Kitabu: Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924-1968)

Sina ugomvi na fikra yako na unavyoamini. Mimi nimendika kama nilivyoona katika utafiti.
Nyerere amesoma kitabu na akaombwa atoe maelezo yake.

Kwa nini hakufanya hivyo mimi siwezi kujua. Padri Sivalon kaandika kitabu

"Kanisa Katoliki na Siasa Tanzania Bara..." kaeleza yale niliyoeleza na mengine
makubwa na mazito.

Waislam tumeyasoma na imetuthibitishia dhana yetu.

Si Kanisa Katoliki wala Nyerere wametoa majibu.

Ikiwa wewe unataka kumjibia Nyerere na Kanisa Katoliki uhuru
huo unao na nitakusikiliza kwa makini.

Mohammed,
Hata kijitabu cha kasisi Sivalon ninacho. Lakini hakuna mahala kaandika kuwa kanisa la Katoliki lilihimiza au kuchochea kufutwa kwa EAMWS.

Hiyo ndiyo point yangu. Kama ulifanya utafiti toa basi ushahidi wa kuhusika kwa kanisa Katoliki katika kufutwa kwa EAMWS. Kama hakuna ushahidi basi kiri tu kuwa ni dhana yako tuendelee na mjadala. Nyerere kadhalika hakujibu kitabu cha Jumbe. Lakini hii haikifanyi kuwa factual badala ya opinionated.

Lakini wewe umejiannoint kuwa mwana historia lazima ukumbuke kuwa unabeba wajibu wa kuwa factual. Mimi siwezi kumsemea Nyerere na siwezi kulisemea kanisa Katoliki, lakini wewe umetoa allegation ya kuhusika kwa kanisa hilo una wajibu wa kutoa ushahidi. Tuendelee.
 
Hivi katika fikra zako, Nyerere kwa jema lipi alilofanya atake kupewa u Saint? ukilieleza hilo utapata jibu, na ukishindwa kulieleza tutakupa jibu.
Sasa unaulizaje kitu ambacho umeshakiri kuwa una jibu lake tayari? Basi jijibu mwenyewe. Mimi siwezi kuwajibia Wakatoliki kwa sababu mimi si mmoja wao. Mimi point yangu ni moja tu: ushahidi kuwa kanisa la Katoliki lilihusika katika kufutwa kwa EAMWS. Nipeni ushahidi katika hilo ili tuendelee na mada.
 
Nadhani ingekuwa na maana zaidi kama ushahidi ungedaiwa na Nyerere na Kanisa Katoliki

Wao ndiyo watuhumiwa.

Hii ndiyo sheria ya ushahidi.

Ushahidi haudaiwi na mchezea pembeni.

Wewe kazi yako ni kusoma na kuuliza pale unapohitaji kueleweshwa zaidi.
 
Nadhani ingekuwa na maana zaidi kama ushahidi ungedaiwa na Nyerere na Kanisa Katoliki

Wao ndiyo watuhumiwa.

Hii ndiyo sheria ya ushahidi.

Ushahidi haudaiwi na mchezea pembeni.

Wewe kazi yako ni kusoma na kuuliza pale unapohitaji kueleweshwa zaidi.
Hapana. Hapo sikubali. Sisi ndio mashahidi wa historia. Sisi ndio tunaoishi na historia na tutawarithisha wanetu historia hiyo. Tunayo haki ya kudai ushahidi pale kunapoonekana kuwepo mushkeli.
 
Sijajua bado lengo la makala hii. Si ubishi hata kidogo Nyerere alikaribishwa Dar enzi zile na wenyeji wa Dar. Sidhani hawa walikuwa na hisia za kidini kama mwandishi anavyotaka tuamini. Na wala Nyerere sidhani aliwaona wale ni watu wa dini; wote walikuwa na nia moja, ya kujikomboa kutoka ukoloni. FULLSTOP. Leo hii tunatazama historia kiugomvi ugomvi. Pengine ni vizuri ukawaza na kutwazua urafiki wa Nyerere na Rashid kuona kama ulikuwa na sura ya namna gani. Hawa wtu ni wakombozi, full stop. Udini usingeweza kufanikisha azma yao, na bado sijawahi kuona udini wa Nyerere katika kutekeleza majukumu yake ya kitaifa. Acheni porojo FANYENI KAZI. Kitabu hiki ni cha kuleta ubaguzi, na kinastahili kichomwe.
Walio yaona ndio wanasimulia sasa, sio lazima uyaone wewe ndio iwe kweli, ushahidi c kuona tu. kunamengi umeyamini kwa kuambiwa tu wala haujayaona.
 
Nadhani ingekuwa na maana zaidi kama ushahidi ungedaiwa na Nyerere na Kanisa Katoliki

Wao ndiyo watuhumiwa.

Hii ndiyo sheria ya ushahidi.

Ushahidi haudaiwi na mchezea pembeni.

Wewe kazi yako ni kusoma na kuuliza pale unapohitaji kueleweshwa zaidi.

duuh Aisee....hiyo hadhira unayoitaka ikuulize ushahidi haipo rasmi hapa JF.........hapa JF wako watu na mitizamo mbali mbali......unapoleta mada watu tumesoma.......na ukiulizwa swali jibu............wewe ni mtafiti...........sioni ugumu wa wewe kujibu swali la Mkuu Jasusi...........otherwise rekebisha maandiko ya kitabu chako kilichotufaidisha kumfahamu Mzee Abdu et al...............
 
MOHAMED said,mahojiano yako na marehemu Hamza Aziz ni batili,how come uli mpa ukumbi ilhali ukijua kwamba akiwa IGP aligonga mtu,akaua na kukimbia,how can we trust such man on sensitive issues of our history?
 
Nadhani ingekuwa na maana zaidi kama ushahidi ungedaiwa na Nyerere na Kanisa Katoliki

Wao ndiyo watuhumiwa.

Hii ndiyo sheria ya ushahidi.

Ushahidi haudaiwi na mchezea pembeni.

Wewe kazi yako ni kusoma na kuuliza pale unapohitaji kueleweshwa zaidi.

Lakini Mkuu maswali yenyewe si ndio hayo? sasa kama watuhumiwa hawakutaka/hawataki kuuliza....basi wajibu angalau watu waliosoma hicho kitabu ......
 
Imam Shaffi (Rahmatullah Aleihy) anasema, "Mimi naweza kusimama na hata watu 100 kwa hoja lakini mjinga mmoja tu hunishinda."

Hivi kweli nyie nyote mmeshindwa kusoma majibu yangu na kuona ushahidi?

Siamini.

Tafadhali kabla hamjasoma zaidi ya hapa hebu rudini nyuma na khasa kama umseoma kitabu hebu
tafakarini taarifa za hawa wafuatao:

Mufti Sheikh Hassan bin Amir
Bilal Rehani Waikela
Shaban Kayugwa
Hamza Aziz
Godfrey Sawaya
Bibi Titi Mohamed

Ushahidi wanao hawa siyo mimi.

Katika orodha hiyo kuna watu kutoka Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi na viongozi wa EAMWS
Hawa ndiyo watakaohojiwa mahakamani na watatoa ushahidi wao.

Nyerere na Kanisa Katoliki ni wajuzi na wanajua nililokuwa nikiandika. Nyerere hakuwa na ujasiri
wa hata kujibu hizo tuhuma na kushikilia kama mnavyoshikilia nyie wacheza pembeni nije na ushahidi
kwa kuwa alijua nisingeweza kuandika yale isipokuwa wenyewe wahusika wamenieleza ukweli.

Mwaka wa 1968 mimi nilikuwa kijana mdogo niliishi katika wakati wa sakata la EAMWS lakini sikuwa na
fahamu za upembuzi wa kuweza kuelewa kwa nini palikuwa na askari mbele ya ofisi za EAMWS.

Jifunzeni kusoma, kufanya tafakuri na kuandika kutoka katika kichwa siyo kwenye mioyo.

Huu ungekuwa mtihani unadhani profesa wako angekupa alama gani F au E au D?

Ila nitakuongezeeni kitu.

Godfrey Sawaya Director of Criminal Investigation baada ya Nyerere kuivunja EAMWS akawa sasa anapita
mikoani na mkoba wa fedha anawahonga watu aliowaona wana ushawishi katika Waislam waiunge mkono
BAKWATA ambayo Nyerere aliwaundia Waislam badala ya EAMWS.

Mradi wa kujenga shule na Chuo Kikuu ukafa pamoja na EAMWS.

Tanzania Episcopal Conference (TEC) ikawa imebaki peke yake inafanya inavyotaka nchini.
Propaganda ikawa inaenezwa kuwa Waislam hatupendi shule ndiyo maana nafazi zote za juu
zimeshikwa na Wakrsto.

Wapo wanaoamini uongo huu hadi leo niandikapo.

Wako watu walichukua hongo ile na wako waliomuogopa Allah wakaikataa.

Bilal Rehani Waikela alikataa hongo ile na ni huyu mzee tukiwa nyumbani kwake ndiye aliyenifunulia
mkasa wote wa EAMWS na akanipa jalada zima alilolitunza kwa miaka 20.

Anasema yeye alikuwa alijua Allah ni muadilifu hataweza kuacha dhulma itawale.

Iko siku Allah atamtuma mtu kuja kufichua yote waliyofanyiwa Waislam na Nyerere na kanisa lake.

Hamza Aziz aliyekuwa IGP yeye alikataa kutii amri ya Waziri wa Ndani Lawi Sijaona ya kumkamata Mufti Sheikh
Hassan kwa tuhuma za kutaka "kupindua serikali ya Nyerere."

Hamza Aziz alimwambia waziri wake kuwa huo ni uzushi yeye hawezi kutuma askari kumkamata mtu mwenye heshima
na mzalendo aliyepigania uhuru na kumjenga Nyerere kama Sheikh Hassan bin Amir.

Je, mngependa kujua Nyerere alihisi vipi alipoelezwa kauli ya Hamza Aziz?
 
Hivi katika fikra zako, Nyerere kwa jema lipi alilofanya atake kupewa u Saint? ukilieleza hilo utapata jibu, na ukishindwa kulieleza tutakupa jibu.

Ninaona intellectual discourse inachukua sura tofauti kidogo. Siku zote huwa nasema tunaposoma vitabu basi pia lazima tufikirie. Hii ina maana tumeze kila kitu bila pinch of thought.
Sidhani kitabu cha Bill Clinton kinaeleza kuhusu siasa za marekani au maisha yake kwa ukweli.Ni akili zetu zitakazotusaidia kujua je alichosema ndio ukweli wa mambo?

Ninachoomba hapa ni kutoa na kujibu changamoto na si suala la nani anajua zaidi na kwa imani gani. Suala la Nyerere kupewa u-saint hilo si hoja kwasababu ni kikundi cha watu wenye imani fulani wameamua hivyo kwa imani na matakwa yao. Hii haifuti hisia au maswali juu yake kutoka kwa wenye mtizamo tofauti. Kwahiyo hili waachiwe wahusika si suala la kitaifa. Kama wataamua kumfanya 'Pope' aliyefariki ni juu yao kama vile mpagani fulani anapoamua kuabudu mbuyu. Ni shauri yake.

Kuhusu, EAMS mimi nadhani yapo madai ya msingi kuwa ni kwanini ilifutwa na Bakwata kuanzishwa haraka haraka. Tunajua kuwa Bakwata imekuwa chombo cha serikali kwa muda mrefu. Lakini sikubaliani na hoja kuwa Nyerere alipaswa kutoa ushahidi au kanisa Katoliki. Hawa ni watuhumiwa watatoa vipi ushahidi wenye mashiko? Ili kuondoa sintofahamu kwa yule anayedai EAMWS ilifanyiwa hila, basi atupe ushahidi ya hilo. Hapa ndipo swali muhimu lilipo.

Mtu akiniambia kuna ushahidi basi weka ushahidi huo hadharani.
Hii ni sawa na wale waliokuwa wanasema CUF ni chama cha waislamu lakini hawakuweza kututhibitishia kwa ushahidi juu ya madai yao. Ndiyo maana leo CUF bado ipo kwa mujibu wa sheria.

Mohamedi, ni rahisi mtu kusoma kitabu na kuamini kuwa EAMWS ilifanyiwa hila, lakini mtu huyo ukimwambia 'prove' atasema nimesoma kitabu cha Mohamed Said, jee hii inaweza kuwa proof!

Mimi si challenge kitabu au maoni ndani yake, ninachokitaka ni kujua kwa evidence. Kwa mfano, Mshume Kiyate alimpa mwalimu pesa, inaweza kuwa alimpa pesa nyingi sana, halina ubishi! wasi wasi ni pale mwalimu anaposema ninakwenda kununa vitu bila senti. Sasa kuna theory kuwa enzi hizo angeweza kudhamiwa na wazee wa mji. Ni kweli! lakini ndio ushahidi kuwa mwalim hakuwa na senti? Dhana si ushahidi.
My main point ni kuwa kila kitu kilichoandikwa kiwe evidence based, na penye nadharia basi isemwe hivyo.

Ndio maana nimekataa hoja ya kuwa enzi hizo hakukuwa na wapagani. Nimetoa ushahidi kuwa hata leo wapagani wapo, evidence! Sikupenda hata kuuliza kwanza definition ya pagan maana majibu yake yangeweza ku embarass zaidi.
 
Tusiwe sawasawa na kichwa cha gramaphone kilichokwama katika santuri.

Ikifika "ushahidi" kinajirudia hapo hapo..."ushahidi, ushahidi, ushahidi..." hadi atokee mtu ainasue.

Tunaweza kusonga mbele na kunogesha ukumbi.
 
Sina ugomvi na jinsi unavyoona mambo.

Mimi simlazimishi mtu kuamini kile nilichoandika.
 
Katika usomi hurekebishi jambo kwa sentensi katika JF.

Mimi niliposoma na kusomeshwa historia ya Tanganyika na maprofesa
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam nilikuwa nikiwaeleza kuwa hiyo historia
imekosewa na wakinisikiliza na kuendelea kufundisha historia ile ile rasmi.

Ndipo nikaamua kuandika kitabu. Sasa nanyi andikeni hiyo historia ambayo
mnaona ndiyo ya kweli.

Mimi nimendika historia ya wazee wangu watu niliokuwa nikiwajua toka utoto
wangu.

Bila shaka huko kwenu nanyi mna wazee hebu andikeni habari zao tuzisome.

Taarifa ninazopata kutoka kwa wanafunzi wanaofanya uzamili hapo Mlimani
ambao huja kunihoji katika tafiti zao wananiambia kuwa waalimu wao wanawaonya
kuhusu kukitumia kitabu changu kama rejea.

Wao bado wako na historia ile ile ya Nyerere ndiye aliyeanzisha TANU peke yake.
 
Siku Kanisa watakapodai ushahidi Insha Allah utatolewa.

Tuendelee na majadiliano.
 
Imam Shaffi (Rahmatullah Aleihy) anasema, "Mimi naweza kusimama na hata watu 100 kwa hoja lakini mjinga mmoja tu hunishinda."

Hivi kweli nyie nyote mmeshindwa kusoma majibu yangu na kuona ushahidi?

Siamini.

Tafadhali kabla hamjasoma zaidi ya hapa hebu rudini nyuma na khasa kama umseoma kitabu hebu
tafakarini taarifa za hawa wafuatao:

Mufti Sheikh Hassan bin Amir
Bilal Rehani Waikela
Shaban Kayugwa
Hamza Aziz
Godfrey Sawaya
Bibi Titi Mohamed

Ushahidi wanao hawa siyo mimi.

Katika orodha hiyo kuna watu kutoka Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi na viongozi wa EAMWS
Hawa ndiyo watakaohojiwa mahakamani na watatoa ushahidi wao.

Nyerere na Kanisa Katoliki ni wajuzi na wanajua nililokuwa nikiandika. Nyerere hakuwa na ujasiri
wa hata kujibu hizo tuhuma na kushikilia kama mnavyoshikilia nyie wacheza pembeni nije na ushahidi
kwa kuwa alijua nisingeweza kuandika yale isipokuwa wenyewe wahusika wamenieleza ukweli.

Mwaka wa 1968 mimi nilikuwa kijana mdogo niliishi katika wakati wa sakata la EAMWS lakini sikuwa na
fahamu za upembuzi wa kuweza kuelewa kwa nini palikuwa na askari mbele ya ofisi za EAMWS.

Jifunzeni kusoma, kufanya tafakuri na kuandika kutoka katika kichwa siyo kwenye mioyo.

Huu ungekuwa mtihani unadhani profesa wako angekupa alama gani F au E au D?

Ila nitakuongezeeni kitu.

Godfrey Sawaya Director of Criminal Investigation baada ya Nyerere kuivunja EAMWS akawa sasa anapita
mikoani na mkoba wa fedha anawahonga watu aliowaona wana ushawishi katika Waislam waiunge mkono
BAKWATA ambayo Nyerere aliwaundia Waislam badala ya EAMWS.

Mradi wa kujenga shule na Chuo Kikuu ukafa pamoja na EAMWS.

Tanzania Episcopal Conference (TEC) ikawa imebaki peke yake inafanya inavyotaka nchini.
Propaganda ikawa inaenezwa kuwa Waislam hatupendi shule ndiyo maana nafazi zote za juu
zimeshikwa na Wakrsto.

Wapo wanaoamini uongo huu hadi leo niandikapo.

Wako watu walichukua hongo ile na wako waliomuogopa Allah wakaikataa.

Bilal Rehani Waikela alikataa hongo ile na ni huyu mzee tukiwa nyumbani kwake ndiye aliyenifunulia
mkasa wote wa EAMWS na akanipa jalada zima alilolitunza kwa miaka 20.

Anasema yeye alikuwa alijua Allah ni muadilifu hataweza kuacha dhulma itawale.

Iko siku Allah atamtuma mtu kuja kufichua yote waliyofanyiwa Waislam na Nyerere na kanisa lake.

Hamza Aziz aliyekuwa IGP yeye alikataa kutii amri ya Waziri wa Ndani Lawi Sijaona ya kumkamata Mufti Sheikh
Hassan kwa tuhuma za kutaka "kupindua serikali ya Nyerere."

Hamza Aziz alimwambia waziri wake kuwa huo ni uzushi yeye hawezi kutuma askari kumkamata mtu mwenye heshima
na mzalendo aliyepigania uhuru na kumjenga Nyerere kama Sheikh Hassan bin Amir.

Je, mngependa kujua Nyerere alihisi vipi alipoelezwa kauli ya Hamza Aziz?
Hapana, hatutaki kujua Nyerere alihisi vipi alipoelezwa kauli ya Hamza Aziz. Tunataka kwanza utujibu, utoe ushahidi ni vipi kanisa Katoliki lilihusika katika kupigwa marufuku kwa EAMWS.

Ungekuwa umeandika riwaya, au novel, tusingeuliza maswali haya. Lakini unajiita mwanahistoria na unachoandika ni fact wakati ambapo mengi wataalamu wa historia watakwambia ni hearsay.

Kwa sababu fulani alikuwambia hivi au vile does not make it a fact. A fact is something that has been researched and both sides of the issue examined. Ndio maana tunauliza maswali.
 
Katika usomi hurekebishi jambo kwa sentensi katika JF.

Mimi niliposoma na kusomeshwa historia ya Tanganyika na maprofesa
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam nilikuwa nikiwaeleza kuwa hiyo historia
imekosewa na wakinisikiliza na kuendelea kufundisha historia ile ile rasmi.

Ndipo nikaamua kuandika kitabu. Sasa nanyi andikeni hiyo historia ambayo
mnaona ndiyo ya kweli.

Mimi nimendika historia ya wazee wangu watu niliokuwa nikiwajua toka utoto
wangu.

Bila shaka huko kwenu nanyi mna wazee hebu andikeni habari zao tuzisome.

Taarifa ninazopata kutoka kwa wanafunzi wanaofanya uzamili hapo Mlimani
ambao huja kunihoji katika tafiti zao wananiambia kuwa waalimu wao wanawaonya
kuhusu kukitumia kitabu changu kama rejea.

Wao bado wako na historia ile ile ya Nyerere ndiye aliyeanzisha TANU peke yake.

Mkuu MS.....acha dharau ndugu yangu..................ulikuja hapa JF na hoja yako ulifikir watu watameza tu...........wewe umejiita mtafiti......hapa JF wapo watafiti vile vile na sio lazima wajitambulishe kama ulivyofanya wewe.........

Hapa JF kuna mambo mazito yanazungumzwa/jadiliwa...........kuna fumbuzi za maana zimepatikana hapa JF..........

Umeulizwa swali.......jibu......kwa wanaochangia hoja hapa kila kukicha unasisitiza wasome kitabu chako.........sijui kwa nini unasisitiza wasome ili waelewe kitabu chako....... sasa unaulizwa swali.....unataka kanisa zima lije kukuuliza............any sensible person or organisation will never come to you and ask for ushahidi amabo wewe umeshindwa kuuweka............ila kuna watu tuliosoma kitabu chako tutakuuliza ili usipotoshe kutumia maandishi yako........otherwise kitabu chako tutakiita ni PROPAGANDA ZA CHUKI DHIDI YA KANISA KATOLIKI........Wakristo na dini nyingine............
 
Inatosha na tuishie hapo si lazima kila kitu kifike ukomo.

Ni kisa kile kile cha santuri na kichwa cha gramaphone.

Hapana haja ya kuhamaki.
 
Kwani nyie ndiyo wasemaji wa Kanisa Katoliki?

Mbona kanisa lipo kimya?

Maswali hakika yanapashwa kuulizwa lakini tunafanyaje pale tunapokuwa
tumekinzana tunashindwa kwenda mbele?

Itakuwa kisa cha Shylock na dai lake la kilo ya nyama.
 
