Kirusi kinachotisha kuliko Corona ni uoga/ hofu

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,239
113,613
Dunia nzima sasa ni kama imesima kwa sababu ya hofu ya kirusi cha Corona.

Watu hawaendi makazini. Shule zimefungwa. Michezo imesitishwa. Matamasha hakuna. Mikusanyiko marufuku. Madukani kuna uhaba wa baadhi ya bidhaa hadi watu wanatwangana ngumi wakigombea makaratasi ya chooni.

Eti yote hayo ni kwa sababu watu wanakiogopa hicho kirusi cha Corona.

Mimi kirusi cha Corona sikiogopi. Kama malaria haikuwahi kuniua, kama kipindupindu nilikistahimili, nini Corona bana?

Kwa nilichokiona, kirusi pekee kinachotisha sasa hivi ni kirusi cha uoga/ hofu.

Uoga/ hofu hii ndo inayofanya maisha yasimame. Ndo inayofanya watu wanunue na kuhodhi makaratasi ya chooni kupelekea hadi kurushiana ngumi.

Hofu hii imewatoa kabisa akili watu. Watu hawafikiri kabisa kwa kutumia akili. Wanatenda kwa kufuata hofu.

Hofu isiyo na akili [irrational fear] ndiye kirusi wa kuogopwa kushinda hata ukoma.

Mshinde huyo kirusi wa uoga/hofu.
 
Sawa ndio mgeni CORONA keshaingia Tanzania.Lakini nafikiri hatutakiwi kupanic.Maana HAMAKI ni mbaya kuliko ugonjwa wenyewe.Tuendelee kujikinga huku tukiomba hili nalo lipite.Mbona hata EBOLA ilitingisha lakini nayo ilipita.
Mungu ibariki Dunia
Mungu ibariki Africa
Mungu ibariki Tanzania.
 
Sawa ndio mgeni CORONA keshaingia Tanzania.Lakini nafikiri hatutakiwi kupanic.Maana HAMAKI ni mbaya kuliko ugonjwa wenyewe.Tuendelee kujikinga huku tukiomba hili nalo lipite.Mbona hata EBOLA ilitingisha lakini nayo ilipita.
Mungu ibariki Dunia
Mungu ibariki Africa
Mungu ibariki Tanzania.

Hamaki ndo kinachoendelea sasa hivi!
 
Ndugu yangu, hofu haijajitengeneza, imekuja baada ya matokeo yatokanayo na huyo Virus, so you want people to ignore the existence of this epidemic disease? Ni sahihi kuwa na hofu na kuchukua hatua kama inavyofanyika,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kweli tupunguze uoga na kuogopeshana. Ndui iliua sana watu na wako walioishi hadi leo, corona sio ya kwanza, hii nayo itapita na maisha yataendelea. Tumekuwa waoga utadhani hakujawahi tokea ungonjwa mwingine toka dunia ianze! tusiogopeshane tuchukuwe tahadhali kwa kujiamini tu. Bwana asipoilinda afya yako... wailindao wakesha bure!
 
Kwa kweli tupunguze uoga na kuogopeshana. Ndui iliua sana watu na wako walioishi hadi leo, corona sio ya kwanza, hii nayo itapita na maisha yataendelea. Tumekuwa waoga utadhani hakujawahi tokea ungonjwa mwingine toka dunia ianze! tusiogopeshane tuchukuwe tahadhali kwa kujiamini tu. Bwana asipoilinda afya yako... wailindao wakesha bure!

Kabisa!

Na naamini tunaweza kuwa makini bila hamaki!
 
jamii forum imekufa jamii forum ya sasa sio ya mwaka 2012,13 ,14,15 mwanzoni jf ya sasa imevamiwa na watoto wa dogo wa facebook na instagram mtoto mdogo anatoa hoja ya kishamba kabisa na alafu wahusika wanauwacha . hiii ni aibu sana kwa wahusika na sisi wadau wa muda mrefu maana bila sisi wadau wa muda mrefu leo hii hawa watoto wadogo wasigeijua jf . hivi wahusika kwann hawa watoto msiwape jukwaa lao . jukwaa la watoto chini ya 18 . kuliko kuja humu wanatuaharibia sana jukwaa linakosa mvuto jukwaa limepoteza ushawishi wada wengine wanatoka wanenda twitter
 
Dunia nzima sasa ni kama imesima kwa sababu ya hofu ya kirusi cha Corona.

Watu hawaendi makazini. Shule zimefungwa. Michezo imesitishwa. Matamasha hakuna. Mikusanyiko marufuku. Madukani kuna uhaba wa baadhi ya bidhaa hadi watu wanatwangana ngumi wakigombea makaratasi ya chooni.

Eti yote hayo ni kwa sababu watu wanakiogopa hicho kirusi cha Corona.

Mimi kirusi cha Corona sikiogopi. Kama malaria haikuwahi kuniua, kama kipindupindu nilikistahimili, nini Corona bana?

Kwa nilichokiona, kirusi pekee kinachotisha sasa hivi ni kirusi cha uoga/ hofu.

Uoga/ hofu hii ndo inayofanya maisha yasimame. Ndo inayofanya watu wanunue na kuhodhi makaratasi ya chooni kupelekea hadi kurushiana ngumi.

Hofu hii imewatoa kabisa akili watu. Watu hawafikiri kabisa kwa kutumia akili. Wanatenda kwa kufuata hofu.

Hofu isiyo na akili [irrational fear] ndiye kirusi wa kuogopwa kushinda hata ukoma.
Hofu hiyo hiyo ndio aliyonayo Mzee Meko kiasi cha kutumia jeshi la magereza kupambana na wakina dada watatu wasio hata na kiboko eti wameenda kuvamia magereza! Mzee Meko amejawa na hofu isiyokua na akili kama ulivyoandika!
 
Watu kama wewe huwa mnazingua sana,hoja imewekwa nyingine umekurupuka kuwasimanga wengine. Mzee baba kama unajiona una busara nenda LinkedIn,twitter au magrup ya wazee watsup

#mhengapoteaJF
jamii forum imekufa jamii forum ya sasa sio ya mwaka 2012,13 ,14,15 mwanzoni jf ya sasa imevamiwa na watoto wa dogo wa facebook na instagram mtoto mdogo anatoa hoja ya kishamba kabisa na alafu wahusika wanauwacha . hiii ni aibu sana kwa wahusika na sisi wadau wa muda mrefu maana bila sisi wadau wa muda mrefu leo hii hawa watoto wadogo wasigeijua jf . hivi wahusika kwann hawa watoto msiwape jukwaa lao . jukwaa la watoto chini ya 18 . kuliko kuja humu wanatuaharibia sana jukwaa linakosa mvuto jukwaa limepoteza ushawishi wada wengine wanatoka wanenda twitter
 
Dunia nzima sasa ni kama imesima kwa sababu ya hofu ya kirusi cha Corona.

Watu hawaendi makazini. Shule zimefungwa. Michezo imesitishwa. Matamasha hakuna. Mikusanyiko marufuku. Madukani kuna uhaba wa baadhi ya bidhaa hadi watu wanatwangana ngumi wakigombea makaratasi ya chooni.

Eti yote hayo ni kwa sababu watu wanakiogopa hicho kirusi cha Corona.

Mimi kirusi cha Corona sikiogopi. Kama malaria haikuwahi kuniua, kama kipindupindu nilikistahimili, nini Corona bana?

Kwa nilichokiona, kirusi pekee kinachotisha sasa hivi ni kirusi cha uoga/ hofu.

Uoga/ hofu hii ndo inayofanya maisha yasimame. Ndo inayofanya watu wanunue na kuhodhi makaratasi ya chooni kupelekea hadi kurushiana ngumi.

Hofu hii imewatoa kabisa akili watu. Watu hawafikiri kabisa kwa kutumia akili. Wanatenda kwa kufuata hofu.

Hofu isiyo na akili [irrational fear] ndiye kirusi wa kuogopwa kushinda hata ukoma.
Kwa hili leo tuko wote, binafsi mpaka nife kwa mafua Mungu atakuwa ameamua tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
jamii forum imekufa jamii forum ya sasa sio ya mwaka 2012,13 ,14,15 mwanzoni jf ya sasa imevamiwa na watoto wa dogo wa facebook na instagram mtoto mdogo anatoa hoja ya kishamba kabisa na alafu wahusika wanauwacha . hiii ni aibu sana kwa wahusika na sisi wadau wa muda mrefu maana bila sisi wadau wa muda mrefu leo hii hawa watoto wadogo wasigeijua jf . hivi wahusika kwann hawa watoto msiwape jukwaa lao . jukwaa la watoto chini ya 18 . kuliko kuja humu wanatuaharibia sana jukwaa linakosa mvuto jukwaa limepoteza ushawishi wada wengine wanatoka wanenda twitter
Unamaanisha mtoa mada kaja na hoja za kitoto?

Ungeleta vielelezo/hoja za kuonesha utoto wa post.
Vinginevo acha porojo za kitoto kutuaminisha kuwa hoja ya mtoa mada ni ya kitoto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom