Kumbe members wa JF wanaamini Mungu hadi zama hizi ni kwa sababu hawajui kiingereza hivyo wanakosa maarifa yaliyo kwenye vitabu viliandikwa kwa kiingereza.
Sasa je,hao wengine wanaojua kiingereza na ni wasomi mbona bado hadi zama hizi wanaamini Mungu?
Sababu ni nyingi sana.
Hata Papa anaweza kuwa kiongozi msomi haamini Mungu na anajua Kiingereza mpaka Kilatini lakini ana sababu zake za kuendeleza imani ya Mungu.
Kwanza kabisa.
1. Ni vigumu kujua imani ya mtu, kwa matendo yao utawajua, hata hao wanaosema wanaamini Mungu, imani yao inatia shaka, wengi ni walevi, wazinzi, wezi, wajivuni etc. Mambo ambayo mnasema Mungu anakataza. Mpaka hapo tukisema wanaamini Mungu unawezea kauli hiyo shaka.
2. Watu wengine wanasema wanaamini Mungu kwa uvivu tu. Kusema unaamini Mungu ni kama maji yanayoshuka mlima. Huulizwi sana, huwakwazi wapendwa wako kwenye familia, huhatarishi kazi yako, huonekani mtu wa ajabu. Katika maisha yenye matatizo mengi, wengi wanaamua kusema hivyo wasipate maswali mengi, hata pale wanapoona stories za Mungu hazi add up.
3.Wengine wanajua Kiingereza lakini hawana uwezo/ access wakufuatilia arguments za kuwepo na kutokuwepo Mungu.
4. Wengine wanajua Kiingereza na wanaweza kufuatilia arguments, lakini wameshajikubalisha kwamba suala la kuamini Mungu ni la imani, sila argument, kwa hiyo wameamua kuamini tu.
5.Wengine wanaona kwamba hata kama Mungu hayupo, ni vizuri watu wenye fikra ndefu kusema yupo, ili isije kuwa vurugu watu wasio na simile wakigundua Mungu hayupo na kukosa sababu ya kuishi kwa adabu.
6. Wengine wana maslahi. Viongozi wa makanisa, serikali, mashirika, sehemu yoyote inayokusanya watu wengi, wanaona ni rahisi kuwaongoza watu kama wanaamini Mungu yupo, zaidi ya wale ambao hawaamini Mungu yupo.
7. Wengine wamelelewa katika kuamini Mungu na washakunywa sana maji ya bendera, hata wakijua Mungu hayupo, wataona kashakuwa sehemu kuwa sana ya maisha yao, hawawezi kubadili imani uzeeni.
8. Wengine wanaona Mungu ni dhana ya maana, kwa sababu inatumika kama kichaka cha kuficha ujinga wote wa watu, swali lolote ambalo hatujui jibu lake, tunalipachika kwenye kichaka cha Mungu. Hivyo, watu wanaonekana wanajua mambo. Ukimuondoa Mungu ujinga wetu unatonekana ulivyo mkubwa, na hiliwengine wanaona si jambo zuri.
9. Wengine wanaona mawazo ya kutokuwapo Mungu ni ya hatari na yataleta maangamizi makubwa. Ili kuepuka maangamizi haya, imani ya Mungu ni bora iendelezwe. Hata kama hayupo na wanajua hayupo.
10. Wengine wanaona mifumo mingi wanayoitaka iliyopo sasa imeegemea imani ya Mungu. Wanaokandamiza wanawake watasema dini imepitisha hilo, wanaokandamiza weusi nao wana mistari yao, wanaokandamiza watu tofauti nao wana mistari yao ya dini. Hata watawala wakitaka urahisi kutwawalawanasema "fulani chaguola Mungu". Ukiwaondoela mfumo wa Mungu, mifumo yao mingi sana kandamizi itaanguka na hawataki hilo. Leo mtu wa ISIS anayeua watu kwa jina la dini na kujipatia mafao mengi hivyo, ukimwambia Mungu hayupo,unamuharibia namna yake ya kukandamiza watu. Watu wanaosema "fulani chaguo la Mungu"ukiwaondolea Mungu, unawaharibia msingi wa ukandamizaji wao. Hawa, hata wakijua Mungu hayupo, hawatakubali.