Kiswahili ni Kibantu au Kiarabu?

Kiswahili asili yake ni mwambao wa afrika mashariki ili uelewa maana yake nenda ukawaone hao watu wenyewe wa mwambao muonekano wao na tamaduni zao utapata jibu sahihi.
 
Asilimia kuubwa ya maneno ya kiswahili yanatokana na Kiarabu, hakuna lugha duniani inaitwa kibantu, kibantu ni mchanganyiko wa lugha nyingi za watu wenye asili ya kibantu. Watu wenye asili ya kibantu hupatikana kusini mwa sahara. Wale wa Afrika wengine wasio wabantu, ambao na hapa kwetu wapo wengi tu, kama vile wamasai, waIraqw, waRangi, wa Zanaki, waJaluo na kadhalika, utakuta wana asili za kiarabu kwenye lugha zao. Ikumbwe pia uArabu ni lugha na si utaifa. Kuna mataifa mengi katika Afrika yanayoongea kiarabu na wao hujiita wa Arabu, si kwa uTaifa bali kwa lugha.

Ukichukuwa Kiarabu na lugha ambazo si za kibantu lakini za kiafrika zilizongiza maneno yake kwenye kiswahili utakuta kuwa maneno ya lugha za kibantu si mengi sana katika kiswahili, hayawezi fika asilimia 40%, asilimia chache zingine zinatokana na lugha za nchi ambazo zilikuwa na muingiliano mkubwa wa kibiashara na utawala katika pwani ya afrika mashariki, kama vile Kireno, Kijerumani, Kiingereza, Kihindi, Kichina.

Duniani, kila mawasiliano yanavyozidi ndio lugha huchukuwa maneno kila muingiliano wa mataifa unapozidi, ni lugha chache sana zinazojitolesheza na maneno yake yeneyewe, na hizi ni lugha za zamani na huitwa kugha tajiri, utajiri wa kuwa na maneno mengi.

Kiswahili kimebahatika kuwa na maneno mengi ya Kiarabu (Kiarabu ni Lugha tajiri) na nadhani ni hivi ppunde tu na chenyewe kitakuwa moja ya lugha tajiri.

Kwa sasa, kuna hujuma za wazi za kukitowa kishahili kutoka uasili wa kiarabu kwa sababu tu uarabu unahusishwa na uIslaam. Kilanjia zinafanyika kubuni maneno mapaya ambayo hayana hata msamiati wala lafdhi za kiswahili, ili mradi tu, kitoke kwenye asili yake ya asili.

Baraza la kiswahili limeingiliwa na watu wasio na asili ya lugha ya kiswahili. Wenye asili ya lugha ya kiswahili ni watu wa pwani ya Afrika Mashariki na wanaoongea kiswahili kama lugha mama.

Hta neno ki- swahili lenyewe linatokana na kiarabu "sahil", pwani, "sawahil" watu wa pwani.


Mimi bwana zomba sikubaliani na wewe juu ya unacho kisema kwamba hakuna lugha inayoitwa kibantu, lugha ya kibantu ipo na inatoka Afrika ya magharibi ambayo imefika Afrika ya mashariki kwa njia mbali mbali ikiwemo njia ya vita na hata njia ya kutafutia wanyama malisho, hivyo bsi kupitia msururu huo ndio lugha ya kibantu imepatikana Afrika. Jambo la pili si kuungi mkono muheshimiwa zomba pale usemapo kiswahili ni kiarabu, hili mimi niko mbali na wewe na ninasema kiswahili sio kiarabu na badala yake ni kibantu kupitia njia mbali mbali zikiwemo kihistoria na hata kiismu, kupitia njia hizo kiswahili kinajithibitisha wazi kua ni kibantu, tukiangalia hoja ya kiismu kupitia msamiati na tungo za kiswahili na kibantu zimefanana sana lakini hata ile njia ya kihistoria kuna wana historia mbali mbali wana thibitisha kwamba kiswahili ni kibantu kupitia misingi mbalimbali, kwa mfano ugunduzi wa marco polo unathibitisha kwamba kiswahili ni kibantu.
Kwa hoja hizo ni wazi kwamba kiswahili ni kibantu na sio kiarabu kama unavyo dai eti msamiati wenyewe wa neno ka kiswahili, sio kweli kwani kufanana na kulingana kwa neno hilo sio hoja madhubuti inayothibitisha na kama ni hoja basi ni wazi kwamba kiswahili ni kibantu kwani ukiangalia msamiati wa kiswahili na wa kibantu umefanana na unalingana sana.
Naomba ni ishie hapo ni subirie hoja zako juu ya nilicho kisema.
 
