Mkuu iko hivi, Kitabu cha Joshua nimekisoma na hiyo habari iliyoandikwa kwamba jua lilisimama, naifaham vizuri sana.
Pili, kwamba Papa aliomba radhi kwa kitendo cha kuuwawa kwa Gallileo sio kigeni, nafaham pia.
Hoja iko hapa, nimekuomba urekebishe usemi wako kwamba maandiko yamesema jua
lilisimama na wewe kwa
mtazamo wako unaona ni
maandiko yamedanganya,
ukasema kanisa limeomba
msamaha ukimaanisha ni
ushahidi wa kuungama kwamba
makosa yalifanywa na kanisa.
Kwa muktadha huo ukathibitisha
kwamba Mungu amedanganya.
Hilo sio hitimisho sahihi, ndio
maana nilitoa mfano hapa
kwamba endapo utakutana na
maandiko yenye maelezo ya
Kiranga ukayasoma, itakua
sahihi kuhitimisha kwamba
Kiranga hayupo? (Sikupata jibu
ikaleta mlolongo mrefu sana wa
majibizano kufikia hatua ya
Kiranga kusema hawezi jibizana
na mimi uelewa wangu mdogo).
Naomba uelewe kwamba, tatizo
langu halipo kwenye maandiko
au maelezo uliyoyaleta kama
rejea, la hasha. lipo kwenye
kauli yako ya awali kwamba
Mungu amedanganya ( Ina
maana ni kitendo ambacho
umekishuhudia kwamba
kimefanya na huyo mhusika
unaemtuhumu) ndio maana
nilikua nakuuliza mara kadhaa,
una uhakika Mungu
amedanganya? Ili tupate
ushuhuda kutoka kwako jinsi
ilivyotokea.