Kitendo cha kutaka kuhamisha familia 400 zinazozunguka eneo la kimondo cha Ndolezi Mbozi bila fidia ni cha kishenzi

Haya ndo mambo ambayo CHAWA km Mwashambwa wangekuwa wanapigia kelele tena MBOZI ndo kwao kabisa, Yani ni the NYIA BOY lakini yeye utamkuta anabwabwaja mambo yasio ya msingi. Kusifia tu mambo ya hovyo hovyo wakati mambo nyeti km haya huwezi kumuona.
Lucas Mwashambwa anawaza tumbo lake tu!
 
Mpaka sasa hilo eneo hajatokea mjanja ajikatie hati miliki ili wakihamishwa apate madola kadhaa?
 
Mpaka sasa hilo eneo hajatokea mjanja ajikatie hati miliki ili wakihamishwa apate madola kadhaa?
Wananchi walisimama kidete kuhakikisha linabaki kuwa hifadhi ya kijiji hadi hapo serikali kuu ilipolitwaa!
 
Wananchi wa kijiji cha Ndolezi kilipo kimondo maarufu cha Mbozi wamekuwa wakiishi hapo kabla ya wanasayansi kuthibitisha kuwa jiwe lile ni kimondo, hivyo kulipa jiwe hilo hadhi ya pekee kulinganisha na mawe mengine yaliyopo kijijini hapo.

Baada ya uthibitisho huo wanasayansi, watalii, na watu wengine wadadisi kwa mamia wamekuwa wakitembelea eneo hilo. Hapo awali ilikuwa kutembelea eneo hilo ilikuwa bure kabisa lakini baadaye serikali ikaweka ada ya kuliangalia jiwe hilo. Jambo hilo halikuwa baya kwani kijiji na serikali vilipata fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Tofauti na awali ambapo wanakijiji walifurahia kupokea wageni na kunufaika kiuchumi sasa jiwe lile (kimondo) limezua balaa. Wananchi wanatakiwa kuondoka eneo hilo ili serikali ijenge wigo kwa ajili ya wanyama wa porini (Zoo) ili kuongeza vivutio kwa watu wengi zaidi kutembelea eneo hilo.

Kitendo hicho hakikubalika kabisa na hasa kuwaondoa wananchi bila stahiki na fidia za mali zao. Kwa nini serikali hii inayojinasibu kuheshimu haki za binadamu inataka kuwafanyia dhuluma wananchi wake kwa sababu ya wanyama wa porini? Kwani hakuna vivutio vingine nchi hii zaidi ya wanyama? Kwa nini serikali hii inapenda kuanzisha migogoro isiyo ya msingi na wananchi wake?

Hii inaonyesha wazi kabisa kuwa serikali hii haina watu wabunifu, wamekaririshwa kuwa wanyama pekee ndiyo kivutio cha utalii. Hivi haiwezekani serikali kujenga nyumba ya makumbusho (Museum) ambayo kwanza itachukua eneo dogo lakini pia itahifadhi vitu vya kale na vya utamaduni wa jamii ya watu wa mkoa wa Songwe. Pili itawawezesha wananchi wanaoishi eneo hilo kuendelea kukaa kwa amani na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi.

Wakati umefika kwa serikali kujisafisha kwa kuondoa watumishi wanaokosa ubunifu katika kutekeleza majukumu yao na kuajiri wanaoweza kubuni miradi ambayo itawanufaisha wananchi na serikali kupata kipato bila kuathiri maisha ya watu na mazingira yaliyopo!
Kwani Serikali imesema haitawapa fidia?
 
Watawafukuza halafu wajengee maeneo kwa Ajili ya Utalii wa Kimondo.😂😂😂😂

Mtaja uzwa mazima!
 
Wananchi wa kijiji cha Ndolezi kilipo kimondo maarufu cha Mbozi wamekuwa wakiishi hapo kabla ya wanasayansi kuthibitisha kuwa jiwe lile ni kimondo, hivyo kulipa jiwe hilo hadhi ya pekee kulinganisha na mawe mengine yaliyopo kijijini hapo.

Baada ya uthibitisho huo wanasayansi, watalii, na watu wengine wadadisi kwa mamia wamekuwa wakitembelea eneo hilo. Hapo awali ilikuwa kutembelea eneo hilo ilikuwa bure kabisa lakini baadaye serikali ikaweka ada ya kuliangalia jiwe hilo. Jambo hilo halikuwa baya kwani kijiji na serikali vilipata fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Tofauti na awali ambapo wanakijiji walifurahia kupokea wageni na kunufaika kiuchumi sasa jiwe lile (kimondo) limezua balaa. Wananchi wanatakiwa kuondoka eneo hilo ili serikali ijenge wigo kwa ajili ya wanyama wa porini (Zoo) ili kuongeza vivutio kwa watu wengi zaidi kutembelea eneo hilo.

Kitendo hicho hakikubalika kabisa na hasa kuwaondoa wananchi bila stahiki na fidia za mali zao. Kwa nini serikali hii inayojinasibu kuheshimu haki za binadamu inataka kuwafanyia dhuluma wananchi wake kwa sababu ya wanyama wa porini? Kwani hakuna vivutio vingine nchi hii zaidi ya wanyama? Kwa nini serikali hii inapenda kuanzisha migogoro isiyo ya msingi na wananchi wake?

Hii inaonyesha wazi kabisa kuwa serikali hii haina watu wabunifu, wamekaririshwa kuwa wanyama pekee ndiyo kivutio cha utalii. Hivi haiwezekani serikali kujenga nyumba ya makumbusho (Museum) ambayo kwanza itachukua eneo dogo lakini pia itahifadhi vitu vya kale na vya utamaduni wa jamii ya watu wa mkoa wa Songwe. Pili itawawezesha wananchi wanaoishi eneo hilo kuendelea kukaa kwa amani na kuendeleza shughuli zao za kiuchumi.

Wakati umefika kwa serikali kujisafisha kwa kuondoa watumishi wanaokosa ubunifu katika kutekeleza majukumu yao na kuajiri wanaoweza kubuni miradi ambayo itawanufaisha wananchi na serikali kupata kipato bila kuathiri maisha ya watu na mazingira yaliyopo!
Kama wanahamishwa bila fidia wakatae ila kama walivamia eneo la kimondo basi watakachopewa na Serikali ndio stahiki Yao.

Mwendazake asingewapa hata mia kama alivyofanya Kwa vyeti fake na waliopisha ujenzi wa Barabara
 
Adhabu zimekaaje?
Screenshot_20240505_134143_Chrome.jpg


 
Kama wanahamishwa bila fidia wakatae ila kama walivamia eneo la kimondo basi watakachopewa na Serikali ndio stahiki Yao.

Mwendazake asingewapa hata mia kama alivyofanya Kwa vyeti fake na waliopisha ujenzi wa Barabara
Kimodo unanifahamu?

Kimondo kilivamia dunia kijiji cha Ndolezi hivyo kama serikali inakitaka haina budi kuwalipa wanakijiji!
 
Wanaotunga sera wanakaa masaki na osterbay hawapo field so madhila hayawahusu.
Wanaotunga sera sio wahanga. Mfano tu WA reli ya SGR unawawekea uzio kuwatenganisha wananchi pande mbili bila kuacha sehemu za kupita wananchi utadhani wote wanamiliki magari
 
Wanataka fidia stahiki na ya haki kulingana na hali ya maendeleo ilivyo! Kifupi hawataki dhuluma!
Watalipwa kama wanavyolipwa fidia stahili Watanzania wengine mahala pengine. Huku Jijini Mwanza watu wamefurahia sana fidia ya SGR. Hope na hao watafurahia!
 
Kama fidia ipo na watu wamekubal nini tatizo? Hio museum unaposema kwan haipo pale? Si kuna bonge la jengo pale ambalo nadhan ndio linahifadhi historia .labda wanataka kuliongezea thamani, tena wakiweka na michezo ya watoto na eneo la byakula na finywaji patakua pazur sana,mana ukiwa mombo sijiu momba hamnaga sehem ya kwenda kutembea zaid ya labda tunduma mabaa
 
Kama fidia ipo na watu wamekubal nini tatizo? Hio museum unaposema kwan haipo pale? Si kuna bonge la jengo pale ambalo nadhan ndio linahifadhi historia .labda wanataka kuliongezea thamani, tena wakiweka na michezo ya watoto na eneo la byakula na finywaji patakua pazur sana,mana ukiwa mombo sijiu momba hamnaga sehem ya kwenda kutembea zaid ya labda tunduma mabaa
Wananchi ndiyo wanakataa kuhamishwa wakidai ni eneo lao la asili na kuna makaburi ya vizazi kadhaa vya wapendwa wao!
 
Ukiwa Tanzania epuka kukaa / kujenga karibu na hifadhi ya mimea, mbuga za wanyama, sehemu zenye madini, watu Kama Lucas Mwashambwa, kimondo, bandari, barabara, matajiri na wanasiasa.
Utanishukuru uzeeni.
 
Hivi inawezekana eeeeenh?
inawezekana na Nina mifano hai ilitokeaga ruvuma ilitokea Lindi pia serikali ilitaka eneo wanchi wakagoma kwasauti moja ila muwe na ushilikiano asiwe chawa kat yenu au mtoa nyeti zenu taarifa no iwe no haswa
 
inawezekana na Nina mifano hai ilitokeaga ruvuma ilitokea Lindi pia serikali ilitaka eneo wanchi wakagoma kwasauti moja ila muwe na ushilikiano asiwe chawa kat yenu au mtoa nyeti zenu taarifa no iwe no haswa
Na nchi ilivyo na machawa wengi sasa!
 
Back
Top Bottom