Sina ugomvi na jinsi unavyoona mambo.

Mimi simlazimishi mtu kuamini kile nilichoandika.

Mohamed, kwanza nikufahamishe kuwa mjadala huu ni kwa manufaa ya watu wote wenye kutaka kuelewa na werevu. Fuatilia mjadala utaona una mantiki kuliko zile thread zinazoletwa JF na washabiki wa mambo ya dini hata kama hawazielewi dini zao. Ni mjadala usiolenga nani kashinda au kashindwa, bali kupanuana mawazo.

Kama ulivyowahi kuwa challenge maprofesa baada ya kuona something wrong, ndio hivyo watu wengine wanajaribu kuhoji pale wanapotatizwa.

Ni vizuri umeleta hoja ya EAMWS, kwani mimi ni miongoni mwa watu waliosoma vitabu mbali mbali na kushangaa jumuiya hii ilivyo toweka ghafla. Nimekuwa nasikia Bakwata ni serikali lakini kila nilipohoji ushahidi nilijibiwa ''hujui sytem inavyofanya kazi''. Nilipofuatilia nikagundua kuwa serikali ilikuwa inahudumia Bakwata kwa fedha za walipa kodi kwa mikutano na hata mishahara na nyumba za viongozi. Nilipohoji kuwa ni kwanini Bakwata na si dini zingine sikupewa jibu. Nilihoji iweje waislamu wenyeji wa mji mkuu wa nchi yetu washindwe kujihudumia tukijua wengi walikuwa wafanya biashara wazuri? sikupewa jibu. Huu ukawa ushahidi tosha kuwa waislam wana genuine concern ambayo ni evidence based, na leo mbele ya intellectuals ninaweza kuhoji hili la bakwata.

Tumesikia kuwa wamishenari wa kikristo walishiriki biashara ya utumwa, leo tuna ushahiidi kwani kanisa la pale cape gold cost, (point of no return) kwa watumwa lilisimamimiwa na kanisa (ushahidi). Hata wale waliokuja EA walishiriki na kuna document zinaonyesha (evidence based). Tunajua mwali Nyerere alisomeshwa na kanisa kuna documents (ushahidi). Tuna document kwamba majority ya watu waliounda TANU ni waislam (ushahidi). Tumemsikia mwali Nyerere akisema kwa kauli yake, alipokewa n kuombewa dua pale Bagamoyo(ushahidi). Tunajua pia waarabu walishiriki biashara ya utumwa (ushahidi)

Lipanokuja suala la Bakwata kuwa sehemu ya serikali (ushahidi). Linapokuja suala la serikali kuua EAMWS ghafla na ku-support Bakwata establishment (ushahidi).

Swali ni kuwa kuna evidence gani ya ku link kuuawa EAMWS na ushiriki wa kanisa Katoliki 'specific'? lau kama ingekuwa wakristo kwa ujumla tungeowaomba ushaidi wote, lakini kwa vile ni 'specific Catholic' inaweza kuwa kuna ushahidi na hii ndiyo watu wanataka. Kama tutakwenda kwa masimulizi bila kuwa na evidence basi mwaka kesho atatokea mtu na kutueleza kuwa aliwahi kumsikia mzee mmoja kuwa 'Lutheran Church' ndio walioanzisha vugu vugu la Uhuru. Should we trust him simple like that!

Ulipkwenda kwa mzee akakupa faili alilotunza miaka 20, that was the right thing. Kama kuna document inayo link (Nyerere/IGP/Catholic) that could be a big evidence to support your opinion. My point is, the hypothesis could be absolutely right, but how do you connect the dots to make it right. There is a missing link which raises doubt to some readers.

Mimi binafsi si 'challenge' kitabu chako au maoni yako, wala sikatai mahojiano yako, lakini katika tafiti kama unavyojua ni lazima iwe na ukweli na ushahidi. Na kwa vile ni kitabu cha historia na si riwaya nina haki ya kuhoji pale nisipoelewa.

Kuna watu wanasema Hitler alijiua kwa acid ndio maana mabaki yake hayakuonekana. Hatukubali hili kwasababu hakuna evidence. Kuna watu wanasema alionekana vijijini Peru miaka ya 80 na ni mganga mzuri wa watoto. Hatukubali maana hakuna ushahidi. Ndivyo kanuni za tafiti zilivyo, na kama ni nadharia huwa inasemwa hivyo.

Ninapenda mijadala inayoheshimu utu na imani zetu. Ahsanteni wote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom