 
Less creative

Kijiji kingeachwa na kuboreshwa ili watalii wakija wapige story na Mashuhuda jinsi kimondo kilivyo piga hiyo siku....mijitu inawaza kupiga tu
Kimondo kinaibwa,nilipokua msingi 1990s picha za kimondo kulikua kubwa,juzi nimeona kimepungua,halafu waondoke tu kwa maslahi ya taifa,sisi akina ngosha tulitimuliwa bhulyanhulu kupisha mgodi,na kuuawa juu
 
Less creative

Kijiji kingeachwa na kuboreshwa ili watalii wakija wapige story na Mashuhuda jinsi kimondo kilivyo piga hiyo siku....mijitu inawaza kupiga tu
Umesahau ndani ya miaka 30, kijiji kitakuwa mji, mazingira yote ya asili yanapotea, wale watu walioona kimondo hawapo tena ,


Btw siungi mkono kuwaondoa bila kulipa fidia, ni upuuzi grade A
 
Kimondo kinaibwa,nilipokua msingi 1990s picha za kimondo kulikua kubwa,juzi nimeona kimepungua,halafu waondoke tu kwa maslahi ya taifa,sisi akina ngosha tulitimuliwa bhulyanhulu kupisha mgodi,na kuuawa juu
Utakuwa uliangalia kwa jicho la kengeza vinginevyo kimondo kiko vilevile ukiondoa sehemu chache zilizokatwa kwa msumeno.
 
Serikali ya CCM inajali wanyama kuliko binadamu Watanganyika.

Ukitaka kuthibitisha hili angalia adhabu ya kugonga fisi na binadamu ndipo utajua hali ni mbaya sana
juzi kati tembo alikatiza barabarani bahati mbaya akagongwa paja na basi moja akajeruhika, viongozi wa kijiji wakataoa taarifa kwa wanaohusika na wanyama pori wakaja mbio haraka bila kuchelewa. Lakini wanyama wakiharibu mazao ya wananchi au kujeruhi watu wakipigiwa simu waje wanakuja kwa kuchelewa hawajali maisha ya watu. Wana majibu mabaya kuwa wanyama wana thamani kubwa kuliko watu na wanaingiza fedha nyingi. Mwananchi haingizi fedha kama wanyamapori
 
juzi kati tembo alikatiza barabarani bahati mbaya akagongwa paja na basi moja akajeruhika, viongozi wa kijiji wakataoa taarifa kwa wanaohusika na wanyama pori wakaja mbio haraka bila kuchelewa. Lakini wanyama wakiharibu mazao ya wananchi au kujeruhi watu wakipigiwa simu waje wanakuja kwa kuchelewa hawajali maisha ya watu. Wana majibu mabaya kuwa wanyama wana thamani kubwa kuliko watu na wanaingiza fedha nyingi. Mwananchi haingizi fedha kama wanyamapori
Hiyo ndiyo akili ya Serikali ya CCM kwao wanyama wana thamani kuliko binadamu
 
Safi sana .

Walianza na wamasai sasa wamekuja kwa wanyaki.

Ngoja wachaga nao wahamishwe maana wanasumbua mlima kilimanjaro.

Kila kabila litafikiwa kwa wakati wake.
 
Nimezaliwa pembeni ya hicho kimondo mita kama 30 hivi, enzi hizo ulikuwa hauwezi kukatisha pale mida ya usiku ikiwa peke yako, kilikuwa kinatoa mwanga mkali sana,
Tafadhali nifahamishe zaidi hili!

Kinatoa mwanga? Kwa maana kina meremeta? Na huo mwanga kwenye kimondo ni baada ya kumulikwa na mbaramwezi?
 
Tafadhali nifahamishe zaidi hili!

Kinatoa mwanga? Kwa maana kina meremeta? Na huo mwanga kwenye kimondo ni baada ya kumulikwa na mbaramwezi?
Nadhani ni hadithi tu za kunogesha Baraza kwa sababu hicho kimondo ni jiwe chuma. Yaani kina madini mengi ya iron (Fe) ambayo hayang'ai na kwa kuwa kiko wazi na kinapigwa mvua na jua kina rangi ya kutu nyeusi au dark brown.
 
Nadhani ni hadithi tu za kunogesha Baraza kwa sababu hicho kimondo ni jiwe chuma. Yaani kina madini mengi ya iron (Fe) ambayo hayang'ai na kwa kuwa kiko wazi na kinapigwa mvua na jua kina rangi ya kutu nyeusi au dark brown.
Nashukuru kwa ufafanuzi.

Kwa hakika ulichokielezea ndicho nami ninachokijua hicho. Maelezo yake yamenishitua! Hivyo nikataka kujua zaidi.

Nashukuru kwa kuniweka sawa mkuu.
 
Wananchi wa kijiji cha Ndolezi kilipo kimondo maarufu cha Mbozi wamekuwa wakiishi hapo kabla ya wanasayansi kuthibitisha kuwa jiwe lile ni kimondo, hivyo kulipa jiwe hilo hadhi ya pekee kulinganisha na mawe mengine yaliyopo kijijini hapo.

Baada ya uthibitisho huo wanasayansi, watalii, na watu wengine wadadisi kwa mamia wamekuwa wakitembelea eneo hilo. Hapo awali ilikuwa kutembelea eneo hilo ilikuwa bure kabisa lakini baadaye serikali ikaweka ada ya kuliangalia jiwe hilo. Jambo hilo halikuwa baya kwani kijiji na serikali vilipata fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Tofauti na awali ambapo wanakijiji walifurahia kupokea wageni na kunufaika kiuchumi sasa jiwe lile (kimondo) limezua balaa. Wananchi wanatakiwa kuondoka eneo hilo ili serikali ijenge wigo kwa ajili ya wanyama wa porini (Zoo) ili kuongeza vivutio kwa watu wengi zaidi kutembelea eneo hilo.

Kitendo hicho hakikubalika kabisa na hasa kuwaondoa wananchi bila stahiki na fidia za mali zao. Kwa nini serikali hii inayojinasibu kuheshimu haki za binadamu inataka kuwafanyia dhuluma wananchi wake kwa sababu ya wanyama wa porini? Kwani hakuna vivutio vingine nchi hii zaidi ya wanyama? Kwa nini serikali hii inapenda kuanzisha migogoro isiyo ya msingi na wananchi wake?

Hii inaonyesha wazi kabisa kuwa serikali hii haina watu wabunifu, wamekaririshwa kuwa wanyama pekee ndiyo kivutio cha utalii. Hivi haiwezekani serikali kujenga nyumba ya makumbusho (Museum) ambayo kwanza itachukua eneo dogo lakini pia itahifadhi vitu vya kale na vya utamaduni wa jamii ya watu wa mkoa wa Songwe. Pili itawawezesha wananchi wanaoishi eneo hilo kuendelea kukaa kwa amani na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi.

Wakati umefika kwa serikali kujisafisha kwa kuondoa watumishi wanaokosa ubunifu katika kutekeleza majukumu yao na kuajiri wanaoweza kubuni miradi ambayo itawanufaisha wananchi na serikali kupata kipato bila kuathiri maisha ya watu na mazingira yaliyopo!
Tatizo ni thamani ya hicho kimondo, material yake ni muhimu
 
Back
Top Bottom