Kipindi kigumu jimboni Kawe

Mkuu sasa unabore kilasiku thread zako ni Mnyika na Halima Mdee mbona huku kigamboni husemi acha unafiki una ujinga wa kitoto

Halafu walivyo mapuruzai wakizungumzia Mnyika wanajifanya wakazi wa Ubungo na walimpa kura zao.. Baadae wakija kwa Mdee wanajifanya wakazi wa kawe na kura walimpa..! Hawajui wanatakiwa wawe na kumbukumbu wanapokuwa waongo..
 
Kwa maajabu ya Tanzania na mfumo wake wa elimu, unaweza kuta mtu mwenye mawazo kama haya yako amemaliza chuo.

Parking ya gari anaamua mbunge kupanda au kushuka gharama yake?

Shida yetu hatufahamu mfumo wa maamuzi na utekelezaji katika maeneo yetu. Halmashauri zina nguvu ya kuamua hilo, sasa sijui juu ya nini hamzitumii kufanya maamuzi hayo. Kitu pekee anachoweza kufanya mbunge katika hilo ni kuwaomba madiwani wa chama chake waligomee hilo kwenye vikao vya halmashauri, Je, wapo wangapi katika halmashauri?
una akili kama za kuku yaani mbili tu!kuwa na upinzani sio kwamba wote watakuwa wasafi,tuwe na ngozi ngumu ya kukosolewa,mwanza mea alikuwa chdm na madiwani wengi ni cdm na sheria za miji zinatungwa na kusimamiwa na cdm na mbunge akiwepo,unasemaje sasa?
 
AU ULITAKA AFANYE HAYA YA MAGAMBA?

Mbunge aweka kando ubunge, afanya kazi ya kutoa `uchawi`


Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) , Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu, juzi aliweka ubunge wake kando na kurejea kazi yake ya uganga kwa kutoa ‘wachawi' katika kijiji cha Kwemazandu.




Mbunge huyo alifanya kazi hiyo baada ya kuhudhuria mkutano wa kijiji uliopitisha maamuzi ya kumtimua mmoja wa wanakijiji wao kwa tuhuma za kishirikina.Akizungumza na NIPASHE kwa simu kutoka Korogwe, alisema alilazimika kufanya kazi hiyo wakati wa mkutano wa halmashauri ya kijiji ambao pamoja na mambo mengine, ulijadili suala la kijiji hicho kukosa mvua kwa kipindi kirefu.


Kufuatia kutonyesha kwa mvua hiyo, wakazi wa kijiji hicho walikuwa wakimtuhumu mkazi mwenzao, (jina limehifadhiwa) kwamba amekuwa akijigamba mitaani kuwa mvua kijijini hapo haitanyesha.




Baada ya wajumbe wa kijiji kuchangia kuhusu suala hilo, ndipo mbunge alipoondoka huku akiongozana na wajumbe hao pamoja na wananchi waliofurika kumwangalia, wakielekea katika nyumba ya mtuhumiwa huyo kwenye kitongoji cha Kimunyu."Jamani mnakumbuka kwenye kampeni nilivyosema, napenda niwakumbushe, nilisema kazi ya ubunge ni ya miaka mitano lakini kazi yangu ya uganga siwezi kuiacha nitaifanya hadi nitakapokufa," alisema Profesa Majimarefu.
Mbunge huyo baada ya kueleza hivyo aliongozana na mwenyekiti wa kijiji hicho, mtendaji wa kijiji na mwenye nyumba hizo kuingia nao ndani ya nyumba ya mtuhumiwa.


Baada ya kuingia katika nyumba hiyo, Profesa Maji Marefu alitoka akiwa na tunguri mbalimbali zilizodaiwa kumilikiwa na mtuhumiwa huyo.CHANZO: NIPASHE
 
hapo manake hatoshi.inabidi uchaguzi ujao tumpe mbunge wa chama kilichopo madarakani ili aweze kutekeleza

kabla ya mdee alikuwepo rita wa ccm tena ni kipindi hicho alikuwa waziri mdogo viwanda na biashara aliwasaidia nini zaidi ya kuuza viwanda vyetu kama chuma chakavu au unafikiri tumesahau.labda ungesema hivi alipokuwepo wa ccm tulikuwa na kila kitu lakini alipokuja huyu mdee ameviondoa

 
Mimi nshapata taarifa ya vikao kama mara 3 ivi..nasijaenda hatA kimoja..sasa sijui vikao gani unatAka uitwe wewee...

Wavamiz wa Mabwepande ambao Wako juu ya sheria unawasaidiaje ???

Kwa kifupi utakuwa umeandika kwa interest zako tuu..kuna kitu umefaiL,unatafutA mchawi

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Wananchi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi kigumu cha kukosa mwakilishi aliye makini bungeni katika kipndi cha mwaka 2010 kuelekea 2015. Mbunge aliyeingia kwa mbwembwe nyingi Halima Mdee amekuwa ni zigo lisilosaidia wapiga kura badala yake anajisaidia mwenyewe.

Tangu amechaguliwa:
1. Hapendi kuitisha mikutano ili kupata mawazo ya wananchi
2. Wananchi wa Madale waliopatwa na mashambulizi ya polisi wamekosa pole na msaada wake
3. Wakazi wa Majipwande wanamlilia kwa kutopata msaada wa mali na faraja toka kwake
4. Mfuko wa Jimbo haujatolewa maelelezo kwa wananchi
5. Kushindwa kutekeleza ahadi zake za kuinua kiuchumi vikundi vya vijana na wanawake
6. Kushindwa kutatua matatizo wanayoyapata vijana wa bodaboda na bajaji

Hizo ni kero chache ambazo zilitakiwa zifanyiwe kazi na mbunge wetu.

Kwa kweli wakazi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi tete tunamkumbuka RITA Mlaki ambaye alikuwa karibu na wapiga kura.
Wenye akili timamu tunajua tunachofanya. Huyu mafilili kwani ye ni mkazi wa Jimbo gani! Segerea yupo, Ubungo yupo yupo kwenye majimbo yote yanayoongozwa na CDM. Fuatilieni thread zake za e nyingi tu ni kero kwa wabunge wa CDM.
 
Wananchi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi kigumu cha kukosa mwakilishi aliye makini bungeni katika kipndi cha mwaka 2010 kuelekea 2015. Mbunge aliyeingia kwa mbwembwe nyingi Halima Mdee amekuwa ni zigo lisilosaidia wapiga kura badala yake anajisaidia mwenyewe.

Tangu amechaguliwa:
1. Hapendi kuitisha mikutano ili kupata mawazo ya wananchi
2. Wananchi wa Madale waliopatwa na mashambulizi ya polisi wamekosa pole na msaada wake
3. Wakazi wa Majipwande wanamlilia kwa kutopata msaada wa mali na faraja toka kwake
4. Mfuko wa Jimbo haujatolewa maelelezo kwa wananchi
5. Kushindwa kutekeleza ahadi zake za kuinua kiuchumi vikundi vya vijana na wanawake
6. Kushindwa kutatua matatizo wanayoyapata vijana wa bodaboda na bajaji

Hizo ni kero chache ambazo zilitakiwa zifanyiwe kazi na mbunge wetu.

Kwa kweli wakazi wa jimbo la Kawe tupo katika kipindi tete tunamkumbuka RITA Mlaki ambaye alikuwa karibu na wapiga kura.

Binafsi nakupongeza kwa kutoa kero zako hadharani, nakushauri uwasiliane na Mbunge wako. Bila shaka Halima atapita hapa.
Ninawashauri wabunge kuwa makini sana na malalamiko kama haya na kujisahihisha kama ni kweli au kutolea maelezo stahili kama ni shutuma za uongo.
 
Gombea basi wewe tukupe. We unataka mbunge ashugulikie kila kitu? hao wabunge wengine wamefanya nini? Magamba mna shida sana,, hizo pesa za jimbo waulize magamba wenzio maana wao ndo wanajua ziko wapi,,, wala usimlaumu Mdee. Na aliyekutuma mwambie huku JF tuko vizuri magorofani hatujadili hoja zisizo na mshiko. Huwezi anza kumlaumu mbunge wakati bado ana miaka miwili na ushee. Haya zile ahada 77 za mheshimiwa sana mbona huuliziii? kuna meli ngapi zimeshatengenezwa? Je kigoma imekuwa kama Dubai? Reli je? Nakushauri ukiwa bored badala ya kupost vitu kama hivi ingia hapa www.theudaku.blogspot.com:A S-coffee:
CHADEMA kubalini kupokea ushauri ili huyo mbunge wenu wa kawe aendelea kutawala..... badala ya kutukana ..tatizo lenu hamtaki kupokea ushauri kwa mambo yanayohusu chama chenu..mnajiona muda wote mko sawa... ukweli uko wazi mdee hakuna alichokifanya hadi muda huu zaidi ya kupiga kelele bungeni kwa mambo ya jumla jumla tu..... mi nawambia ukweli 2015 wabunge wa upinzani hasa CHADEMA ni wa chache sana watakaorudi kuwa wabunge .... ushauri pokeeni ushauri huu haitajiki hata laki tano kwenda kufanya mkutano na wananchi kwenye maeneo ya wananchi wenye matatizo , yani kufanya mkutano kusikiliza kelo za wananchi nalo linahitaji ela za CCM???.AU USAIDIWE NA SERIKALI???. JITAZAMENI UPYA CHADEMA WENZENU WANATEKELEZA AHADI NINY MNAENDELEE NA MAANDAMANO SASA SIJUI 2015 MTASEMA TULIFANYA MAANDAMANO 100 AU TUMEJENGA ZAHANATI..KAZI MNAYO
 
Mkuu usikubali kusombwa na mafuriko ya siasa za maji ya chooni toka magamba.
Halima amekuwa anakutana na wananchi wa jimbo lake tangu bunge lilipomalizika. Mathalani wiki hii yote alikuwa na ratiba ya kukutana na wapigakura wake ofisini kwake kinondoni.
Lakini pia amekuwa akifanya mikutano mingi na wananchi huko mitaani, hata weekend hii ana mikutano kadhaa huko huko madale, mabwepande, chasimba na maeneo ya jirani.
Hawa magamba wanamzushia Halima ili kuhalalisha posho zao za kila siku.
Angalau wewe Mkuu Mwita Maranya umejibu bila jazba lakini jawabu zako hazitoshelezi. Ingefaa ungeweka angalau data kidogo na/au ratiba kuhusu mikutano hiyo.

Ikiwa hoja ya mleta mada tunaona ni ya kipuuzi, ingekuwa busara na pigo kwa propaganda za Magwanda kuzizima kwa matokeo halisi na data, kuliko kulinganisha kwa kauli kavu na yaliyofanywa na Mkuu wa Wilaya/serikali, vyenginevyo kusingekuwa na haja ya kuwa na wabunge.

Mimi sielewi kile ambacho Mhe. Mdee aliahidi, alichotekeleza na kilichoko katika aajenda za muda mfupi na mrefu, lakini kwa kuwa huwa anaingia humu, na kama haiingii wanaompenda wamtonye, nahisi ingekuwa busara kwake kufanya kama vile alivyofanya Marahemu Regia (R.I.P) au anavyofanya Mhe. Mnyika, kuweka orodha ya ahadi zake jimboni na aliyomudu kuyatekeleza, kulikoni sisi wapambe, wafuasi, wapenzi na wanachama wa CDM kuvurumisha makombora tu.

Mara kadhaa kuna watu humu JF wanasema kuwa udhaifu mmoja wa wapambe wa vyama vyetu vya upinzani ni kuwa wanasukumwa na jazba tu, hawapendi kukosolewa wala kupokea ushauri. Hapa pametajwa mambo sita tu, tuangalie ukweli wa madai haya. Yepi yalikuwa katika ahadi zake, yepi ni ya kibinadamu, hayakutolewa ahadi lakini yametokea na kayashughulikia vipi. Tuchukulie haya yanayosemwa kama ni changamoto, ikiwa ni kweli zifanyiwe kazi na kama ni uongo zizimwe kwa nguvu ya hoja.
 
CHADEMA kubalini kupokea ushauri

Ushauri tunapokea sana lakini si haya majungu yanayotengenezwa na wanamagamba. Na kama kwa uelewa wako unaona huu ndio ushauri, na tunapaswa kuupokea basi nakuhakikishia kwamba hatutaupokea kamwe.
 
Halima no jembe wewe .....achana na hicho Kichwa kabisa ...ni mzuri kuanzia kichwani hadi bungeni ....
 
Katika thread za namna hii nilitegemea kuona watu wakishusha data za mambo aliyofanya mbunge katika kutekeleza ahadi zake na kutatua kera za wananchi na mikakati endelevu ya maendeleo, ulinzi na usalama. Unfortunately inaonekana hakuna cha kujivunia kilichofanywa...business as usual...
 
Angalau wewe Mkuu Mwita Maranya umejibu bila jazba lakini jawabu zako hazitoshelezi. Ingefaa ungeweka angalau data kidogo na/au ratiba kuhusu mikutano hiyo.

Ikiwa hoja ya mleta mada tunaona ni ya kipuuzi, ingekuwa busara na pigo kwa propaganda za Magwanda kuzizima kwa matokeo halisi na data, kuliko kulinganisha kwa kauli kavu na yaliyofanywa na Mkuu wa Wilaya/serikali, vyenginevyo kusingekuwa na haja ya kuwa na wabunge.

Kwa kuwa Mhe. Mdee huwa anaingia humu nahisi ni busara na yeye pia kufanya kama vile alivyofanya Marahemu Regia (R.I.P) au anavyofanya Mhe. Mnyika, aweke orodha ya ahadi zake jimboni na aliyofanya huko au pengine nchini, kulikoni sisi wapambe, wafuasi, wapenzi na wanachama wa CDM kuvurumisha makombora tu.

Mara kadhaa kuna watu humu wamesema kuwa udhaifu mmoja wa wapambe wa vyama vyetu vya upinzani hawapendi kukosolewa wala kupokea ushauri. Ni vizuri basi, haya yanayosemwa kuchukuliwa kama ni changamoto, ikiwa ni kweli zifanyiwe kazi na kama ni uongo zizimwe kwa nguvu ya hoja.

Mkuu MAMMAMIA hawa watu wanafahamu fika shughuli anazofanya Halima Mdee isipokuwa kwakuwa wako kazini ndio maana wako busy kila siku kumtuhumu hajafanya hiki ama kile. Wakimaliza kwa Halima wanahamia kwa Mnyika, tena ni watu wale wale, leo wanasema wanakaa jimbo la kawe lakini kesho utawasikia wanajinadi kwamba wanakaa jimbo la ubungo.

Wakati mwingine mtu unaona hata uvivu kuwaandikia ratiba nzima ya mikutano ya Halima kwakuwa hawako hapa kwa nia nzuri. Mimi nakaa jimbo la Ukonga lakini bado ninafuatilia na kujua kinachofanyika kawe sembuse mtu anayejiita mwanakawe?
 
Last edited by a moderator:
Mfuku wajimbo kwamimi mkazi wakata yamakongo mwaka huu,unatujengea vivuko viwili vyawenda kwamiguu naumesaidia kukarabati barabara yamakongo juu kuja savey!Tembele uliza wamtendaji kata yamakongo utayapata haya!Gharama kama naikumbuka vizuri ni 8 to 10m!Wewe mtoa mada uko kata gani mtaa gani?
 
Mkuu MAMMAMIA hawa watu wanafahamu fika shughuli anazofanya Halima Mdee isipokuwa kwakuwa wako kazini ndio maana wako busy kila siku kumtuhumu hajafanya hiki ama kile. Wakimaliza kwa Halima wanahamia kwa Mnyika, tena ni watu wale wale, leo wanasema wanakaa jimbo la kawe lakini kesho utawasikia wanajinadi kwamba wanakaa jimbo la ubungo.

Wakati mwingine mtu unaona hata uvivu kuwaandikia ratiba nzima ya mikutano ya Halima kwakuwa hawako hapa kwa nia nzuri. Mimi nakaa jimbo la Ukonga lakini bado ninafuatilia na kujua kinachofanyika kawe sembuse mtu anayejiita mwanakawe?
Ninakubaliana kabisa na wewe mkuu, lakini kuwanyamazia ndiko kunakowapa kidomodomo na kueneza propaganda zao. Kama nilivyosema, hapa pametolewa madi sita tu, pata muda au mwengine yeyote kutoka kawe, wamwagieni hapa data na matukio tuone kama akina MAFILILI na mwanakawe watakuwa na la kusema.
 
Huyo ni mbunge tu wa kajimbo kama kawe ndo hivo .kazi yake kwenda kutwanga umbea salaoon kinondoni .
Mungu mkubwa hawakupewa nchi sijui tungetokea wapi
 
Back
Top Bottom