Mimi bwana zomba sikubaliani na wewe juu ya unacho kisema kwamba hakuna lugha inayoitwa kibantu, lugha ya kibantu ipo na inatoka Afrika ya magharibi ambayo imefika Afrika ya mashariki kwa njia mbali mbali ikiwemo njia ya vita na hata njia ya kutafutia wanyama malisho, hivyo bsi kupitia msururu huo ndio lugha ya kibantu imepatikana Afrika. Jambo la pili si kuungi mkono muheshimiwa zomba pale usemapo kiswahili ni kiarabu, hili mimi niko mbali na wewe na ninasema kiswahili sio kiarabu na badala yake ni kibantu kupitia njia mbali mbali zikiwemo kihistoria na hata kiismu, kupitia njia hizo kiswahili kinajithibitisha wazi kua ni kibantu, tukiangalia hoja ya kiismu kupitia msamiati na tungo za kiswahili na kibantu zimefanana sana lakini hata ile njia ya kihistoria kuna wana historia mbali mbali wana thibitisha kwamba kiswahili ni kibantu kupitia misingi mbalimbali, kwa mfano ugunduzi wa marco polo unathibitisha kwamba kiswahili ni kibantu.
Kwa hoja hizo ni wazi kwamba kiswahili ni kibantu na sio kiarabu kama unavyo dai eti msamiati wenyewe wa neno ka kiswahili, sio kweli kwani kufanana na kulingana kwa neno hilo sio hoja madhubuti inayothibitisha na kama ni hoja basi ni wazi kwamba kiswahili ni kibantu kwani ukiangalia msamiati wa kiswahili na wa kibantu umefanana na unalingana sana.
Naomba ni ishie hapo ni subirie hoja zako juu ya nilicho kisema.
Kwani hamna vichwa vya kugundua vitu vyenu mpaka muambiwe na Marco polo
 
Mimi bwana zomba sikubaliani na wewe juu ya unacho kisema kwamba hakuna lugha inayoitwa kibantu, lugha ya kibantu ipo na inatoka Afrika ya magharibi ambayo imefika Afrika ya mashariki

Samahani hapo juu ni kweli hakuna lugha 1 ya Kibantu; nadhani inakubalika kuwa kuna kundi ya lugha zinazoitzwa "Kibantu" kwa hiyo kuna "Lugha za Kibantu" lakini hakuna "Lugha ya Kibantu yenyewe". Zinafanana katika msamiati na sarufi. Na kweli hoja ni wasemaji wa lugha zuilizotangulia walitoka Afrika ya Kati-Magharibi.

[QUOTE="adaamhaji, post: 16373901, member: 342670"]Kwa hoja hizo ni wazi kwamba kiswahili ni kibantu na sio kiarabu kama unavyo dai eti msamiati wenyewe wa neno ka kiswahili, sio kweli kwani kufanana na kulingana kwa neno hilo sio hoja madhubuti inayothibitisha na kama ni hoja basi ni wazi kwamba kiswahili ni kibantu kwani ukiangalia msamiati wa kiswahili na wa kibantu umefanana na unalingana sana.[/QUOTE]
Ni kweli sehemu kubwa ya msamiati wa Kiswahili ni Kibantu. Ila tu Kiswahili kimepokea idadi kubwa ya maneno ya nje hasa kutoka Kiarabu, makadirio ni 30-40%. Tabia hii inalingana sana na Kiingereza ambayo ni pia lugha ya kundi moja (=Kigermanik) iliyopokea karibu nusu ya msamiati kutoka kwa lugha ya familia nyingine (yaani kutoka Kifaransa hasa).
Inaonekana lugha si bora kama ni "safi"; kinyume chake tunaona lugha zilizofaulu sana katika historia zilikuwa lugha hai zilizoendelea kukua na kupokea maneno (pamoja na mawazo, yaani neno haliji peke yake) kutoka nje na kuyaingiza kwao. Hii inawezakana kuona kwenye Kilatini, Kiarabu, Kituruki, Kiingereza, Kidaransa, Kihispania, na sasa pia Kiswahili.
(bila shaka kuna nyingine )
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom